Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • jv kur. 724-725
  • Amkeni!—Gazeti Linalovutia Sana Umma

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Amkeni!—Gazeti Linalovutia Sana Umma
  • Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
  • Habari Zinazolingana
  • Biblia Itakaziwa Zaidi
    Huduma ya Ufalme—2005
  • Kwa Wasomaji Wetu
    Amkeni!—2006
  • Mnara wa Mlinzi na Amkeni!—Majarida ya Wakati Ufaao Yenye Kweli
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • Kutangaza Mnara wa Mlinzi
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
Pata Habari Zaidi
Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
jv kur. 724-725

Amkeni!—Gazeti Linalovutia Sana Umma

Hapo awali gazeti hilo lilikuwa na kichwa The Golden Age. Toleo la kwanza lilikuwa la Oktoba 1, 1919. Gazeti hilo liliripoti juu ya nyanja nyingi za jitihada za binadamu. Liliwafahamisha watu juu ya yale yaliyokuwa yakiendelea ulimwenguni na likawaonyesha kwamba suluhisho halisi kwa matatizo ya wanadamu ni Utawala wa Mileani wa Kristo, ambao kwa kweli utaleta “muhula bora ajabu” kwa wanadamu. Muundo wa jalada la gazeti hilo ulipata mabadiliko, lakini ujumbe ulibaki uleule. The Golden Age lilibuniwa ili ligawanywe kwa umma, na kwa miaka mingi hesabu ya nakala zilizotokezwa ilikuwa kubwa kuliko ile ya The Watch Tower.

Kuanzia toleo la Oktoba 6, 1937, kichwa kilibadilishwa kuwa Consolation. Hicho kilifaa sana kwa sababu ya uonevu ambao wengi walikuwa wakipata na msukosuko ambao ulimwengu ulijitia ndani yao katika Vita ya Ulimwengu 2. Hata hivyo, kitulizo ambacho gazeti hilo lilitoa, kilikuwa cha aina ile inayovutia wale tu walio na upendo halisi wa ile kweli.

Kuanzia toleo la Agosti 22, 1946, kichwa Amkeni! kilianza kutumiwa. Mkazo uliwekwa juu ya kuwaamsha watu waone umaana wa matukio ya ulimwengu. Gazeti hili lilitumia vyanzo vya habari vilivyo mashuhuri, lakini pia lilikuwa na waleta habari walo lenyewe duniani pote. Makala za Amkeni! zilizo na usawaziko, zinazotumika na za kina kirefu ambazo huzungumzia habari nyingi mbalimbali hutia moyo wasomaji wafikiri juu ya ujumbe wa maana zaidi wa gazeti hili, yaani, kwamba matukio ya ulimwengu hutimiza unabii wa Biblia, unaoonyesha kwamba tunaishi katika siku za mwisho na kwamba karibuni Ufalme wa Mungu utaleta manufaa za milele kwa wale wanaojifunza na kufanya mapenzi ya Mungu. Gazeti hili limekuwa chombo chenye matokeo katika kupiga mbiu juu ya habari njema za Ufalme wa Mungu duniani pote na limekuwa daraja kwa funzo la habari ya kina kirefu inayopatikana katika Mnara wa Mlinzi na vitabu vilivyojalidiwa.

Kufikia mapema 1993, Amkeni! lilikuwa likichapwa katika lugha 67, nakala 13,240,000 kwa kila toleo.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki