Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • lfb somo la 74 uku. 176-uku. 177 fu. 4
  • Yesu Anakuwa Masihi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Yesu Anakuwa Masihi
  • Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • Habari Zinazolingana
  • Ubatizo wa Yesu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Yohana Anambatiza Yesu
    Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
  • Yesu Abatizwa
    Yesu—Njia, Kweli, na Uzima
  • Alikuwa Mtangulizi wa Mesiya
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
Pata Habari Zaidi
Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
lfb somo la 74 uku. 176-uku. 177 fu. 4
Baada ya Yesu kubatizwa na Yohana, roho ya Mungu inashuka juu yake kama njiwa

SOMO LA 74

Yesu Anakuwa Masihi

Yohana alihubiri hivi: ‘Kuna mtu mwenye nguvu kuliko mimi anayekuja.’ Yesu alipokuwa na umri wa miaka 30 hivi, alitoka Galilaya na kwenda kwenye Mto Yordani ambapo Yohana alikuwa akiwabatiza watu. Yesu alitaka Yohana ambatize, lakini Yohana akasema: ‘Sipaswi kukubatiza. Wewe ndiye unayepaswa kunibatiza.’ Yesu akamwambia Yohana hivi: ‘Yehova anataka wewe unibatize.’ Kwa hiyo, wakaingia ndani ya Mto Yordani, na Yohana akamzamisha Yesu ndani ya maji.

Baada ya Yesu kubatizwa, alisali. Wakati huohuo, mbingu zikafunguliwa, na roho ya Mungu ikashuka juu yake kama njiwa. Kisha Yehova akasema kutoka mbinguni: “Wewe ni Mwanangu, mpendwa; nimekukubali.”

Roho ya Yehova iliposhuka juu ya Yesu, akawa Kristo, au Masihi. Sasa angeanza kufanya kazi ambayo Yehova alimtuma afanye duniani.

Mara tu baada ya ubatizo wake, Yesu akaingia nyikani na kukaa huko kwa siku 40. Aliporudi, akaenda kumwona Yohana. Yesu alipomkaribia, Yohana akasema: ‘Huyu ndiye Mwana-Kondoo wa Mungu ambaye huondolea mbali dhambi ya ulimwengu.’ Kwa kusema hivyo, Yohana alikuwa akiwajulisha kwamba Yesu ndiye Masihi. Je, unajua kilichompata Yesu alipokuwa nyikani? Acheni tuone.

“Sauti ikasikika kutoka mbinguni ikisema: ‘Wewe ni Mwanangu, mpendwa; nimekukubali.’”​—Marko 1:11

Maswali: Kwa nini Yesu alibatizwa? Kwa nini Yohana alisema kwamba Yesu alikuwa Mwana-Kondoo wa Mungu?

Mathayo 3:13-17; Marko 1:9-11; Luka 3:21-23; Yohana 1:29-34; Isaya 42:1; Waebrania 10:7-9

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki