Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w74 10/1 uku. 455
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • Habari Zinazolingana
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
  • ‘Wamewanda na Kung’aa’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
  • Naweza Kupunguzaje Uzito?
    Amkeni!—1994
  • Mbona Mimi Ni Mnene Sana?
    Amkeni!—1994
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
w74 10/1 uku. 455

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

● Sababu gani sheria ya Musa ilikataza kula mafuta?​—U.S.A.

Katika Sheria iliyopewa kwa Waisraeli, vyote damu na mafuta vilionwa kama vya Yehova Mungu peke yake. Sheria ilisema: “Neno hilo litakuwa amri ya daima, katika vizazi vyenu vyote, ndani ya nyumba zenu zote, ya kwamba hamtakula mafuta wala damu kabisa.”​—Law. 3:17.

Damu inafananisha uhai wa mtu au mnyama. Kwa sababu hiyo Biblia inasema juu ya “nafsi” kama ikiwa “katika hiyo damu.” (Mwa. 9:4; Law. 17:11, 14, NW) Kwa kuwa ni Yehova Mungu peke yake anayeweza kutoa uhai, au kinachofananisha uhai, damu, kwa haki ni chake.

Mafuta yalionwa kama sehemu bora kupita zote. Hii ni wazi kutokana na usemi wa mfano kama “unono wa nchi,” na “yaliyo bora [manono] katika mafuta,” na “yaliyo bora [manono] katika divai mpya na nafaka.” (Mwa. 45:18; Hes. 18:12, NW) Hivyo makatazo ya kula mafuta kwa wazi yalikuwa ya kukazia mioyo ya Waisraeli kwamba sehemu ‘za kwanza’ au zilizo bora ni za Yehova, za kumtolea kama dhabihu. Kwa hiyo kula mafuta kungekuwa ni kuchukua kitu ambacho kilikuwa kimetakaswa kwa Yehova. Kungekuwa ni mwingilio wa haki zake. Lakini, kwa habari ya mnyama ambaye alikufa mwenyewe au akauawa na mnyama mwingine, mafuta yangeweza kutumiwa kwa makusudi mengine.​—Law. 7:23-25.

Waelezaji wengi wa Biblia wanaamini kwamba ile amri juu ya mafuta ilikamatana na wanyama waliokubaliwa kuwa dhabihu peke yao. Lakini kuna mambo ya kuonyesha kwamba makatazo haya ya kula mafuta yalitumika kwa mafuta ya wanyama wote. Amri juu ya mafuta inakamatana na ile ya damu. Na damu ya wanyama wote ilikatazwa isiliwe. (Law. 17:13, 14; Kum. 12:15, 16) Kwa kweli, basi, sheria juu ya mafuta vile vile ilitia ndani na mafuta ya wanyama wote.

Tunaweza kuangalia vile vile kwamba kutoa damu kunakofaa hakukuondoa kila tone dogo sana la damu katika nyama, na hali iliyosalia haikufanya nyama isifae kwa kuliwa. Vivyo hivyo, makatazo juu ya kula mafuta hayakufanya nyama yenye mafuta yaliyosalia isifae kuliwa.

Ndiyo, kulisha au kunonesha kondoo au mifugo ya kuliwa hakukukatazwa. Maandiko hata yanataja “kuku walionona.” (1 Fal. 4:23) Kwa sababu ya kizuio juu ya matumizi ya mafuta kwa chakula, kwa wazi kule ‘kunonesha’ hakukuwa kwenye kusudi la kutokeza mafuta, bali kwamba wanyama wanone, kwamba wasikonde.

Katika Kumbukumbu 32:14 mtajo wa “mafuta ya wana-kondoo” kana kwamba yalipewa Waisraeli ni wa mfano. Unamaanisha walio bora katika kundi la kondoo. Kwa hiyo The Jerusalem Bible inasema, “chakula kinono cha malisho.” Maneno ya Nehemia 8:10, “Enendeni zenu, mle kilichonona,” yanapaswa kueleweka vivyo hivyo. “Kilichonona” kina maana ya mfano ya sehemu bora, zilizo tamu sana, bila shaka kutia ndani na vitu vyenye ladha vilivyotayarishwa na mafuta ya mboga. Tafsiri ya James Moffatt inasema, “mle sehemu zenye ladha nzuri.” Vitu vingine, kama keki inayotengenezwa kwa ngano, vilipikwa katika “mafuta mengi.” Haya hayakuwa mafuta ya mnyama, bali yalikuwa mafuta ya mboga, zaidi mafuta ya mzeituni.​—Law. 2:7.

Tofauti na makatazo ya damu, ambayo yamekuwa yakitumika kwa jamii yote ya kibinadamu tangu gharika ya siku za Nuhu, Wakristo leo hawako chini ya vizuio vya sheria ya Musa juu ya vyakula. (Mwa. 9:4) Chini ya uongozi wa roho ya Mungu mtume Paulo aliandika: “Mtu asiwahukumu ninyi katika vyakula au vinywaji, au kwa sababu ya sikukuu au mwandamo wa mwezi, au sabato; mambo hayo ni kivuli cha mambo yajayo; bali [uhakika] ni wa Kristo.” (Kol. 2:16, 17) Hata hivyo, sheria juu ya mafuta inapasa kuwakumbusha Wakristo juu ya takwa la kuendelea kumtolea Yehova Mungu kilicho bora. (Mit. 3:9, 10) Hii inapaswa ionyeshwe katika kila sehemu ya maisha ya Mkristo. Shauri la Biblia ni: “Lo lote mfanyalo, lifanyeni kwa moyo, kama kwa [Yehova], wala si kwa wanadamu, mkijua ya kuwa mtapokea kwa [Yehova] ujira wa urithi.”​—Kol. 3:23, 24.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki