Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w75 6/15 kur. 267-273
  • Kutopatwa na Madhara Huku Maelfu Yanapoanguka

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kutopatwa na Madhara Huku Maelfu Yanapoanguka
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • SABABU YA UHURU WA KUTOKUWA NA WOGA WA DHARA LA KIROHO
  • WOKOVU WA KIROHO KATI YA HATARI ZENYE KUTISHA
  • Yehova Ni Kimbilio Letu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
  • Faida na Thawabu Kutokana na Kuwa Salama Kiroho
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Ni Ulinzi Gani kwa Watu wa Mungu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • Usalama wa Kiroho Wapewa Kwetu na Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
w75 6/15 kur. 267-273

Kutopatwa na Madhara Huku Maelfu Yanapoanguka

“Elfu moya wataanguka kando yako, na elfu kumi kwa mukono wako wa kuume; lakini hakutafika karibu nawe.”​—Zab. 91:7, Swahili Congo Bible.

1. Katika kumfananisha Yehova na ndege mwenye nguvu, mtunga zaburi alikuwaje na maoni ya Mungu yaliyosemwa kupitia kwa Musa?

WAKATI mwandikaji wa Zaburi 91 aliyeongozwa na Mungu alipomfananisha Yehova Mungu na ndege mwenye mbawa zenye nguvu, alikuwa na maoni ya Mungu mwenyewe. Baada ya Mungu kuleta Waisraeli kwenye Mlima Sinai, alimwagiza Musa awaambie hivi: “Mmeona jinsi nilivyowatendea Wamisri, na jinsi nilivyowachukua ninyi juu ya mbawa za tai, nikawaleta ninyi kwangu mimi.” (Kut. 19:4) Miaka 40 baadaye Yeye alimwongoza Musa kuimba hivi mbele ya Israeli: “Kama vile tai asukasukavyo kiota chake, na kupapatika juu ya makinda yake, na kutandaza mbawa zake, kuwachukua, kuwabeba juu ya nyoya zake, Yehova peke yake aliendelea kumwongoza, na hakukuwa na mungu wa kigeni pamoja naye.”​—Kum. 32:11, 12, NW.

2, 3. (a) Ulinganifu kati ya Mungu na ndege mwenye nguvu unafanywaje katika habari ya “mwanamke” wake wa kimbinguni, katika Ufunuo, sura ya kumi na mbili? (b) Kwa hiyo, tunaposoma sasa Zaburi 91:4, twaweza kukumbuka ndege gani?

2 Kulingana na mfano wa unabii wa Ufunuo 12:6, 14, baada ya “mwanamke” wa Mungu wa kimbinguni kuuzaa ufalme wa Kimasihi na kulazimika kukimbilia “nyikani” apate kuwa peke yake, Mungu alimpa njia ya kukimbia upesi sana: “Mwanamke yule akapewa mabawa mawili ya tai yule mkubwa, ili aruke, aende zake nyikani hata mahali pake, hapo alishwapo kwa wakati na nyakati na nusu ya wakati, mbali na nyoka huyo.” Ni ulinganifu mzuri namna gani uonyeshwao kwa njia hiyo kati ya Yehova Mungu na “tai yule mkubwa,” mfalme wa ndege, bwana wa mbingu, mkuu wa anga!

3 Basi twaweza kumkumbuka ndege huyu wa kifalme tusomapo maneno ya Zaburi 91:4 yaliyoongozwa na Mungu: “Kwa manyoya yake atakufunika, chini ya mbawa zake utapata kimbilio; uaminifu wake ni ngao na [boma].”

4. (a) Ndege aweza kufanya nini kwa kutumia sehemu za nchani za mbawa? (b) Ni nani anayekingwa asitufikie na “mbawa” za Mungu zilizotandazwa juu yetu?

4 Ndege aweza kukinga na kulinda makinda yake karibu na mwili wake kwa kutumia sehemu za nchani za mbawa. Hivyo ndege aweza kukinga ndege wote walao wenzao wasiyafikie makinda yake. Sisi, pia, kama makinda yaliyo hoi, twaweza kupata kinga chini ya manyoya yaliyotandazwa ya ndege wa mfano mwenye kulinda, Yehova Mungu, na hapo twaweza kufurahi katika usalama wetu wa kiroho. Ni kama vile mtunga zaburi Daudi alivyomwambia Yehova: “Wote wanaopata kimbilio katika wewe watafurahi; kwa wakati usiojulikana wao watapaza sauti kwa shangwe. Nawe utawakinga, nao wanaolipenda jina lako watakufurahia.” (Zab. 5: maelezo ya juu ya mwandikaji 1, 11, NW) Kwa kukingwa wasitukaribie, wale wanaotamani kutudhuru kiroho hawawezi kufanya hivyo, Hawawezi kutunyakua kutoka kwa tengenezo la Mungu. “Mwinda ndege” mkuu, Shetani Ibilisi, azuiliwa mbali.

5. Kimbilio la peke yake lililo salama na tengenezo la Shetani liko wapi, na hii ilionyeshwaje kwa njia nzuri katika habari ya Ruthu?

5 Kama makinda yaliyohatirishwa, sisi hatuna mahali pengine pa kukimbilia kwa usalama isipokuwa kwa Mungu Mwenye Nguvu Zote. “Chini ya mbawa zake utapata kimbilio.” (Zab. 91:4) Kwa kuwa kuna matengenezo mawili tu, la Mungu na la Shetani, kupata usalama huku tusidhuriwe na tengenezo la Shetani kwataka tuingizwe katika tengenezo la Mungu la usalama wa kiroho. Ni kwa uzuri namna gani hii ilivyoonyeshwa katika habari ya Ruthu mwanamke Mmoabu, aliyeacha miungu ya Moabu, akaenda Israeli pamoja na mama-mkwewe Naomi aliye mjane! Kwa shukrani, Boazi, ambaye baadaye akawa mume wa Ruthu, alimwambia Ruthu hivi: “[Yehova] na akujazi kwa kazi yako, nawe upewe thawabu kamili na [Yehova], Mungu wa Israeli, ambaye umekuja kukimbilia chini ya mabawa yake.” (Ruthu 2:12) Kwa kumpa thawabu, Yehova alimchagua Ruthu awe mke wa Boazi, ashiriki kuendeleza ukoo wa Yesu Kristo.​—Mt. 1:5-25.

6. Zaidi ya kupata usalama wa kiroho chini ya “mbawa” za Yehova waabudu wa Yehova wanaupata chini ya “mbawa” za nani wakati ule ule?

6 Yesu Kristo mwenyewe alitumia ufanani wa ndege na makinda yake, alipouambia hivi Yerusalemu uliomkataa kama Masihi: “Ni mara ngapi nimetaka kuwakusanya pamoja watoto wako, kama vile kuku avikusanyavyo pamoja vifaranga vyake chini ya mabawa yake, lakini hamkutaka!” (Mt. 23:37) Kitabu cha Maombolezo (4:20) chamzungumza Mtiwa Mafuta wa Yehova au Masihi kama “pumzi ya mianzi ya pua zetu, masihi wa [Yehova], . . . ambaye kwa habari zake tulisema, Chini ya kivuli chake tutakaa kati ya mataifa.” Kwa hiyo, leo, Waisraeli wa kiroho na wenzi wao wa kidunia wakimbiliao chini ya “mbawa” za Yehova wanapata kinga chini ya Masihi wa Yehova wakati ule ule, Bwana Yesu Kristo, kama vifaranga chini ya mbawa za kuku. Kimbilio watafutalo huko kwa usalama wa kiroho hawakosi kulipata.

SABABU YA UHURU WA KUTOKUWA NA WOGA WA DHARA LA KIROHO

7, 8. Ni sifa gani ya Yehova iliyo kama ngao kubwa kwetu, nayo hii yamwonyeshaje Yeye alivyo?

7 Akiendelea kutoa masimulizi zaidi juu ya ulinzi wa usalama wa kiroho, mtunga zaburi sasa aacha habari za ndege kuanza za vita. Akiendelea kumtaja Mungu Aliye Juu Zaidi Sana, mtunga zaburi aongeza: “Uaminifu wake ni ngao na [boma].”​—Zab. 91:4.

8 Uaminifu wa Mungu washirikishwa na fadhili zake za upendo. (Zab. 40:10, 11; 57:3; 61:7; 86:15) Yeye aufahamu wajibu wake kuwa mwaminifu kwa wale wamwabuduo na kumtumaini. Hii yaonyesha kiti Chake cha enzi kilivyo. (Mit. 20:28) Yeye anakuwa mwaminifu sikuzote kwa ahadi yake kwetu. Anakuwa mwaminifu kwa jina lake Yehova na kuwa anachohitaji kuwa kwa ajili yetu. Sifa hii Yake inakuwa ulinzi wetu wa kiroho. Ni kama ngao kubwa kwetu, Naye anakuwa kama mchukua ngao kwetu. Uaminifu wake waonyeshwa kwa matendo maaminifu kwa ajili yetu. Hivyo unatukinga.

9. Uaminifu wa Yehova unatumikiaje kama “ngao” kubwa, na lazima nini kifuatane nao kwa upande wetu?

9 Ngao hii ya uaminifu wa kimungu yazuia vishale vyenye moto au mishale yenye kuwaka ya Adui Mkuu na pia kuondolea mbali mapigo au kumaliza mchomo wa upanga wa adui kabisa. Twaweza kuutegemea uaminifu wa Mungu wenye ulinzi. Lazima tuutegemee, tuuamini. Unafuatana na imani yetu, ambayo pia imepaswa iwe “ngao” kubwa katika “silaha zote” ambazo Mungu atupa sisi. (Efe. 6:11-16) Kuamini kwetu uaminifu “wake” (Mungu) wenye mfano wa ngao kutatuweka huru na woga.​—Mwa. 15:1; Zab. 84:11.

10. Boma ni kifaa cha namna gani cha wakati wa vita, na uaminifu wa Mungu ni kama boma kwetu kwa njia gani?

10 Boma ni ulinzi mkubwa zaidi kuliko ngao. Katika vita ni ukuta unaojengwa kuzunguka mahali patakapopigwa kambi. Ukuta huo unaambia adui wenye kupiga mwendo nchini: “Ni hapo tu mwezapo kufika!” Uaminifu wa Yehova ndivyo ulivyo. Uaminifu wake ni wa lazima sana wakati huu, unaosimuliwa na Ufunuo kama wakati ambapo Nyoka mkuu, Shetani Ibilisi, anapiga vita juu ya mabaki ya “uzao” wa “mwanamke” wa Mungu wa kimbinguni. Twaweza kusimama nyuma ya boma la uaminifu wa Mungu na kupambana na shambulio la ghafula la adui zetu wa kiroho. Boma hili la kimungu halishindiki, haliwezekani; kwa hiyo na tukae nyuma yake. Kulingana na uaminifu wa Mungu na ukweli wake, yeye hatatuacha sisi kamwe katika siku hii ya pigano la kiroho. “Boma” lake latuhakikishia Ushindi!

11. Ni roho ya amri gani inayomvuta mtunga zaburi sasa aseme kwa busara anavyosema katika Zaburi 91:5, 6?

11 Roho ya amri ya kimungu, “Msiogope!” ndiyo inayomvuta mtunga zaburi anapoendelea kusema hivi kwa busara: “Hutaogopa kwa woga wa usiku, wala kwa mushale unaoruka muchana; kwa tauni inayotembela katika giza, wala kwa kuharibu kunakoharibu azuhuri.”​—Zab. 91:5, 6, Swahili Congo Bible.

12. Ni nini kinachoongezea giza la usiku woga mwingi, na ni jambo gani juu ya Yehova usiku linaloondoa woga wa mambo ya usiku yenye kuogofya?

12 Giza la usiku linaelekea kuongeza woga mwingi ambao mtu anaona katika ujirani wenye hatari au katika wakati wa hatari, kwa maana katika giza hatuwezi kuona adui ye yote anayejificha au vyombo vyenye kudhuru. Lakini ingawa tumo katika kipindi cha giza la adili na weusi tititi wa kiroho wa vikundi vya kidunia vya kitaifa, Yehova hasinzii kamwe wala kulala kwa kuwa ni mlinzi wa watu wake. (Isa. 60:2; Zab. 121:4) Kwa hiyo yeye hakosi kamwe kuona maovu ambayo adui Zake wanajaribu kufanya kwa siri wakiwa gizani. Mambo ya hila yenye kutia woga mwingi ambayo kwayo adui wanajaribu kudhuru na kuharibu hali yetu ya kiroho hayapaswi kuogopwa. Tukiwa na hakika yenye nguvu tunaweza kufuata maneno yaliyomo katika Zaburi 64:1, 2: “Sikia sauti yangu, Ee Mungu, katika kilio changu; chunga maisha yangu kwa woga wa adui. Unifiche kwa siri ya wabaya; kwa makelele ya watenda maovu.”​—Swahili Congo Bible.

13. Ingawa hatuoni woga mwingi, lazima tufanye nini tunapomtumaini Mungu?

13 Tunaweza kuwa na hakika kwamba mambo yenye kutia woga yanayopangwa na adui kwa hila wakiwa wamejificha na kuzungumza kwa siri hayatakuwa na matokeo mazuri yatakapotokezwa kwa ghafula. Ingawa hatuogopi mambo hayo yanayotoka katika vyanzo vilivyofichwa, hatupaswi kutokuwa tayari kamwe tunapoendelea kumtumaini Mungu wa uaminifu.

14. Kwa sababu gani hatuuogopi “mushale unaoruka muchana”?

14 Walakini, ziko hatari mchana pia wakati ambapo tunaweza kuona mambo yenye kutisha. Ingawa tunatazamia na tunayajua mambo hayo, haitupasi tuogope mno. Katika wakati huu wa vita ya kiroho, “hutaogopa kwa woga wa usiku, wala kwa mushale unaoruka muchana.” (Zab. 91:5, Swahili Congo Bible) Kwa sababu gani? Ni kwa sababu tuko nyuma ya “ngao” kubwa ya uaminifu na ukweli wa Yehova unaoweza kufanya mishale inayoruka isiwe na matokeo yo yote. Mchana ndicho kipindi cha kulenga mishale bila kukosea.

15. ‘Mishale’ inayoruka mchana ni nini, nao wapiga upinde ndio akina nani?

15 Katika vita ya kiroho inayopigwa juu yetu, ‘mishale’ hii ni mashambulio ya maneno, mashtaka ya uongo, porojo za uongo, machongezi yenye nia ya kuumiza, masingizio mabaya sana, vitisho vyenye jeuri, matumizi mabaya ya sheria katika korti, ndiyo, kutunga fujo kwa kutumia sheria, ‘kutunga madhara kwa njia ya sheria’ juu ya wasio na hatia! (Zab. 94:20) Daudi aliyetiwa mafuta anasimulia wapiga upinde wa adui katika Zaburi 64:3-5 kama wale “walionoa ulimi wao kama upanga, na kupiga maneno machungu kama mishale. Wapigie wakamilifu kwa maficho; wanamupigia kwa gafula wala hawaogopi. Wanayitia roho nguvu kwa neno baya; wanasemezana yulu ya kuweka mitego kwa maficho; wanasema: Nani atakayeiona [mitego hiyo]?” (Swahili Congo Bible)

16. Ijapokuwa ‘mishale’ hiyo ya adui, mashahidi wa Yehova wameendeleaje nyuma ya “ngao” kubwa Yake?

16 Ijapokuwa ‘mishale’ yote hiyo ya mfano ambayo imeruka wakati wa mchana kuanzia mwaka wa 1919 juu ya mashahidi wa Yehova wa Kikristo, wao hawakuacha kumwabudu Mungu mmoja aliye hai na wa kweli wala hawakuacha kuzitangaza habari njema za ufalme wake wa Kimasihi ulimwenguni pote. Imekuwa kama ambavyo Yehova amewaambia wale walio wa tengenezo lake sasa: “Kila silaha inayotengenezwa yulu yako haitasitawi; na kila ulimi unaonyanyuka yulu yako katika hukumu, utauhukumu kuwa mukosa.” (Isa. 54:17, Swahili Congo Bible) Bila kuogopa ‘mishale’ ya adui, mashahidi wa Yehova wameendelea kukaa nyuma ya “ngao” kubwa ya Yehova, nao wapiga upinde wa adui wameonekana kuwa wadanganyifu, ijapokuwa waabudu wa Yehova wameshuhudiwa na wanaendelea kuwa hai kiroho.

17, 18. “Tauni Inayotembela katika giza” inatoka wapi, inakusudiwa iwapate nani hasa, nayo hairuhusiwi kuponywa kati ya akina nani kwa njia gani?

17 Tena mtunga zaburi anatofautisha giza na nuru na hatari za kila moja, kwa maana anasema hivi: “Hutaogopa . . . tauni inayotembela katika giza, wala kwa kuharibu kunakoharibu azuhuri.”​—Zab. 91:5, 6, Swahili Congo Bible.

18 “Tauni” inayotajwa hapa, kama ile ya mstari wa tatu, si tauni inayopelekwa na Yehova juu ya adui zake wa kidunia, au juu ya wale wasiomtii Yeye. Ni tauni ya kilimwengu inayozaliana katika ulimwengu wenye ugonjwa kwa adili na kwa njia ya dini katikati ya giza lake. Kusudi lake ni kuambukia na kuua si walimwengu peke yao, bali waabudu wa Yehova hasa. Inapenda kukaa katika “giza” la adili, la kijamii, la kisiasa na la kidini la ulimwengu huu katika wakati wake wa usiku wa uharibifu unaokaribia sana, nao walimwengu hawaachi giza lenye kujawa na tauni liondolewe mbali na “jua la haki” lenye “kuponya katika mbawa zake,” miali yake yenye kuponya. (Mal. 4:2) Zaidi ya hayo, tunaambiwa katika 2 Wokorintho 4:4, NW, kwamba “mungu wa taratibu hii ya mambo amepofusha akili za wasioamini, ili mwangaza wa habari njema zenye utukufu juu ya Kristo, ambaye ni mfano wa Mungu, usipate kung’aa kwa kupenya.”

19, 20. “Tauni” inayotajwa hapa ni nini, na ni nini kinachosaidia kuieneza?

19 Giza linalotokea linasaidia kueneza “tauni” ya mfano. Kuongezea maogofyo ya giza hilo, tauni hii inaingia gizani, yaani, wakati wa hali ya mambo ambapo akili na mioyo ya watu imepofushwa kwa habari ya Mungu wa kweli na utu wake, kusudi lake na mipango yake yenye upendo. Kwa hiyo chini ya hali hizi tauni hiyo inatokeza hali yenye hatari ya ugonjwa wa akili na moyo katika wale wanaoambukiwa. (1 Tim. 6:4) Kwa hiyo, ni wazi kwamba “tauni” ya mfano ina mafundisho ya adili na ya kidini yenye kuongozwa na mashetani yanayokuja kupitia kwa mawakili wa kibinadamu yakitoka kwa wanaoitwa na Waefeso 6:12 “wakuu [wa ulimwengu] wa giza hili, . . . majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho.”

20 Kwamba malaika hawa wenye ugonjwa wa kiroho wangepenyeza kidogo kidogo mafundisho yao yasiyo na afya kati ya Wakristo wa kujidai, mtume Paulo alimwandikia Timotheo hivi: “Nyakati za mwisho wengine watajitenga na imani, wakisikiliza roho zidanganyazo, na mafundisho ya mashetani; kwa unafiki wa watu wasemao uongo.”​—1 Tim. 4:1, 2.

21. “Tauni”‏ hii yenye kujaza giza imeenea umbali wa kadiri gani?

21 Kwa utimizo wa unabii, tauni hii ya mafundisho ya adili na ya kidini yenye kuongozwa na mashetani, pamoja na mapokeo ya kutungwa na wanadamu yanayotofautiana na Biblia, imeenea katika upagani na hata ikaingia katika Jumuiya ya Wakristo yote. Hivyo waenda kanisani wa Jumuiya ya Wakristo wameambukiwa na kutiwa katika hali yao ya ugonjwa wa kidini, ikahatirisha wokovu wao. Lakini Mungu ametupa sisi mwangaza tusipatwe na “giza” lenye kuzaa tauni.

22. Kwa habari ya “kuharibu kunakoharibu azuhuri,” tunaweza kufahamu ni kwa namna gani?

22 Namna gani, hata hivyo, juu ya “kuharibu kunakoharibu azuhuri,” ambako Wakristo wa kweli walio nyuma ya “ngao” kubwa ya “uaminifu” wa Mungu hawakuogopi? Adhuhuri, sehemu yenye mwangaza zaidi ya siku yenye jua, ni tofauti kabisa na giza la usiku. (Ayubu 11:17) Lakini kuna “kuharibu” kunakofuatana na uangavu na joto la “azuhuri” hii. Kunakwenda sambamba (wakati ule ule) na “mushale unaoruka muchana.” “Kuharibu” huku hakusimuliwi kama kitu kinachoonekana wala kugusika, hata hivyo kunaharibu kama wenye kuharibu wanaoshambulia adhuhuri. (Yer. 6:4; 15:8; 20:16) Kunaweza kufahamika kwa akili kuwa pigo la kuambukiza lenye kuenea sana (la kipuku) linaloua wengi, likiwaharibia uhai.

23. “Azuhuri” inayomaanishwa hapa ni nini, nako “kuharibu kunakoharibu” wakati huo ni nini?

23 “Azuhuri” hii ina maana ya kilimwengu. Mwangaza wenye kung’aa ndio unaoitwa “mwangaza” wa Kizazi cha Wenye Elimu cha ulimwengu, kizazi chake cha silaha za atomiki, kizazi chake cha uvumbuzi wa anga za juu. Mafundisho yake na porojo zake zinajisifia akili ya kibinadamu nazo ni zenye maoni ya kufuatia vitu vya kimwili tu. Wenye kukubali mafundisho hayo wanapatwa na uharibifu wa kiroho, kwa maana yanapinga Neno la Mungu, ibada yake, ufalme wake wa Kimasihi. Kwa hiyo ni yenye kuambukiza tauni, na wengi wanavurugika akili na kupoteza imani kwa sababu ya “mashindano ya elimu iitwayo elimu kwa uongo.” (1 Tim. 6:20, 21) Mwishowe wenye kupatwa wanaona uchungu mwingi wa kukata tamaa, kuvurugika moyoni. Ulimwengu leo unakula matunda machungu ya kufuatia akili ya kibinadamu. Wanasayansi na wanafilosofia wenye kung’aa sana wa kisiasa, wa elimu na wa mambo ya kijamii wameongeza tu ‘joto’ juu ya jamii ya kilimwengu. Kwa mafundisho yao yasiyomcha Mungu wamechafua hali ya akili na adili ambamo jamii ya kisasa inaishi.

24. ‘Kuharibu huko kunakoharibu azuhuri’ kulifunuliwa wakati gani hasa, na ni mwangaza gani wa kiroho uliotofautishwa nako?

24 “Kuharibu kunakoharibu azuhuri” kwenye hatari ya kiroho kulifunuliwa wazi hasa na ‘pigo la nne’ linalosimuliwa katika Ufunuo 16:8, 9. Kitasa kilichojaa cha ‘pigo’ hili kilianza kumiminwa juu ya “jua” la akili ya kibinadamu mwaka wa 1925, katika kusanyiko la Indianapolis (Indiana) la mashahidi wa Yehova wakati wa kiangazi hicho. Mwaka uo huo kuzaliwa kwa ufalme wa Mungu wa Kimasihi na kutupwa kwa Shetani na mashetani wake watoke mbinguni kulielezwa kutokana na masimulizi ya unabii yaliyotolewa katika Ufunuo 12:1-13. Hivyo mwangaza wa kiroho wenye kutoa uzima wa waabudu wa Yehova ulitofautishwa na mwangaza wa kisasa wa kilimwengu wa wale wanaoharibiwa uhai wao wa kiroho na “kuharibu” kwa adhuhuri yao.

WOKOVU WA KIROHO KATI YA HATARI ZENYE KUTISHA

25, 26. “Elfu moya” ‘wanaoanguka kando yako’ ni akina nani, nao wanaanguka kwa njia gani, na kwa sababu gani?

25 Matisho yaliyosimuliwa tayari kwa uhai wa kiroho ni mambo wasiyoyaogopa wale waliomo “pahali pa maficho yake Aliye yulu” na walio “chini ya kivuli cha Mwenyezi.” Uhakikisho wenye kutia imani sasa unatolewa na mtunga zaburi katika maneno yake yanayofuata yakisemwa kwa hawa kama jamii: “Elfu moya wataanguka kando yako, na elfu kumi kwa mukono wako wa kuume; lakini hakutafika karibu nawe.”​—Zab. 91:7, Swahili Congo Bible.

26 Wale wanaosemwa kama wakiwa “kando” ya waabudu hawa walio wakf wa Yehova Mungu ni watu wa Jumuiya ya Wakristo na Wayahudi wanaojidai kumwabudu Mungu wa Biblia Takatifu. ‘Wanaanguka’ katika kifo cha kiroho kwa sababu hawamo katika mahali pa Yehova pa usalama wa kiroho. Kwa hiyo, wanawekwa nje wapatwe na mambo yenye kufisha yanayosimuliwa na mtunga zaburi, jambo lenye kuogofya la usiku wa dunia, mshale unaoruka wa mchana, tauni yenye kueneza giza pote, “kuharibu kunakoharibu azuhuri.” Wao kwa kweli hawakumfanya Mungu “kimbilio” lao.

27. “Elfu kumi” wanaoanguka “mukono wako wa kuume” ni akina nani?

27 Kana kwamba elfu wakilinganishwa na mmoja si tofauti kubwa, mtunga zaburi anasema kwamba wanaoanguka watakuwa “elfu kumi kwa mukono wako wa kuume.” Kama vile katika habari ya Mungu Mwenye Nguvu Zote, ‘mukono wa kuume’ unafananisha mkono na upande wenye nguvu zaidi. (Zab. 98:1) Wale ambao imekuwa lazima kwetu tuwapinge zaidi kiroho kwa sababu ya nguvu zao nyingi zaidi za kidini wanaanguka kwa sababu hawana kinga ya ulimwengu, usasa, porojo zenye kupinga dini, ualimu wa kidini unaopendwa na watu wengi na mafundisho na mazoea ya kidini yenye kuongozwa na mashetani. Roho ya Mungu haiwafanyi wawe wasioweza kupatwa na mambo hayo.

28. Imekuwaje kweli kabisa kwamba elfu kumi wameanguka mkono wa kuume wa mabaki yaliyotiwa mafuta, na Mungu ameinua akina nani wawe wenzi wa mabaki?

28 Leo, tunapotofautisha hesabu ya mabaki yaliyotiwa mafuta ya Israeli wa kiroho, karibu elfu kumi, na maelfu ya mamilioni ya washiriki wa Babeli Mkuu wa kidini, tunaweza kuona ni kweli kabisa kwamba elfu kumi wameanguka mkono wa kuume wa mabaki haya ya “uzao” wa “mwanamke” wa Mungu. (Ufu. 12:17) Lakini Yehova Mungu ameinua “mkutano mkubwa” wa waamini wenye mfano wa kondoo ambao wameweka maisha zao wakf kwa Yehova Mungu kupitia kwa Yesu Kristo Mchungaji Mwema badala ya makumi hayo ya maelfu ambao wameanguka katika kifo cha kiroho mkono wa kuume wa mabaki haya. (Ufu. 7:9-17; Yohana 10:16; Mt. 25:31-46) Yehova amekuwa akiwainua hawa kama wenzi wa mabaki hasa kutoka mwaka wa 1935. Leo wao ni mamia ya maelfu, hata mashahidi wa Yehova wa Kikristo sasa ni karibu milioni mbili wanaotangaza ufalme wa Mungu.

29. Wakili mwenye kuharibu imani kutokana na vyanzo vya kilimwengu hakukaribia akina nani, lakini amekaribia akina nani?

29 Kwa wale ambao wameanguka kiroho wakili mwenye kuharibu imani kutoka vyanzo vya kilimwengu amekaribia. Lakini kwa wale wanaosimama katika mahali pa Mungu pa usalama wa kiroho, “hakutafika karibu nawe.” Kuanzia mwaka uliofuata vita wa 1919 C.E., mabaki wamekubali kuponya kwa kiroho kunakotolewa na Daktari Mkuu, Yehova Mungu. (Zab. 103:1-3) Lakini Jumuiya ya Wakristo haikukubali, kama ilivyosemwa mapema kwa unabii katika Isaya 6:9-12; Mathayo 13:14,15. Kwa hiyo, washiriki zaidi ya milioni elfu moja wa Jumuiya ya Wakristo wanashindwa na maongozi na mikazo yenye kuharibu kiroho ya ulimwengu huu wenye ugonjwa. Lakini Mungu amefanya mabaki yake na “mkutano mkubwa” wa wenzi wao wa Kikristo wawe wasioweza kupatwa na ugonjwa huo. Mungu haruhusu kuenea kwa ugonjwa wa kilimwengu kukaribie mahali pao pa hali ya kiroho ya kutoweza kupatwa na ugonjwa. Kukaa kwao kwa utii katika “pahali pa maficho” pa Mungu kunawafanya salama salimini.

30, 31. (a) Wale waliomo katika “pahali pa maficho yake Aliye yulu” wanatazama na kuona thawabu ya akina nani inayokuja katika wakati wake? (b) Ni kwa njia gani na kwa sababu gani thawabu hiyo imewajia hao?

30 Baada ya miaka mingi sasa ya kukaa katika “pahali pa maficho yake Aliye yulu” kwa tumaini, mabaki yaliyotiwa mafuta ya Israeli wa kiroho na, mwishowe, “mkutano mkubwa” wa mashahidi wenzao wameona ukweli wa anayofuata kusema mtunga zaburi: “Na macho yako tu utatazama, na kuona zawabu ya waovu.”​—Zab. 91:8, Swahili Congo Bible.

31 Ni wazi kwamba hapa Mungu Aliye Juu Zaidi Sana hawatii wale waliomo katika “mahali pa siri” pake Yeye katika jamii moja na “waovu,” ambao wako nje na ambao ni sehemu ya ulimwengu mwovu huu. Hasa sasa, kuelekea mwisho wa taratibu hii ya mambo iliyohukumiwa, wale ambao wamekuwa wakijitia katika njia za ulimwengu mwovu huu wanakula matunda ya mwendo wao kama adhabu wanayoistahili. Malipo yapasayo yanakuja juu ya walimwengu magumu yao yanapoongezeka sana katika mambo ya kisiasa, ya kibiashara, ya adili, ya kijamii na ya kidini. Kama walivyopanda, ndivyo wanavyovuna. Jamii ya kisasa, ambayo imekuwa yenye kuendekeza sana inayoitwa “adili mpya,” “mageuzi yapasayo wanaume na wanawake,” haiwezi kufanya wapotovu wa ngono ‘wasipate nafsini mwao malipo ya upotevu wao yaliyo haki yao.’​—Rum. 1:27; Luka 21:25, 26.

32. Tayari kabla ya “dhiki kubwa,” wale waliomo katika “pahali pa maficho” wanaona tofauti ya matokeo kati ya nani?

32 Walimwengu wanaangushwa na mipango yao wenyewe. Wale ambao wameikataa hekima ya Neno la Mungu wakajiacha wazi wapatwe na hila za Shetani wamekuwa wajinga wa “madanganyo yote ya udhalimu kwa hao wanaopotea; kwa sababu hawakukubali kuipenda ile kweli, wapate kuokolewa.” (2 The. 2:9, 10) Tayari, kabla ya “dhiki kubwa” inayokaribia, watu wa Yehova wanaolindwa wanatazama na kuona kwa macho yao tofauti, kwa habari ya matokeo, “kati ya wenye haki na waovu, na kati ya yeye amtumikiaye Mungu na yeye asiyemtumikia.”​—Mal. 3:18.

[Picha katika ukurasa wa 268]

“Uaminifu wake ni ngao”

[Picha katika ukurasa wa 272]

MAGEUZI

UCHAWI

MATUMIZI MABAYA YA KULEVIA

UTUKUZO WATAIFA

KUFUATIA VITU VYA KIMWILI

KUABUDU SAYANSI

ABUDU “MPYA” YA MAMBO YA WANAUME NA WANAWAKE

UCHAMBUAJI WA BIBLIA

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki