Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • bm seh. ya 26 uku. 30
  • Paradiso Yarudishwa!

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Paradiso Yarudishwa!
  • Biblia—Ina Ujumbe Gani?
  • Habari Zinazolingana
  • Kitabu cha Biblia Namba 66—Ufunuo
    “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
  • Kutazama Ufunuo kwa Njia ya Uchunguzi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
  • Kitabu cha Ufunuo—Kinamaanisha Nini?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • “Taarifa za Mteremo” Kutoka Kwenye Apokalipsi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
Pata Habari Zaidi
Biblia—Ina Ujumbe Gani?
bm seh. ya 26 uku. 30
Yesu akiwa ameketi kwenye kiti chake cha Ufalme

Sehemu ya 26

Paradiso Yarudishwa!

Kupitia Ufalme wa Kristo, Yehova alitakasa jina Lake, atetea enzi Yake kuu, na kuondolea mbali uovu

KITABU cha mwisho cha Biblia, Ufunuo, kinawapa wanadamu wote tumaini. Kitabu hicho kilichoandikwa na mtume Yohana, kina maono mbalimbali ambayo upeo wake ni kutimizwa kwa kusudi la Yehova.

Katika maono ya kwanza, Yesu aliyefufuliwa anapongeza na kurekebisha makutaniko kadhaa. Katika maono yanayofuata tunaona kiti cha Ufalme cha Mungu, ambapo viumbe wa roho wanamsifu.

Huku kusudi la Mungu likizidi kutimizwa, Mwana-Kondoo, Yesu Kristo, apokea kitabu cha kukunjwa chenye mihuri saba. Anapofungua mihuri ya kwanza minne, wapanda-farasi wa mfano watokea. Mpanda-farasi wa kwanza ni Yesu akiwa juu ya farasi mweupe naye amevishwa taji la kifalme. Kisha wapanda-farasi juu ya farasi wenye rangi mbalimbali, wanaowakilisha vita, njaa, na tauni, mambo ambayo yanatendeka katika siku za mwisho za mfumo huu wa mambo. Muhuri wa saba unapofunguliwa, tarumbeta saba za mfano zinapulizwa zikiashiria kutangazwa kwa hukumu za Mungu. Kisha yafuata mapigo saba ya mfano, yanayowakilisha hasira ya Mungu.

Ufalme wa Mungu, unaofananishwa na mwana wa kiume aliyetoka kuzaliwa, wasimamishwa mbinguni. Vita vyatokea mbinguni, Shetani na malaika wake waovu watupwa duniani. Sauti kubwa inasema: “Ole wa dunia.” Ibilisi ana hasira kali, akijua ana kipindi kifupi cha wakati.—Ufunuo 12:12.

Yohana amwona mwana-kondoo, Yesu, pamoja na wale 144,000 ambao wamechaguliwa kati ya wanadamu, ‘watakaotawala wakiwa wafalme pamoja’ na Yesu. Hivyo, kitabu cha Ufunuo kinafunua kwamba sehemu ya pili ya ule uzao inafanyizwa na jumla ya watu 144,000.—Ufunuo 14:1; 20:6.

Watawala wa dunia wanakusanyika pamoja kwa ajili ya Har–Magedoni, “vita vya ile siku kuu ya Mungu Mweza-Yote.” Wanapigana vita na yule anayeketi juu ya farasi mweupe—Yesu, anayeyaongoza majeshi ya mbinguni. Watawala wote wa ulimwengu huu wanaharibiwa. Shetani anafungwa, naye Yesu na wale 144,000 wanatawala juu ya dunia kwa “miaka elfu.” Mwishoni mwa ile miaka elfu, Shetani aharibiwa.—Ufunuo 16:14; 20:4.

Utawala huo wa Kristo na watawala wenzake utawatimizia nini wanadamu watiifu? Yohana anaandika: “[Yehova] atafuta kila chozi kutoka katika macho yao, na kifo hakitakuwapo tena, wala maombolezo wala kilio wala maumivu hayatakuwapo tena. Mambo ya zamani yamepitilia mbali.” (Ufunuo 21:4) Kisha, dunia inakuwa paradiso!

Hivyo, kitabu cha Ufunuo kinakamilisha ujumbe wa Biblia. Ufalme wa Kimasihi, utalitakasa jina la Yehova na kuitetea enzi yake kuu milele!

—Inatoka kwenye Kitabu cha Ufunuo.

  • Wapanda-farasi wa mfano wanawakilisha nini?

  • Ni mambo gani ya ajabu yanayotokea huku kusudi la Mungu likizidi kutimizwa?

  • Har–Magedoni ni nini, nayo itafanya nini?

“BABILONI MKUBWA”

Katika kitabu cha Ufunuo, dini zote za uwongo— yaani, dini zinazompinga Mungu wa kweli—kwa ujumla zinatambulishwa kuwa “yule kahaba mkubwa.” Kahaba huyo anaitwa “Babiloni Mkubwa,” naye hufanya ukahaba na serikali za ulimwengu. Kitabu cha Ufunuo kinasema kwamba wakati uliowekwa na Yehova Mungu utakapofika, serikali hizo zitamshambulia kahaba huyo na kumharibu. —Ufunuo 17:1-5, 16, 17.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki