Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • lfb somo la 73 uku. 172-uku. 173 fu. 2
  • Yohana Atayarisha Njia

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Yohana Atayarisha Njia
  • Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • Habari Zinazolingana
  • Alikuwa Mtangulizi wa Mesiya
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • Yohana Mbatizaji Atayarisha Njia
    Yesu—Njia, Kweli, na Uzima
  • Yesu Anakuwa Masihi
    Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • Yohana Aitayarisha Njia
    Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi
Pata Habari Zaidi
Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
lfb somo la 73 uku. 172-uku. 173 fu. 2
Yohana Mbatizaji akiwafundisha watu kwenye fuo za Mto Yordani

SOMO LA 73

Yohana Atayarisha Njia

Yohana, mwana wa Zekaria na Elisabeti, alikuwa nabii alipokuwa mtu mzima. Yehova alimtumia Yohana kuwafundisha watu kwamba Masihi angekuja. Lakini badala ya kufundisha katika masinagogi au katika miji, Yohana alihubiri nyikani. Watu walitoka Yerusalemu na sehemu zote za Yudea ili wafundishwe na Yohana. Aliwafundisha kwamba ili wampendeze Mungu, walihitaji kuacha kufanya mambo mabaya. Baada ya kumsikiliza Yohana, wengi walitubu dhambi zao, na Yohana akawabatiza katika Mto Yordani.

Yohana aliishi maisha rahisi. Alivaa mavazi yaliyotengenezwa kwa manyoya ya ngamia na alikula nzige na asali ya mwituni. Watu walishangazwa na Yohana. Hata Mafarisayo na Masadukayo wenye kiburi walikuja kumwona. Yohana aliwaambia hivi: ‘Mnahitaji kubadili njia zenu na kutubu. Au je, mnafikiri kwamba ninyi ni watu wa pekee kwa sababu tu mnasema ninyi ni watoto wa Abrahamu? Hilo halimaanishi kwamba ninyi ni watoto wa Mungu.’

Watu wengi walimwendea Yohana na kumuuliza: ‘Tunapaswa kufanya nini ili tumpendeze Mungu?’ Yohana akawaambia Wayahudi: ‘Ikiwa una mavazi mawili, mpe moja yule aliye na uhitaji.’ Unajua kwa nini alisema hivyo? Alitaka wanafunzi wake wajifunze kwamba ili wampendeze Mungu, ni lazima wawapende watu.

Yohana aliwaambia hivi wakusanya-kodi: ‘Iweni wanyoofu na msimdanganye mtu yeyote.’ Aliwaambia wanajeshi hivi: ‘Msichukue rushwa wala kusema uwongo.’

Makuhani na Walawi walimwendea Yohana na kumuuliza: ‘Kila mtu anataka kujua, wewe ni nani?’ Yohana akawaambia: ‘Mimi ni sauti nyikani inayowaongoza watu kwa Yehova, kama tu Isaya alivyotabiri.’

Watu walipenda sana mambo ambayo Yohana alikuwa akiwafundisha. Wengi walijiuliza ikiwa Yohana ndiye Masihi. Lakini aliwaambia: ‘Kuna mtu mwenye nguvu kuliko mimi anayekuja. Sistahili hata kufungua kamba za viatu vyake. Mimi ninawabatiza kwa maji, lakini yeye atawabatiza kwa roho takatifu.’

“Mtu huyo alikuja akiwa shahidi, ili atoe ushahidi kuhusu nuru, ili watu wa namna zote waamini kupitia kwake.”​—Yohana 1:7

Maswali: Kwa nini Yehova alimtuma Yohana kwa watu? Watu waliitikiaje ujumbe wake?

Mathayo 3:1-11; Marko 1:1-8; Luka 3:1-18; Yohana 1:19-28; Isaya 40:3

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki