WIMBO NA. 106
Kusitawisha Sifa ya Upendo
Makala Iliyochapishwa
1. Twasali kwa Yehova Mungu,
Tusitawishe sifa zake.
Zaidi ya yote upendo
Unaotokana na roho.
Vipawa vyetu vyote bure,
Ikiwa hatuna upendo.
Basi na tuwe na upendo;
Na kumpendeza Yehova.
2. Upendo ni wenye fadhili.
Huwafikiria wengine.
Upendo hauna kinyongo,
Bali husamehe wengine.
Upendo hutusaidia,
Kustahimili mambo yote.
Huhimili mizigo yote.
Upendo haushindwi kamwe.
(Ona pia Yoh. 21:17; 1 Kor. 13:13; Gal. 6:2.)