Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • be uku. 282-uku. 285
  • Miongozo ya Waangalizi wa Shule

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Miongozo ya Waangalizi wa Shule
  • Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
  • Habari Zinazolingana
  • Shule ya Huduma ya Kitheokrasi ya 2015 Itatusaidia Kuboresha Ufundishaji Wetu
    Huduma Yetu ya Ufalme—2014
  • Shule Inayotuzoeza Kufanya Kazi Muhimu Zaidi Maishani
    Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Maagizo ya Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo
    Maagizo ya Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo
  • Sanduku la Swali
    Huduma Yetu ya Ufalme—1991
Pata Habari Zaidi
Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
be uku. 282-uku. 285

Miongozo ya Waangalizi wa Shule

KATIKA kila kutaniko, kuna mzee ambaye amewekwa kuwa mwangalizi wa Shule ya Huduma ya Kitheokrasi. Kama una daraka hilo, shule inaweza kufaidi sana ikiwa una shauku na unapendezwa na maendeleo ya kila mwanafunzi.

Sehemu muhimu ya mgawo wako ni kuongoza Shule ya Huduma ya Kitheokrasi kila juma katika kutaniko lenu. Kumbuka kwamba mbali na wanafunzi ambao wana migawo siku yoyote ile, kuna wasikilizaji pia. Ongoza shule kwa njia ambayo kutaniko lote linapokea makumbusho mazuri yanayochochea na yanayohusiana na angalau mojawapo ya malengo ya shule hii ambayo yametajwa kwenye ukurasa wa 5 hadi 8 wa kitabu hiki.

Pendezwa na wanafunzi wote, iwe wana mgawo wa usomaji, kutoa maonyesho, au kutoa hotuba. Wasaidie waone kwamba kusudi si kutimiza mgawo tu bali kutumia nafasi hiyo kufanya maendeleo katika utumishi wao kwa Yehova. Bila shaka maendeleo yao yanategemea hasa jitihada zao katika shule. Lakini ni muhimu pia upendezwe nao kwa fadhili, uwasaidie kuelewa umuhimu wa mashauri ya shule, na kuwaeleza jinsi ya kutumia mashauri hayo. Ili ufaulu, sikiliza kila hotuba kwa makini ili uweze kuandaa mashauri yanayofaidi.

Hakikisha shule inaanza na kuisha kwa wakati. Weka mfano mzuri kwa kutunza wakati unapotoa mashauri. Hotuba ya wanafunzi ikipitisha wakati, wewe ama msaidizi wako mnaweza kumtolea ishara, na mwanafunzi anapaswa kumaliza sentensi yake na kuondoka jukwaani. Sehemu nyingine ya shule ikipitisha wakati, fupisha maelezo yako na baada ya mkutano uzungumze na ndugu aliyepitisha wakati.

Ikiwa umehudhuria mkutano, unapaswa kuongoza shule. Lakini endapo umekosa kuhudhuria mkutano, ndugu mwingine ambaye tayari alichaguliwa na baraza la wazee anapaswa kuongoza shule. Ukihitaji msaada wa kutayarisha ratiba, kuandika migawo na kuwapa wanafunzi, au kupanga watu wa kutoa hotuba za kujitolea, mtumishi wa huduma ambaye amepewa mgawo na baraza la wazee anaweza kukusaidia katika mambo hayo.

Kuandikisha Wanafunzi. Watie moyo wahubiri wote wajiandikishe katika shule. Wengine ambao hushirikiana vizuri na kutaniko wanaweza kujiandikisha ikiwa wanakubaliana na mafundisho ya Biblia na maisha yao yanapatana na kanuni za Kikristo. Mtu akiomba kujiandikisha katika shule, mpongeze sana. Ikiwa hajawa mhubiri, wewe mwangalizi wa shule zungumza naye matakwa ya kuandikishwa katika shule, ikiwezekana mwalimu wake wa Biblia akiwapo (au mzazi anayeamini akiwapo). Matakwa hayo ni kama yale ya mtu anayetaka kuwa mhubiri asiyebatizwa, na yanapatikana kwenye ukurasa wa 97 hadi 99 wa kitabu Tumefanywa Tengenezo Tutimize Huduma Yetu. Weka orodha kamili ya wote ambao wamejiandikisha katika shule.

Kutumia Fomu ya Mashauri. Fomu ya mashauri ya kila mwanafunzi iko katika kitabu chake mwenyewe cha shule kwenye ukurasa wa 79 hadi 81. Kama inavyoonyeshwa na rangi tofauti-tofauti, mwanafunzi anapokuwa na mgawo wa kusoma anaweza kupewa shauri lolote kuanzia shauri la 1 hadi 17. Wakati wa kutoa onyesho, wanafunzi wanaweza kutumia shauri lolote ila 7, 52, na 53. Mashauri yote yanaweza kutumiwa kwa hotuba ila 7, 18, na 30.

Mwanafunzi anapopewa mgawo wa kushughulikia shauri fulani, mwangalizi wa shule anapaswa kuandika kwa penseli (kalamu ya risasi) sehemu ambayo imeandikwa “Tarehe ya Kupokea Mgawo” katika nafasi iliyoko kando ya shauri hilo kwenye fomu ya shauri katika kitabu cha mwanafunzi. Baada ya mwanafunzi kushughulikia mgawo wake, mwulize kwa faragha kama alifanya yale mazoezi ambayo yako mwishoni mwa shauri hilo. Ikiwa ndivyo, tia alama sanduku lililo katika fomu hiyo. Kama unapendekeza aendelee kufanyia kazi shauri hilo, usiandike jambo lolote katika fomu yake ya shauri; usijaze ile nafasi ya “Tarehe Uliotimizwa.” Unapaswa kutia alama sehemu hiyo wakati tu mwanafunzi yu tayari kufanyia kazi shauri jingine. Kwa kuongezea, kwenye ukurasa wa 82 wa kitabu cha mwanafunzi, baada ya kila hotuba ya mwanafunzi, andika tarehe upande wa kushoto wa kikao ambacho mwanafunzi ametumia. Kuna nafasi katika fomu ya mashauri na kwenye orodha ya vikao ya kuruhusu kila kikao kitumiwe mara mbili. Wanafunzi wanapaswa kuja na vitabu vyao shuleni.

Toa mgawo wa shauri moja tu la usemi kwa wakati mmoja. Kwa kawaida ni vizuri kushughulikia mashauri kama yanavyofuatana kwenye orodha. Lakini wanafunzi wengine wakionyesha uwezo mkubwa, unaweza kuwatia moyo wajifunze na kutumia mashauri fulani peke yao. Kisha unaweza kuwasaidia kutimiza mashauri ambayo unaona yataboresha sana uwezo wao wakiwa wasemaji na walimu stadi.

Hata kama mwanafunzi amekuwa katika shule kwa miaka mingi, bado anaweza kufaidika sana akijifunza kila somo na kulitumia. Ili uwasaidie wanafunzi wenye mahitaji hususa, unaweza kuchagua sifa fulani za usemi ambazo wanaweza kufanyia kazi badala ya kufuata kila shauri kama lilivyoorodheshwa katika fomu ya shauri.

Kutoa Mashauri. Unapotoa mashauri, tumia vizuri mifano na kanuni za Biblia. Wanafunzi wanapaswa kutambua kwamba mashauri unayotoa na njia unayotumia kuyatoa zinaongozwa na kanuni bora za Neno la Mungu.

Kumbuka kwamba wewe ni ‘mfanyakazi mwenzi’ wa akina ndugu na dada. (2 Kor. 1:24) Hata wewe pia unahitaji kuendelea kutia bidii kuwa msemaji na mwalimu stadi. Jifunze kitabu Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi, tumia mashauri yake, na uweke mfano mzuri kwa wengine.

Fanya hivyo kwa lengo la kuwasaidia wanafunzi wawe wasomaji wazuri, wasemaji bora, na walimu stadi. Ili ufaulu, jitahidi kuwasaidia wanafunzi inapohitajika ili waelewe sifa mbalimbali za usemi, umuhimu wake, na jinsi ya kuzikuza. Kitabu hiki kimetayarishwa kwa njia ambayo itakusaidia kutimiza kusudi hilo. Unahitaji kufanya mengi zaidi mbali na kukisoma tu kitabu hiki. Fafanua mawazo ya kitabu hiki na kuonyesha jinsi ya kuyatumia.

Mwanafunzi akitimiza vizuri shauri, mpongeze. Taja kifupi kwa nini amefanya vizuri au kwa nini jambo alilofanya ni muhimu. Ikiwa inafaa ashughulikie shauri jingine, hakikisha anaelewa ni kwa nini anapaswa kushughulikia shauri hilo. Mweleze jinsi ya kutimiza sifa hiyo. Taja mambo kihususa, na uwe mwenye fadhili vilevile.

Tambua kwamba watu wengi hushindwa kutoa hotuba mbele ya watu. Mtu akihisi hakufanya vizuri, anaweza kukata tamaa. Mwige Yesu ambaye hakuponda “tete lililochubuliwa” wala hakuzima “utambi wa kitani-ghafi.” (Mt. 12:20) Fikiria hali ya kihisia-moyo ya mwanafunzi. Unapotoa mashauri, fikiria kama mwanafunzi ni mpya ama ni mhubiri wa zamani. Pongezi changamfu inayotoka moyoni inaweza kuwatia moyo watu wafanye kadiri wawezavyo.

Mheshimu kila mwanafunzi. Waroma 12:10 linatuambia: “Katika kuonyeshana heshima iweni wenye kuongoza.” Shauri hilo linamfaa sana mshauri wa Shule ya Huduma ya Kitheokrasi. Ikiwa mwanafunzi ana umri mkubwa kuliko wewe, tumia kwa uangalifu mwelekezo wa 1 Timotheo 5:1, 2. Hata mwanafunzi awe na umri gani, kwa kawaida atakubali rekebisho linalotolewa kwa fadhili.—Mit. 25:11.

Unapotoa mashauri, mkazie mwanafunzi kusudi la mazoezi hayo. Kusudi la shule si kufanya vizuri ili apongezwe na kupewa shauri jingine jipya. Lengo si kuwa msemaji na mwalimu anayevutia wengine. (Mit. 25:27) Tamaa yetu ni kutumia zawadi ya usemi kumsifu Yehova na kuwasaidia wengine wamjue na kumpenda. Lengo la mazoezi haya ni kutusaidia tufanye vizuri zaidi kazi inayotajwa katika Mathayo 24:14 na 28:19, 20. Ndugu ambao wamebatizwa na ambao baadaye wanastahili wanaweza kupewa migawo ya ‘kuchunga kundi la Mungu’ wakiwa wasemaji na walimu wanapohutubia watu.—1 Pet. 5:2, 3.

Watajie wanafunzi wasome shauri watakalofanyia kazi siku chache baada ya kupokea mgawo huo. Watie moyo watumie yale wanayojifunza wanapotayarisha migawo kwa ajili ya shule, katika mazungumzo ya kawaida, wanapotoa maelezo katika mikutano, na katika utumishi wa shambani.

Kutoa Migawo. Kwa kawaida unapaswa kutoa migawo angalau majuma matatu mapema. Andika migawo yote ikiwezekana.

Migawo inayohusu kufundisha kutaniko inafaa ishughulikiwe na wazee, hasa wale ambao wataitunza vizuri, na pia watumishi wa huduma ambao ni walimu stadi.

Fuata maagizo yaliyo katika ratiba ya shule unapoamua hotuba utakazowapa akina ndugu na zile utakazowapa akina dada. Ikiwa kuna ndugu wachache na dada wengi wanaotoa hotuba za wanafunzi, uwe mwangalifu ili uwape akina ndugu migawo ya kutosha ya kutoa hotuba ambazo hazihusu usomaji tu.

Fikiria hali za watu mmoja-mmoja unapowapa mgawo. Je, ni lazima umpe mgawo mzee au mtumishi wa huduma ikiwa siku hiyohiyo ana sehemu katika Mkutano wa Utumishi au ikiwa juma hilohilo ana hotuba ya watu wote kutanikoni? Je, ni lazima umpe mgawo dada siku ileile ambayo mmoja wa watoto wake wadogo, ambaye anaweza kuhitaji msaada wake, ana mgawo pia? Je, mgawo huo unafaa kijana mdogo au mwanafunzi wa Biblia ambaye hajabatizwa? Hakikisha mgawo huo unafaa shauri ambalo mwanafunzi huyo anafanyia kazi.

Kuhusu migawo ya akina dada, kwa kawaida mwanafunzi mwenyewe atachagua kikao anachotaka akifuata maagizo yaliyo kwenye ukurasa wa 78 na 82. Anapaswa kupewa msaidizi mmoja, lakini anaweza kutumia msaidizi mwingine zaidi. Mwanafunzi akiomba msaidizi fulani hususa ili hali ifaane kabisa na kikao anachotaka kutumia, anaweza kuruhusiwa.

Shule za Ziada. Ikiwa kuna zaidi ya wanafunzi 50 katika shule, mnaweza kutumia mahali pengine kwa ajili ya hotuba nyingine za wanafunzi. Ikitegemea hali zenu, shule ya ziada inaweza kuwa na hotuba zote za wanafunzi au hotuba mbili tu za mwisho.

Kila shule ya ziada inapaswa kuwa na mshauri anayestahili, ikiwezekana mzee. Ikiwa lazima, mtumishi wa huduma anayestahili vizuri anaweza kutumiwa. Baraza la wazee linapaswa kutoa idhini ya kutumia ndugu hao kuongoza shule. Mwangalizi wa shule anapaswa kushirikiana sana na ndugu hao ili aweze kufuatilia maendeleo ya wanafunzi hata ikiwa wanatoa hotuba katika shule nyingine.

Darasa la Pekee la Kusoma. Baraza la wazee likiamua kwamba kuna watu kadhaa kutanikoni wanaohitaji kufundishwa kujua kusoma lugha inayotumiwa kutanikoni, mnaweza kufanya mpango kwa kushirikiana na Shule ya Huduma ya Kitheokrasi. Mafundisho hayo yanaweza kuhusu kujua kusoma, au lengo lake linaweza kuwa kuboresha usomaji.

Si lazima madarasa hayo yapangwe wakati uleule wanafunzi wanapotoa hotuba katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi. Ili kuandaa msaada wa kutosha, huenda mkahitaji wakati mwingi zaidi kuliko wakati unaotumiwa kwenye shule. Wazee wanaweza kuamua mahitaji ya kwenu na wakati wa kuwa na darasa hilo. Ikitegemea hali, mipango inaweza kufanywa ili watu fulani wafundishwe wakiwa kikundi au wafundishwe wakiwa mmoja-mmoja.

Mnahitaji mwalimu anayestahili. Ikiwezekana mgawo huo upewe ndugu ambaye ni msomaji stadi na anayefahamu vizuri lugha. Ikiwa hakuna ndugu anayeweza kufanya kazi hiyo, wazee wanaweza kumwomba dada mwenye uwezo na mwenye mfano mzuri kusaidia. Avae kitambaa anapofundisha darasa hilo.—1 Kor. 11:3-10; 1 Tim. 2:11, 12.

Kitabu Jitahidi Kusoma na Kuandika kinapatikana katika lugha nyingi. Kimekusudiwa kumsaidia mtu kujua kusoma. Mnaweza kutumia vitabu vingine pia vya mafundisho, ikitegemea uwezo wa wanafunzi. Wanafunzi wanapofanya maendeleo mazuri, wanaweza kutiwa moyo kushiriki katika programu ya kawaida ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi.

Mwangalizi wa Shule ya Huduma ya Kitheokrasi anaweza kusaidia sana kutaniko. Tayarisha vizuri, na kulingana na shauri la Waroma 12:6-8, tunza mgawo wako kama amana yenye thamani kutoka kwa Mungu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki