Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • jt kur. 25-26
  • Tengenezo Lao na Kazi Yao ya Ulimwenguni Pote

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Tengenezo Lao na Kazi Yao ya Ulimwenguni Pote
  • Mashahidi wa Yehova—Wao Ni Nani? Wanaamini Nini?
  • Habari Zinazolingana
  • Tengenezo na Kazi Yao ya Ulimwenguni Pote
    Mashahidi wa Yehova Katika Karne ya 20
  • Waangalizi Wanaochunga Kundi
    Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
  • Ni Kazi Gani Zinazofanywa Katika Ofisi ya Tawi?
    Ni Nani Wanaofanya Mapenzi ya Yehova Leo?
  • Jinsi Ambavyo Mashahidi wa Yehova Wamefanywa Kuwa Tengenezo
    Mungu Anataka Tufanye Nini?
Pata Habari Zaidi
Mashahidi wa Yehova—Wao Ni Nani? Wanaamini Nini?
jt kur. 25-26

Tengenezo Lao na Kazi Yao ya Ulimwenguni Pote

KUNA njia mbalimbali zinazotumiwa kuelekeza kazi ya kutoa ushahidi inayofanywa katika nchi zaidi ya 230. Mwelekezo wa jumla unatoka kwa Baraza Linaloongoza katika makao makuu Brooklyn, New York. Baraza Linaloongoza hutuma wajumbe kila mwaka kwenye maeneo mbalimbali ulimwenguni ili kushauriana na wawakilishi wa ofisi za tawi katika maeneo hayo. Katika ofisi hizo za tawi, kuna Halmashauri za Tawi zenye washiriki wapatao watatu hadi saba wanaosimamia kazi katika nchi zilizo chini yao. Baadhi ya ofisi hizo za tawi zina vifaa vya kuchapia, nyingine zinaendesha matbaa za rotary zenye mwendo wa kasi sana. Nchi au eneo linalotumikiwa na kila ofisi ya tawi hugawanywa kwa wilaya, wilaya nazo hugawanywa kwa mizunguko. Kila mzunguko una makutaniko 20 hivi. Mwangalizi wa wilaya hutembelea mizunguko ya wilaya yake kwa zamu. Makusanyiko mawili hufanywa kila mwaka kwa ajili ya kila mzunguko. Pia kuna mwangalizi wa mzunguko, naye kwa kawaida hutembelea kila kutaniko katika mzunguko wake mara mbili kwa mwaka, akisaidia Mashahidi wapange na kuifanya kazi ya kuhubiri katika eneo ambalo kutaniko hilo limegawiwa.

Kutaniko la kwenu na Jumba la Ufalme lake ndilo kituo cha kuwaambia watu habari njema katika jumuiya yenu. Sehemu zilizo chini ya kila kutaniko hugawanywa kwa maeneo madogo katika ramani. Hayo hugawiwa Mashahidi mmoja-mmoja ambao hujitahidi kutembelea kila nyumba na kusema na watu waliomo. Kila kutaniko, ambalo laweza kuwa na Mashahidi wachache hadi kufikia 200 hivi, lina wazee waliopewa mgawo wa kusimamia kazi mbalimbali. Kila mtangazaji mmoja-mmoja wa habari njema ni wa muhimu sana katika tengenezo la Mashahidi wa Yehova. Kila mmoja wa Mashahidi, awe anatumikia katika makao makuu ya ulimwengu, katika ofisi za tawi, au katika makutaniko, hufanya kazi hiyo ya shambani yeye binafsi kwa kuwaambia wengine juu ya Ufalme wa Mungu.

Mwishowe, ripoti za utendaji huo hufikia makao makuu ya ulimwengu, na Yearbook huandikwa na kuchapishwa kila mwaka. Vilevile, chati huchapishwa kila mwaka katika toleo la Januari 1 la Mnara wa Mlinzi. Vichapo hivyo viwili hutoa ripoti zenye kueleza habari nyingi juu ya mambo yanayotimizwa kila mwaka katika kutoa ushahidi kwa Yehova na Ufalme wake ulio mikononi mwa Kristo Yesu. Katika miaka ya hivi majuzi, Mashahidi na watu wenye kupendezwa wapatao 14,000,000 wamekuwa wakihudhuria Ukumbusho wa kifo cha Yesu kila mwaka. Mashahidi wa Yehova hutumia zaidi ya saa 1,000,000,000 kwa mwaka wakitangaza habari njema, na wapya zaidi ya 300,000 hubatizwa. Mamia ya mamilioni ya vitabu hugawanywa.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki