Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w75 2/15 kur. 93-94
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Habari Zinazolingana
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2024
  • Maswali kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
  • Wenye Furaha ni Wale Ambao Mungu huwatia adabu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
w75 2/15 kur. 93-94

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

● Ni kwa njia gani mtu anavyokuwa ‘wa kujihadhari naye’ katika maana inayosimuliwa katika 2 Wathesalonike 3:14, 15?​—America Samoa.

Mtume Paulo aliliandikia kundi katika Thesalonike hivi: “Ikiwa mtu awaye yote halishiki neno letu la waraka huu, jihadharini na mtu huyo, wala msizungumze naye, apate kutahayari; lakini msimhesabu kuwa adui, bali mwonyeni kama ndugu.” (2 The. 3:14, 15) Mapema kidogo katika barua yake alikuwa ametoa maagizo kama hayo, akisema: “Ndugu, twawaagiza katika jina la Bwana Yesu Kristo, jitengeni nafsi zenu na kila ndugu aendaye bila utaratibu, wala si kwa kufuata mapokeo mliyoyapokea kwetu.” (Mstari wa 6) Kisha Paulo aliendelea kuonyesha “mapokeo” yaliyokuwa yamepokewa kutoka kwake na wenzake katika mfano wenye bidii waliokuwa wameuweka walipokuwa pamoja na akina ndugu huko Thesalonike. Ijapokuwa wengi zaidi katika kundi walikuwa wanaendelea vema, walikuwako wengine “waendao bila utaratibu, hawana shughuli zao wenyewe, lakini wanajishughulisha na mambo ya wengine.”​—Mistari ya 7-11.

Hivyo, hawa ‘wasio na utaratibu’ hawakuwa wakifanya makosa mazito kama vile uasherati, ibada ya sanamu ama utozaji wa bei isiyostahili, makosa ambayo yangelilazimisha kundi kuwaondoa, wasipotubu, likiwatenga na ushirika. (1 Kor. 6:9-13) Hata hivyo, watu hawa walikuwa mifano mibaya na maongozi yasiyofaa ndani ya kundi. Wao hawakuwa, walau katika mambo fulani ya maana, wawakilishaji wa ambavyo Ukristo wa kweli umepaswa kuwa. Ijapokuwa haukuwa mzito, wala mwenendo wao mbaya halikuwa jambo dogo sana hivyo kwamba ungeweza kusahauliwa ama kufunikwa na upendo. (1 Pet. 4:8) Kwa hiyo, walipaswa hao ‘wajihadhariwe.’ Lakini nani angefanya hivi na kwa njia gani?

Angalia kwamba barua ya Paulo haikutumwa kwa mwangalizi, kama Timotheo ama Tito, wala waangalizi hawatajwi wazi (kama katika Wafilipi 1:1), barua imeandikwa “kwa [kundi]” kwa jumla. (2 The. 1:1) Kwa hiyo, badala ya wazee kuwaita watu fulani ‘wasio na utaratibu’ rasmi na kwa waziwazi, ingewapasa washiriki mmoja mmoja wa kundi wajihadhari nao. Kwa maneno, “jihadharini na mtu huyo,” tafsiri nyingine zinasema: “jihadharini naye sana” (New English Bible), “mwangalieni sana” (New Berkeley Version), “mwangalieni huyo” (Jerusalem Bible), “mwangalieni sana mtu huyo” (New American Standard Bible).

Kujihadhari huku na watu fulani au kuwaangalia kama mifano mibaya huenda kukaonyeshwa kwa kukutofautisha na kuangalia kunakofaa kunakotakiwa katika Zaburi 37:37. Humo mtunga Zaburi anaonya: “Umwangalie sana mtu mkamilifu, umtazame mtu mnyofu, maana mwisho wake mtu huyo ni amani.” Vile vile Wakristo wanasihiwa ‘wakawatazame’ wale wawekao mfano mwema kati yao, wakiuchunguza mwenendo wao na kuiiga imani yao. (Flp. 3:17; Ebr. 13:7) Bila shaka, hii haihitajiwi ifanywe kwa kutaja majina ya mifano hiyo myema waziwazi. Mwenendo wao mwema unajisemea wenyewe nao unajulikana kwa watazamaji. Kwa hiyo, vile vile ndivyo ufanyavyo mwenendo mbaya wa hawa wasio na utaratibu, nao washiriki mmoja mmoja wa kundi ‘wanajihadhari’ nao kwa kuwaangalia kama watu wasio wa kuiga.

Ni kwa kadiri gani wanaacha ‘kuzungumza’ nao (‘kuacha kushirikiana’ nao, NW) walio wa ‘kujihadhariwa’? Mstari wa 6 wa sura hii unasema “jitengeni [“kaeni mbali,” New American Standard Bible] na kila ndugu aendaye bila utaratibu.” Kwa wazi ‘kujitenga’ kwao ni kwa namna inayoelezwa katika Wagalatia 2:12. Humo inaelezwa kwamba Petro, kwa kukosea kwa habari hii, “akarudi nyuma akajitenga” na watu wa mataifa, na hali kabla ya hapo alikuwa anakula nao. Hivyo inaonekana kwamba washiriki wa kundi wangeacha kuwa na uhusiano wa kijamii na wale ambao wenyewe ‘wanajihadhari’ nao, na hii kwa kusudi la kuonyesha kwamba hawazikubali tabia ama mwendo ambao hawa wanachukua.

Kwa mfano, katika kundi huenda wengine wakakosa kulitii onyo la Maandiko juu ya mashirika ya kilimwengu, pengine hata ‘kuchumbia’ mtu asiyeamini. (1 Kor. 7:39; 15:33; 2 Kor. 6:14) Huenda wakafanya hivi ingawa wameonywa mara nyingi juu ya jambo hili. Wazee, kutoka jukwaani na kwingineko, huenda hata wakawa wametilia mkazo onyo la Biblia juu ya mwenendo huo, hata hivyo, bila ya kuwataja watu wanaohusika. Halafu? Halafu, wakifikiwa na kukaribishwa washiriki katika ushirika huo wa kilimwengu na mshiriki wa kundi, wale wanaofikiwa ‘wangejihadhari’ na mtu kama huyo kama ‘asiye na utaratibu’ kwa habari hii. Bila shaka wasingetaka kushirikiana naye katika mwendo wake. Nyakati nyingine, huenda wazazi wakaona ni lazima kuwaagiza watoto wao wasije wakashirikiana na vijana fulani katika kundi ambao huenda wanajionyesha kuwa ‘wasio na utaratibu’ katika njia hizo. Bila shaka, wazee watakuwa waangalifu kutowatumia hao katika cheo cho chote chenye mfano unaostahili kufuatwa.

Hii haimaanishi kwamba akina ndugu wangekataa kumsalimu mtu kama huyo, kana kwamba alikuwa wa namna ya watu wanaoelezwa katika 2 Yohana 9-11. Wanapokuwa katika mahali pa Kikristo pa mikutano, wangempokea na kumtendea huyo kwa njia ya kidugu. Lakini wangeukumbuka mfano wake mbaya na kushindwa kwake kuitikia shauri na, ikipatikana nafasi inayofaa, ‘wangemwonya kama ndugu.’ Na, bila shaka, ni jambo la maana zaidi wao wenyewe waweke mfano mwema katika jambo linalopaswa.​—Tito 2:7, 8.

Basi, je! kuna tofauti kati ya hawa walio wa ‘kujihadhariwa’ na watu ambao huenda walifanya dhambi nzito lakini ambao hawakutengwa na ushirika kwa sababu ya toba lao lenye unyofu? Ndiyo, kunayo. Ni kweli, hawa wa pili huenda wakawa walikaripiwa waziwazi, kwa kupatana na 1 Timotheo 5:20, lakini tayari wameyakubali makosa ya mwendo wao, wakaona haya kwa ajili yake na wakatubu. Sivyo ilivyo kwa habari ya wale wanaopaswa ‘kujihadhariwa.’ Ni kwa sababu hiyo ya kutoyakubali makosa ya mwendo wao kusudi watubu kwamba wanapaswa waaibishwe, na ndiyo sababu akina ndugu wanaacha kushirikiana nao katika nyakati nyingine zilizo za lazima, kama vile penye mikutano ya Kikristo.

‘Kujihadhari’ huku hakumaanishi kwamba ‘tunawahukumu’ ndugu zetu​—tukiwakataa kama wasio Wakristo ama wanafunzi wenzetu ama ndugu. Wala hatuwahukumu katika mambo yaliyo ya kuamuliwa na dhamiri ya mtu mwenyewe. (Rum. 14:10) Tunakataa tabia fulani au mwendo ambao kwa wazi unatofautiana na kanuni za Biblia. Watu hawa wakiyashinda mambo hayo tunafurahi kuwaona si tena kama wanaopaswa kujihadhariwa nasi tunafurahi kuweza kushirikiana pamoja nao kwa uhuru.

Basi, haitupasi tuitumie amri hii ya mtume kama sababu ya kumdharau au kumtendea kwa uadui mtu ye yote asiyetimiza kabisa kile ambacho sisi wenyewe tunaona kama mwendo au mfano “mkamilifu.” Watu wengine ni wapya katika imani nao wana mengi ya kujifunza. Wamepaswa watendewe kwa huruma na kwa uvumilivu. (Rum. 14:1-4; 15:1) Kwa hiyo, mtu aweza kujiuliza mwenyewe ulizo, ‘Je! mtu huyo kwa kweli ni ‘asiye na utaratibu’ vya kutosha kustahili kujihadhariwa?’ Kosa dogo katika mwenendo la wakati mmoja si sawa na kufuata mwendo usiopatana na onyo la waziwazi la Maandiko kwa kutoacha. Vile vile uangalifu ungepaswa kufanywa mtu anapokuwa akishindana kwa bidii na udhaifu na anapotaka kufanya maendeleo kwa unyofu. Imetupasa tuilinde afya yetu ya kiroho na ile ya ndugu zetu. Hata hivyo, vile vile imetupasa “tufuate mambo ya amani na mambo yafaayo kwa kujengana,” tukionyesha upendo ulio kweli kweli na kupendezwa kwa mtu na mwenzake.​—Rum. 14:19.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki