Kwa Nini Ufurahi Yajapokuwa Magumu ya Kipekee?
1, 2. (a) Wale wanaoweza kufurahi penye Har–Magedoni wanaitwa nini? (b) Ni wonyesho gani wa uwezo upitao wa mwanadamu wa kutumia maji kwa upande wa Yehova ambao sasa Habakuki anasimulia?
WENYE baraka ni wale watakaoweza kufurahi penye Har–Magedoni yajapokuwa magumu ya kipekee yatakayowapata wakati huo. Mwishowe Habakuki anaionyesha sababu ya kufurahi huko anapoendelea mbele na sala yake ya unabii. Akiwa angali anayasimulia matendo hodari ya Yehova Mungu wakati Yeye anapoingia katika “vita ya siku ile kuu ya Mungu Mwenyezi” penye Har–Magedoni, nabii anasema:
2 “Je! [Yehova] aliikasirikia mito? Je! hasira yako ilikuwa juu ya mito, au ghadhabu yako juu ya bahari, hata ukapanda farasi zako, katika magari yako ya wokovu? Uta wako ukafanywa wazi kabisa; viapo walivyopewa kabila vilikuwa neno thabiti; ukaipasua nchi kwa mito. Milima ilikuona, ikaogopa; gharika ya maji ikapita; vilindi vikatoa sauti yake, vikainua juu mikono yake. Jua na mwezi vikasimama makaoni mwao; mbele ya nuru ya mishale yako ilipotapakaa, mbele ya mwangaza wa mkuki wako umeremetao.”—Hab. 3:8-11.
3. Katika mwaka wa 1513 na wa 1473 B.C.E., Yehova alionyeshaje kwamba vitu kama bahari na mto si kizuizi kwake Yeye?
3 Si kwamba tu vizuizi vyenye mfano wa mlima vinashindwa kumzuia Yehova katika mwendo wake, lakini vile vile vitu vinavyoelekea kuwa visivyovukika kama vile mito na bahari vinashindwa. Mwaka wa 1513 B.C.E. Bahari ya Shamu ilijifunza uhakika huo, Yehova alipoyagawanya maji yake kutoka mashariki hata magharibi ili awapitishe watu wake waliokombolewa wakiwa salama katika pwani za Mkono wa Nchi wa Sinai. Mwaka wa 1473 B.C.E. Mto Yordani wenye kufurika ulifunzwa uhakika ule ule wakati ambapo Mungu Mwenye Nguvu Zote alipoyatenga mafuriko yake tokea kaskazini na kulikausha bonde la mto ili watu wake wakiwa chini ya Jemadari Yoshua wavuke na mwishowe kuingia katika Nchi ya Ahadi. Kwa sababu ya tendo hilo juu ya maji yenye kuzuia, nabii angeweza kuuliza vile vile kama ghadhabu na hasira vilikuwa juu ya mito na bahari. Ijapokuwa Farao wa Misri na wapanda farasi wake na magari ya vita walimezwa kabisa katika jaribio la kuvuka Bahari ya Shamu, Yehova na majeshi yake ya kimbinguni, wakiwa wamepanda kana kwamba ilikuwa farasi za vita, wanajitumbukiza ndani kabisa na kujipenyeza katika kitu cho chote kama mito na bahari kinachoelekea kufunga njia. Magari yake ya vita ya mfano, mahali pa kuwapeleka waendeshaji wake kwenye kaburi lenye maji, yanawapeleka wapandaji kwenye wokovu, kwenye ushindi!
4. Mungu awezaje kuipasua dunia kwa mito na kufanya vilindi viiinue “mikono” yavyo juu?
4 Lo! hili linatia nguvu imani ya mabaki yaliyotiwa mafuta ya Yehova ya Israeli wa kiroho kama nini leo, ambao, kama makabila ya Israeli wa kale, wako chini ya viapo kwake Yeye, kupitia kwa agano jipya na Yeye kama lilivyopatanishwa kupitia kwa Mwanawe Yesu Kristo! Wao wanajua kwamba mafuriko ya mfano yako chini ya amri ya Muumba kuipasua dunia na kuwagharikisha maadui, kama vile katika siku za Mwamuzi Baraka na nabii wa kike Debora. Maji kutoka angani juu yaweza kumiminika chini kwa ngurumo. Tofauti na maji yanayomwagika kutoka juu, maji ya vilindi chini ya dunia yaweza kufanywa yaruke juu sana, kana kwamba vilindi vilikuwa vikiinua mikono yake juu vishiriki katika uharibifu wa maadui.—Hab. 3:9, 10.
5. Habakuki 3:11 anazifananishaje silaha tukufu mno za vita za Yehova?
5 Milima inapogaa-gaa kana kwamba katika maumivu makali, Yehova anajionyesha kama shujaa wa vita kwa silaha za vita zilizo kali kupita zile za wanadamu. Mishale yake ya kifo yenye mabawa na njia yake ya kuisukumia mbele si mishale wala upinde uliotengenezwa na mwanadamu. Haitaachwa imefunikwa, kufichwa, kana kwamba katika kifuniko cha upinde na podo. Radi zenye kunguruma na umeme wenye kuwaka-waka vimo katika ghala yake ya silaha za kimungu. Kwa sababu ya kuwaka-waka kwa njia ya Mungu ya kufisha maadui wake nuru itakuwa nyingi sana mchana na usiku, hata jua la kawaida na mwezi, kana kwamba ilikuwa, vitajisikia havihitajiwi kwa kumulika. Itakuwa kana kwamba ‘vilisimama,’ visitende kama mianga, lakini vikiacha mishale miangavu ya Yehova ionyeshe uwezo wa kumulika. Kuongezea kwa tamasha ya kuogofya ya mishale ya uharibifu yenye kuwaka-waka ikisafiri kasi, silaha kubwa zaidi ya Yehova, kama mkuki, itatupwa ikipita kasi kasi hewani na kuongezea uangavu kwa umeme wake. Ebu wazia matokeo juu ya akili ya tendo hilo la vita juu ya maadui wa Yehova na wa watu wake!
WATU AMBAO KWA AJILI YAO VITA YAPIGANWA
6. Ni onyo gani ambalo yamepaswa mataifa yapate kwa habari ya wale watakaookolewa penye Har–Magedoni?
6 Acha mataifa ya dunia yapate onyo. Watu wale wale ambao wao wamewafanya “vyombo vya chuki ya mataifa yote” kwa makumi ya miaka ndio ambao Yehova ataokoa penye Har–Magedoni, huku mataifa hayo yenyewe yakitaabika kwa sababu ya kuwachukia wale ambao Yeye anawapenda. Akiongozwa na roho ya Mungu, nabii Habakuki anaonyesha hili wazi, anapoendelea kusema: “Ulikwenda katikati ya nchi kwa ghadhabu; ukawapura mataifa kwa hasira. Ukatokea kwa ajili ya wokovu wa [mtiwa mafuta] wako: ukakiponda kichwa cha nyumba ya waovu, ukiuweka wazi msingi hata mwambani.”—Hab. 3:12, 13; Mt. 24:9, NW.
7, 8. (a) Ni nyuma ya tukio gani kuu la kidini ambapo wokovu huu utatokea? (b) Yehova ataufanya wokovu huu ili ahifadhi nini duniani, naye atayatendeaje mataifa?
7 Hivyo waabudu wa Yehova Mungu wanaweza kuwa na matumaini kwamba Yeye atakuja awasaidie penye Har–Magedoni. Wao ndio watakaoshambuliwa na mataifa yote ya kilimwengu. Kama vile kitabu cha Ufunuo, sura ya kumi na saba mpaka ya kumi na tisa, kinavyoonyesha, hii itakuwa nyuma ya uharibifu wenye kushangaza wa yule kahaba wa mataifa yote, Babeli Mkuu, milki ya ulimwengu ya dini ya uongo, kutia ndani na Kristendomu. Waabudu wa Yehova waliotoka utumwani mwa milki hiyo ya kidini ya Kibabeli, watahifadhiwa hai waupite kabisa uharibifu wa Kristendomu na sehemu nyingine yote ya Babeli Mkuu.
8 Ndipo mataifa yasiyotaka dini yatakayokuwa yameuleta uharibifu huu yatakaposhughulikia kuifutilia mbali ibada safi ya Mungu aliye wa pekee aishiye na wa kweli, Yehova, itoke duniani. Ili asiyaruhusu mataifa yasiyomcha Mungu yafaulu katika hili, itampasa Yehova kuondoka akawaokoe ‘watu wake.’ Kwa hiyo katika “ghadhabu” juu ya mataifa yenye nia mbovu Yeye atapita katika dunia na kwa hasira ayapure mataifa, akiyaponda-ponda mguuni pake kama nafaka katika sakafu ya kupuria.
9, 10. N’nani ‘mtiwa mafuta’ ambaye Yehova anaondoka akamwokoe?
9 ‘Mtiwa mafuta’ ambaye Yehova anaondoka akamwokoe si Mwanawe aliyetukuzwa, Yesu Masihi au Mtiwa Mafuta. Ufunuo 17:14 na 19:11-16 waonyesha wazi kwamba Yesu Kristo hahitaji wokovu wo wote kutoka kwa mataifa ya kidunia, bali yeye anayaongoza majeshi ya malaika wa kimbinguni kuyaelekea mataifa yanayowashambulia “watu” wa Yehova penye Har–Magedoni. “Watu” hawa ndio mabaki ya wanafunzi waliotiwa mafuta wa Yesu Kristo, nao, wakiwa pamoja, washiriki hawa waliotiwa mafuta na kuzaliwa kwa roho wa Israeli wa kiroho wanamfanyiza ‘mtiwa mafuta’ wa Yehova penye Har–Magedoni. Kama ilivyoandikwa katika Zaburi 28:8, 9, kwa unabii, juu ya Israeli wa kiroho:
10 “[Yehova] ni nguvu za watu wake, naye ni ngome ya wokovu kwa [mtiwa mafuta] wake. Uwaokoe watu wako, uubariki urithi wako, uwachunge, uwachukue milele.”—Tazama vile vile 1 Yohana 2:20, 27; 2 Wakorintho 1:21.
11. N’nani mwingine duniani atakayeokolewa pamoja na ‘mtiwa mafuta’ penye Har–Magedoni?
11 Pamoja na ‘mtiwa mafuta’ wa Yehova kutakuwako “mkutano mkubwa” wa waabudu wenzao watakaookolewa penye Har–Magedoni. Hawa nao watakuwa wamekwisha kimbia kutoka milki ya ulimwengu ya dini ya uongo ya Kibabeli mbele ya uharibifu wa Babeli Mkuu. Wajapokuwa si wa Waisraeli wa kiroho wanaomfanyiza ‘mtiwa mafuta’ wa Yehova, wao wataungana na ‘mtiwa mafuta’ katika kumwabudu na kumtumikia Yehova penye hekalu lake la kiroho. Ufunuo 7:9-15 watuhakikishia kwamba wataiokoka “dhiki kubwa.”
12. Lakini, n’nini kitakachotukia kwa “nyumba ya waovu”?
12 Tofauti kabisa na wokovu wa ‘mtiwa mafuta’ na “mkutano mkubwa” kutakuwako uharibifu kamili wa “nyumba ya waovu.” Kama vile nyumba iliyobomolewa na kuharibiwa kutokea darini mpaka msingi, taratibu mbovu ya mambo waliyoisimamisha chini ya uongozi usioonekana wa Shetani Ibilisi itavunjwa-vunjwa. Wakuu wa “nyumba” hii ya mataifa yote watapondwa, watavunjwa-vunjwa, nao wale wafanyizao msingi wa jengo la ulimwenguni pote watabomolewa hata chini, usiachwe hata “msingi” wa jengo jipya. Msingi utabomolewa, ukiachwa katika hali ya kuharibika. “Nyumba ya waovu” haitaonekana tena duniani.
13, 14. (a) Anapozungumza juu ya mataifa wakija kama kisulisuli ili “kunitawanya,” Habakuki anazungumza juu ya nani? (b) Ni nani “maskini” ambaye mataifa yanatazamia kummeza kwa furaha nyingi katika mahali pa siri?
13 Katika uwanja wa vita wa Har–Magedoni maadui wenye kutukuza taifa wa ‘mtiwa mafuta’ wa Yehova watatupwa katika bumbuazi ya kujiua wenyewe. Katika njozi ya unabii juu ya hili, nabii Habakuki katika sala anamwambia Yehova hivi kama Shujaa wa Vita: “Ukakichoma kichwa cha mashujaa wake kwa fimbo zao wenyewe; wakaja kama kisulisuli ili kunitawanya; kama wakifurahi kuwameza maskini kwa siri. Ukaikanyaga bahari kwa farasi zako, chungu ya maji yenye nguvu.”—Hab. 3:14, 15.
14 Anapozungumza juu ya jaribio la mataifa yote la “kunitawanya” kwa nguvu za kisulisuli, Habakuki anasema juu yake mwenyewe kama anayemfananisha ‘mtiwa mafuta’ wa Yehova, watu Wake wanaohitaji kuokolewa kutoka kwa washambuliaji. Kama wanyang’anyi wanaolala wamejificha wakingoja mateka, mataifa yaliyokusanyika yamejipanga safusafu penye Har–Magedoni watamrukia ‘mtiwa mafuta’ wa Yehova na “mkutano mkubwa” wa waabudu wenzao wawaharibu hawa wote kama walivyomharibu Babeli Mkuu wa kidini. “Maskini” ambaye wanatazamia kummeza kwa furaha nyingi katika ‘mahali pao pa siri’ ni ‘mtiwa mafuta’ wa Yehova, ambaye mataifa ya kilimwengu yamemsumbua sikuzote kwa kuwachukia waabudu wa Yehova. Lakini mahali pao pa siri hapafichiki kwa Yehova Mungu.
15. (a) Ni kwa njia gani ambavyo vichwa vya mashujaa wa mwovu vinavyochomwa “kwa fimbo zao wenyewe” na Yehova? (b) Uharibifu wa majeshi ya adui utakamilishwaje na Yehova?
15 Yehova hatazukiwa kwa ghafula. Yeye hatamwongoza ‘mtiwa mafuta’ wake na wenzi wao waaminifu katika mtego wo wote wa adui. Wakati mataifa yenye kumpinga Mungu yatakapovuma sana kama kisulisuli yawatawanye wazoeao dini iliyo ya kweli na safi, Mungu Mwenye Nguvu Zote atazielekeza silaha za mataifa yenye kushambulia juu yao wenyewe wapigane wao kwa wao. (Zek. 14:13; 2 Nya. (Sik.) 20:22-24) Lakini, Mungu Mwenye Nguvu Zote atafanya mengi zaidi kuliko tu kuwafanya maadui wa mataifa yote watumie fimbo zao za kijeshi kuvichoma vichwa vya mashujaa wao wenyewe. Yeye mwenyewe vile vile atatumia majeshi yenye nguvu kupita zile za mwanadamu kwa amri Yake yaukamilishe uharibifu. “Farasi” za majeshi yake ya kimbinguni wakiwa chini ya Yesu Kristo, yeye atasonga mbele kwa ushindi kupita katika “bahari” na “chungu ya maji yenye nguvu” ya maadui yenye kunguruma na kusukasuka. Hivyo watu Wake mwenyewe hawatagharikishwa katika uharibifu penye Har–Magedoni. Wao watakuwa washuhudiaji wa ushindi wa Yehova ulio mtukufu mno!
KUINGOJA “IIE SIKU YA DHIKI” KWA UNYAMAVU
16. Taraja la itakachomaanisha Har–Magedoni kwa watu linatufanya tuwe namna gani, kama inavyoonyeshwa na matokeo ya “habari” juu ya Habakuki mwenyewe?
16 Leo tunapoitazamia “vita ya siku ile kuu ya Mungu Mwenyezi” inayokuja penye Har–Magedoni, hatusahau itakachomaanisha kwa habari ya hali za maisha za watu, zaidi za wale wenye kushambuliwa na mataifa yaliyo hatari sana. Kwa hiyo, taraja lililo hakika la magumu linakuwa kubwa zaidi na zaidi kwetu na kutufanya wenye kuwaza sana. Angalia namna ambavyo nabii Habakuki alivyojisikia alipoiona njozi ya unabii ya wakati huo wa kutisha. Yeye anasema: “Nikasikia, na tumbo langu likatetemeka, midomo yangu ikatikisika kwa sauti ile; ubovu ukaingia mifupani mwangu, nikatetemeka katika mahali pangu; ili nipate kuingoja ile siku ya dhiki [kwa unyamavu], kundi lao washambuliao wakweapo juu ya watu.”—Hab. 3:16.
17. (a) Fadhaa ya Habakuki kwa sababu ya zile “habari” ilimsukuma kufanya nini, na kwa nini? (b) Yawapasa mabaki na “kutano mkubwa” watendeje leo kama matokeo ya zile “habari”?
17 Alipozifikiria habari tu juu ya “ile siku ya dhiki” inayokuja katika maana yake yote yenye kutuliza, kama zilivyoandikwa katika Habakuki 3:2-15, nabii alijisikia kana kwamba alikuwa karibu kuzimia. Mifupa yake ilielekea kuyeyuka kwa kuoza, bila ya kuwa na maungo yenye nguvu kuusimamisha mwili wake wima; mwili wake wote ulitetemeka; midomo yake haikuweza kusema lo lote, ila kutikisika tu. Hali yake kweli ilikuwa ya fadhaa hata mbele ya kufika kwenyewe kwa “ile siku ya dhiki” yenye kuogofya. Lakini je! fadhaa yake ilimsukuma ajiue kama njia ya kuepukia, au kutumia dawa za kulevya apoteze fahamu? Hapana! Fadhaa yake ililetwa na Mungu kwa habari zilizoongozwa na roho yake alizopewa kama nabii. Kwa hiyo fadhaa yake ilimpata ilivyofaa, kwa upande uliofaa, yaani, “ili nipate kuingoja ile siku ya dhiki [kwa unyamavu].” Hivi ndivyo imewapasa mabaki ya Waisraeli wa kiroho kutenda leo, na vile vile “mkutano mkubwa” wa wenzi waaminifu, wanapouona ushuhuda wa kwamba “ile siku ya dhiki” yenye kuogofya inakaribia zaidi katika kizazi hiki. Yawapasa kuzidi kuwa watulivu na kungoja.
18, 19. (a) “Ile siku ya dhiki” italetwa kwa ajili ya nani? (b) Siku hii yafananishwaje na mtu, kwa matokeo gani kwa “watu”?
18 Yawapasa kuangalia kwamba Habakuki hasemi kwamba “ile siku ya dhiki” ni kwa ajili ya watu wa Yehova, ‘mtiwa mafuta’ Wake. Habakuki alisema kwamba yeye mwenyewe angeingoja kwa unyamavu “ile siku ya dhiki” ije kutoka kwa Yehova “juu ya watu,” au, kwa njia halisi, “juu ya kundi la watu.” Katika Maandiko ya Kiebrania neno “watu” mara nyingi latumiwa kwa jeshi, kama vile katika unabii wa Danieli 9:26. Kwa hiyo “watu” ambao kwa ajili yao “ile siku ya dhiki” yatayarishwa ni jeshi lenye kushindana la mataifa yanayomshambulia ‘mtiwa mafuta’ wa Yehova penye Har–Magedoni. ‘Siku hiyo ya dhiki’ itawapambazukia “watu” hao au jeshi lenye kumpinga Mungu.
19 Kwa kuwa “watu” hao wenye kushindana wanakusudia kumshambulia ‘mtiwa mafuta’ wa Yehova penye Har–Magedoni, “ile siku ya dhiki” kutoka kwa Yehova itakuwa kama mshambuliaji atakayewashambulia “watu” wenye silaha. Hivyo “ile siku ya dhiki” yafananishwa na mtu anayekuja juu ya watu au jeshi la maadui ‘awashambulie.’ (Hab. 3:16) Kama vile Jewish Publication Society Version inavyosema: “Ili nipate kuingoja siku ya taabu, wakati atakapokuja juu ya watu anaowashambulia.” Hii itamaanisha uharibifu kwa “watu” walio maadui.
20. (a) Sikuzote vita inaleta hali za namna gani, na zaidi kwa akina nani? (b) Kwa hiyo ni hali gani mbaya ya uchumi ambayo Habakuki anasimulia, na je! anaisimulia kama inayoweza kutokea au itakayotokea?
20 Sikuzote vita inaleta hali ngumu kwa wale waliomo, zaidi kwa wale wanaoshambuliwa. “Vita ya siku ile kuu ya Mungu Mwenyezi” penye Har–Magedoni yaweza kutazamiwa kuleta magumu kwa wale watakaokuwa wakishambuliwa wakati huo na maadui walioungana wa waabudu wa Yehova. Haikuwa kama uwezekano tu wa kutokea kwa magumu hayo kwamba nabii Habakuki akazungumza juu ya jambo hilo, akisema: “Ujapokuwa mtini wenyewe usichanue, na kusiwe na mazao katika mizabibu; kazi ya mzeituni ikiwa bure, na sehemu zilizoinuka zenyewe zisipozaa chakula; kundi likifarakishwa na zizi, na kusiwepo kundi la mifugo mabomani; hata hivyo, kwangu mimi, mimi nitamfurahia Yehova mwenyewe; mimi nitamshangilia Mungu wa wokovu wangu.” (Hab. 3:17, 18, NW) Habakuki analizungumza hili kama jambo litakalotukia hasa.
21. Habakuki aliona katika njozi kwamba hali hizo ngumu sana za uchumi zitawapata akina nani, na kwa sababu ya nini?
21 Kwa unabii Habakuki aliona katika njozi ugumu wa uchumi kwa ‘mtiwa mafuta’ wa Yehova kwa sababu ya jaribio la mataifa yote la kuwatawanya waabudu wa Yehova. Ilionekana kana kwamba hawa hawakuwa na kitu cha kula. Ilionekana kana kwamba wasingeokoka!
22. (a) Kulingana na unabii Wake mbalimbali, Yehova atachukua hatua kwa kutumia nini juu ya maadui wake wakati wa “dhiki kubwa”? (b) Kwa sababu gani waabudu Wake hawawezi wakatazamia kutendewa vema na kupata ondoleo la masumbufu ya ulimwenguni pote?
22 Hata leo, katika huu “wakati wa mwisho,” wakati ambapo njaa kubwa, magonjwa ya kipuku, na matetemeko ya ardhi na vita vya mataifa yote vinapowaua wakaaji wengi wa dunia hata mbele ya kutokea kwa “dhiki kubwa,” hali za uchumi na nyingine za maisha ya wanadamu wote zinaleta ugumu kwa watu zaidi na zaidi. Hata mnamo “dhiki kubwa” yenyewe, kulingana na unabii Wake mwenyewe, Yehova Mungu atachukua hatua juu ya maadui wake wa kidunia kwa pigo, matetemeko ya ardhi na nguvu nyingine za asili ambazo maadui wake Yeye hawawezi kupigana nazo kwa makombora yao ya atomiki na mipango ya uchumi na utabibu. N’nani awezaye kuokoka asipatwe kwa kadiri fulani? Ni kweli kwamba mabaki yaliyotiwa mafuta na roho wa Waisraeli wa kiroho na “mkutano mkubwa” wanaoshirikiana nao, kama Yesu, “si sehemu ya ulimwengu,” na hali wao ‘wamo ulimwenguni’ nao hawana la kufanya ila kupatwa na magumu kwa sababu ya hali za ulimwengu. Zaidi ya hayo, kama “vyombo vya chuki” ya mataifa yote na watu, wao hawawezi kutazamia kutendewa vema na kupata maondoleo ya masumbufu ya ulimwenguni pote.—Yohana 15:19; 17:11, NW.
23. “Mamlaka zilizo kuu” zitageuka kutoka wahudumu wa Mungu wa faida ziwe nini, nalo hili litakuwa na matokeo gani juu ya mashahidi wa Yehova?
23 Hata hivyo, namna gani wakati mataifa, yakiisha kufikiliza kisasi chao juu ya Babeli Mkuu, yatakaposongamana pamoja katika vita kamili juu ya waabudu wa Yehova wenye kuokoka ili yawatawanye na kuwameza? “Mamlaka zilizo kuu” za ulimwengu huu hazitatumikia tena kama ‘mhudumu wa Mungu’ kwa ajili ya faida ya mashahidi wa Yehova wa Kikristo. (Rum. 13:1-4, NW) Njia yao ya kuwatumikia watu wote itavunjika au kuharibiwa kabisa. Zaidi ya kushindwa kama ‘wahudumu wa Mungu’ kwa habari hii, sasa watajifanya wenyewe wafanya vita na Yehova Mungu kwa kuwashambulia watu wake wakiwa wameungana, hivyo wakiichochea vita ya Har–Magedoni. Bila shaka, hali za uchumi na maisha na uhuru wa kipekee wa mashahidi wa Yehova wa Kikristo zitakuwa hafifu. Wao watakutana barabara na uharibifu! Loo! magumu yatakayokuwapo wakati huo!
24. Ni maulizo gani yanayotokea juu ya mwenendo wa mashahidi wa Yehova wakati huo, lakini Habakuki anawajibiaje kwa unabii?
24 Je! wao watashikwa na hofu ya ghafula? Je! watashindwa na maadui wenye kushambulia na kuikana imani yao na kuacha kuwa mashahidi wa Yehova wa Kikristo? Au, watakata tumaini na kulegea na kufa kwa kiroho? Hapana! anajibu Habakuki akiwasemea kwa unabii. Yajapokuwa magumu haya yote waliyoletewa kwa sababu ya uaminifu wao kwa Mungu aliye wa pekee aishiye na wa kweli, mashahidi wa Yehova wa Kikristo watapiga kelele: “Hata hivyo, kwangu mimi, mimi nitamfurahia Yehova mwenyewe; mimi nitamshangilia Mungu wa wokovu wangu.”—Hab. 3:18, NW.
25. Wakati huo Yehova atajishuhudiaje kama Mwokozi, na ni akina nani duniani watakaoona akiishuhudia enzi yake yote?
25 Mungu wao, Yehova, ni Mungu wa wokovu, naye atawaokoa. Yehova atajishuhudia mwenyewe kama Mwokozi wao na Mkombozi. Watakapoelekea kuwamo katika hali mbaya kabisa na kuelekea kukomeshwa, “ile siku ya dhiki” itawazukia watesi wao na washambuliaji. Itawaingilia kwa ghafula kama mshambuliaji, kwa maana wakati huo Yehova atatokea akiwa na malaika wake wa kimbinguni wakiwa chini ya amri ya Yesu Kristo naye atawaokoa mashahidi wake waaminifu duniani. Watakuwa mashahidi wa Yehova kwa njia nyingine zaidi, watakapomwona akiwaharibu maadui wake wote duniani na kuishuhudia enzi yake yote ya ulimwengu wote.
26. (a) Kulingana na maneno ya mwisho ya Habakuki, huu sio wakati wa nini, kwa habari ya mashahidi wa Yehova? (b) Watatendaje kana kwamba wana miguu ya kulungu kutoka kwa Yehova?
26 Huu sio wakati wa mashahidi wa Yehova wa Kikristo kulegea wanapoyaona magumu yatakayotokea wakati wa Har–Magedoni yakitokeza na kukaribia. Mahali pake, na wazipaze sauti zao kwa maneno ya mwisho ya ushindi ya nabii Habakuki: “YEHOVA aliye BWANA, ni nguvu zangu, yeye huifanya miguu yangu kuwa kama ya kulungu, naye ataniendesha katika mahali pangu palipoinuka.” (Hab. 3:19) Wakiwa wametiwa nguvu katika miguu yao ya kiroho na furaha yao na shangwe katika Yehova Mungu, wataruka kwenye sehemu zilizoinuka za ukamilifu usioshindwa kwa Bwana Mwenye Enzi Yote Yehova. Huko wataendelea kutembea bila ya wasiwasi kama wafuasi wa Mfalme Yesu Kristo anayetawala. Kama kulungu (“paa jike,” NW) wenye kuruka-ruka wataruka waingie katika baraka za taratibu mpya ya haki ya Mungu, kama waokokaji wa magumu yote ya Har–Magedoni.
—Kutoka The Watchtower, Dec. 15, 1973.