Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • lfb somo la 85 uku. 198-uku. 199 fu. 1
  • Yesu Aponya Siku ya Sabato

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Yesu Aponya Siku ya Sabato
  • Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • Habari Zinazolingana
  • Mafarisayo Wamhoji Mtu Aliyekuwa Kipofu
    Yesu—Njia, Kweli, na Uzima
  • Kutoitikadi kwa Mafarisayo kwa Sababu ya Ugumu wa Moyo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Mafarisayo Wakosa Kuamini kwa Kupenda
    Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi
  • Kuponya Mwanamume Aliyezaliwa Akiwa Kipofu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
Pata Habari Zaidi
Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
lfb somo la 85 uku. 198-uku. 199 fu. 1
Mafarisayo wakimuuliza maswali mwanamume aliyekuwa kipofu

SOMO LA 85

Yesu Aponya Siku ya Sabato

Mafarisayo walimchukia Yesu, na walitafuta sababu za kumkamata. Walidai kwamba hakupaswa kuponya wagonjwa siku ya Sabato. Katika siku fulani ya Sabato, Yesu alikutana na mwanamume kipofu akiombaomba barabarani. Yesu akawaambia wanafunzi wake: ‘Oneni jinsi nguvu za Mungu zitakavyomponya mwanamume huyu.’ Yesu akatema mate kwenye udongo akatengeneza tope, kisha, akapaka kwenye macho ya yule mwanamume. Halafu akamwambia: “Nenda ukanawe katika dimbwi la Siloamu.” Mwanamume huyo akafanya kama alivyoagizwa, na kwa mara ya kwanza maishani akaanza kuona.

Watu walishangaa sana. Wakawa wakiulizana hivi: ‘Je, huyu ni yule aliyekuwa akiketi na kuombaomba au ni mtu mwingine anayefanana naye?’ Mwanamume huyo akawajibu: ‘Ni mimi niliyezaliwa kipofu!’ Nao wakamuuliza: ‘Macho yako yalifunguliwaje?’ Alipowasimulia jambo lililotokea, wakampeleka kwa Mafarisayo.

Mwanamume huyo akawaambia Mafarisayo hivi: ‘Yesu alinipaka tope katika macho, kisha, akaniambia niende nikanawe. Nilifanya hivyo, na sasa ninaona.’ Mafarisayo wakasema: ‘Ikiwa Yesu anaponya siku ya Sabato, basi nguvu zake hazitoki kwa Mungu.’ Wengine wakasema: ‘Ikiwa nguvu zake hazitoki kwa Mungu, asingeweza kuponya.’

Mafarisayo wakawaita wazazi wa mtu huyo na kuwauliza: ‘Ni nini kilichofanya mtoto wenu aanze kuona?’ Wazazi waliogopa kwa sababu Mafarisayo walikuwa wamesema kwamba ikiwa mtu yeyote angemwamini Yesu angefukuzwa katika sinagogi. Kwa hiyo, wakajibu hivi: ‘Hatujui. Muulizeni mwenyewe.’ Mafarisayo wakaendelea kumuuliza maswali yule mwanamume, hatimaye akasema: ‘Nimewaambia kila kitu. Kwa nini mnaendelea kuniuliza?’ Mafarisayo wakakasirika na kuamua kumfukuza.

Yesu akamtafuta mwanamume huyo na alipompata akamuuliza hivi: ‘Je, unamwamini Masihi?’ Mtu huyo akamjibu: ‘Ikiwa ningemjua ningemwamini.’ Yesu akamwambia: ‘Mimi ndiye Masihi.’ Kwa kweli, Yesu alimtendea mtu huyo kwa fadhili, sivyo? Hakumponya tu mwanamume huyo bali alimsaidia pia kuwa na imani.

“Ninyi mmekosea, kwa sababu hamjui Maandiko wala nguvu za Mungu.”—Mathayo 22:29

Maswali: Yesu alimsaidiaje mwanamume aliyekuwa kipofu? Kwa nini Mafarisayo walimchukia Yesu?

Yohana 9:1-41

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki