Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w74 1/15 kur. 42-48
  • Mipaka ya Ufalme wa Mungu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mipaka ya Ufalme wa Mungu
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • UFAHAMU UONGOZAO KWENYE AZIMIO
  • HAKI​—MPAKA MKUU
  • Ujumbe Ambao Ni Lazima Tuutangaze
    Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
  • Mtafute Mungu Maadamu Anapatikana
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • Namna Ufalme wa Mungu Unavyoweza Kukufaidi Wewe
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
  • Pendezwa na Uadilifu wa Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2002
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
w74 1/15 kur. 42-48

Mipaka ya Ufalme wa Mungu

1. Katika Mathayo 5:3, 19. ni matakwa gani mawili yanayotajwa yanayokamatana na ufalme wa Mungu?

KATIKA Mahubiri yake juu ya Mlima yajulikanayo sana, Yesu alitilia mkazo umuhimu wa kuutafuta ufalme wa Mungu kwa kusimulia sawasawa mipaka yake, yaani, watu ambao ungetia ndani katika ushirika wake. Akitaja kwanza haja ya warithi wa Ufalme kuwa wenye unyenyekevu na hali ya kuomba, yeye alisema: “Heri waijuao haja yao ya kiroho, kwa maana ufalme wa mbingu ni wao.” Kwa njia ya kuonya na kufariji, vile vile alitilia mkazo haja ya warithi wa Ufalme kukaa ndani ya mipaka ya amri za Mungu, akisema: “Kwa hiyo, ye yote atakayevunja mojawapo wa hizi amri ndogo [za Torati ya Musa] na kufundisha wanadamu hivyo, yeye ataitwa ‘mdogo kabisa’ [kwa hiyo asiyefaa] kwa habari ya ufalme wa mbingu. Na ye yote atakayezitenda na kuzifundisha, huyu ataitwa ‘mkuu’ kwa habari ya ufalme wa mbingu.”​—Mt. 5:3, 19, NW.

2. Maombi ya Sala ya Bwana yanawezaje na yamepaswaje kutumiwa kwa kipekee?

2 Sasa angalia maneno ya kwanza ya sala ya kielelezo inayofanyiza sehemu ya hotuba hiyo: “Baba yetu uliye mbinguni, jina lako na litakaswe. Ufalme wako na uje. Mapenzi yako na yatimie duniani vile vile, kama ilivyo mbinguni.” (Mt. 6:9,10, NW) Haya si maombi ya kawaida tu. Kwa kweli, yanafanyiza mipaka, au viongozi, ambavyo lazima tuvitumie kwetu wenyewe. Lazima tulitakase jina la Yehova mioyoni mwetu na akilini na katika mwenendo wetu wote. Kama vile mtume Paulo alivyoandika juu ya mwenendo wetu: “Haya ndiyo mapenzi ya Mungu, kutakaswa kwenu, mwepukane na uasherati; kila mmoja wenu ajue kuuweza mwili wake katika utakatifu na heshima . . . Maana Mungu hakutuitia uchafu, bali tuwe katika utakaso. Mungu wa amani mwenyewe awatakase kabisa.” Haitupasi kutamani tu kuona mapenzi ya Mungu yakifanywa duniani kwa njia kubwa, bali kujaribu kujua na kuyatimiza mapenzi yake katika maisha zetu wenyewe kwa unyofu sasa hivi, na hivyo kuuhakikisha upendo wetu kwake. Hii maana yake wakf wetu. Mtume Yohana aliandika: “Msiipende dunia, wala mambo yaliyomo katika dunia. Mtu akiipenda dunia, kumpenda Baba hakumo ndani yake . . . dunia inapita, pamoja na tamaa zake, bali yeye afanyaye mapenzi ya Mungu adumu hata milele.”​—1 The. 4:3-7; 5:23; 1 Yohana 2:15-17.

3. Mbali na kuutafuta Ufalme, nini zaidi alichokitaja Yesu, na wengi wameonaje ugumu juu ya jambo hili?

3 Nyumaye katika hotuba ya Yesu, alipokwisha kuonya juu ya hatari za mambo ya kimwili, “mambo ambayo mataifa yanayafuatia kwa bidii,” alisema: “Endeleeni, basi, kuutafuta ufalme kwanza na haki yake [Mungu], na mambo haya mengine yote mtaongezewa.” (Mt. 6:32, 33, NW) Jambo la ajabu kama liwezavyo kuonekana, Yesu aligusia hapa kimojawapo cha vizuizi vikubwa vinavyokutanwa navyo katika kumtafuta Mungu, si kwa Wayahudi tu, lakini kwa watu wote. Watu walio wengi wanataka kujitetea wenyewe na kuonekana wenye haki, walau machoni pa washiriki wao. Hii inaamuliwa na kanuni zao wenyewe, zinazotofautiana sana kati ya watu mbalimbali, zaidi katika jamii ya kisasa itoayo ruhusa. Wayahudi kwa ujumla walijaribu kuimarisha haki yao wenyewe, wakiutumaini uwezo wao wa kuishika Torati iliyotolewa kupitia kwa Musa. Kama vile alivyosema Paulo: “Wana juhudi kwa ajili ya Mungu, lakini si katika maarifa. Kwa maana, wakiwa hawaijui haki ya Mungu, na wakitaka kuithibitisha haki yao wenyewe, hawakujitia chini ya haki ya Mungu. Kwa maana Kristo ni mwisho wa sheria, ili kila aaminiye ahesabiwe haki.”​—Rum. 10:2-4; tazama vile vile Wagalatia 3:10-14.

4. Nini sababu ya ugumu? Unatendaje kazi, nao waweza kushindwa namna gani?

4 Bila shaka, kiburi, tofauti ya unyenyekevu, ndicho chanzo cha ugumu huo. Kilianza na Ibilisi, “mungu wa dunia hii,” nayo ni njia ambayo kwayo yeye “amepofusha fikira zao wasioamini, isiwazukie nuru ya injili ya utukufu wake Kristo aliye sura yake Mungu.” Kiburi kinakuwa kama kizuizi cha kutafuta kwetu Mungu wa kweli. Kinaigeuza mioyo yetu kutuelekea sisi katika kujisifu. Kwa hiyo uwezo wetu wa akili unapumbazwa katika kutokuamini, na hii inakuwa kama utaji. “Lakini wakati wo wote watakapomgeukia [Yehova kwa unyenyekevu na unyofu], ule utaji huondolewa.” Huenda kiburi kiwe ni sehemu ya umbo letu la asili, lakini, kama alivyosema Paulo, lazima ‘tuuvue kabisa utu wa kale,’ na, mahali pake, ‘tujivike unyenyekevu wa akili.’​—2 Kor. 4:4; 3:13-16; Kol. 3:9, 12.

5. (a) Yesu aliyasimuliaje masharti ya kutafuta uzima, na kwa sababu gani hivyo? (b) Je! njia ya ulimwengu ni ya uhuru wa kweli?

5 Karibu na mwisho wa hotuba yake juu ya huo mlima katika Galilaya, Yesu alionyesha mipaka ya wazi kwa wale wanaotafuta uzima, akisema: “Ingieni kwa kupitia mlango ulio mwembamba; maana mlango ni mpana, na njia ni pana iendayo upotevuni, nao ni wengi waingiao kwa mlango huo. Bali mlango ni mwembamba, na njia imesonga iendayo uzimani, nao waionao ni wachache.”’ (Mt. 7:13, 14) Usiache uvunjwe moyo na hili. Yesu hakusema kwamba ni mapenzi ya Mungu kwamba wachache tu waione. Wewe waweza kuwa kati ya wale wanaouona mlango huo uliowekewa mipaka na njia inayoongoza kwenye uzima, ikiwa u tayari kuyakubali masharti ya uanafunzi yaliyomo. (Luka 9:23, 24) Kwa ufupi, twaweza kuongeza kwamba njia ya ulimwengu, mwendo wa kujichagulia mtu atakayo na wa anasa, ingawa kwa kuonekana hauna mipaka, ‘mipana,’ kwa kweli ni mwendo wa utumwa, uliozungukwa na dhambi na choyo, ukielekeza kwenye kuvunjika moyo na uharibifu.​—Rum. 6:16, 21.

6. Ni onyo gani la mwisho alilolitoa Yesu, likitegemezwa na mfano gani wenye nguvu?

6 Mwishowe, tena akitilia mkazo haja ya utii na akionya juu ya shughuli tu ya kumtafuta Mungu, Yesu alisema: “Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni.” Alimalizia kwa mfano wenye nguvu, akiyaonyesha matokeo kwa mtu “asikiaye hayo maneno yangu, na kuyafanya,” na matokeo kwa mtu “asikiaye hayo maneno yangu asiyafanye.”​—Mt. 7:21-27; 15:7-9.

UFAHAMU UONGOZAO KWENYE AZIMIO

7. (a) Ni sifa gani zilizo za lazima katika kumtafuta Mungu, zikiongoza kwenye matokeo gani mema? (b) Hii ilionyeshwaje na Habili, Henoko na Nuhu?

7 Tukiwa na misemo hii ya Yesu akilini, twaweza kufahamu kwa njia bora zaidi kwamba katika kumtafuta Mungu lazima tuwe tayari na wenye kutaka kujipatanisha na matakwa yake yote. Imani na ibada ni vya lazima. Hizi si sifa za kuwazika tu. Zikikuzwa sawasawa, zitatuvuta tumkaribie Mungu katika ukamatano wa karibu pamoja naye, zikitufanya tutembee pamoja naye. Ndivyo ilivyokuwa kwa wale wanaume na wanawake wa imani wanaotajwa katika Waebrania, sura ya kumi na moja. Kama Habili, Henoko “alikuwa ameshuhudiwa kwamba amempendeza Mungu.” Halafu, Nuhu “kwa jinsi alivyomcha Mungu, aliunda safina, apate kuokoa nyumba yake.” Juu ya wanaume hawa, yasemekana kwamba wao ‘walitembea pamoja na Mungu wa kweli.’ Bila shaka, huwezi kuwa unamtafuta mtu ikiwa tayari unatembea na huyo, sivyo? Kwa wanaume hao kutafuta kulimalizwa, ingawa nyakati zote walijaribu kushika upendeleo wa Yehova na kibali. Mashahidi hao wote wa mbele ya Ukristo waliihakikisha imani yao na ibada kwa matendo yao, uaminifu wao na uvumilivu.​—Ebr. 11:5, 7; Mwa. 5:22; 6:9, NW; Yak. 2:17; 1 Yohana 3:18.

8. Ni ukweli gani unaotajwa katika Waebrania 11:6, nasi leo tunayo misingi yenye nguvu ya imani namna gani?

8 Ifikirie sana kweli ya msingi iliyosemwa na Paulo kwa habari ile ile: “Pasipo imani haiwezekani kumpendeza; kwa maana mtu amwendeaye Mungu lazima aamini kwamba yeye yuko, na kwamba huwapa thawabu wale wamtafutao.” (Ebr. 11:6) Kwa kweli, tunayo misingi yenye nguvu zaidi kupita mashahidi hao wa kwanza. Sisi tunalo Neno la Mungu lote pamoja na utajiri wake wa habari na maono. Vile vile tunayo maono mazuri ya mkutano mkubwa wa mashahidi wa kisasa kama yanavyotolewa katika Yearbook of Jehovah’s Witnesses cha kila mwaka. Zaidi ya hayo, twaweza kuona katika siku zetu utimizo wa unabii mwingi uliotolewa na Mungu ulioandikwa na watu waaminifu wa kale. Kama ilivyotabiriwa, ushuhuda wote waonyesha kwamba Kristo Yesu, Mfalme wa kimbinguni, alitawazwa mwaka wa 1914 C.E. Hii ni siku ambapo watu wa mataifa yote wanabaguliwa, kama vile mchungaji abaguavyo kondoo na mbuzi. Karibuni itakuja Har–​Magedoni, ikifuatwa na siku ya hukumu ya miaka 1,000 ambayo katika hiyo Mungu ‘atawahukumu walimwengu kwa haki’ kwa mtu aliyewekwa na kuahidiwa, Mwana wa Adamu. Twaishi katika siku iliyotazamiwa na Habili na Henoko, na iliyofananishwa na siku za Nuhu. Naye Yesu alisema kwamba, “mambo hayo yaanzapo kutokea, changamkeni, mkaviinue vichwa vyenu, kwa kuwa ukombozi wenu umekaribia . . . [kwa kuwa mwajua] ya kwamba ufalme wa Mungu u karibu.”​—Matendo 17:31; Luka 21:28-31; tazama vile vile Mwanzo 3:15; Mathayo 24:37-39; Yuda 14, 15; Ufunuo 20:1-3.

9. Yakobo anaikamatanishaje imani na saburi (uvumilivu), naye anatoa shauri gani zaidi?

9 Ili tuongeze ufahamu wetu, maoni yetu ya mambo bora, kusudi kwamba mioyo yetu ituchochee tuushike mwendo ufaao wa tendo, liangalie shauri lifaalo la Yakobo: “Ndugu zangu, hesabuni ya kuwa ni furaha tupu, mkiangukia katika majaribu mbalimbali; mkifahamu ya kuwa kujaribiwa kwa imani yenu huleta saburi.” ‘Ukiiruhusu saburi iwe na kazi kamilifu,’ itatokeza “taji ya uzima, Bwana aliyowaahidia wampendao.” Yakobo vile vile anatilia mkazo unyenyekevu na tendo la wazi katika kumtafuta Mungu: “Mungu huwapinga wajikuzao, bali huwapa neema wanyenyekevu. Basi mtiini Mungu. Mpingeni Shetani, naye atawakimbia. Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia ninyi.” Ili tupate wingi huo wa ufahamu, ukituchochea kwenye mwendo wa ibada isiyo ya kusita-sita, inahitaji uvumilivu, kama anavyoeleza Yakobo: “Mkulima hungoja mazao ya nchi yaliyo ya thamani, huvumilia kwa ajili yake hata yatakapopata mvua ya kwanza na ya mwisho. Nanyi vumilieni, mthibitishe mioyo yenu.”​—Yak. 1:2-4, 12; 4:6-8; 5:7, 8.

10. Mungu anatenda juu ya kanuni gani ya njia mbili, na kuelekea nani?

10 Yakobo hakuwa wa kwanza kuitaja kanuni ya njia mbili ambayo juu yake Mungu anatenda kwa kuwalaki njiani wale wanaotamani kumkaribia yeye, kama tuwezavyo kusema. Karne nyingi mapema, Daudi aliongozwa na roho ya Mungu kutoa faraja hii na onyo kwa mwanawe: “Nawe, Sulemani mwanangu, mjue Mungu wa baba yako, ukamtumikie kwa moyo mkamilifu, na kwa nia ya kumkubali; kwa kuwa [Yehova] hutafuta-tafuta mioyo yote . . . ukimtafuta, ataonekana nawe; ukimwacha, atakutupa milele.” Vivyo hivyo, Hanani mtabiri nyumaye alimwambia Mfalme Asa: “Kwa maana macho ya [Yehova] hukimbia-kimbia duniani mwote, ili ajionyeshe mwenye nguvu kwa ajili ya hao, waliokamilika moyo kuelekea kwake. Kwa hayo umetenda upumbavu [kwa kumtegemea mfalme wa Shamu mahali pa Yehova]; kwani tangu sasa utakuwa na vita.”​—1 Nya. (Sik.) 28:9; 2 Nya. (Sik.) 16:9.

11. Ni kwa namna gani na kwa sababu gani kanuni hii ya njia mbili yaweza kutenda kazi kwa njia ya pili?

11 Ndiyo, kanuni hii ya njia mbili yaweza kutenda kazi kwa njia ya pili. Kwa roho yake, nguvu yake ya utendaji isiyoonekana, Yehova anajifunua mwenyewe na kuonyesha nguvu zake kwa ajili ya wale walio na hali ifaayo ya moyo. Mungu, “ajuaye mioyo,” atawapa wale wamwulizao kwa unyofu roho takatifu yake. Lakini yeye aweza na ataiondoa roho yake ikiwa mtu anautoa moyo wake kutoka kwake Yeye, kama ilivyotukia kwa Sulemani. Kama ilivyoandikwa juu yake: “Ikawa, Sulemani alipokuwa mzee, wake zake wakamgeuza moyo wake, afuate miungu mingine, wala moyo wake haukuwa mkamilifu kwa [Yehova], Mungu wake, kama moyo wa Daudi baba yake.”​—Matendo 15:8; Luka 11:13; 1 Fal. 11:4.

12. (a) Nini kilichotiliwa mkazo katika maneno ya Mungu juu ya Sulemani, ikiongoza kwenye tendo gani jema? (b) Lakini nini kilichotokea mwishowe juu ya Sulemani, na kwa sababu gani?

12 Angalia mkazo unaowekwa juu ya umuhimu wa kuja kujua amri za Mungu na kukaa ndani kabisa ya mipaka yazo ya kitheokrasi. Mbele tu ya maneno yaliyonenwa katika 1 Mambo ya Nyakati (Siku) 28:9, Daudi alimwambia Sulemani Mungu alivyokuwa amesema kwake: “Ufalme wake [Sulemani] nitauweka imara milele, akijitia kwa bidii kuzitenda amri zangu na hukumu zangu, kama hivi leo,” kisha Daudi akaongeza ombi lake mwenyewe. Daudi alimalizia kwa kumpa mwanawe shauri hili lenye kuchochea: “Jihadhari basi; kwani [Yehova] amekuchagua wewe ili ujenge nyumba itakayokuwa mahali patakatifu; uwe hodari ukatende hivyo.” Yeye alilitimiza agizo hilo, lakini nyumaye akashindwa katika jaribu la maana sana la kuiweka ibada ya moyo ya kweli kwa Yehova. Kwa matokeo gani? “Kwa hiyo [Yehova] akamwambia Sulemani, Kwa kuwa umefanya hayo [kwa kufuata miungu mingine], wala hukuyashika maagizo yangu, na sheria zangu nilizokuamuru, hakika nitaurarua ufalme usiwe wako, nami nitampa mtumishi wako.”​—1 Nya. (Sik.) 28:7, 8, 10; 1 Fal. 11:9-11.

13. Kupitia kwa Malaki, Yehova alifanya ombi gani, na hii imekuwaje na utimizo mdogo na mkubwa?

13 Kwa Sulemani, kanuni ya njia mbili ilimalizika kwa njia ya pili, kwa aibu yake na suto. Lakini si lazima iwe hivyo. Kwa Israeli, ingawa katika siku za Malaki walikuwa na kumbukumbu refu katika hali ya kutopendwa, Yehova alilifanya ombi hili lenye uhakika na la moja kwa moja: “Tokea siku za baba zenu mmegeuka upande, mkayaacha maagizo yangu, wala hamkuyashika. Nirudieni mimi, nami nitawarudia ninyi.” Katika siku ya mwisho ya hukumu juu ya Israeli, mabaki yalirudi nao wakawa wanafunzi wa Yesu Masihi wao. Vivyo hivyo katika siku hii ya hukumu juu ya Kristendomu, ambayo ndiyo sehemu kubwa zaidi ya Babeli Mkuu, mabaki ya Wakristo wa kweli wametakaswa na kusafishwa nao wanaonekana kuwa mashahidi wa Kikristo wa Yehova. Angalia kinachowatofautisha. “Nao watakuwa wangu, asema [Yehova] wa majeshi, katika siku ile niifanyayo; naam, watakuwa hazina yangu hasa; . . . nanyi mtapambanua kati ya wenye haki na waovu, na kati ya yeye amtumikiaye Mungu na yeye asiyemtumikia.”​—Mal. 3:2-4, 7, 17, 18; tazama vile vile Luka 12:8, 9.

14. (a) Ni kazi gani njema ya kujenga iliyoanza katika Pentekoste ya mwaka wa 33 C.E.? (b) Ni mkusanyo gani wa ulimwenguni pote unaoendelea leo? (c) Kama ilivyoandikwa na Petro, ni mambo gani yaliyo ya lazima kwa ujenzi mzuri?

14 Kwa kweli Sulemani alikuwa na agizo zuri katika kulijenga hekalu, patakatifu pa Mungu, lakini sisi leo tunalo pendeleo kubwa hata zaidi. Majengo mengi ambayo Sulemani aliyasimamia yalikuwa yamejengwa kwa mbao na mawe. Lakini, tangu Pentekoste, mwaka wa 33 C.E., kundi la Kikristo linajulikana kama “jengo la Mungu.” “Kristo Yesu mwenyewe ni jiwe kuu la pembeni. Katika yeye jengo lote . . . [linakua] hata liwe hekalu takatifu . . . maskani ya Mungu katika [roho].” Lo! ni wazo bora namna gani la “jengo la Mungu,” lenye “mawe yaliyo hai”! Leo, mbali na mabaki ya kundi la Kikristo, Yehova ameanzisha mkusanyo wa ulimwenguni pote unamoweza kushiriki, matokeo yake yakiwa ni “mkutano mkubwa” unaosimama upande wa Mungu na ufalme wake, wakishirikiana sana na mabaki ya warithi wa Ufalme. Akimtaja Kristo Yesu kama ‘jiwe kuu lililo hai,’ Petro anataja kutoka unabii wa Isaya: “Bwana, [Yehova], asema hivi, Tazama, naweka jiwe katika Sayuni, liwe msingi, jiwe lililojaribiwa, jiwe la pembeni lenye thamani,... Nami nitafanya hukumu kuwa ndiyo [chenezo] na haki kuwa ndiyo timazi.” Ni jambo la muhimu namna gani kwamba tuishike mipaka iliyoonyeshwa na “chenezo” cha Mungu na “timazi” katika hii siku ya hukumu!​—1 Kor. 3:9, 17; Efe. 2:20-22; 1 Pet. 2:4-6; Isa. 28:16, 17.

HAKI​—MPAKA MKUU

15. Haki yaweza kufafanuliwaje, ikionyesha wazi sifa gani za Mungu?

15 Tofauti na taratibu mbovu ya mambo iliyopo, Petro anasema: “Kuna mbingu mpya na dunia mpya . . . na ndani ya hizi haki itakaa.” (2 Pet. 3:13, NW) Haki inasimulia kile kilicho kinyofu, chenye uadilifu na kilicho sawa. Lakini, machoni pa wanadamu na katika mambo yao kanuni ya yaliyo haki inatofautiana sana, na mara nyingi inavutwa, ikiwa si kuongozwa, na hila. Katika mapigano makali juu ya mipaka ya eneo kati ya mataifa, kila upande unadai kuwa katika haki, lakini matokeo ni kulingana na usemi wa kale kwamba ‘uwezo ni wenye haki.’ Sivyo ilivyo kwa Yehova wakati wo wote. Kweli, yeye ndiye “Mungu Mwenye Nguvu Zote.” Vile vile yeye ni mwenye hekima sana. Kwa kweli, sifa zake zote zinapita nyingine zote nazo zimesawazika vizuri sana. Haki yake, hata hivyo, inaonyeshwa zaidi katika upendo wake na uadilifu. Yeye ndiye “Mwamba, kazi yake ni kamilifu; maana, njia zake zote ni haki. Mungu wa uaminifu, asiye na uovu, yeye ndiye mwenye haki na adili.” Enzi yake yote, zaidi kama inavyokamatana na ufalme wake chini ya Kristo, ambaye aliutoa uhai wake kama ukombozi, inautukuza upendo wa Mungu na uadilifu kwa njia ya ajabu.​—Ufu. 16:14, NW; Kum. 32:4; tazama vile vile Malaki 3:6.

16. (a) Je! yawezekana kupatanisha maisha zetu na kanuni ya Mungu, na kwa njia gani hivyo? (b) Mungu amefanya mpango gani mzuri kutusaidia tuendelee kuwa ndani ya mipaka ifaayo?

16 Kwa kadiri tunavyofahamu hivi, ndivyo mioyo yetu inavyovutwa katika shukrani nyingi sana, ikitusukuma tupatanishe maisha zetu wenyewe na kanuni ile ile. Kama alivyosema Paulo: “Na mfanywe wapya katika roho ya nia zenu; mkavae utu mpya, ulioumbwa kwa namna ya Mungu katika haki na utakatifu wa kweli.” Zaidi juu ya upendo, kumbuka kwamba umewekwa kwetu kama sheria na amri, si mwaliko tu. (Efe. 4:23, 24; tazama vile vile Mathayo 22:36-40; Yohana 13:34; Yakobo 2:8; 1 Yohana 4:7-12.) Ili akusaidie na kukuongoza katika hili, Yehova amewakusanya watu wake katika umoja wenye kufungamana sana, sawa na kukaa katika mji wa nyakati za Biblia, uliozungukwa na ukuta wenye nguvu kwa ulinzi. Hii inasimuliwa vizuri katika Isaya 26:1-4, 7: “Sisi tunao mji ulio na nguvu; ataamuru wokovu kuwa kuta na maboma. Wekeni wazi malango yake, taifa lenye haki, lishikalo kweli, liingie. . . . Mtumainini [Yehova] sikuzote, maana [Yehova] YEHOVA ni mwamba wa milele. Njia yake mwenye haki ni unyofu; wewe uliye mnyofu wainyosha njia ya mwenye haki.”​—Tazama vile vile Ufunuo 22:15-21.

17. Tukiona kwamba kanuni i juu kupita kadiri, Neno la Mungu linatoaje msaada na faraja?

17 Pengine unajisikia kuvunjika moyo kwa kadiri fulani, ukiona kwamba kanuni i juu mno kwako mwenyewe. Huenda ukasema unajijua namna ulivyo kupita kadiri. Ikiwa ndivyo, usisahau kwamba Yehova anakujua wewe vema zaidi kupita ujijuavyo. “Kama vile baba awahurumiavyo watoto wake, ndivyo [Yehova] anavyowahurumia wamchao. Kwa maana Yeye anatujua umbo letu, na kukumbuka ya kuwa sisi tu mavumbi.” Wingi wa ugumu, hata wingi wa uovu, unaletwa zaidi na kutojali kwa kusudi la Mungu na misaada ya fadhili. Je! wayakumbuka maneno ya Paulo kwa Baraza ya Areopago juu ya hili? “Zamani zile za ujinga Mungu alijifanya kama hazioni; bali sasa anawaagiza watu wote wa kila mahali watubu.” Haya si maneno yasiyo na maana. Wakati wa ujinga umepita; wakati wa kutubu huu. Mara nyingi Maandiko yanaonyesha kwamba katika mchanganuo wa mwisho, si shauri la wajibu wa mtu mwenyewe tu lililoko, lakini vile vile uwezekano wa kufanya uchaguzi wa mtu mwenyewe. Kumbukumbu lako lililopita na utu huenda vikafunua mambo ya ndani ambayo katika hayo u mlegevu, au hata mambo mabaya zaidi, unayoona hayawezi yakazuiwa. Lakini, kwa kuwa nyakati nyingi Mungu amewasihi hata waovu inaonyesha kwamba hakuna shauri la ye yote lisiloweza kuponyeka, isipokuwa kama mtu amempinga Mungu na kanuni zake kwa makusudi, bila ya kusikitikia kutojali ama kuonyesha toba. Onyo na ombi la Mungu kwa Kaini vyaonyesha kwamba wakati huo angaliweza kujirudisha mwenyewe, zaidi kama angeomba msaada.​—Zab. 103:13, 14; Matendo 17:30; Mwa. 4:6, 7.

18. Pamoja na wajibu wa mtu mwenyewe, ni maombi gani yanayofanywa kwa waovu katika unabii wa Ezekieli?

18 Katika unabii wote wa Ezekieli, sura ya 18 wajibu wa mtu mwenyewe unatiliwa mkazo. “Nafsi itendayo dhambi​—hiyo yenyewe ndiyo itakayokufa.” Ombi linalorudiwa-rudiwa vile vile linafanywa “kwa habari ya mtu mwovu, kama akigeuka kutoka kwa dhambi zake zote alizozitenda naye kwa kweli azishike sheria zangu zote na kutimiliza uadilifu na haki, kwa hakika yeye ataendelea kuishi. Hatakufa.” Ombi linalofanana lilifanywa kwa taifa: “‘Geukeni, naam, geukeni kutoka kwa makosa yenu yote, . . . nanyi mjifanyie moyo mpya na roho mpya . . . Kwa maana mimi sifurahii hata kidogo kifo cha mtu anayekufa,’ ndio usemi wa Bwana Yehova Mwenye Enzi Yote. ‘Kwa hiyo geukeni nanyi mwendelee kuishi, Enyi watu.’”​—Eze. 18:4, 20, 21, 27, 30-32; 33:11, 14-19, NW; tazama vile vile Yoeli 2:12-14.

19. Ni wajibu gani na uwezekano ulioko juu ya kila mmoja wetu, nalo kumbukumbu la Paulo mwenyewe latusaidiaje katika habari hii?

19 Kama ilivyoangaliwa mapema, kanuni ile ile yaweza kutenda kazi kwa njia ya pili. (Eze. 18:26) Katika njia yo yote, uchaguzi na wajibu vipo. Waweza kufanya uchaguzi mzuri, ufaao, na kuwa na mwanzo mzuri ‘umtafute Mungu, ikiwa watamani kupapasa-papasa ukamwone.’ Yeye hayuko mbali. Je! ulijua kwamba Paulo anajitia mwenyewe katika maandishi kama mfano wa kushangaza wa mtu aliyekuwa na kumbukumbu baya sana kwa habari ya utu wake wa kwanza na matendo, lakini ambaye, kama asemavyo, “nalipata rehema kwa kuwa nalitenda hivyo kwa ujinga”?​—Matendo 17:27; 1 Tim. 1:12-16; Gal. 1:13.

20. Yesu aliutiliaje mkazo uwezekano uu huu na wajibu?

20 Habari ile ile yenye rehema imo katika maneno ya Yesu katika Yohana 3:16-19: “Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, . . . [si] auhukumu [aulaani] ulimwengu, bali ulimwengu uokolewe katika yeye.” Hayo hayakusemwa kwa mzaha. Ulikuwa uwezekano wa kweli. Yesu alikuwa ndiye “Nuru halisi, amtiaye nuru kila mtu.” Lakini, kama alivyosema Yesu: “Watu wakapenda giza kuliko nuru; kwa maana matendo yao yalikuwa maovu.” Huo ndio uliokuwa uchaguzi wao. Walipendelea kukaa namna hiyo.​—Yohana 1:9.

21. Kizazi cha wale wanaomtafuta Yehova kinasimuliwaje katika Zaburi 24:3-6?

21 Kwa upande wako, sababu gani usijiunge na kizazi kinachosimuliwa katika Zaburi 24:3-6? “Ni nani atakayepanda katika mlima wa [Yehova]? Ni nani atakayesimama katika patakatifu pake? Mtu aliye na mikono safi na moyo mweupe, asiyeiinua nafsi yake kwa ubatili, wala hakuapa kwa hila. Atapokea baraka kwa [Yehova], na haki kwa Mungu wa wokovu wake. Hiki ndicho kizazi cha wamtafutao, wakutafutao uso wako, Ee Mungu wa Yakobo.”

22. Ni ombi gani jema linalosemwa katika Isaya 55:6, 7?

22 Kwa sababu gani usiliitikie ombi kama lilivyosemwa katika Isaya 55:6, 7? “Mtafuteni [Yehova], maadamu anapatikana, mwiteni, maadamu yu karibu; mtu mbaya na aache njia yake, na mtu asiye haki aache mawazo yake; na amrudie [Yehova], naye atamrehemu; na arejee kwa Mungu wetu, naye atamsamehe kabisa.” Haya yaweza kuwa maono yako na baraka.

​—Kutoka The Watchtower, July 15, 1973.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki