BOAZI, II
(Boazi) [labda, Katika Nguvu].
Nguzo ya kaskazini zaidi kati ya nguzo mbili kubwa za shaba zilizosimamishwa mbele ya ukumbi wa hekalu lenye utukufu la Sulemani iliitwa Boazi, labda kumaanisha “Katika Nguvu.” Nguzo ya kusini iliitwa Yakini, maana yake “Naye [yaani, Yehova] Aimarishe Kabisa.” Kwa hiyo, maneno hayo yanapowekwa pamoja na kusomwa kutoka kulia kwenda kushoto mtu anapoangalia upande wa Mashariki yatatokeza wazo hili ‘Naye [yaani, Yehova] aimarishe kabisa [hekalu] katika nguvu.’—1Fa 7:15-21; tazamaKIFUNIKO.