Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • rq somo la 14 kur. 28-29
  • Jinsi Ambavyo Mashahidi wa Yehova Wamefanywa Kuwa Tengenezo

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Jinsi Ambavyo Mashahidi wa Yehova Wamefanywa Kuwa Tengenezo
  • Mungu Anataka Tufanye Nini?
  • Habari Zinazolingana
  • Kundi la Kikristo na Utendaji Wake
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
  • Kwa Nini Mungu Ana Kikundi au Tengenezo la Watu Wanaomwabudu?
    Habari Njema Kutoka kwa Mungu!
  • Mikutano Kwa Ajili ya Ibada, Funzo, na Kitia-moyo
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
  • Kwa Nini Mungu Amewapanga Watu Wake kwa Utaratibu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
Pata Habari Zaidi
Mungu Anataka Tufanye Nini?
rq somo la 14 kur. 28-29

Somo la 14

Jinsi Ambavyo Mashahidi wa Yehova Wamefanywa Kuwa Tengenezo

Mashahidi wa Yehova walikuwa na mwanzo wao wa siku ya kisasa wakati gani? (1)

Mikutano ya Mashahidi wa Yehova huongozwaje? (2)

Gharama zinashughulikiwaje? (3)

Ni nani huongoza katika kila kutaniko? (4)

Ni mikutano ipi mikubwa zaidi hufanywa kila mwaka? (5)

Ni kazi gani inafanywa kwenye makao yao makuu na kwenye ofisi za tawi? (6)

1. Mashahidi wa Yehova walikuwa na mwanzo wao wa siku ya kisasa katika miaka ya 1870. Mwanzoni, wao waliitwa Wanafunzi wa Biblia. Lakini katika 1931 walikubali kirasmi na kutumia jina la Kimaandiko Mashahidi wa Yehova. (Isaya 43:10) Kutoka mianzo midogo tengenezo limekua hadi kufikia mamilioni ya Mashahidi, walio na shughuli ya kuhubiri katika chini zaidi ya 230.

2. Makutaniko yaliyo mengi ya Mashahidi wa Yehova yana mikutano mara tatu kila juma. Unaalikwa kuhudhuria wowote kati yayo. (Waebrania 10:24, 25) Biblia ndiyo msingi wa yale yanayofundishwa. Mikutano hufunguliwa na hufungwa kwa sala. “Nyimbo za kiroho” zenye kuhisiwa moyoni huimbwa pia kwenye mikutano iliyo mingi. (Waefeso 5:18, 19, New World Translation) Kuingia ni bure, na hakuna sadaka zinazokusanywa.—Mathayo 10:8.

3. Makutaniko yaliyo mengi hufanya mikutano katika Jumba la Ufalme. Hayo ni majengo sahili yanayojengwa na wajitoleaji walio Mashahidi. Wewe hutaona sanamu, visalaba, au vitu kama hivyo kwenye Jumba la Ufalme. Gharama zinalipwa kutokana na utoaji wa hiari. Kwa wale watakao kufanya utoaji, kuna sanduku la michango.—2 Wakorintho 9:7.

4. Katika kila kutaniko, kuna wazee, au waangalizi. Wao huongoza katika kufundisha kutanikoni. (1 Timotheo 3:1-7; 5:17) Wanasaidiwa na watumishi wa huduma. (1 Timotheo 3:8-10, 12, 13) Wanaume hao hawakwezwi juu ya wengine kutanikoni. (2 Wakorintho 1:24) Wao hawapewi majina ya pekee ya cheo. (Mathayo 23:8-10) Hawavalii tofauti na wengine. Wala hawalipwi mshahara kwa kazi yao. Wazee hutunza kwa hiari mahitaji ya kiroho ya kutaniko. Wanaweza kuandaa faraja na mwongozo katika nyakati za taabu.—Yakobo 5:14-16; 1 Petro 5:2, 3.

5. Mashahidi wa Yehova hufanya pia makusanyiko au mikusanyiko mikubwa kila mwaka. Kwenye nyakati hizo makutaniko mengi hukusanyika kwa ajili ya programu ya pekee ya mafunzo ya Biblia. Kubatizwa kwa wanafunzi wapya ni sehemu ya kawaida ya kila programu ya kusanyiko au mkusanyiko.—Mathayo 3:13-17; 28:19, 20.

6. Makao makuu ulimwenguni ya Mashahidi wa Yehova yamo katika New York. Lililoko huko ni Baraza Linaloongoza, kikundi kikuu cha wazee wenye uzoefu wanaosimamia kutaniko la ulimwenguni pote. Pia kuna ofisi za tawi zaidi ya 100 kotekote ulimwenguni. Penye mahali hapo wajitoleaji husaidia kuchapa na kusafirisha fasihi za Biblia. Mwelekezo hutolewa pia kwenye kule kupanga kazi ya kuhubiri. Kwa nini usipange kuzuru ofisi ya tawi iliyo karibu zaidi na wewe?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki