Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • jy sura 87 uku. 204-uku. 205 fu. 3
  • Panga Mapema​—Tumia Hekima Inayotumika

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Panga Mapema​—Tumia Hekima Inayotumika
  • Yesu—Njia, Kweli, na Uzima
  • Habari Zinazolingana
  • Andalia Wakati Ujao kwa Hekima Inayotumika
    Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi
  • Andalia Wakati Ujao kwa Hekima Inayotumika
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • “Kwa Kweli ni Nani Yule Msimamizi wa Nyumba Mwaminifu Mwenye Akili?”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
  • Je, Wajua?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2019
Pata Habari Zaidi
Yesu—Njia, Kweli, na Uzima
jy sura 87 uku. 204-uku. 205 fu. 3
Bwana aliye tajiri amfuta kazi msimamizi wake

SURA YA 87

Panga Mapema​—Tumia Hekima Inayotumika

LUKA 16:1-13

  • MFANO WA MSIMAMIZI ASIYE MWADILIFU

  • “JIFANYIENI MARAFIKI” KUPITIA UTAJIRI WENU

Mfano wa mwana aliyepotea ambao Yesu ametoka kusimulia, ulipaswa kuwafundisha wakusanya kodi, waandishi, na Mafarisayo kwamba Mungu yuko tayari kuwasamehe watenda dhambi wanaotubu. (Luka 15:1-7, 11) Sasa Yesu anazungumza na wanafunzi wake. Anasimulia mfano mwingine, kuhusu tajiri anayetambua kwamba msimamizi wa nyumba yake, hajatenda vizuri.

1. Msimamizi akipanga jambo atakalofanya; 2. Msimamizi akipunguza deni ambalo mtu fulani anadaiwa na bwana wake

Yesu anasimulia kwamba msimamizi huyo ameshtakiwa kuwa anatumia vibaya mali ya bwana wake. Basi bwana wake anasema kwamba msimamizi huyo atafutwa kazi. Yule msimamizi anajiuliza: “Nitafanya nini kwa kuwa bwana wangu ananiondoa kazini? Sina nguvu za kulima na ninaona aibu kuombaomba.” Ili kushughulika na hali itakayompata baadaye, anasema: “Najua nitakachofanya, ili nitakapoachishwa kazi, watu wanikaribishe nyumbani mwao.” Mara moja anawaita wale walio na madeni na kuwauliza: “Unadaiwa kiasi gani na bwana wangu?”—Luka 16:3-5.

Mtu wa kwanza anasema: “Vipimo 100 vya mafuta ya zeituni.” Yaani, karibu lita 2,200 za mafuta. Huenda mtu huyo aliyekopa alikuwa na shamba kubwa la mizeituni au alikuwa mfanyabiashara aliyeuza mafuta. Yule msimamizi anamwambia: “Chukua hati yako ya mapatano, uketi na upesi uandike 50 [lita 1,100].’—Luka 16:6.

Yule msimamizi anamuuliza mtu mwingine: “Na wewe, unadaiwa kiasi gani?” Anajibu: “Vipimo vikubwa 100 vya ngano.” Yaani, karibu tani 16. Msimamizi anamwambia mtu huyo: “Chukua hati yako ya mapatano uandike 80.” Basi anapunguza deni hilo kwa asilimia 20.—Luka 16:7.

Bado msimamizi huyo anasimamia hesabu za bwana wake, basi kwa njia fulani ana mamlaka ya kupunguza madeni ambayo bwana wake anawadai watu. Kwa kupunguza madeni wanayodaiwa, msimamizi huyo anajifanyia marafiki na watu wanaoweza kumwonyesha fadhili baada ya kufutwa kazi.

Baada ya muda, bwana wake anatambua jambo lililotokea. Ingawa jambo hilo linamletea hasara, anafurahishwa na msimamizi huyo na kumpongeza kwa sababu “ingawa hakuwa mwadilifu, alitenda kwa hekima inayotumika.” Yesu anaongezea hivi: “Wana wa mfumo huu wa mambo wana hekima zaidi katika kizazi chao kuliko walivyo wana wa nuru.”—Luka 16:8.

Yesu hakubaliani na njia ambayo yule msimamizi alitumia, wala haungi mkono kutumia udanganyifu katika biashara. Basi, anafundisha somo gani? Anawahimiza hivi wanafunzi: “Jifanyieni marafiki kupitia mali zisizo za uadilifu, ili zitakapokwisha wawapokee katika makao ya milele.” (Luka 16:9) Naam, hapa kuna somo kuhusu kupanga mapema na kutumia hekima inayotumika. Watumishi wa Mungu, yaani, “wana wa nuru,” wanapaswa kutumia mali zao za kimwili kwa njia ya hekima, wakifikiria kuhusu wakati ujao wa milele.

Yehova na Yesu ndio tu wanaoweza kumpokea mtu katika Ufalme wa mbinguni au Paradiso duniani chini ya Ufalme huo. Tunapaswa kujitahidi kusitawisha urafiki pamoja nao kwa kutumia mali zetu za kimwili kuunga mkono kazi ya Ufalme. Kwa njia hiyo, wakati wetu ujao wa milele utakuwa salama wakati dhahabu, fedha, na utajiri mwingine wa kimwili utakapokwisha au kuangamia.

Pia, Yesu anasema kwamba wale walio waaminifu katika kutunza na kutumia mali zozote au vitu vyao vya kimwili watakuwa waaminifu katika kutunza vitu muhimu zaidi. Basi, Yesu anasema: “Kwa hiyo, msipokuwa waaminifu kuhusu mali zisizo za uadilifu, ni nani atakayewakabidhi kilicho cha kweli [kama vile mali za Ufalme]?”—Luka 16:11.

Yesu anawaonyesha wanafunzi wake kwamba watadaiwa mengi ikiwa wanataka kupokelewa “katika makao ya milele.” Mtu hawezi kuwa mtumishi wa kweli wa Yehova na wakati uleule awe mtumwa wa utajiri wa kimwili usio wa uadilifu. Yesu anamalizia kwa kusema: “Hakuna mtumishi anayeweza kuwatumikia mabwana wawili, kwa maana atamchukia mmoja na kumpenda mwingine, au atashikamana na mmoja na kumdharau mwingine. Hamwezi kuwa watumwa wa Mungu na wa Utajiri.”—Luka 16:9, 13.

  • Katika mfano wa Yesu, yule msimamizi anajifanyiaje urafiki pamoja na wale wanaoweza kumsaidia baadaye?

  • “Mali zisizo za uadilifu” ni nini, na Wakristo wanawezaje ‘kujifanyia marafiki’ kupitia mali hizo?

  • Ni nani wanaoweza kutupokea katika “makao ya milele” ikiwa tutakuwa waaminifu katika kutumia “mali [zetu] zisizo za uadilifu”?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki