Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w74 2/1 kur. 70-71
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • Habari Zinazolingana
  • Ikiwa Mtu wa Ukoo Ametengwa na Ushirika...
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
  • Kuendeleza Maoni Yaliyosawazika Juu ya Waliotengwa na Ushirika
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Kutenga na Ushirika—Jinsi Kunavyopasa Kuonwa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
  • Onyesha Uaminifu wa Kikristo Mtu wa Ukoo Anapotengwa na Ushirika
    Huduma Yetu ya Ufalme—2002
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
w74 2/1 kur. 70-71

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

● Imempasa Mkristo mwaminifu atende namna gani juu ya mtu wa jamaa yake ya karibu ambaye ametengwa na ushirika wa kundi?​—N.W., Canada.

Hali hii ni moja ambayo inaweza kuwa jaribu kwa Mkristo anayetaka kuwa mwaminifu kwa Yehova lakini mwenye upendo wa kawaida kwa mtu wa jamaa yake aliyetengwa na ushirika wa kundi. Tunaweza kushukuru kwamba Mungu ameeleza wazi jambo hili katika Neno lake.

Biblia inaonyesha kwamba Yehova anataka kusamehe. Wanadamu wote ni wenye dhambi, lakini Yeye analo kusudi la kuwasamehe dhambi za namna hiyo juu ya msingi wa dhabihu ya Kristo kama kila mtu kwa kutubu anatafuta msamaha.​—Rum. 3:23; Matendo 26:20.

Hata hivyo, ni jambo gani linalotukia ikiwa mtu aliyetafuta msamaha wa namna hiyo wakati uliopita na akawa mtumishi wa Mungu aliye wakfu anafanya dhambi? Yehova anafahamu kutokamilika kwa wanadamu na atasamehe bado kama mfanya dhambi huyo anakubali kosa lake na kuhakikisha kwa njia ya mwenendo wake kwamba ametubu. (1 Yohana 1:9) Walakini, kama mtu anayejidai kuwa Mkristo anafanya mazoea ya dhambi na anakataa kutubu na kugeuka, amri za Mungu ziko wazi. Hili lilionekana katika karne ya kwanza, kwa maana mtu katika kundi la Korintho alizoea kufanya ufisadi. Amri iliyoongozwa na roho ya Mungu kwa kundi hilo ilikuwa: “Mwondoeni yule mbaya miongoni mwenu.” Ndiyo, mfukuzeni katika kundi.​—1 Kor. 5:13.

Hatua hiyo ilikuwa ya muhimu. Lisiwepo shawishi linalokubaliwa kukaa katika tengenezo la Mungu. Kama vile mtume Paulo alivyoandika, “chachu kidogo hulichachusha donge zima.” Kama mtu huyo mwenye ufisadi angekaa, hali nzuri ya kiroho ingepotea.​—1 Kor. 5:5-7; Yos. 7:1-25.

Walipaswa Wakristo waaminifu huko Korintho wamtendee mtu huyo namna gani? Paulo aliandika: “Msichangamane na mtu aitwaye ndugu, akiwa ni mzinzi au mwenye kutamani au mwenye kuabudu sanamu au mtukanaji au mlevi au mnyang’anyi; mtu wa namna hii msikubali hata kula naye.” (1 Kor. 5:11) Kwa hiyo kuondolewa huku katika kundi kwa kufaa kunaweza kuitwa kutengwa na ushirika, kwa sababu Wakristo waaminifu wanaacha kushiriki na mtu mzoevu wa dhambi. Kwa kadiri gani?

Mtume Yohana anatusaidia hapa. Huenda mtu aliyetengwa na ushirika amekuwa kafiri, akifundisha mafundisho yasiyopatana na Maandiko. Au kwa njia yake ya maisha ya ufisadi huenda, kweli, akawa anafundisha ya kwamba mtu anaweza kuwa Mkristo na, wakati uo huo, anaweza kuwa mzinzi au mwasherati. Hii kwa wazi si kukaa katika mafundisho ya haki ya Yesu. Juu ya watu wa namna hiyo ambao wakati mmoja walikuwa ndugu au dada wa Kikristo Yohana anaandika: “Kila apitaye cheo, wala asidumu katika mafundisho ya Kristo, yeye hana Mungu. Yeye adumuye katika mafundisho hayo, huyo ana Baba na Mwana pia. Mtu akija kwenu, naye haleti mafundisho hayo, msimkaribishe nyumbani mwenu, wala msimpe salamu.”​—2 Yohana 9, 10.

Mstari ufuatao unasisitizia uzito wa jambo hili: “Maana yeye ampaye salamu azishiriki kazi zake mbovu.” (2 Yohana 11) Hii haimaanishi kwa lazima kwamba Mkristo anayezungumza na mtu ambaye alitengwa na ushirika kwa sababu ya kuiba, kwa mfano, yeye mwenyewe anageuka kuwa mwizi, hata ingawa hilo linaweza kutukia kwa wepesi. Lakini kwa kutojali shauri la Mungu na kuzungumza na mtu huyo ni kama anasema kwamba anakubali mwenendo wake mwizi, kana kwamba si kitu.

Kwa hivyo tumehakikisha kutoka Biblia yenyewe hali ya msingi ya Mkristo mwaminifu kuelekea mtu aliyetengwa na ushirika​—⁠kutokuwa na ushirika naye hata kidogo, hata kuzungumza naye. Sasa namna gani kama mtu huyo aliyefukuzwa ni ndugu wa jamaa?

Mahali ambapo mtu mwenye kutengwa na ushirika na Mkristo mwaminifu wamo katika jamaa moja, wanaishi katika nyumba moja, kama vile mume na mke, sehemu nyingine za Biblia zinatumika. Kama mke wa mwanamume Mkristo alitengwa na ushirika kwa sababu ya kusema uongo, yeye bado amemwoa; Biblia inasema kwamba wao wameambatana kuwa mwili mmoja. (Efe. 5:31) Katika hali hiyo yeye ataendelea bado kumtunza kama mke wake kama kiungo cha nyumba yake. Hii itatia ndani na kuzungumza naye juu ya mambo ya kila siku ya maisha yao. Walakini, kwa kuheshimu sheria ya kutenga na ushirika, iliyovunja ukamatano wao kama ndugu na dada wa kiroho, kwa hakika yeye hataongoza funzo la Biblia naye au kuwa na ushirika wo wote juu ya mambo ya kiroho. (Kwa maelezo zaidi, tazama The Watchtower la Julai 15, 1963, kurasa za 444-446.)

Lakini ulizo la msingi ambalo linafikiriwa ni juu ya mtu wa jamaa anayeishi nje ya jamaa hiyo, mtu ambaye haishi nyumba moja. Je! ushirikiano wo wote unawezekana?

Tena, kutengwa na ushirika hakuvunji udugu wa nyama na damu, lakini, katika hali hii, ushirika kama ungekuwa wa lazima, ungekuwa si wa kawaida kama wa watu wanaoishi katika nyumba moja. Lakini, kunaweza kuwako mambo yaliyo ya lazima kabisa ya jamaa yanayohitaji njia za kupelekeana habari, kama vile haki za wosia au mali. Lakini jamaa aliyetengwa na ushirika afahamishwe kwamba hali yake imegeuka, kwamba yeye sasa hakaribishwi tena nyumbani wala yeye si mwenzi anayetamanika.

Njia hii inalingana na Maandiko na ni ya busara vile vile. Kama tulivyoona, Mungu anaarifu Wakristo ‘kutochangamana’ na watu wa namna hiyo, “hata kula naye.” Yeye vile vile anaagiza Wakristo ‘wasimpokee katika nyumba zao hata kumpa salamu.’ Kama ushirika wa kawaida unakuwapo katika watu wa jamaa na mtu ambaye alitengwa na ushirika, jambo ambalo si la lazima kwa kuwa yeye anaishi nje ya nyumba hiyo, je! Mkristo angekuwa anamtii Mungu? Katika kundi dogo lenye jamaa za ukoo mmoja, kama kila mtu angemtendea mtu aliyetengwa na ushirika kama vile alivyokuwa akimtendea mbele ya kutengwa kwake na ushirika​—kwenda pamoja naye kununua vitu madukani, kwenda kula kwenye bustani pamoja (pikiniki), kusaidiana kuchunga watoto wa mtu na mwenzake​—mtu huyo hataona ya kwamba ndugu zake ambao ni Wakristo waaminifu wanauchukia uovu alioufanya. (Zab. 97:10) Wala watu wa nje wasingeweza kuona mageuzi yo yote hata ingawa huenda wanaijua njia isiyofaa kwa Mkristo ya huyo mwenye kufanya dhambi.

Lazima tukazie wazi kwamba kutoweza kwa mtu aliyetengwa na ushirika kuufurahia urafiki wa jamaa zake za Kikristo si kosa lao, kana kwamba walikuwa wakimtendea kwa kujifanya. Wao wanatenda kwa kulingana na kanuni, kanuni za juu sana, kanuni za Mungu. Mtu aliyetengwa na ushirika ana lawama mwenyewe kwa sababu ya hali yake; amejiletea hali hiyo mwenyewe. Uacheni mzigo ukae mahali ambapo umetokea!

Kama mfanya dhambi aliyefukuzwa anataka kurudishwa tena kwenye ushirika mtamu na Yehova na Wakristo waaminifu vile vile, hilo linawezekana. Isaya aliandika: “Mtu mbaya na aache njia yake, na mtu asiye haki aache mawazo yake; na amrudie [Yehova], naye atamrehemu; na arejee kwa Mungu wetu, naye atamsamehe kabisa.” (Isaya 55:7) Mtu aliyetengwa na ushirika ambaye anatubu anaweza kusamehewa na kurudishwa katika kundi.​—2 Kor. 2:6-8.

Lakini mpaka hayo yatokee, Wakristo waaminifu wanalo sharti la kushikilia hatua ya kutenga na ushirika kwa kuukwepa ushirika wa mtu aliyetengwa na ushirika. Kama huyo ni ndugu wa kimwili ambaye hawaishi naye katika nyumba moja, watajaribu kutokuwa na ushirika wo wote naye hata kidogo. Na kama jambo fulani la lazima kabisa linatokea, watakutana na huyo kwa kadiri ndogo iwezekanavyo, bila shaka kwa kutokutoleana mawazo yo yote juu ya mambo ya kiroho. Kwa njia hiyo watahakikisha uaminifu wao kwa Mungu, Neno lake na kundi lake.

● Ikiwa Mkristo anafanya uzinzi, atubu na aungame dhambi yake kwa halmashauri ya hukumu ya kundi la Kikristo, ni lazima yeye vile vile ajulishe uzinzi wake kwa mwenzi wake wa ndoa hata ingawa itamdhuru sana huyu mwingine?​—U.S.A.

Ndiyo Mkristo yu chini ya wajibu kujulisha kosa lake kwa mwenzi asiye na hatia mbele ya washiriki wa halmashauri ya hukumu kuweza kukubali kutubu kwake kama kwa kweli. Uzinzi ni kuchafua malazi ya ndoa na ni jambo zito kutosha kumruhusu mwenzi asiye na hatia kupata talaka na awe huru kulingana na Maandiko kuoa (kuolewa) tena. (Mt. 19:9) Hivyo basi, mwenzi asiye na hatia ana haki yote kujua kumetukia nini.

Kwa uhakika, si kule kuungama, lakini uzinzi ndio unaomdhuru mwenzi asiye na hatia. Kwa sababu hii mwenzi mwenye kuzini lazima awe amekwisha fanya uangalizi mzito mapema kwa matokeo haya mabaya ya uzinzi na hangekuwa amejiachilia kwa majaribu. Baada ya uzinzi kufanyika ni kuchelewa mno kuanza kufikiri juu ya kumzuilia mwenzi asiye na hatia kutokuona uchungu.

Ijapokuwa mwenzi asiye na hatia angeweza kuona uchungu kwa wepesi akiisha elewa juu ya uzinzi, hii haimaanishi kwa lazima ndio mwisho wa ndoa. Nyuma ya kusikia ungamo la moyoni na ombi la msamaha, mume au mke anaweza kufikiria kumsamehe mwenzi mzinifu. Halafu, tena, ungamo linatoa nafasi kwa wote mume na mke kuitazama ndoa yao kwa uzito kufikiria nini kiwezacho kufanywa kwa kuleta maendeleo na kuepuka kurudia kosa. Mwenzi asiye na hatia anaweza kuwa hata alishiriki kuleta kutoaminika kwa mwenzi wake wa ndoa. Ikiwa, kwa mfano, mke amemnyima mumewe haki ya ndoa kwa makusudi, anachukua lawama fulani kwa kile ambacho kimetukia. Si kwamba yeye hana hatia kulingana na maoni ya Mungu, kwa maana Biblia inashauri: “Mume na ampe mkewe haki yake, na vivyo hivyo mke na ampe mumewe haki yake. . . . Msinyimane isipokuwa mmepatana kwa muda, ili mpate faragha kwa kusali; mkajiane tena, Shetani asije akawajaribu kwa kutokuwa na kiasi kwenu.”​—1 Kor. 7:3-5.

Labda zaidi ya kuweka msingi kwa ndoa inayoendelea, ungamo linaweza vile vile kuzuia magumu mengine mazito. Kadiri mwenzi mzinifu anavyoficha jambo lenyewe, hawezi kuwa na dhamiri njema kuelekea mwenzi wake wa ndoa. Hili linaweza kujionyesha lenyewe kwa neno na tendo. Mwenzi asiye na hatia anaweza kuona kuna kosa fulani na ataje jambo hili. Kwa kujikinga mwenyewe, mwenzi aliye na hatia anaweza kuanza kusema uongo, na hii inaweza kuchanganya makosa yake. Hivyo huenda mwishowe madhara zaidi yakatokea kuliko kama yanavyoweza akitubu makosa yake na kutafuta msamaha wa mwenzi wake.

Hivyo ikiwa yule aliye na hatia ya uzinzi anatubu kwa kweli na anataka kuhifadhi ndoa, imempasa autafute msamaha wa mwenzi asiye na hatia. Kutoka hapo na kuendelea, ikiwa msamaha unatolewa, wote wawili wanaweza kufanya kazi pamoja katika kujaribu kuhifadhi malazi bila uchafu. (Ebr. 13:4) Kwa kuwa usafi wa adili wa kundi unatiwa ndani, inawabidi vile vile kuieleza halmashauri ya hukumu wazi kilichotukia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki