Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w75 2/15 kur. 87-90
  • Je! Wewe Ungemtendeaje Balozi?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Wewe Ungemtendeaje Balozi?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • SABABU KWA NINI MABALOZI WA KRISTO WAMECHUKIWA
  • NAMNA AMBAVYO WENYE MFANO WA MBUZI WANAJIONYESHA WAZI
  • THAWABU KWA “MBUZI”
  • UAMUZI TUNAOKABILI SOTE
  • “Furahini, Enyi Mataifa, Pamoja na Watu Wake”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
  • Je, Inawezekana Kuwapenda Adui Zako?
    Amkeni!—2009
  • Watawala kwa Ajili ya Faida za Watu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • Raia za Kidunia za Ufalme wa Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
w75 2/15 kur. 87-90

Je! Wewe Ungemtendeaje Balozi?

Makala hii ni ya kutumia kwa mafunzo ya kitabu ya kundi

1. Je! matendo mabaya yanayofanywa mara nyingi kwa mabalozi na majengo ya mabalozi yanavutwa na chuki juu ya mabalozi wenyewe, au nini?

NYAKATI za karibuni twasikia mara nyingi juu ya kushambuliwa kwa makao ya mabalozi ambassadeurs na hata kutoroshwa au kuuawa kwa balozi kwa sababu watu wanachukizwa na nchi hiyo au maongozi yake. Lakini nyakati zilizopita kulipokuwa na amani ya kadiri kati ya mataifa, kwa ujumla mabalozi walitendewa vema.

2. Toa mfano wa nyakati za kale wa kutendwa vibaya kwa wajumbe rasmi wa taifa fulani, na matokeo.

2 Walakini, kuna mfano mmoja nyakati za kale “wajumbe” wa kifalme wa taifa lenye amani walipotendwa kwa njia ya aibu (haya). Mfalme Daudi wa Israeli alikuwa ametoa ishara ya kirafiki kwa kupeleka wajumbe rasmi kwa Mfalme Hanuni wa Amoni. Lakini Hanuni alionyesha dharau mbaya sana kwa Daudi kwa kuwaaibisha wajumbe sana. Tendo hili la uhaini lilichochea vita iliyofanya taifa la Waamoni likaribie kufutiliwa mbali kabisa.​—1 Nya. (Sik.) 19:1–20:3.

3. Mwana wa Mungu alipokewaje na taifa la Kiyahudi, kwa matokeo gani?

3 Karne nyingi kufuata hapo, mfano mbaya zaidi ulikuwa kutendwa kwa Mwana wa Yehova Mungu, ambaye Yehova alimtuma kama tendo la fadhili za upendo kwa taifa la Kiyahudi. (Yohana 8:18, 19, 49) Viongozi wao walimtenda kikatili na mwishowe wakamfanya auawe. Hii ilimfanya Mungu alitupilie mbali taifa la Kiyahudi kama watu wake wateule na kuleta uharibifu wa mji wao Yerusalemu na hekalu lake, mwaka wa 70 C.E., mikononi mwa majeshi ya Kirumi.

4. Mabalozi wa Kristo walitendewaje karne ya kwanza; aliyekuwa wa kulaumiwa alikuwa nani hasa, na kwa sababu gani?

4 Lakini Wayahudi wenye kupinga hawakutosheka na walivyomtenda Yesu Kristo. Kabla ya uharibifu wa Yerusalemu, waliwatenda kwa aibu pia wale ambao Kristo aliwatuma kama mabalozi, wanafunzi wake waliotiwa mafuta, wakawaua wengi wao. (2 Kor. 5:20) Ingawa watu walichochewa washiriki katika matendo haya ya ukatili, viongozi wa kidini wa Kiyahudi ndio waliokuwa wa kulaumiwa hasa, kwa sababu waliwazuia watu kwa makusudi wasimjue Mungu. Yesu aliwaambia hivi: “Mmeuondoa ufunguo wa maarifa; wenyewe hamkuingia, na wale waliokuwa wakiingia mmewazuia.” (Luka 11:52) Viongozi hawa waliogopa kwa choyo wasipoteze cheo chenye uwezo. Walisemezana hivi: “Tukimwacha [Yesu] hivi, watu wote watamwamini; na Warumi watakuja, watatuondolea mahali petu na taifa letu.”​—Yohana 11:48.

SABABU KWA NINI MABALOZI WA KRISTO WAMECHUKIWA

5. Kwa sababu gani mabalozi wa karne ya kwanza wa Kristo walichukiwa?

5 Haikuwa chuki ya kipekee iliyofanya wapinzani kati ya Wayahudi wawatese mabalozi wa Kristo wa karne ya kwanza. Ilikuwa kwa sababu mabalozi hawa walitangaza na kuueleza ufalme wa Mungu kwa watu. Waliwaonyesha Wayahudi waliodhani ufalme huo ungekuwa ufalme wa Kiyahudi wa kidunia, kwamba ni serikali ya kimbinguni, kwamba utaharibu serikali zote za kibinadamu na kuleta “nchi mpya,” jamii yenye haki ya wanadamu. Walionyesha kwamba takwa la Mungu kwa uzima wa watu mmoja mmoja ni kwamba wageuze nyutu zao kulingana na kanuni za Mungu kama zilivyoonyeshwa katika Biblia. Lazima waonyeshe upendo kwa wanadamu wenzao bila ubaguzi au chuki isiyo na sababu. Hii iliufunua ubaya wa viongozi wa kidini wenye choyo na kuwafanya wawachukie mabalozi wa Ufalme.​—2 Pet. 3:7, 12, 13; Efe. 4:22-24.

6. Ni hali gani iliyoko juu ya mabalozi wa Kristo waliotiwa mafuta leo?

6 Leo, mabalozi waliotiwa mafuta wa Mungu wangepaswa kwa lazima kuwa wakizitangaza kweli zile zile. Ni habari njema kwa watu wenye mioyo minyofu, lakini zachochea uadui wa viongozi wengi wa kidini. Kwa sababu ya maenezi ya porojo juu ya mabalozi hawa, watu wengi wanafanywa ama walipinge ama wasilisikilize tangazo linalofanywa. Mara nyingi mabalozi wa Ufalme wanatukanwa, wanateswa au kukaribishwa vibaya.

7. Ni maulizo gani ambayo kila mtu aweza kujiuliza, na ni maneno gani ya Yesu yanayoonyesha kwamba ukarimu kwa mabalozi wake wahitaji mengi zaidi kuliko roho ya huruma tu?

7 Walakini, kama wewe ungejua kwamba mtu alikuwa kweli balozi au mjumbe wa ufalme wa Mungu, ungemtendeaje? Je! ungemfanyia mambo zaidi kuliko kwa roho yenye huruma tu? Je! usingempa heshima na usikivu wa pekee, ukisikiliza kwa makini mambo atakayosema? Yesu aliwaambia wanafunzi wake hivi: “Ye yote atakayewanywesha ninyi kikombe cha maji, kwa kuwa ninyi ni watu wa Kristo, amin, nawaambia, hatakosa thawabu yake.” (Marko 9:41) Kwa kutofautisha, alisema kwamba wengine wangewatenda wanafunzi wake mabaya kwa ajili ya jina lake.​—Mt. 24:9; Yohana 15:20, 21.

NAMNA AMBAVYO WENYE MFANO WA MBUZI WANAJIONYESHA WAZI

8, 9. “Mbuzi” katika mfano wa kondoo na mbuzi ni akina nani, nao wanajaribuje kujitafutia udhuru kwa kushindwa kuwaonyesha mabalozi wa Kristo ukarimu?

8 Katika toleo lililotangulia la gazeti hili tuliuzungumza mfano wa Yesu wa kondoo na mbuzi, tukikaza fikira kwenye “kondoo” na thawabu ya uzima wa milele watakayopewa kwa sababu ya kutendea mabalozi wa Kristo vema na kwa ukarimu. Basi, ni nani walio “mbuzi,” nao wanapokea thawabu gani, na sababu gani?​—Mt. 25:31-46.

9 Yesu aonyesha “mbuzi” ni wale watu wa “mataifa yote” ambao, wakiwa tofauti na “kondoo” wenye ukarimu na upendo, hawawakaribishi wala kuwasaidia mabalozi wa Kristo ifaavyo. Wanaonyeshwa katika mfano kuwa wataitwa na Yesu ‘waliolaaniwa.’ Wao wanamjibu Yesu kwa sababu ya laana yake juu ya nia isiyo ya ukarimu kwa kusema: “Bwana, ni lini tulipokuona wewe una njaa, au una kiu, au u mgeni, au u uchi, au u mgonjwa, au u kifungoni, tusikuhudumie?”​—Mt. 25:44.

10. Sababu gani udhuru wa “mbuzi” haufai kitu?

10 Ndiyo, wanamwita “Bwana,” lakini ni kwa njia ya unafiki (udanganyifu) ikiwa kwa kusema hivyo wanamaanisha kwamba yeye ndiye Bwana wao. Kwa maana, kama kweli wanampenda, wangezipenda kweli zinazomhusu yeye nao wangetaka kuuona ufalme wake ukija. (Mt. 6:10) Udhuru wao haufai kitu, kwa maana matendo yao yakanusha dai lao. Si lazima mtu amwone mwingine yeye mwenyewe ili aamue kumsaidia au kukataa kumsaidia. Ulizo ni, Mtu huyo anamtendeaje wakili aonekanaye wa Kristo ambaye ameonyesha waziwazi kwamba kwa kweli yeye anamwakilisha Kristo?

11, 12. (a) Kwa sababu gani Kristo anazungumza juu ya kukosa kwa “mbuzi” kuwa wenye ukarimu kwa ‘hao walio wadogo’? (b) Je! ni lazima “mbuzi” wawatese mabalozi wa Kristo ili kupata laana ya Kristo?

11 Hili ndilo jambo kuu analoonyesha Yesu katika mfano, wakati mfalme anapowajibu “mbuzi” wenye kujitafutia udhuru wakiwa mkono wake wa kushoto wa kuchukiwa: “Amin, nawaambia, Kadiri msivyomtendea mmojawapo wa hao walio wadogo, hamkunitendea mimi.”​—Mt. 25:45.

12 Si kitu mmojawapo wa “ndugu” za Kristo waliozaliwa kwa roho na kutiwa mafuta ni mdogo namna gani. Kwa kweli, hakuna wo wote wa “ndugu” za Kristo walio na vyeo katika siasa wala katika dini za Kristendomu, kwa maana “ndugu” wa kweli wa Kristo, mabalozi wake, si sehemu ya ulimwengu huu kama vile Kristo mwenyewe asivyokuwa wakati wo wote sehemu ya ulimwengu huu. (1 Kor. 1:26-31; Yohana 15:19; 17:14,16) Si lazima “mbuzi” wawatese mabalozi hawa, ingawa wengine wao wamewatorosha, wakawatia kifungoni na kuwaua watumishi hawa wa Kristo. Kwa kukataa kuwapa msaada au ukarimu, kwa kutowajali, kwa kukataa kutoa tegemezo lo lote kwa kazi yao ya kuutangaza ujumbe wa Ufalme, “mbuzi” wanafanya uamuzi wa akili juu ya shauri hili. Kwa kweli wanajipanga kuupinga ufalme wa Mungu wa Kimasihi, katika mioyo yao, ambao mabalozi wanautangaza, na kwa hiyo wanajipanga kumpinga Kristo, kana inavyoonyeshwa wazi na nia yao na matendo.​—Linganisha Mathayo 7:21-23.

THAWABU KWA “MBUZI”

13, 14. Ni nini thawabu ambayo “mbuzi” wanapokea, nao wengine wanadhani hii yamaanisha nini?

13 Kwa hiyo, ni nini thawabu ya “mbuzi” hawa? Kristo awaambia: “Ondokeni kwangu, mliolaaniwa, mwende katika moto wa milele, aliowekewa tayari Ibilisi na malaika zake.”​—Mt. 25:41.

14 Ni nini ‘moto aliowekewa tayari Ibilisi na malaika zake’? Je! ni mateso ya milele mtu akijisikia katika kitu kama moto katika makao yasiyoonekana? Mtu aweza kusema, Bila shaka ndivyo, kwa maana Ufunuo 20:10 wasema: “Na yule Ibilisi, mwenye kuwadanganya, akatupwa katika ziwa la moto na kiberiti, alimo yule mnyama yule nabii wa uongo. Nao watateswa mchana na usiku hata milele na milele.”

15. Ni nini “moto wa milele” ambamo “mbuzi” wanaondoka wakaingie?

15 Walakini, mtu akiyaangalia maneno haya yaliyomo katika Ufunuo kwa uangalifu zaidi aweza kuona kwamba ni usemi wa mfano. Namna gani? Basi, “mnyama” na “nabii” wanatupwa katika “ziwa la moto.” Kwa wazi hawa si mnyama wa halisi na mwanadamu mmoja tu, bali wanafananisha matengenezo. (Ufu. 17:8-14) Zaidi ya hayo, Biblia yenyewe yaendelea kueleza: “Mauti na Kuzimu zikatupwa katika lile ziwa la moto. Hii ndiyo mauti ya pili, yaani, hilo ziwa la moto.” (Ufu. 20:14) Mauti na Kuzimu (Hades, kaburi la kawaida la wanadamu) ni mambo yasiyoonekana wala kugusika, ikiendelea kuonyesha kwamba “ziwa la moto” ni la mfano. Linafananisha maangamizi kamili, uharibifu wa sikuzote, “mauti ya pili,” mauti ambayo hakuna kurudi kutoka kwayo tena.

16. Ni maneno gani zaidi ya Kristo yaonyeshayo kwamba “mbuzi” hawapatwi na mateso yo yote ya halisi motoni?

16 Zaidi ya hayo, Kristo asema kwamba “mbuzi” wataondoka wakaingie katika “kukatiliwa mbali” milele. (Mt. 25:46, NW) Neno la Kigiriki lililotumiwa hapa lamaanisha, kwa halisi, “kukata matawi.” “Mbuzi,” kwa kupatwa na mauti ya milele, “mauti ya pili,” wanakatiliwa mbali kutoka uzimani katika makao yo yote.

UAMUZI TUNAOKABILI SOTE

17. Lazima tufanye uamuzi gani, na ni maulizo gani ambayo kila mmoja wetu aweza kujiuliza?

17 Hakuna shaka kwamba Kristo ana mabalozi duniani leo. Uamuzi uliowekwa mbele yetu kufanya ni, Mabalozi hawa ni nani? Ni nani wanaotuletea habari njema za Ufalme, wakitueleza juu ya kukaribia kwake na baraka utakaozileta duniani baada ya kuharibiwa kwa uovu? Na kila mmoja wetu aweza kuuliza, Ninafanya nini kuendeleza maarifa juu ya Mungu? Je! mimi mwenyewe natumikia kama wakili wa Kristo kwa maneno yangu na mwendo wenye haki wa tendo? Ikiwa sivyo, basi lazima tutambue ni nani wanaofanya hivyo. Lazima tuwaonyeshe ukarimu kama ambavyo tungefanyia mabalozi wa mfalme mwenye kuheshimiwa sana. Hatuwezi ‘kusita-sita’ juu ya mawazo mawili.​—1 Fal. 18:21.

18. Kwa sababu gani kutendewa kwa mabalozi wa Kristo ni kwa lazima zaidi kuliko kutendewa kwa mabalozi wa mfalme wa kidunia?

18 Ungemkaribisha balozi huyo nyumbani mwako. Ungependezwa sana na ujumbe ambao angeleta kutoka kwa mfalme wake au serikali. Ungemtendea kwa heshima. Mabalozi wa Kristo hawana ujumbe wa vivihivi tu. Ni habari zinazotoka kwa Muumba wa ulimwengu wote na Mfalme wake, Yesu Kristo. Kwa hiyo, ni lazima kufikiria wanayosema mabalozi hawa, kwa maana mengi zaidi kuliko kuwaheshimu tu yahusika. Yaonyesha nia yako juu ya Mungu na Kristo, na kwa hiyo yamaanisha uzima au mauti kwako.

19. Ni ukarimu gani umeonyeshwa kwa mabalozi wa Kristo waliotiwa mafuta na mamia ya maelfu ya watu wakati wa sasa?

19 Mamia ya maelfu ya watu katika wakati wa sasa wamewatendea mabalozi hawa kwa fadhili, si kwa kuwapa msaada wa vitu vya kimwili hasa, bali kwa kuwatetea mabalozi hawa watendewapo vibaya na adui zao. (2 Kor. 1:6, 7; Flp. 4:14; Ebr. 10:33) Zaidi ya hayo, wameungana na mabalozi ili kuwasaidia wazitangaze habari njema ulimwenguni pote. (Zek. 8:23) Kwa kufanya hivyo, hawa wenye mfano wa kondoo wanakuwa wajumbe, wenzi wa mabalozi wa Mfalme, Yesu Kristo, (Zab. 45:14, 15) Je! umewatambua mabalozi wa kweli na wajumbe wenzao, na je! unawatendea kwa heshima, ukijua kwamba kwa kadiri unavyomtendea aliye mdogo zaidi wa ndugu za Kristo, na wenzi wao wenye upendo wenye mfano wa kondoo, wamtendea Kristo?

​—Kutoka Kitabu God’s Kingdom of a Thousand Years Has Approached.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki