Matukio ya Maana Katika Historia ya Kisasa ya Mashahidi wa Yehova
1870 Charles Taze Russell na kikundi kutoka Pittsburgh na Allegheny, Pennsylvania, Marekani, waanza funzo la utaratibu la Biblia
1870-75 Russell na washiriki wake wa funzo wajifunza kwamba wakati Kristo ajapo tena, yeye hataonekana kwa macho ya kibinadamu na kwamba kusudi la kurudi kwake latia ndani kubarikiwa kwa familia zote za dunia
1872 Russell na kikundi chake cha funzo wapata kufahamu bei ya fidia ambayo Kristo aliandalia wanadamu
1876 C. T. Russell apokea nakala ya Herald of the Morning, katika Januari; akutana na N. H. Barbour, mhariri, kiangazi hicho katika Philadelphia, Pennsylvania
Makala ya C. T. Russell, iliyochapwa katika toleo la Oktoba la Bible Examiner, katika Brooklyn, New York, yaelekeza kwenye 1914 kuwa mwisho wa Nyakati za Mataifa
1877 Kitabu Three Worlds chatangazwa, kwa sababu ya jitihada za pamoja za N. H. Barbour na C. T. Russell
C. T. Russell atangaza kijitabu The Object and Manner of Our Lord’s Return, kwenye ofisi za Herald of the Morning, katika Rochester, New York
1879 Russell aacha kabisa kutegemeza Herald of the Morning, katika Mei, kwa sababu ya mtazamo wa Barbour juu ya fidia
Toleo la kwanza la Zion’s Watch Tower and Herald of Christ’s Presence, la Julai 1879
1881 Trakti za kwanza zilizotangazwa na Wanafunzi wa Biblia; kabla ya 1914, ugawanyaji wa trakti wa kila mwaka wajumlika kuwa makumi ya mamilioni ya nakala katika lugha 30
Zion’s Watch Tower Tract Society yaanzishwa; mwito watolewa kusema “Wahubiri 1,000 Watakwa,” wengine kuwa makolpota wa kawaida, wengine kutumia muda wowote wawezao ili kueneza kweli ya Biblia
Kugawanywa kwa nakala 300,000 za Food for Thinking Christians kwa waenda-kanisani katika majiji makuu katika Uingereza
1883 Watch Tower lafika China; aliyekuwa mishonari Mpresbiteri upesi aanza kutoa ushahidi kwa wengine huko
1884 Kichapo Food for Thinking Christians chafika Liberia, Afrika; msomaji mwenye kuthamini aandika akiomba nakala ili azigawanye
Zion’s Watch Tower Tract Society yakatibiwa kisheria katika Pennsylvania; yasajiliwa kisheria Desemba 15
1885 Vichapo vya Watch Tower tayari vinasomwa na baadhi ya watu wenye njaa ya kweli katika Amerika Kaskazini na Kusini, Ulaya, Afrika, na Asia
1886 The Divine Plan of the Ages chatangazwa, buku la kwanza la mfululizo uitwao Millennial Dawn (baadaye liliitwa Studies in the Scriptures)
1889 Bible House yajengwa kwenye Arch Street, katika Allegheny, Pennsylvania, ikiwa makao makuu ya Sosaiti
1891 Kikusanyiko cha kwanza cha Wanafunzi wa Biblia walichokiita mkusanyiko, katika Allegheny, Pennsylvania (Aprili 19-25)
1894 Waangalizi wasafirio ambao walikuja kuitwa mapilgrimu (leo, waangalizi wa mzunguko na wa wilaya) watumwa kuhusiana na programu ya Sosaiti ya kuzuru makutaniko
1900 Ofisi ya tawi ya kwanza ya Watch Tower Society yafunguliwa, katika London, Uingereza
Wanafunzi wa Biblia wamekwisha kutoa ushahidi katika nchi 28, na ujumbe wanaohubiri umefikia angalau nchi 13 nyinginezo
1903 Kugawanywa kwingi kwa trakti za bure nyumba hadi nyumba siku za Jumapili; mapema kidogo, kugawanywa kwingi kwa trakti kulifanywa barabarani karibu na makanisa
1904 Hotuba za C. T. Russell zaanza kutokea kwa ukawaida katika magazeti ya habari; katika muda wa mwongo mmoja zachapwa na magazeti kama 2,000
1909 Makao makuu ya Sosaiti yahamishiwa Brooklyn, New York, katika Aprili
1914 Wonyesho wa kwanza wa “Photo-Drama of Creation,” katika New York, katika Januari; kabla ya mwisho wa vita, inaonwa na watazamaji wanaojumlika kuwa zaidi ya 9,000,000 katika Amerika Kaskazini, Ulaya, na Australia
Oktoba 2, katika chumba cha kulia cha Betheli katika Brooklyn, C. T. Russell athibitisha, “Nyakati za Mataifa zimekwisha”
Wanafunzi wa Biblia ni watendaji wakihubiri katika nchi 43; walioshiriki kutolea wengine ushahidi ni 5,155; hudhurio la Ukumbusho lililoripotiwa ni 18,243
1916 Kifo cha C. T. Russell akiwa na umri wa miaka 64, Oktoba 31, akisafiri kwa gari-moshi kupitia Texas
1917 J. F. Rutherford awa msimamizi wa Sosaiti mnamo Januari 6, baada ya halmashauri ya utekelezi ya watu watatu kusimamia shughuli za Sosaiti kwa karibu miezi miwili
Kitabu The Finished Mystery chatolewa kwa familia ya Betheli katika Brooklyn Julai 17; wanne waliokuwa wametumikia katika baraza la waelekezi la Sosaiti wakipinga kwa dhati; baada ya hayo makutaniko mengi yagawanyika
1918 Hotuba “Ulimwengu Umekwisha—Mamilioni Wanaoishi Sasa Huenda Wasife Kamwe” inatolewa kwa mara ya kwanza, Februari 24, katika Los Angeles, California. Machi 31, katika Boston, Massachusetts, hotuba hiyo ina kichwa “Ulimwengu Umekwisha—Mamilioni Wanaoishi Sasa Hawatakufa Kamwe”
J. F. Rutherford na washiriki wa karibu wanatajwa katika waranti za kukamatwa za jimbo zilizotolewa Mei 7; kusikizwa kwa kesi kwaanza mnamo Juni 5; wao wahukumiwa kifungo kirefu katika gereza la jimbo mnamo Juni 21 (mmoja wao Julai 10)
Makao makuu ya Brooklyn yafungwa katika Agosti, na shughuli zayo zahamishiwa Pittsburgh tena kwa zaidi ya mwaka
1919 Maofisa wa Sosaiti na washiriki wao waachiliwa kwa dhamana, Machi 26; Mei 14 rufani za mahakamani zabadilisha uamuzi wa mahakama ya chini, na kusikizwa upya kwa kesi kwaagizwa; mwaka unaofuata, Mei 5, serikali yajiondoa kwenye kesi, ikikataa kushtaki
Akifanya jaribio kuona ikiwa kazi ya Wanafunzi wa Biblia yaweza kuhuishwa, J. F. Rutherford apanga kutoa mhadhara wa watu wote “Tumaini kwa Ajili ya Wanadamu Wenye Taabu,” kwenye Clune’s Auditorium, jijini Los Angeles, California, Mei 4; umati wote hauwezi kutoshea, na hotuba inawajibika kutolewa mara ya pili
Wanafunzi wa Biblia wafanya mkusanyiko kwenye Cedar Point, Ohio, Septemba 1-8; kichapo kinachokuja cha gazeti The Golden Age (sasa chaitwa Amkeni!) chatangazwa
Bulletin (sasa yaitwa Huduma ya Ufalme Yetu) yatangazwa ikiwa kichochezi cha utumishi wa shambani
Ripoti ya mwaka yaonyesha Wanafunzi wa Biblia 5,793 wakihubiri kwa bidii katika nchi 43; hudhurio la Ukumbusho lililoripotiwa, 21,411
1920 Watch Tower Society yaanza shughuli zayo yenyewe za uchapaji, katika Brooklyn
1922 Redio yatumiwa kwa mara ya kwanza na J. F. Rutherford, Februari 26, katika California, ili kutangaza mhadhara wa Biblia
Mkusanyiko wa Wanafunzi wa Biblia katika Cedar Point, Ohio, Septemba 5-13; mwito watolewa “Mtangazeni, mtangazeni, mtangazeni, Mfalme na ufalme wake”
Makasisi katika Ujerumani wachochea polisi wawakamate Wanafunzi wa Biblia wakati hao wanaposhiriki katika kugawanya fasihi za Biblia kwa umma
1924 WBBR (stesheni ya kwanza ya redio iliyo mali ya Watch Tower Society) yaanza kutangaza Februari 24
1925 Watch Tower la Machi 1, katika kuzungumzia kuzaliwa kwa Ufalme wa Mungu katika 1914, laonyesha kwamba kuna matengenezo mawili tofauti yenye kupingana—la Yehova na la Shetani
1926 Kuhubiri nyumba hadi nyumba na vitabu siku ya Jumapili kunatiwa moyo
1928 Wanafunzi wa Biblia wakamatwa katika New Jersey (Marekani) kwa sababu ya kugawanya fasihi ikiwa sehemu ya kuhubiri nyumba hadi nyumba; katika muda wa mwongo mmoja, kuna visa zaidi ya 500 vya kukamatwa kila mwaka katika Marekani
1931 Jina Mashahidi wa Yehova laanza kutumiwa baada ya azimio kwenye mkusanyiko katika Columbus, Ohio, Julai 26, na baada ya hapo kwenye mikusanyiko duniani pote
1932 Vindication, Kitabu cha 2, chaeleza ni kwa nini unabii wa kurudishwa wa Kibiblia hautumiki kwa Wayahudi wa asili bali kwa Israeli wa kiroho
Mpango wa “wazee waliochaguliwa” unakomeshwa, kupatana na maelezo katika matoleo ya Watch Tower ya Agosti 15 na Septemba 1
1933 Mashahidi wa Yehova wapigwa marufuku katika Ujerumani. Wakati wa mnyanyaso mkali kufikia mwisho wa Vita ya Ulimwengu 2, watu 6,262 wakamatwa, na jumla ya miaka ya kifungo chao ikawa 14,332; watu 2,074 wapelekwa kwenye kambi za mateso, ambamo vifungo vyao vyajumlika kuwa miaka 8,332
Mashine za kutangazia (nyingine zikiwekwa juu ya magari) zatumiwa na Mashahidi kutangaza mihadhara ya Biblia katika sehemu za umma
1934 Vinanda vinavyobebeka vinatumiwa na Mashahidi ili kutolea wale wanaopendezwa hotuba fupi za Biblia
1935 Katika hotuba ya mkusanyiko katika Washington, D.C., Mei 31, “halaiki kubwa” yatambulishwa kuwa jamii ya kidunia; watu 840 wabatizwa kwenye mkusanyiko huo; mkazo mkubwa zaidi waendelea kutolewa kwa tumaini la uhai wa milele katika dunia-paradiso kwa ajili ya watumishi wa Mungu waaminifu wanaoishi sasa
Mahali pa kukutana paitwa Jumba la Ufalme kwa mara ya kwanza katika Honolulu, Hawaii
1936 Mabango ya matangazo yavaliwa kwa mara ya kwanza na wahubiri wa Ufalme ili kujulisha umma juu ya mihadhara ya Biblia
Kitia-moyo chatolewa kuanzisha mafunzo na watu wanaopendezwa, kwa kutumia kitabu cha Sosaiti Riches pamoja na Biblia; mara nyingi hayo ni mafunzo ya kikundi
1937 Vinanda vinavyobebeka vinatumiwa na Mashahidi kwenye milango ya nyumba ili kutoa hotuba za Biblia zilizorekodiwa
1938 Mipango ya kitheokrasi ya kuchagua waangalizi katika makutaniko inachukua mahali pa utaratibu wa kidemokrasia, kwa kupatana na matoleo ya Mnara wa Mlinzi (Kiingereza) ya Juni 1 na 15
Makusanyiko ya kanda ya dunia (sasa yaitwa makusanyiko ya mzunguko) yapangwa kwa ajili ya vikundi vya makutaniko
1939-45 Kotekote katika Milki ya Uingereza na Jumuiya ya Madola ya Uingereza, mataifa 23 yapiga marufuku Mashahidi wa Yehova au yakawekea vizuizi fasihi zao za Biblia
1940 Kugawanywa barabarani kwa Mnara wa Mlinzi na Consolation kwawa jambo la kawaida la utendaji wa Mashahidi wa Yehova
Uamuzi wa Mahakama Kuu ya Marekani, Juni 3, ukiunga mkono sharti la kusalimu bendera bila kujali imani ya kidini waanzisha jeuri ya magenge ya taifa lote dhidi ya Mashahidi wa Yehova
1941 Mashahidi watendaji wapita alama ya 100,000, wakifikia kilele cha 109,371 katika nchi 107, kujapokuwa uhakika wa kwamba Vita ya Ulimwengu 2 imekumba Ulaya na inaenea barani Afrika na Asia
1942 J. F. Rutherford afa Januari 8, jijini San Diego, California
N. H. Knorr awa msimamizi wa tatu wa Sosaiti Januari 13
Jumla ya chapa ya Mnara wa Mlinzi kwa mwaka huu ni 11,325,143 katika lugha zote
Mtaala wa Hali ya Juu wa Huduma ya Kitheokrasi waanzishwa kwa ajili ya wafanyakazi wa makao makuu ya Sosaiti, Februari 16
Watch Tower Society yachapa Biblia kamili, King James Version, kwenye matbaa yayo yenyewe (rotari ya web)
1943 Darasa la kwanza la Shule ya Biblia ya Gileadi ya Watchtower laanza mafunzo yalo Februari 1
Mtaala katika Huduma ya Kitheokrasi (sasa waitwa Shule ya Huduma ya Kitheokrasi) kwa makutaniko ya Mashahidi wa Yehova waanzishwa kwenye makusanyiko katika Aprili
Mahakama Kuu ya Marekani yatoa maamuzi yanayopendeleka kwa Mashahidi wa Yehova katika kesi 20 kati ya 24; Mahakama Kuu katika Australia yaondoa marufuku juu ya Mashahidi huko, Juni 14
1945 Kuanzia Oktoba 1, baraza la waelekezi la Sosaiti halichaguliwi tena na wachaguzi wanaostahili kuchagua kwa sababu ya upaji wa kifedha
Wastani wa idadi ya mafunzo ya Biblia nyumbani bila malipo yanayoongozwa kila mwezi sasa ni 104,814
1946 Wakati wa miaka saba iliyotangulia, Mashahidi wa Yehova zaidi ya 4,000 katika Marekani na 1,593 katika Uingereza wakamatwa na kuhukumiwa vifungo gerezani kuanzia mwezi mmoja hadi miaka mitano kwa sababu ya kutokuwamo kwao kwa Kikristo
Katika mwaka huu wa kwanza baada ya Vita ya Ulimwengu 2, watu 6,504 washiriki katika utumishi wa wakati wote wakiwa mapainia
Gazeti Amkeni! (mwandamizi wa The Golden Age na Consolation) laanza kutangazwa; jumla ya chapa ni nakala 13,934,429 kwa mwaka huu
Mashahidi zaidi ya 470 wapelekwa mbele ya mahakama katika Ugiriki kwa sababu ya kushiriki mafundisho ya Biblia na wengine
1947 Katika Quebec, Kanada, kesi 1,700 zinazohusu kazi ya kueneza evanjeli ya Mashahidi wa Yehova zangoja kusikizwa mahakamani
Hesabu ya makutaniko sasa yapita 10,000, ikifikia jumla ya 10,782 ulimwenguni pote
1950 Biblia New World Translation of the Christian Greek Scriptures yatolewa katika Kiingereza, Agosti 2, kwenye mkusanyiko katika New York
1953 Programu ya mazoezi yenye mambo mengi ya Mashahidi wa Yehova katika kuhubiri nyumba hadi nyumba yaanza, Septemba 1
1957 Katika nchi 169, muda wa saa 100,135,016 watumiwa na Mashahidi wa Yehova katika kupiga mbiu juu ya Ufalme wa Mungu na kuongoza mafunzo ya Biblia na watu waliopendezwa karibuni
1958 Mapenzi ya Kimungu Kusanyiko la Kimataifa, katika New York, lavutia hudhurio la 253,922 kutoka nchi 123; watu 7,136 wabatizwa
1959 Vipindi vya kwanza vya Shule ya Huduma ya Ufalme, vikianza Machi 9, katika South Lansing, New York, vikikusudiwa waangalizi wa kutaniko na waangalizi wasafirio
1961 Kikundi cha kwanza cha waangalizi wa tawi wa Sosaiti chahudhuria mtaala wa mazoezi ya pekee wa miezi kumi katika Brooklyn, New York, kwa kusudi la kuendeleza umoja wa kazi ya Mashahidi wa Yehova ulimwenguni pote
Biblia kamili katika buku moja, New World Translation of the Holy Scriptures, yatolewa katika Kiingereza
1963 New World Translation of the Christian Greek Scriptures yatolewa katika lugha sita zaidi (Kiholanzi, Kifaransa, Kijerumani, Kiitalia, Kireno, na Kihispania), nyingine nyingi zikifuata miaka ya baadaye
Mashahidi wa Yehova zaidi ya milioni moja ni watendaji sasa katika nchi 198; kilele cha wahubiri kwa mwaka huu ni 1,040,836; watu 62,798 zaidi wabatizwa
1965 Jumba la Kusanyiko la kwanza, lililokuwa jumba la michezo na likarekebishwa, latumiwa na Mashahidi wa Yehova katika New York
1967 Mnyanyaso wa kinyama na wa muda mrefu wa Mashahidi wa Yehova waanza kotekote Malawi na kuendelea kwa miaka mingi baadaye
1969 Mafunzo ya Biblia nyumbani yapita milioni moja; ripoti yaonyesha wastani wa 1,097,237
1971 Baraza Linaloongoza lapanuliwa; Oktoba 1, uenyekiti waanza kuzunguka kwa zamu miongoni mwa washiriki walo kila mwaka
1972 Makutaniko ya Mashahidi wa Yehova yaanza kusimamiwa na baraza la wazee, badala ya mtu mmoja, kuanzia Oktoba 1
1974 Kilele cha wahubiri ulimwenguni pote chafika 2,021,432; mapainia waongezeka kutoka 94,604, katika 1973, hadi 127,135
1975 Baraza Linaloongoza lapangwa tena kitengenezo; mnamo Desemba 4, daraka la kazi nyingi lapewa kwa halmashauri sita, zinazoanza kufanya kazi Januari 1, 1976
1976 Kuanzia Februari 1, kila ofisi ya tawi ya Watch Tower Society yaanza kusimamiwa na halmashauri ya watu watatu au zaidi walio wakomavu kiroho, badala ya mwangalizi mmoja
1977 Shule ya Utumishi wa Painia yaanza kuandaa mazoezi hususa kwa makumi ya maelfu ya mapainia ulimwenguni pote
1984 Mafunzo ya Biblia nyumbani yanayoongozwa na Mashahidi wa Yehova sasa ni wastani wa 2,047,113
1985 Mpango wa wenye kujitolea wa kimataifa waanzishwa, ukiratibu kazi ya ujenzi ya Sosaiti ya ulimwenguni pote kutoka kwa makao makuu
Ripoti yaonyesha 3,024,131 wakishiriki katika kazi ya kuhubiri Ufalme katika nchi 222; wastani wa mapania sasa ni 322,821; watu 189,800 wabatizwa mwaka huu
1986 Halmashauri za Ujenzi za Kimkoa zawekwa kusaidia kuratibu ujenzi wa Majumba ya Ufalme
1987 Kazi ya kufanya wanafunzi yaendelea kupanuka, huku mafunzo ya Biblia yakiongozwa sasa na watu mmoja-mmoja na vikundi vya familia 3,005,048, mengi yayo kila juma; jumla ya waliobatizwa mwaka huu ni 230,843
Shule ya Mazoezi ya Kihuduma yaanza kutenda mnamo Oktoba 1, darasa la kwanza likiwa Coraopolis, Pennsylvania
1989 Hali zinazobadilika katika Ulaya Mashariki zasaidia kufanya mikusanyiko mitatu mikubwa ya kimataifa iwezekane katika Poland, na kisha katika nchi nyinginezo katika miaka iliyofuata
1990 Kuondolewa kwa vizuizi juu ya Mashahidi wa Yehova katika nchi za Afrika na Ulaya Mashariki kwawezesha kuenezwa kwa evanjeli miongoni mwa watu 100,000,000 zaidi
Wahubiri wa Ufalme wafikia kilele kipya cha 4,017,213; idadi ya mapainia yapanda kufikia 536,508; jumla ya muda wa saa 895,229,424 zatumiwa kwa kazi ya maana ya kupiga mbiu ya Ufalme
1991 Marufuku zilizoondolewa katika Ulaya Mashariki na Afrika zafanya iwe rahisi kufikia watu 390,000,000 zaidi na habari njema za Ufalme wa Mungu
1992 Mnara wa Mlinzi lina wastani wa chapa 15,570,000 katika lugha 111; Kwa wastani, nakala 13,110,000 za Amkeni! zatokezwa, katika lugha 67
Ushahidi mkubwa zaidi uliopata kutolewa, huku 4,472,787 wakishiriki kupiga mbiu ya Ufalme katika nchi 229; wastani wa kila mwezi wa mapania ukiwa 605,610; muda wa saa 1,024,910,434 watumiwa kutoa ushahidi hadharani; mafunzo ya Biblia 4,278,127 yaongozwa; wanafunzi wapya 301,002 wabatizwa