Utangulizi wa Sehemu ya 9
Sehemu hii inatufundisha kuhusu vijana, manabii, na wafalme walioonyesha imani ya pekee kumwelekea Yehova. Kule Siria, msichana mdogo Mwisraeli alikuwa na imani kwamba nabii wa Yehova angemponya Naamani. Nabii Elisha alikuwa na uhakika kwamba Yehova angemlinda kutokana na jeshi adui. Kuhani Mkuu Yehoyada alihatarisha uhai wake ili kumlinda Yehoashi, aliyekuwa bado mtoto, kutokana na nyanya (au bibi) yake mwovu, Athalia. Mfalme Hezekia alikuwa na uhakika kwamba Yehova angeliokoa Yerusalemu, na hata alipotishiwa na Waashuru hakusalimu amri. Mfalme Yosia aliondoa kabisa ibada ya sanamu katika nchi yote, akarekebisha hekalu, na akarudisha ibada ya kweli nchini.