Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ie kur. 3-4
  • Je! Kuna Uhai Baada ya Kifo?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Kuna Uhai Baada ya Kifo?
  • Ni Nini Hutupata Tunapokufa?
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Ulizo Moja Lenye Majibu Mengi
  • Jambo Linaloenea Pote
  • Uhai Baada ya Kifo—Watu Huamini Nini?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
  • Je, Kuna Uhai Baada ya Kifo?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
  • Je, Nafsi ni Isiyoweza Kufa?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
  • Je! Nafsi Huendelea Kuishi Baada ya Kifo?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
Pata Habari Zaidi
Ni Nini Hutupata Tunapokufa?
ie kur. 3-4

Je! Kuna Uhai Baada ya Kifo?

“Maana kuna matumaini ya muti; ya kuwa ukikatwa, utachipuka tena . . . Kama mutu akikufa, ataishi tena?”—MUSA, NABII WA ZAMANI.

1-3. Namna gani watu wengi hutafuta kitulizo wanapopoteza mpendwa katika kifo?

KATIKA jumba la kulinda maiti kwa ajili ya mazishi katika mji wa New York, marafiki na watu wa familia waandamana polepole karibu ya sanduku lenye kufunuliwa. Watazama kwa mshangao mwili wa kijana mwenye umri wa miaka 17. Marafiki zake wa shuleni wamtambua kwa shida. Utunzaji wa kutumia dawa za kemikali umemuondoa nywele zake; ugonjwa wa kansa umemfanya apoteze uzito wake. Je! huyu ndiye kweli waliyemjua kuwa rafiki yao? Miezi michache tu kabla ya hapo alikuwa mwenye kujaa mawazo, maulizo, nguvu—yaani uhai! Mama wa kijana mwenye kuvunjika moyo ajaribu kupata tumaini na kujituliza na wazo la kwamba kwa vyovyote mwana wake bado ni mwenye kuishi. Kwa machozi arudilia tena na tena yale amefundishwa: “Tommy ni mwenye furaha zaidi sasa. Mungu alipenda kuwa pamoja na Tommy mbinguni.”

2 Mbali kadiri ya kilomita 11,000, katika Jamnagar, India, wale wana watatu wa mfanyabiashara mwenye umri wa miaka 58 wasaidia kuulaza mwili wa baba yao juu ya chungu ya kuni ya kuchomea maiti. Wakati wenye kungaa wa jua la mchana-kati, mwana aliye mkubwa zaidi aanza kuunguza maiti kwa kuwasha moto magogo ya kuni na kuumwangia mwili wa baba yake usiokuwa na uhai mchanganyiko wenye kunukia vizuri wa marashi-vikolezo na uvumba. Mlio wenye kutatarika wa moto unapitwa na misemwa ya sala ya dini ya Kihindu yenye kurudiliwa ya Brahman inayomaanisha: “Acha nafsi hiyo isiyokufa kamwe iendelee katika nguvu yayo kuwa mwishowe jambo halisi.”

3 Ndugu hao watatu wanapoendelea kutazama kuunguzwa kwa mwili, kila mmoja kwa kimya hujiuliza, ‘Je! mimi naamini kuwako kwa uhai baada ya kifo?’ Wakiwa wameelimishwa kutoka sehemu mbalimbali za dunia, wanatoa majibu yenye kutofautiana. Aliye mdogo zaidi anajisikia kuwa hakika kwamba baba yao mpendwa atazaliwa upya katika mwili mwingine wa hali ya juu zaidi. Ndugu yake wa kati anaamini kwamba wafu ni wenye kulala, hawajui lolote. Aliye mkubwa wao ajaribu tu kukubali kifo kuwa jambo la kawaida, sababu yeye hufikiri kwamba hakuna mtu anayeweza kujua hakika jambo linalotufikia tunapokufa.

Ulizo Moja Lenye Majibu Mengi

4. Ni ulizo gani limekuwa likisumbua wanadamu kwa miaka mingi?

4 Je! kuna uhai baada ya kifo? Hilo ni ulizo ambalo limehangaisha wanadamu muda wa maelfu ya miaka. “Hata wanateolojia wanatatanishwa wanapopambana na ulizo hilo,” asema Hans Küng, msomi Mkatoliki. Miaka mingi imepita watu katika kila jamii wamekuwa wakifikiri sana juu ya jambo hilo, na majibu yanayotolewa ni mengi.

5-8. Dini nyingi hufundisha nini kuhusu uhai baada ya kifo?

5 Wakristo wengi wa jina tu wanaamini katika mbingu na helo. Kwa upande mwingine, Wahindu wanaamini kuzaliwa upya katika mwili mwingine. Akieleza kuhusu maoni ya Waislamu, Amir Muawiyah, msaidizi kwenye makao makuu ya dini ya Kislamu, asema: “Tunaamini kutakuwa siku ya hukumu kisha kufa, wakati uendapo mbele ya Mungu, Allah, ambayo itakuwa tu namna mambo yanavyoendeshwa kwenye korti [mahakama].” Kulingana na imani ya Kiislamu, ndipo Allah atakapokadiria mwendo wa maisha wa kila mmoja na kumpeleka kwenye paradiso au helo ya moto.

6 Katika Sri Lanka, Wabuddha na Wakatoliki huiacha milango na madirisha wazi kabisa wakati kifo kinapotokea katika jamaa yao. Taa yenye mafuta huashwa, na sanduku linalazwa hivi kwamba miguu ya mtu aliyekufa inaangalia kwenye mlango. Wanaamini kwamba kufanya hivyo kutawezesha roho au nafsi ya mtu aliyekufa kuondoka nyumbani kwa urahisi.

7 Ronald M. Berndt kutoka Chuo Kikuu cha Australia ya Magharibi asema kwamba Waborijeni wa Australia wanaamini kwamba “viumbe vya kibinadamu wanayo roho isiyoweza kuharibiwa.” Makabila mengine ya Kiafrika yanaamini kwamba kisha kufa watu wa kawaida hugeuka kuwa mizuka, wakati uohuo watu kabaila hugeuka roho za mababu, ambao wataheshimiwa na kutolewa maombi wakiwa viongozi wasiyoonekana wa jamii ya watu.

8 Katika inchi nyingine, zile imani kuhusiana na vinavyowaziwa kuwa nafsi za watu waliokufa ni mchanganyiko wa mapokeo ya kienyeji na Ukristo wa jina tu. Kwa mfano, katika Afrika ya mashariki, kati ya Wakatoliki na Waprotestanti wengi, ni jambo la kawaida kufunika kioo mtu anapokufa ili kwamba yeyote asije akatazama ndani na hivyo kuiona roho ya mtu aliyekufa. Ndipo, baada ya siku 40 tangu kufa kwa mpendwa, familia na marafiki husherehekea kupanda kwa nafsi mbinguni.

Jambo Linaloenea Pote

9, 10. Ni juu ya imani gani ya msingi dini mbalimbali hukubaliana?

9 Majibu kwa ulizo kuhusu jambo linalotufikia tunapokufa yanatolewa kwa kutofautiana kulingana na desturi pia imani za watu wanaoyatoa. Lakini, dini nyingi hukubaliana juu ya wazo moja la msingi: Kwamba kitu fulani ndani ya mtu—nafsi, roho, muzimu—ni kisichoweza kufa na hivyo huendelea kuishi baada ya kifo.

10 Imani ya kutoweza kufa kwa nafsi inaenea karibu pote katika maelfu ya dini na mifarakano ya Jumuiya ya Wakristo. Hilo ni fundisho la kawaida katika dini ya Kiyahudi pia. Katika dini ya Wahindu imani hii ndiyo msingi wenyewe wa fundisho la kuzaliwa upya katika mwili mwingine. Waislamu huamini kwamba nafsi huja kwenye uhai pamoja na mwili lakini huendelea kuishi mwili ufapo. Imani nyingine—fundisho la Afrika la kuwako kwa roho ziwezazo kutenganishwa na mwili, dini ya Shinto, na hata ya Buddha—hufundisha mambo tofauti juu ya jambo hili.

11. Wataalamu wengine wana maoni gani kuhusu wazo la kwamba nafsi ni isiyoweza kufa?

11 Wengine huchukua msimamo tofauti, kwamba uhai wenye ufahamu unamalizika mtu afapo. Kwao, jambo la kwamba uhai wenye hisia na akili huendelea katika kitu kisicho na utu, nafsi yenye kivuli inayoachana na mwili ni wazo lisilo la akili. Miguel de Unamuno, mwandikaji na pia msomi Mhispania wa karne ya 20 aandika: “Kuamini katika kutoweza kufa kwa nafsi ni kutaka kwamba ile nafsi iwe isiyokufa, lakini kutaka hilo kwa nguvu kama hiyo ya kuazimia kutamfanya mtu akose kufikiria sababu vizuri na kuwa hivyo mpumbavu.” Miongoni mwa wale waliokataa kuamini kutoweza kufa kwa nafsi wamo wanafalsafa wenye kujulikana sana wa kale Aristote na Epicure, mwanafizikia Hippocrates, mwanafalsafa Mskoti David Hume, Msomi Muarabu Averroës, na waziri-mkuu wa kwanza wa India baada ya uhuru, Jawaharlal Nehru.

12, 13. Ni maulizo gani ya lazima yanayotokea kuhusu fundisho la kutokufa kwa nafsi?

12 Ulizo ni, je! kweli tunayo nafsi isiyoweza kufa? Ikiwa hakika nafsi si isiyoweza kufa, basi fundisho kama hili la uongo lingewezaje kuwa sehemu ya maana zaidi ya dini nyingi leo? Chanzo cha wazo hili ni gani? Na ikiwa kweli nafsi yakoma kuwapo kisha kufa, kuna tumaini gani kwa wafu?

13 Je! tunaweza kupata majibu yenye ukweli na yenye kutosheleza kwa maulizo hayo? Ndiyo! Maulizo hayo na mengine yatajibiwa katika kurasa zinazofuata. Kwanza, acheni tuchunguze namna fundisho la kutokufa kwa nafsi lilivyoanza.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki