Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w83 2/15 uku. 23
  • Maswali kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
  • Habari Zinazolingana
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2024
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Wenye Furaha ni Wale Ambao Mungu huwatia adabu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
w83 2/15 uku. 23

Maswali kutoka kwa Wasomaji

◼ kwa habari ya ‘kumtia alama’ mtu asiye na utaratibu katika kundi’ je! mimi naweza kufanya hivyo wakati wo wote nionapo inahitajiwa kufanya hivyo, au inanipasa kungoja mpaka wazee kwanza watoe hotuba juu ya jambo hilo?

‘Kumtia alama’ Mkristo mwingine kusichukuliwe kuwa jambo jepesi tu kwa maana hiyo ni hatua isiyo ya mchezo. Lakini uamue ni wakati gani wa kuchukua hatua hiyo. Lakini mara nyingi sana ‘kutia alama’ kunapasa kufanywe baada ya wazee kufanya jitihada za kumsaidia mkosaji, na pia baada ya wao kulitolea kundi hotuba juu ya kosa analofanya.

Wakati mtume Paulo alipoandikia Wathesalonike juu ya ‘kutia alama’ washiriki wa kundi hilo, alikuwa akisahihisha watu fulani waliokuwa wameyaacha mashauri ya Mungu kwa kiasi kikubwa. Hao walikuwa ‘wakitembea bila utaratibu, wasifanye kazi hata kidogo bali wakijishughulisha na mambo yasiyowahusu wao.’ (2 Wathesalonike 3:6, 10-12, NW) Ijapokuwa watu hao wasio na utaratibu walipewa mashauri ya Kimaandiko waepuke uvivu, hawakutaka kufanya kazi na waliwalemea sana wenzao kwa kuwategemea katika mambo ya gharama. (Mithali 6:6-11; 10:4, 5; 12:11, 24, 27; 24:30-34; 26:13-16) Kwa hiyo Paulo alitoa shauri la waziwazi kuonyesha ubaya wa mwendo wao. Tena, aliwashauri wote kwamba wasipoitikia shauri hilo thabiti lililotolewa mbele ya kundi zima, inapasa wao ‘watiwe alama’ na kuepukwa. Ni wazi wangeepukwa katika mambo ya kushirikiana kirafiki.

Siku hizi watu fulani wameshindwa kujua kama wanaweza ‘kutia alama’ mtu anayekwenda kinyume cha mashauri ya kimungu ingawa wazee hawajatoa hotuba kuelekea kundi lote juu ya kosa la mtu huyo. Huenda kukawa na nyakati chache sana ambapo uhitaji wa kufanya hivyo unaweza kuwapo (Linganisha 1 Wakorintho 5:1, 2.) Lakini kuna sababu zinazofanya mara nyingi sana liwe jambo bora mtu angoje ‘kutia alama’ mwingine mpaka hatua za wazi zichukuliwe na wazee, kutia na utoaji wa hotuba kulielekea kundi.

Kwanza, kwa kuwa sisi ni wanadamu wasio wakamilifu huenda tukawa na maelekeo ya kutumia vibaya jambo hili la ‘kutia alama,’ kulitumia liwe namna ya kuwapa watu adhabu kuhusu vikosa vidogo au kwa sababu nyutu zetu hazipatani na zao. Huenda katika kundi moja kukawa kuna dada mwenye utu unaogongana na wa wengine. Yeye anaudhi-udhi wengine. Inakuwa shida kupatana naye. Basi huenda dada wengine wakafikiri inawapasa ‘kumtia alama’ na kumwepuka. Kufanya hivyo hakika kungekuwa kinyume cha shauri la Yesu lenye upendo la kusema inatupasa turehemu ndugu na dada zetu, kusahau kupungukiwa kwao na vikosa vyao vidogo. Kwa mfano, kumbuka alivyofundisha katika ile Sala ya Kielelezo juu ya wakati ambao Mungu atasamehe deni au makosa yetu. Naye Yesu alituhimiza tuwe wepesi wa kujaribu kumaliza malalamiko tuliyo nayo juu ya mtu mwingine. (Mathayo 5:23-25; 6:12) Kwa hiyo lingekuwa kosa ‘kumtia alama’ ndugu kwa sababu ya hali ndogo za kutokupatana kwetu naye au kwa sababu ya vikosa vidogo.

Pili, wakati Paulo alipoandika juu ya ‘kuwatia alama’ watu fulani, sababu haikuwa kwamba watu hao walitofautiana na wenzao katika mambo madogo ya kiutu, katika mapendezi au maoni yao. Si lazima wazee wajaribu kujitia ndani ya mambo ya namna hiyo wala si lazima wayatolee mashauri. Lakini wao, kama Paulo, wanapaswa kuwa macho kuwaangalia watu wanaovunja kwa njia kubwa kanuni za Biblia (hata ikiwa makosa yenyewe hayajafikia hatua ya kuwa dhambi nzito inayoweza kufanya watu hao watengwe na ushirika). Inawapasa wazee wawashauri kwa faragha watu hawa wenye kukosa au wasio na utaratibu. Ni kama vile tunavyosoma kwenye Wagalatia 6:1, NW: “Hata ingawa mtu achukua hatua fulani ya uongo kabla ya yeye kuijua, ninyi mlio na sifa za kiroho jaribuni kumrekebisha upya mtu huyo katika roho ya upole.”

Ikiwa wazee wamejaribu mara nyingi kumsaidia mtu huyo kwa faragha bila matokeo, wanaweza kulizungumza jambo hilo na kuamua mmoja wao atolee kundi hotuba ya Kimaandiko yenye kutoboa wazi jambo linalohusika. Ingawa wao watafuata mfano wa Paulo wasitaje majina ya wale wanaopuza mashauri ya Mungu kwa njia nzito, watatoa onyo juu ya kuepuka kufuata fikira au mwendo mbaya. Kwa njia hiyo akili za washiriki wa kundi zitakumbushwa upya mawazo ya Mungu kisha wao wataamshwa wajilinde ili wasije ‘wakaambukizwa’ au kupotezwa. Halafu, kama vile Paulo alivyoandika, Wakristo mmoja mmoja wanaweza ‘kumtia alama’ yule asiye na utaratibu kisha waepuke kushirikiana naye. Na, kwa kuwa wazee wametoa mashauri ya wazi juu ya tatizo hilo, mkosaji ataelewa sababu inayofanya wengine katika kundi wakatae makaribisho yake ya kwenda kushirikiana naye kirafiki.​—2 Wathesalonike 3:13-15.

Kwa hiyo, kwa kawaida ni hekima kuepuka ‘kutia alama’ mtu mwingine isipokuwa kama jambo hilo limeshughulikiwa waziwazi na wazee, kama vile Paulo alivyoshauri waziwazi juu ya jambo zito na baada ya hapo watu mmoja mmoja wangeweza kufuata shauri juu ya ‘kutia alama.’ Tukichukua mambo hivyo, tutaepuka hatari ya ‘kuwatia alama’ watu isivyofaa kwa sababu ya kosa vidogo, kwa sababu ya mapendezi yanayotofautia na yetu. Vilevile, kufanya hivyo kunaonyesha heshima kwa wazee ambao ndio wachungaji wenye upendo wanaoangalia mahitaji ya lile kundi.​—1 Petro 5:2.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki