Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w19 Novemba uku. 31
  • Je, Wajua?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Wajua?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2019
  • Habari Zinazolingana
  • “Kwa Kweli ni Nani Yule Msimamizi wa Nyumba Mwaminifu Mwenye Akili?”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
  • Panga Mapema​—Tumia Hekima Inayotumika
    Yesu—Njia, Kweli, na Uzima
  • Wewe Ni Msimamizi-nyumba Mwenye Kutegemeka!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Uwe Tayari, Msimamizi Mwaminifu!
    Yesu—Njia, Kweli, na Uzima
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2019
w19 Novemba uku. 31
Msimamizi katika Misri ya kale akiwasimamia wafanyakazi

Je, Wajua?

Wasimamizi walikuwa na majukumu gani katika nyakati za Biblia?

KATIKA nyakati za Biblia, msimamizi alisimamia nyumba au mali ya mtu mwingine. Nyakati nyingine, neno la Kiebrania na Kigiriki linalotafsiriwa “msimamizi” linarejelea mwangalizi au msimamizi wa nyumba.

Yosefu, mwana wa mzee wa ukoo Yakobo, alipokuwa mtumwa nchini Misri, aliwekwa kuwa msimamizi wa nyumba ya bwana wake. Isitoshe, bwana wake Mmisri ‘alimwachia Yosefu usimamizi wa vitu vyake vyote.’ (Mwa. 39:2-6) Baadaye, Yosefu mwenyewe alipokuwa mtawala mwenye nguvu katika nchi ya Misri, aliweka msimamizi katika nyumba yake.—Mwa. 44:4.

Katika siku za Yesu, kwa kawaida watu waliomiliki ardhi waliishi katika majiji yaliyokuwa mbali na mashamba yao. Hivyo, wamiliki ardhi hao waliwateua wasimamizi ili kusimamia shughuli za kila siku za wafanyakazi waliotunza mashamba yao.

Msimamizi alipaswa kuwa na sifa gani? Columella, mwandishi Mroma wa karne ya kwanza alisema kwamba mtumwa aliyewekwa kuwa mwangalizi au msimamizi alipaswa kuwa mtu “mwenye uzoefu.” Alipaswa kuwa na “sifa za kiongozi asiye mvivu au mkatili.” Aliongeza hivi: “Hata hivyo alipaswa kuwa na sifa hii kuliko sifa zote—kwamba asifikirie kuwa anajua mambo fulani ilhali hayajui, na sikuzote awe na tamaa ya kujifunza zaidi.”

Neno la Mungu hutumia mfano wa msimamzi kufafanua baadhi ya utendaji unaofanywa katika kutaniko la Kikristo. Kwa mfano, mtume Petro anawatia moyo Wakristo watumie uwezo wao waliopewa na Mungu “kuhudumiana kama wasimamizi wazuri wa fadhili zisizostahiliwa za Mungu.”—1 Pet. 4:10.

Yesu mwenyewe alitumia mfano wa msimamizi katika simulizi lililo kwenye Luka 16:1-8. Zaidi ya hilo, katika unabii wake unaohusu ishara ya kuwapo kwake akiwa Mfalme, Yesu aliwahakikishia wafuasi wake kwamba angemweka rasmi “mtumwa mwaminifu na mwenye busara,” au “msimamizi mwaminifu.” Kazi kuu ya msimamizi huyo ingekuwa kuandaa chakula cha kiroho kwa ukawaida kwa ajili ya wafuasi wa Kristo katika siku za mwisho. (Mt. 24:45-47; Luka 12:42) Tunathamini sana kuwa miongoni mwa watu wanaopokea machapisho yanayoimarisha imani ambayo msimamizi huyo mwaminifu anaandaa na kuhakikisha kwamba yanapatikana ulimwenguni kote.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki