Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • rq somo la 15 uku. 30
  • Kusaidia Wengine Wafanye Mapenzi ya Mungu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kusaidia Wengine Wafanye Mapenzi ya Mungu
  • Mungu Anataka Tufanye Nini?
  • Habari Zinazolingana
  • Unawezaje Kuwahubiria Wengine Habari Njema?
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
  • Lo Lote Ufanyalo—Hubiri!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • Vijana Wenye Furaha Katika Utumishi wa Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Onyesha kwa Matendo Kwamba Wewe Ni Shahidi wa “Habari Njema”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
Pata Habari Zaidi
Mungu Anataka Tufanye Nini?
rq somo la 15 uku. 30

Somo la 15

Kusaidia Wengine Wafanye Mapenzi ya Mungu

Kwa nini uwaambie wengine kuhusu yale ambayo unajifunza? (1)

Unaweza kushiriki na nani habari njema? (2)

Mwenendo wako unaweza kuwa na tokeo gani juu ya wengine? (2)

Unaweza kuhubiri pamoja na kutaniko wakati gani? (3)

1. Kufikia sasa, umejifunza mambo mengi mema kutoka katika Biblia. Ujuzi huu wapaswa uongoze kwenye kusitawisha kwako utu wa Kikristo. (Waefeso 4:22-24) Ujuzi huo ni wa muhimu ili upate uhai wa milele. (Yohana 17:3) Hata hivyo, wengine pia wanahitaji kusikia habari njema ili wao pia waweze kuokolewa. Ni lazima Wakristo wote wa kweli watolee wengine ushahidi. Hiyo ni amri ya Mungu.—Warumi 10:10; 1 Wakorintho 9:16; 1 Timotheo 4:16.

2. Unaweza kuanza kwa kushiriki pamoja na wale walio karibu nawe yale mambo mema unayojifunza. Yasimulie kwa familia yako, marafiki wako, wanashule wenzako, na wafanyakazi wenzako. Uwe mwenye fadhili na mwenye subira unapofanya hivyo. (2 Timotheo 2:24, 25) Kumbuka kwamba mara nyingi watu hutazama mwenendo wa mtu zaidi kuliko kusikiliza yale anayosema. Kwa hiyo mwenendo wako mwema waweza kuvutia wengine wasikilize ujumbe unaowaambia.—Mathayo 5:16; 1 Petro 3:1, 2, 16.

3. Hatimaye, huenda ukastahili kuanza kuhubiri pamoja na kutaniko la Mashahidi wa Yehova la kwenu. Hiyo ni hatua ya maana katika maendeleo yako. (Mathayo 24:14) Ingekuwa shangwe iliyoje ikiwa ungeweza kusaidia mtu mwingineye kuwa mtumishi wa Yehova na kupata uhai wa milele!—1 Wathesalonike 2:19, 20.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki