Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • jy sura 15 uku. 40-uku. 41 fu. 6
  • Afanya Muujiza Wake wa Kwanza

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Afanya Muujiza Wake wa Kwanza
  • Yesu—Njia, Kweli, na Uzima
  • Habari Zinazolingana
  • Muujiza Wa Kwanza wa Yesu
    Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi
  • Muujiza wa Kwanza wa Yesu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Muujiza wa Pili Huko Kana
    Yesu—Njia, Kweli, na Uzima
  • Muujiza wa Pili Anapokuwa Kana
    Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi
Pata Habari Zaidi
Yesu—Njia, Kweli, na Uzima
jy sura 15 uku. 40-uku. 41 fu. 6
Kwenye karamu ya harusi huko Kana, Yesu awaagiza wahudumu wajaze mitungi maji

SURA YA 15

Afanya Muujiza Wake wa Kwanza

YOHANA 2:1-12

  • HARUSI HUKO KANA

  • YESU ABADILI MAJI KUWA DIVAI

Siku tatu zimepita tangu Nathanaeli awe kati ya wanafunzi wa kwanza wa Yesu. Yesu na baadhi ya wanafunzi hao wa kwanza wanaelekea kaskazini kwenye wilaya ya Galilaya, eneo lao la nyumbani. Wanaenda katika mji wa Kana, mji alikozaliwa Nathanaeli. Mji wa Kana uko milimani, upande wa kaskazini wa Nazareti, ambako Yesu alilelewa. Wamealikwa kwenye karamu ya harusi huko Kana.

Mama ya Yesu amekuja pia kwenye harusi. Akiwa rafiki wa familia ya wale wanaofunga ndoa, inaonekana Maria anasaidia kuwahudumia wageni wengi waliopo. Basi anatambua haraka kwamba kuna upungufu, naye anamwambia Yesu: “Hawana divai.”—Yohana 2:3.

Ni wazi, Maria anadokeza kwamba Yesu afanye jambo fulani kuhusu upungufu huo wa divai. Akitumia msemo unaoonyesha kwamba anakataa, Yesu anamjibu: “Mwanamke, jambo hilo linatuhusuje mimi na wewe?” (Yohana 2:4) Akiwa Mfalme aliyechaguliwa na Mungu, matendo ya Yesu yanaongozwa na Baba yake wa mbinguni, bali si familia au marafiki. Kwa hekima Maria anaacha mambo mikononi mwa mwanawe, na anawaambia hivi wale wanaohudumu: “Fanyeni lolote atakalowaambia.”—Yohana 2:5.

Kuna mitungi sita ya maji, na kila mmoja una uwezo wa kubeba zaidi ya lita 40. Yesu anawaagiza wahudumu: “Ijazeni mitungi hiyo maji.” Kisha Yesu anawaambia: “Choteni kidogo na kumpelekea msimamizi wa karamu.”—Yohana 2:7, 8.

Msimamizi wa karamu anampongeza bwana harusi kwa sababu ya divai bora

Msimamizi anafurahishwa na ubora wa divai hiyo lakini hana habari kwamba imeandaliwa kimuujiza. Anamwita bwana harusi na kumwambia: “Kila mtu hutoa divai nzuri kwanza, kisha hutoa divai hafifu wakati ambapo watu wameingiwa na kileo. Lakini wewe umehifadhi divai nzuri mpaka sasa.”—Yohana 2:10.

Huu ndio muujiza wa kwanza ambao Yesu anafanya. Wanafunzi wake wapya wanapoona muujiza huo, imani yao inaimarishwa. Baadaye, Yesu, mama yake, na ndugu zake wa kambo wanasafiri hadi mji wa Kapernaumu ulio kwenye ufuo wa kaskazini magharibi wa Bahari ya Galilaya.

  • Ni wakati gani katika huduma ya Yesu ambapo harusi huko Kana inafanyika?

  • Yesu anaitikiaje dokezo la mama yake kuhusu divai?

  • Yesu anafanya muujiza gani, na muujiza huo una matokeo gani kwa wengine?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki