Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • bm seh. ya 24 kur. 27-28
  • Paulo Ayaandikia Makutaniko

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Paulo Ayaandikia Makutaniko
  • Biblia—Ina Ujumbe Gani?
  • Habari Zinazolingana
  • Mashauri Kuhusu Imani, Mwenendo, na Upendo
    Biblia—Ina Ujumbe Gani?
  • Wewe Ni Mfuasi wa Mfano wa Kristo au Wewe Ni Mkristo wa Kujifanya Tu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
  • Timotheo—“Mtoto Halisi Katika Imani”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
  • Paulo Katika Roma
    Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
Pata Habari Zaidi
Biblia—Ina Ujumbe Gani?
bm seh. ya 24 kur. 27-28
Akiwa kifungoni, Paulo anataja mambo ya kuandikwa kwenye barua

Sehemu ya 24

Paulo Ayaandikia Makutaniko

Barua za Paulo zaliimarisha kutaniko la Kikristo

KUTANIKO changa la Kikristo lilikuwa na kazi kubwa mbele yake. Lingetimiza sehemu muhimu katika kusudi la Yehova. Hata hivyo, baada ya muda usio mrefu Wakristo hao wa karne ya kwanza walishambuliwa. Je, wangedumisha utimilifu wao kwa Mungu wajapokabili mateso na hali nyingine zenye kuhatarisha uaminifu wao kutoka nje na ndani ya kutaniko? Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo yana barua 21 zenye kutia moyo na zenye shauri lililohitajiwa.

Barua 14, Waroma mpaka Waebrania, ziliandikwa na mtume Paulo. Barua hizo zina majina ya wale walioandikiwa—iwe ni mtu binafsi au kutaniko fulani. Fikiria baadhi ya mambo ambayo Paulo anazungumzia katika barua zake.

Mashauri kuhusu maadili na mwenendo. Waasherati, wazinzi, na wanaotenda dhambi nyingine nzito “hawataurithi ufalme wa Mungu.” (Wagalatia 5:19-21; 1 Wakorintho 6:9-11) Waabudu wa Mungu kutoka mataifa yote wanapaswa kuwa na umoja. (Waroma 2:11; Waefeso 4:1-6) Wanapaswa kuwasaidia kwa hiari waamini wenzao walio na uhitaji. (2 Wakorintho 9:7) Paulo anasema: “Salini bila kuacha.” Kwa kweli, waabudu wanatiwa moyo kummiminia Yehova mioyo yao katika sala. (1 Wathesalonike 5:17; 2 Wathesalonike 3:1; Wafilipi 4:6, 7) Ili sala zinazotolewa zisikiwe na Mungu, lazima zitolewe kwa imani.—Waebrania 11:6.

Ni nini kinachoweza kusaidia familia ziwe na furaha? Waume wanapaswa kuwapenda wake zao kama miili yao wenyewe. Wake wanapaswa kuwaheshimu sana waume zao. Watoto wanapaswa kuwatii wazazi wao, kwa kuwa hilo linampendeza Mungu. Wazazi wanapaswa kuwaongoza na kuwafundisha watoto wao kwa upendo, wakitumia kanuni za Mungu.—Waefeso 5:22–6:4; Wakolosai 3:18-21.

Ramani inayoonyesha mahali ambapo Paulo aliandika barua zake

Wakristo wasaidiwa kuelewa kusudi la Mungu. Sheria ya Musa ilikusudiwa hasa kuwalinda na kuwaongoza Waisraeli mpaka wakati ambapo Kristo angefika. (Wagalatia 3:24) Hata hivyo, Wakristo hawahitaji kushika Sheria hiyo ili ibada yao kwa Mungu ikubaliwe. Alipokuwa akiwaandikia Waebrania, Wakristo waliokuwa na asili ya Kiyahudi, Paulo alieleza maana ya Sheria na jinsi kusudi la Mungu linavyotimizwa katika Kristo. Paulo alieleza kwamba sehemu mbalimbali za Sheria hiyo zilikuwa za kinabii. Kwa mfano, dhabihu ya Yesu ilikusudiwa kuleta msamaha wa dhambi, nayo iliwakilishwa na dhabihu za wanyama. (Waebrania 10:1-4) Kupitia kifo cha Yesu, Mungu alifuta agano la Sheria, kwa kuwa halikuwa na kazi tena.—Wakolosai 2:13-17; Waebrania 8:13.

Kutaniko la Kikristo la mapema likisikiliza wakati moja ya barua za Paulo ikisomwa

Maagizo kuhusu utaratibu wa kutaniko. Wanaume wanaotaka kufikia mapendeleo kutanikoni wanapaswa kuwa na mwenendo mzuri na kutimiza sifa za kiroho. (1 Timotheo 3:1-10, 12, 13; Tito 1:5-9) Waabudu wa Yehova Mungu wanapaswa kukusanyika kwa ukawaida pamoja na waamini wenzao ili kutiana moyo. (Waebrania 10:24, 25) Mikutano ya ibada inapaswa kuwa yenye kujenga na kuelimisha.—1 Wakorintho 14:26, 31.

Kufikia wakati ambapo alimwandikia Timotheo barua ya pili, Paulo alikuwa amerudi Roma; alikuwa gerezani akisubiri hukumu. Ni watu wachache tu waliojasiria kumtembelea. Paulo alijua kwamba ana wakati mfupi. Alisema: “Nimepigana pigano zuri, nimekimbia mwendo mpaka mwisho, nimeishika imani.” (2 Timotheo 4:7) Yaelekea kwamba muda mfupi baadaye, Paulo aliuawa kwa sababu ya imani yake. Hata hivyo, barua za mtume huyo zina mwongozo ambao waabudu wa kweli wa Mungu wanafuata mpaka leo.

—Inatoka kwenye Waroma; 1 Wakorintho; 2 Wakorintho; Wagalatia; Waefeso; Wafilipi; Wakolosai; 1 Wathesalonike; 2 Wathesalonike; 1 Timotheo; 2 Timotheo; Tito; Filemoni; Waebrania.

  • Barua za Paulo zina mashauri gani kuhusu maadili na mwenendo?

  • Ni habari gani ambazo Paulo alitoa kuhusu kutimizwa kwa kusudi la Mungu kupitia Kristo?

  • Paulo alitoa maagizo gani kuhusu utaratibu wa kutaniko?

NI NANI ALIYE UZAO ULIOAHIDIWA?

Baada ya Adamu na Hawa kutenda dhambi, Mungu alitumia lugha ya mfano alipomwambia nyoka: “Nitaweka uadui kati yako na yule mwanamke na kati ya uzao wako na uzao wake. Yeye atakuponda kichwa nawe utamtia jeraha kwenye kisigino.” (Mwanzo 3:15) Maandiko yanamtambulisha Ibilisi kuwa “nyoka wa zamani.” (Ufunuo 12:9) Mkombozi au Uzao ulioahidiwa na Mungu ulikuwa siri kwa karne nyingi, nao umekuwa ukifunuliwa hatua kwa hatua katika Biblia.

Miaka 2,000 hivi baada ya Adamu na Hawa kutenda dhambi, Yehova alisema kwamba Uzao ulioahidiwa ungekuja kupitia ukoo wa Abrahamu. (Mwanzo 22:17, 18) Karne nyingi baadaye, Paulo alifunua kwamba Masihi, Yesu Kristo, ndiye sehemu ya msingi ya Uzao huo. (Wagalatia 3:16) Kulingana na Mwanzo 3:15, Yesu alipouawa, ni kana kwamba alitiwa jeraha “kwenye kisigino.” Hata hivyo, Mungu alimfufua Yesu na ‘kumfanya hai katika roho.’—1 Petro 3:18.

Pia, Mungu alikusudia kwamba watu 144,000 wawe sehemu ya pili ya uzao huo. (Wagalatia 3:29; Ufunuo 14:1) Wanafufuliwa wakiwa na mwili wa roho na kuwa warithi pamoja na Kristo katika Ufalme wa mbinguni.—Waroma 8:16, 17.

Akiwa Mfalme mwenye nguvu mbinguni, karibuni Yesu atamwangamiza Ibilisi na uzao wake, wanadamu waovu na roho waovu wanaomfuata Shetani. (Yohana 8:44; Waefeso 6:12) Chini ya utawala wa Yesu, wanadamu wote watiifu wataishi kwa amani na furaha. Hata hivyo, hatimaye atamponda nyoka “kichwa,” na kumwangamiza kabisa asiwepo tena.—Waebrania 2:14.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki