Utangulizi wa Sehemu ya 8
Yehova alimbariki Sulemani kwa kumpa hekima nyingi na akampa pendeleo la kujenga hekalu. Hata hivyo, hatua kwa hatua Sulemani alimwacha Yehova. Ikiwa wewe ni mzazi, mweleze mtoto wako jinsi walioabudu sanamu walivyomfanya Sulemani amwasi Mungu. Ufalme uligawanyika na wafalme wabaya wakawafanya watu wawe waasi-imani na waabudu sanamu. Wakati huo, manabii wengi washikamanifu wa Yehova waliteswa na kuuawa. Malkia Yezebeli aliwafanya watu wa ufalme wa kaskazini watumbukie zaidi katika uasi-imani. Hicho kilikuwa kipindi kibaya sana katika historia ya Israeli. Lakini bado kulikuwa na watumishi wengi waaminifu wa Yehova, kutia ndani Mfalme Yehoshafati na nabii Eliya.