Faida na Thawabu Kutokana na Kuwa Salama Kiroho
1. Ni akina gani walio salama na hatari za ulimwengu unaopeperuka?
USALAMA wa vitu vyenye kuonekana na kuguswa na wa kimwili wa wanadamu unaharibika lakini usalama wa kiroho unaonekana kuwa ulinzi juu ya hatari za adili, za kijamii, za kisiasa na za kidini za ulimwengu huu wenye kupeperuka. Wenye usalama wa kiroho ni wale wanaoweka mambo ya kiroho yaliyoandikwa katika Neno Takatifu la Mungu kwanza katika maisha zao. Wao wanajua kwamba Mungu ataangalia mahitaji mengine yote.
2, 3. Mabaki na “mkutano mkubwa” wamemfanyaje Yehova kuwa “kimbilio” lao kweli?
2 Kwa habari ya kumtanguliza kwetu Mungu katika maisha zetu mwandikaji aliyeongozwa na Mungu wa Zaburi 91 anaendelea kutupa sisi maoni ya usalama kwa kusema hivi: “Maana [ulisema] wewe, Ee [Yehova], ni pahali pangu pa kukimbilia! Umefanya Aliye yulu ikalo lako; mabaya hayatakupata wewe wala tauni haitafika karibu na hema yako.”—Zab. 91:9, 10, Swahili Congo Bible.
3 Lo! ni wazo zuri kama nini, kumfanya Mungu Aliye Juu Zaidi Sana ‘makao yako’! Hii si kwa sababu ya kumwambia tu Yehova, ‘Wewe ni pahali pangu pa kukimbilia,’ bali pia kumfanya Yeye kweli mahali ambapo tunatafuta kimbilio letu kwa ajili ya usalama. Kwa uhodari, wakiwa peupe mbele ya watu wote, mabaki yaliyotiwa mafuta ya Israeli wa kiroho wa Mungu wamemtangaza Yehova kuwa kimbilio lao, hasa kuanzia mwaka wa 1925 na kuendelea. “Mkutano mkubwa” unaotokea siku hizi ambao wamejiunga na mabaki katika kumwabudu Yehova kama Mungu wamefuata mfano wa mabaki katika kumtangaza na kumfanya Yeye kimbilio lao, na kwa hiyo ‘makao’ yao.
4. Vikundi viwili hivi vimeunganishwa katika mwendo wao wa tendo kwa ajili ya ulizo kubwa gani?
4 Kwa umoja vikundi viwili hivi vimemtangaza Aliye Juu Zaidi Sana, Yehova, kuwa ndiye Mwenye Enzi Kuu wa Ulimwengu Wote. Katika ulizo linaloendelea vikali sasa kati ya utawala wa Mungu wa dunia nzima na utawala wa kibinadamu, wao wamesimama upande wa enzi kuu ya Yehova. Wanaendelea kutangaza ulimwenguni pote kwamba ufalme wa Mungu wa Kimasihi mikononi mwa Mwanawe Yesu Kristo ndilo tumaini la peke yake kwa wanadamu wanaotaabika. Wao wanakaa katika Yehova kama Chanzo cha peke yake cha usalama wote. Faida zao za milele kwa ajili ya sasa na wakati ujao ziko salama katika Yeye!
5. Ni mabaya ya namna gani yasiyowapata wale wanaofanya Mungu kimbilio lao la maisha?
5 Mabaya yanauongezekea ulimwengu mwovu huu, si katika mambo ya kisiasa na ya kiuchumi tu, bali kwa kudhuru zaidi katika mambo ya adili, ya kijamii na ya kidini. Lakini wale wanaomfanya Mungu mmoja aliye hai na wa kweli, Yehova, kimbilio lao la maisha, “mabaya hayatakupata wewe.” Ndiyo kusema, hata moja la mabaya yanayosimuliwa katika mistari inayotangulia ya Zaburi 91. Bila shaka, wanaweza kushiriki pamoja na watu wote katika mabaya makubwa kama vile mafuriko ya maji, tufani, matetemeko ya dunia, magonjwa ya kipuku, upungufu wa chakula, uharibifu wa vita za kati ya mataifa na makabila na mapinduzi ya kisiasa, lakini hizi haziharibu hali yao ya kiroho wala kulegeza imani yao na tumaini katika Mungu Mwenye Nguvu Zote. Nao wanaweza kupona kutokana na mabaya hayo ya kidunia kwa kupata mali za kimwili na kupata afya ya kimwili.
6. Kwa sababu gani mabaya ya kiroho ni mabaya zaidi, na ni akina nani wanaotaabishwa nayo?
6 Walakini, mabaya ya kiroho ni tofauti. Hakuna kupona kutokana nayo kama vile katika habari ya Jumuiya ya Wakristo ya kidini na Wayahudi. Vikundi hivi vya kidini ni sawa na upagani, havifanikiwi kiroho. Vinaendelea kuwa katika hali ya ugonjwa wa kidini, mabaya yenye uharibifu yakiwa mbele yao katika “dhiki kubwa” inayokuja. (Mt. 24:21, 22; Ufu. 7:14) Mabaya yako mbele kwa wote wasiokimbilia kwa Yehova na kukaa katika yeye.
7. (a) “Tauni” za mfano zinazoambukia ulimwengu wenye mfano wa mji ni nini? (b) Usalama wapatikana kwetu kwa kufuata mwendo gani tukiwa kama wageni wenye kusimamisha hema?
7 Wale wanaokaa katika Mungu Aliye Juu Zaidi Sana kwa tumaini wanaonyeshwa kuwa wageni, wanaokaa katika hema katika taratibu hii ya sasa ya mambo nje ya mipaka ya mji. (1 Pet. 2:11; Ebr. 11:8-10) Ahadi ya kimungu kwa hawa kama jamii ni: “Wala tauni haitafika karibu na hema yako.” (Zab. 91:10, Swahili Congo Bible) Kati ya “tauni” zenye kudhuru kiroho ambazo sasa zimeujaa sana ulimwengu wenye mfano wa mji ni mambo yenye kuambukia kama vile utukuzo wa taifa, uzalendo mshupavu, fundisho la mageuzi kama jambo la hakika, kufuatia vitu vya kimwili kwa choyo, matumizi mabaya ya dawa za kulevya, kupendezwa na kutiwa damu mishipani, mazoea ya kichawi, “adili ya kisasa ipasayo wanaume na wanawake,” kupenda anasa kuliko kumpenda Mungu, kuwa na madhehebu za kidini, uchambuaji wa Biblia, ibada ya “ng’ombe mtakatifu” wa sayansi, pia ibada ya “mnyama” wa kisiasa na ibada ya “sanamu” yake iliyotokea baada ya vita, Umoja wa Mataifa, mrithi wa Ushirika wa Mataifa. (Ufu. 9:20, 21; 13:1-18) Wao wataepuka “tauni” nyingi za ulimwengu zenye kuambukia kwa kumfanya tu Yehova kimbilio lao na kuiweka “hema” yao mbali sana na “mji” wa ulimwengu huu. Kwa hiyo na tukae mbali, kama tusiokuwa sehemu ya ulimwengu huu.—Yohana 17:14-16; linganisha Waebrania 11:9, 10.
ULINZI WA KIMALAIKA JUU YA KUTOANGUKA
8. Tunahitaji nini badala ya uongozi wa kibinadamu tu, na je! unapatikana kwetu?
8 Tunapotembea hapa na pale katika ulimwengu huu wenye hatari za kiroho, tunahitaji uongozi upitao ule wa mwanadamu ili njia zetu zipate kumpendeza Mungu. Uongozi huo upitao wa mwanadamu unahakikishwa kwetu, “maana,” kama mtunga zaburi anavyoongeza, “ataagiza malaika yake yulu yako, wakuchunge katika njia zako zote.”—Zab. 91:11, Swahili Congo Bible.
9. Hii inatukumbusha juu ya ahadi gani iliyofanywa kwa Israeli wa asili, na juu ya huduma gani iliyofanywa kwa Yesu, na juu ya uhakikisho gani kwa habari ya wafuasi wake wenye mfano wa mtoto mdogo?
9 Ahadi hii inatukumbusha kwamba Mungu aliliambia taifa la Israeli wa asili hivi kupitia kwa nabii Musa: “Tazama ninatuma malaika mbele yako kukuchunga njiani na kukuleta kwa pahali nilipotengeneza. Kwa kuwa malaika yangu atakwenda mbele yako na kukuleta.” (Kut. 23:20, 23; 32:34; 33:2, Swahili Congo Bible) Pia, baada ya Mwana wa Mungu, Yesu Kristo, kupinga vishawishi vitatu vilivyowekwa kwake katika jangwa la Uyahudi, ambavyo kimoja kilitia ndani Zaburi 91:11, 12, “Satani akamwacha; na tazama, malaika wakakuya wakamutumikia.” (Mt. 4:1-11, Swahili Congo Bible) Kwa habari ya wafuasi wake wenye mfano wa mtoto mdogo, Yesu alisema hivi: “Malaika zao mbinguni sikuzote huutazama uso wa Baba yangu aliye mbinguni.” (Mt. 18:10) Malaika hawa wa kimbinguni sasa wako chini ya amri ya kimungu kuangalia mabaki ya Waisraeli wa kiroho na wenzi wao waaminifu.
10. Mgawo wa malaika ‘kukuchunga katika njia zako zote’ unatumika kwa “njia” gani?
10 Mgawo wa malaika hawa ‘kukuchunga katika njia zako zote’ ungetumika kwa “njia” ambazo waabudu wa Yehova wanafuata zinazopatana na Neno Lake lililofunuliwa na kwa hiyo wao wako chini ya kibali Yake na uongozi. Malaika zake hawawezi kufuatana na “mabaki” na “mkutano mkubwa” wa wenzi wao katika njia zilizo tofauti—za kichoyo, za ushupavu.—Mt. 13:41, 42.
11. Unabii wa Yesu juu ya “mwisho wa taratibu ya mambo” na juu ya mjumbe anayeruka katikati ya mbingu ulionyeshaje malaika wangehusika na wafuasi wake duniani?
11 Unabii wa Yesu mwenyewe juu ya “ishara ya kuwapo [kwake] na ya mwisho wa taratibu ya mambo” ulieleza wazi kwamba yeye angetuma malaika zake kwa ajili ya kukusanywa kwa washiriki waliochaguliwa wa Israeli wa kiroho. Pia, wakati ambapo angekuja kutenganisha watu wa mataifa kama kondoo na mbuzi, malaika wangekuwa pamoja naye. (Mt. 24:3, 31, NW; 25:31, 32; Ufu. 7:1-8) Kitabu cha mwisho cha Biblia, Ufunuo uliopewa kupitia kwa Yesu kwa mtume Yohana, kinafunua waziwazi kwamba malaika wa kimbinguni wangeshiriki pamoja na mabaki yaliyotiwa mafuta ya Israeli wa kiroho katika utendaji wao wa kidunia wakati wa ‘mwisho huu wa taratibu ya mambo.’ Kwa mfano, katika utimizo wa njozi ya Yohana ya malaika aliyeruka katikati ya mbingu akiwa na habari njema za milele kutangazia wakaaji wa dunia, uongozi wa kimalaika na ulinzi vinaonyeshwa kwa ajili ya waabudu wa Yehova wanaofanya kazi hiyo duniani. (Ufu. 14:6, 7) Lakini zaidi ya hayo:
12. Kulingana na Ufunuo, mabaki ya wakati huo yaanzapo kumimina ‘mapigo saba ya mwisho,’ kwa sababu gani lazima wawe wamekwisha pata uongozi na ulinzi wa kimungu?
12 Wakati ‘mapigo saba ya mwisho’ yalipoanza kumiminwa wakati wa miaka ya 1911-1928 C.E., kupitia kwa “mabaki” yaliyotiwa mafuta wakati huo, bila shaka kulikuwako uongozi na ulinzi wa kimalaika. Kwa akili hivyo, kwa maana Ufunuo, sura 15-17, unafunua kwamba “vitasa” au “machupa” yaliyokuwa yamejaa ghadhabu ya Mungu yalishikwa na kutumiwa kwa werevu na malaika wa kimbinguni waliopokea vyombo hivi mikononi mwa Mungu. Kwa kufanya hivyo katika njia za Mungu za utumishi waabudu wa Yehova wanahakikishiwa ulinzi wa kimalaika.—Zab. 34:7; Ebr. 1:13, 14.
13. Mawakili wa Shetani wa kidunia wanaweka nini katika kijia cha wale wanaotembea katika “njia” za Yehova, nayo Zaburi 91:12 inasema nini juu yake?
13 “Njia” ambazo sisi kama waabudu wa Yehova Mungu tunafuata zimo katikati ya taratibu hii ya mambo ya kilimwengu ambayo Shetani Ibilisi ndiye “mungu.” (2 Kor. 4:4) Kwa hiyo, inaweza kutazamiwa kwamba mawakili wa kidunia wa mungu huyu wa uongo wataweka katika kijia chetu mawe ya mfano ili waabudu wa Yehova wajikwae na kupatwa na anguko lenye msiba. Lakini kwa habari ya sababu hizo za kujikwaa mtunga zaburi anaendelea kuzungumza juu ya malaika za Yehova, akisema hivi: “Watakuchukua yulu mikononi mwao, usivunje mugulu wako kwa jiwe.”—Zab. 91:12, Swahili Congo Bible.
14. Katika karne ya kwanza ya Wakati wetu wa Kawaida, ni nini kilichokuwa “jiwe la kujikwaza” kwa taifa la Israeli wa asili, na kwa sababu gani?
14 Hii inamaanisha kwamba malaika hawa wa kimbinguni watatutegemeza, kutusaidia, ili tusiumizwe na “jiwe” hilo. Huko nyuma katika karne ya kwanza ya Wakati wetu wa Kawaida Waisraeli wenye kuasi imani, “nyumba za Israeli zote mbili,” hawakuwa na msaada huo wa kimalaika wasijikwae na kuangukia uharibifu wa kiroho. Walijikwaa juu ya Masihi wa kweli wa Yehova, Yesu Kristo, aliyekuwa kwao “jiwe la kujikwaza” na “mwamba wa kujikwaa,” kama ilivyosemwa mapema kwa unabii katika Isaya 8:14. (1 Pet. 2:7, 8) Kukataa kwao Yesu kama Masihi kumedhuru Wayahudi waliotahiriwa kiroho mpaka leo hii. Walakini, hili silo “jiwe” linalosemwa katika Zaburi 91:12.
15. “Jiwe” la Zaburi 91:12 ni tofauti kwa njia gani, na hii inaweza kuonyeshwaje kwa mfano?
15 “Jiwe” hili ni kitu kinachotoka kwa Adui Mkuu wa Yehova, Shetani Ibilisi; na kwa hiyo mtu akikubali “jiwe” hili lilivyo, anaondoka katika upendeleo wa Mungu. Hii ni tofauti na “jiwe” la Kimasihi la karne ya kwanza, ambalo kama lingekubaliwa na taifa la Kiyahudi, lingefanya waendelee kuwa na upendeleo wa Mungu. Lakini huko nyuma Wayahudi wenye kutukuza taifa walifuata Masihi wa uongo wasiotoka kwa Mungu. Akiutazamia wakati wetu pia, Yesu Kristo alionya wanafunzi wake juu ya Masihi au Makristo wa uongo katika ‘mwisho huu wa taratibu ya mambo.’ (Mt. 24:3, 5, 23-26, NW) Kulingana na ilivyokuwa imesemwa mapema, “Makristo wa uongo” hawa wametokea, si hasa kwa namna ya watu mmoja mmoja, bali katika taratibu za kisiasa na za kiuchumi ambazo zimehesabiwa kuwa na nguvu za Kimasihi na ambazo kupitia kwazo baraka za Kimasihi zilitazamiwa. Kwa mfano, kama vile wakati Nikita Krushchev alipoahidi kwamba Ukomunisti wa Kirusi wa namna yake ungeanzishia watu paradiso. Nasi tunawezaje kusahau kwamba, katika Desemba wa 1918, Federal Council of the Churches of Christ in America iliushangilia Ushirika wa Mataifa uliokusudiwa kama “wonyesho wa kisiasa wa Ufalme wa Mungu duniani”?
16. Shukrani kwa malaika, ni nini mengine ya ‘mawe’ ambayo mashahidi wa Yehova hawakujikwaa nayo na kuanguka?
16 Kwa uaminifu malaika za Yehova ‘wamechukua waabudu Wake mikononi mwao’ hata hawakujikwaa mguu wao juu ya “jiwe” lo lote la namna hiyo nao hawakuondoka katika upendeleo wake. Novemba wa 1939, wakati walipotokea mbele ya watu wote kwa kushikamana na “kutokuwamo” kwa Kikristo juu ya magomvi ya kilimwengu, hii iliwaimarisha katika mwendo wao waliokuwa wameuchagua tayari wa kukataa wasilazimishwe kuandikwa kazi ya jeshi, wakati wa amani na wakati wa vita pia. Watawala wenye kutumia nguvu katika serikali za kisiasa walitokea baada ya Vita ya Ulimwengu ya Kwanza, kama vile Adolf Hitler aliyekuwa na lengo la kusimamisha tena Milki Takatifu ya Kirumi ya Taifa la Kijeremani iwe ya miaka elfu. Lakini mashahidi wa Yehova wa Kikristo hawakuwakubalia watawala hao wenye kutumia nguvu wachukue nafasi ya Masihi wa kweli wa Yehova, Yesu Kristo. Katika nyakati za majaribu juu ya ukuu wote wa sheria ya Mungu Aliye Juu Zaidi Sana, wamefuata maneno ya mitume wa Kristo nao wameambia wanasiasa, mahakimu na mapolisi hivi: “Imetupasa kumtii Mungu kuliko wanadamu.” (Matendo 5:29) Shukrani kwa malaika za Yehova, hakuna hata “jiwe” lo lote kama vile marufuku na makatazo juu yao na kuhubiri kwao ufalme wa Mungu limewakwaza na kuwaangusha waabudu Wake.
SALAMA JUU YA MASHAMBULIO YA WAZI NA YA SIRI
17. Kwa habari ya usemi unaotumiwa, Zaburi 91:13 inafananaje na Luka 10:19?
17 Karibu na mwisho wa mwaka wa 32 C.E., Yesu Kristo alituma wanafunzi 70 kama wahubiri wa injili wa ufalme wa Mungu wa Kimasihi. Kwa wazi akisema kwa usemi wa mfano kwao, alisema hivi: “Tazama, nimewapa amri ya kukanyaga nyoka na nge, na nguvu zote za yule adui, wala hakuna kitu kitakachowadhuru.” (Luka 10:19) Vivyo hivyo, kwa njia ya mfano, mtunga zaburi sasa anaiambia hivi jamii ambayo imemfanya Yehova makao yake: “Utakanyaga juu ya simba mdogo na fira; utamkanyaga simba mdogo mwenye manyoyo mengi shingoni na nyoka mkubwa.”—Zab. 91:13, NW.
18. Kwa njia ya mfano, “simba mdogo” amekanyagwa-kanyagwa kwa njia gani?
18 Simba mdogo anashambulia waziwazi kwa mbele. Kwa hiyo, pia, serikali zenye nguvu za kisiasa zimetumia sheria inayoonyesha jina la mwenye kupatwa na mbaya. Wamepitisha waziwazi sheria zenye lengo la kuwapata mashahidi wa Yehova. Au wametumia sheria za utukuzo wa taifa juu ya hawa. Kwa kusudi gani? Kuwatafuna, kuwayeyusha tumboni mwao, kuwatiisha kwa Serikali, wakiwafanya chama cha kidini cha kitaifa, wakiwa wametenganishwa kabisa na jamii ya ulimwenguni pote ya mashahidi wa Yehova inayotawaliwa kutoka kwa Mungu kuja chini. Mashahidi waaminifu wa Yehova wameukataa mpango huo wa chama kimoja, wenye kuongozwa wa Serikali. Wao wameshikamana sana na Utawala wa Mungu kwa njia ya kitheokrasi!
19. Kwa njia ya mfano, “fira” amekanyagwa-kanyagwa kwa njia gani?
19 Tofauti na simba mdogo, fira anashambulia gizani akiwa mafichoni. Yeye ni hatari, kama “nyoka barabarani,” ambaye kabila la Dani lililinganishwa naye na “aumaye visigino vya farasi.” (Mwa. 49:16, 17) Mashambulio yenye sumu yasiyotazamiwa kama yale ya fira yamefanywa juu ya mashahidi wa Yehova duniani pote wanapoendesha kazi yao ya waziwazi ya kutangaza ufalme wa Mungu nyumba kwa nyumba, hata katika nchi ambako dini ya Serikali ina mamlaka. Wakiwa wamejificha nyuma ya Serikali kama mwuaji wao, viongozi wa dini wa Jumuiya ya Wakristo wameshambulia mashahidi wa Yehova kwa siri wakitumia wanasiasa, watunga sheria, wakuu wa polisi na mahakimu wa korti za sheria. (Zab. 94:20) Lakini kwa habari ya mashahidi wa Yehova, wao hawakupigwa bumbuazi ya woga na sumu ya mashambulio yasiyo haki. Wao wameendelea kuwa wenye kufuata sheria na wameomba haki zao za halali kwa amani kwa korti za sheria, wakataka rufani kwa Haki za Sheria zinazotolewa na Serikali. Wao wameendelea kutetea kisheria uhuru wa dini na haki ya kuhubiri ufalme wa Mungu kwenye korti kuu zaidi za nchi. (Flp. 1:7, 16) Mara nyingi jitihada zao zimepata ushindi!
20. Yajapokuwa marufuku juu ya vitabu vyao vya kusaidia kufahamu Biblia, Mashahidi wamefanywaje wanafunzi bado?
20 Hata kama adui walitumia mashambulio ya wazi kwa mbele au kwa siri, wamekanyagwa na mashahidi wenye kuendelea kusonga mbele wa Mungu Aliye Juu Zaidi Sana. Wakati ambapo vitabu vyao vimepigwa marufuku wao wameendelea kusonga mbele katika kazi yao inayolingana na Maandiko ya kufanya wanafunzi wa Kristo kwa kutumia Biblia peke yake katika kazi ya kutoa ushuhuda. Wanafunzi wametokea!—Mt. 28:19, 20.
21. Waabudu wa Yehova wanamkanyaga-kanyaga “simba mdogo mwenye manyoya mengi shingoni” wa mfano kwa njia gani?
21 Mtunga zaburi anazidisha sana usemi wa mfano wakati anapozungumza kwa ulinganifu juu ya kukanyaga-kanyaga “simba mdogo mwenye manyoya mengi shingoni na nyoka mkubwa.” Bila shaka simba mdogo mwenye manyoya mengi shingoni ni mkubwa zaidi kwa umri na pia mwenye kutisha zaidi kuliko simba mdogo tu; na nyoka mkubwa ni jitu la mnyama mwenye damu baridi, ambaye Greek Septuagint Version ya Zaburi inamwita “joka.” Walakini, hata simba mdogo wa mfano mwenye manyoya mengi shingoni awe mwenye kuvutia namna gani, awe mwenye kutisha namna gani anapofanya shambulio lake la wazi kwa mbele, waabudu wa Yehova wanamkanyaga-kanyaga mshambuliaji hatari huyu. Wanaendelea kusonga mbele, wakimtii Mungu Aliye Juu Zaidi Sana kama Mtawala Mwenye Enzi Kuu badala ya wanadamu wenye mfano wa simba au matengenezo ya kufanyizwa na wanadamu yenye mfano wa simba. Wao wanamtolea Kaisari mwenye mfano wa simba vilivyo vya Kaisari peke yake na hawakosi kumpa Mungu cho chote kilicho chake, wakimpa vyote vilivyo vyake Yeye. (Matendo 5:29; Mt. 22:21) Kwa hiyo hawadhuriwi kiroho na tendo lenye kudhuru la “simba.”
22. Waabudu wa Yehova wanamkanyaga-kanyaga “nyoka mkubwa” wa mfano kwa njia gani?
22 “Nyoka mkubwa” mwenye mfano wa joka anatukumbusha juu ya baba ya “uzao” wa nyoka, Shetani Ibilisi, “nyoka wa zamani.” (Mwa. 3:15; Ufu. 12:9) Hapa mtunga zaburi anamwonyesha, si kama “jitu la mnyama wa baharini,” bali kama jitu la mnyama wa nchi kavu, mnyama mwenye damu baridi mwenye ukubwa usio wa kawaida, mwenye urefu wa kutosha kuweza kuzungusha mipindo yake juu ya mwanadamu amvunje-vunje na kummeza. (Yer. 51:34, NW) Kwa hiyo waabudu wa Yehova wakifahamu kwamba Shetani Ibilisi, kwa kutumia tengenezo lake kubwa sana la ulimwengu, anajaribu kuzungusha mipindo yake juu yao na kuwavunja-vunja kwa mikazo ya kilimwengu na kuwameza ndani ya tengenezo lake lenye kuongozwa na mashetani, wanajisuka-suka wajitoe na kumkanyaga-kanyaga “nyoka mkubwa” huyu. Wanaepuka na kupinga namna zote za uchawi, hivyo wasiruhusu mashetani waongoze nia yao na mapenzi yao kwa hila. (Luka 10:17) Kwanza, lazima mabaki yaliyotiwa mafuta ya warithi washirika wa Kristo wafanye hivi ikiwa wanataka kushiriki katika utimizo wa Warumi 16:20, kumponda Shetani chini ya miguu yao karibuni. Lazima wachukue hatua za hakika sasa juu ya “joka” huyu mwekundu kama moto na kumkanyaga sikuzote.—1 Pet. 5:8.
KUMPENDA MUNGU NA KULIJUA JINA LAKE
23. Mungu anasema nini katika Zaburi 91:14 kwa habari ya wale wanaopenda Yeye kwa sababu ya alivyo Yeye?
23 Shetani Ibilisi anakana kwamba viumbe vya kibinadamu haviwezi kumpenda Mungu Muumba kwa alivyo Yeye. Lakini Mungu Aliye Juu Zaidi Sana anauthamini upendo wa kweli wa hata viumbe vyake Yeye vya kidunia. Mtunga zaburi anaonyesha namna Mungu anavyoonyesha kuthamini kwake, wakati sasa anapomfananisha Mungu kama akisema hivi kwa habari ya waabudu Wake wenye upendo kama jamii: “Kwa sababu ametia mapendo yake yulu yangu, kwa hivi nitamuponesha, nitamuweka yulu kwa sababu ameyua jina langu.”—Zab. 91:14, Swahili Congo Bible.
24. Kwa hiyo, badala ya kupata usalama wa kiroho tu, kwa sababu gani waabudu Wake wamekimbilia kwake Yeye?
24 Waabudu wa Mungu mmoja aliye hai na wa kweli wamempenda kwa sababu yeye ndiye mfano bora wa upendo. Wao wameshikamana naye kwa upendano, mioyo yao ikiwa inamwelekea yeye kwa hiari. Wanaamriwa wampende yeye, lakini wanampenda kwa sababu yeye aliwapenda wao kwanza akaonyesha upendo huu kupitia kwa Mwanawe mzaliwa wa pekee, Yesu Kristo. (Kum. 7:7; 10:15; Marko 12:29, 30; 1 Yohana 4:19) Kwa hiyo si shauri tu la kupata usalama wa kiroho ambalo limewafanya wakimbilie kwake Yeye.
25. Yehova amewaokoa waabudu wake na nini, na namna gani juu ya wakati ujao?
25 Kwa kuwaonyesha upendo na wa kuitikia, Mungu Mwenye Nguvu Zote amewapa waabudu wake wokovu wasiwe mateka ya kidini ya ulimwengu huu na wasikomeshwe. Kwa ushuhuda wa hili, waabudu wake wa kweli wako leo katika wakati huu wenye hatari zaidi kupita nyakati zote nao wanaongezeka katika hesabu. Uwezo wake kutoa wokovu katika matukio ya wakati ujao wa shida ni mkuu bado kama zamani!
26. Maana inayotolewa Yehova anaposema: ‘Nitamlinda sababu amejua jina langu’ ni nini?
26 Wanaomwabudu Mungu Aliye Juu Zaidi Sana kwa roho na kweli hawatafutiliwa mbali kamwe watoke usoni pa dunia. Ama sivyo, jina lake lingefutiliwa mbali litoke duniani. Hii ndiyo maana ya kusema kwake hivi kwa habari ya ushirika wa waabudu wake: “Nitamuweka yulu [“ni tamlinda,” NW] kwa sababu ameyua jina langu.”—Zab. 91:14, Swahili Congo Bible.
27. Mwaka wa 1925, fikira zilianza juu ya nini, hii ikachapwa katika makala gani ya Watch Tower la Januari 1, 1926?
27 Kuanzia mwaka wa 1925 C.E. na kuendelea mabaki yaliyotiwa mafuta ya Israeli wa kiroho walifahamu kwamba Maandiko yalionyesha kwamba wakati ulikuwa umefika Mungu ajifanyie jina ulimwenguni pote. (Yer. 32:20; Isa. 63:12) Hii ilikaza fikira kwenye jina la Mungu la kipekee, Yehova. Kwa hiyo mwanzoni mwanzoni mwa mwaka uliofuata, wasomaji wa The Watch Tower walielekeana na ulizo lenye mwito, “Ni Nani Atakayemheshimu Yehova?” hiki kikiwa ndicho kichwa cha makala ya kwanza iliyochapwa katika toleo la gazeti hilo la Januari 1, 1926.
28. Mwaka wa 1928, ili kuonyesha kwamba waabudu wa Yehova walikuwa ‘wamemjua’ jina Lake, walifanya nini Katika kusanyiko la I.B.S.A. katika Detroit?
28 Punde kuliko miaka mitatu baadaye, kuonyesha kwamba walikuwa ‘wamejua’ jina la kimungu, International Bible Students Association walikubali kwa vifijo “Tangazo la Kumpinga Shetani na Kumwunga Yehova Mkono” katika kusanyiko la mataifa yote lililofanyiwa Detroit, Michigan, katika kiangazi cha mwaka wa 1928. Tangazo hili lililochapwa katika nakala nyingi ndipo lilipoenezwa duniani mwote kwa makumi ya mamilioni ya nakala. Mwaka huo wa maana wa 1928 walikuwako Wanafunzi wa Biblia 44,000 wenye kutoa ripoti ya utumishi wa shambani waliofanya ugawaji huo. Halafu kukatokea nini baadaye ili kufikia upeo?
29, 30. (a) Ili kulitangaza jina la kimungu hata zaidi, ni nini kilichofanywa juu ya mwandiko wa ukurasa wa kwanza wa The Watch Tower mwaka wa 1939? (b) Je! Yehova amejifanyia jina, na ikiwa ndivyo, basi kwa kutumia nani?
29 Jumapili alasiri, Julai 26,1931, Azimio lilikubaliwa kwa moyo likipendelea Jina Jipya, mashahidi wa Yehova, lichukuliwe katika kusanyiko la mataifa yote la I.B.S.A. katika Columbus, Ohio. Baada ya hapo Azimio hili lilikubaliwa na makundi ulimwenguni mwote ambayo kuanzia wakati huo na kuendelea walilitambua tengenezo lao la kidini kama mashahidi wa Yehova. Ili kulitangaza jina la kimungu hata zaidi, Machi 1, 1939, miezi kadha kabla ya Vita ya Ulimwengu ya Pili kutokea, gazeti rasmi la Mashahidi lilitokea likiwa na mwandiko, “The Watchtower Announcing Jehovah’s Kingdom.” Na sasa, mwaka wenye hatari wa 1975 unapoendelea, kwa kufaa inaweza kuulizwa hivi: Je! Mungu Aliye Juu Zaidi Sana wa unabii amejifanyia jina? Jibu linajionyesha wazi lenyewe, Ndiyo! Kwa kutumia nani? Si kwa kutumia Jumuiya ya Wakristo au Wayahudi, bali kwa kutumia mashahidi wa Yehova wa Kikristo!
30 Kwa kweli, ulinzi wa Yehova juu ya waabudu wake kwa sababu ‘wamejua jina langu’ umemaanisha kulinda jina lake mwenyewe na kuwa na njia ya kutangazia jina lake ‘katika dunia yote.’—Rom. 9:17; Kut. 9:16.
31. Wameamua kutembea katika jina la nani, na kuomba msaada juu ya jina la nani?
31 Uamuzi wa mashahidi hawa wa Yehova wa Kikristo sasa ni ule wa Mika 4:5, NW: “Mataifa yote, kwa upande wao, watatembea kila moja katika jina la mungu wake; lakini sisi, kwa upande wetu, tutatembea katika jina la Yehova Mungu wetu kwa wakati usiojulikana, hata milele.” Wao wataendelea kuomba msaada juu ya jina Lake, wakiwa na hakika kabisa katika yale anayosema baada ya hapo, katika Zaburi 91:15: “Ataniita na nitamujibu; nitakuwa pamoya naye katika taabu; nitamuponesha na kumuheshimu.” (Swahili Congo Bible)
WOKOVU NA UTUKUZO
32. Yehova anaonyeshaje kwamba hakuwakataa mashahidi Wake wamwombao, na yeye bado ataonyeshaje hivyo?
32 Kwa sababu ya ukatili wa ulimwengu unaoendelea kuongezeka juu yao na kwa sababu ya vita ya Shetani Joka isiyokoma juu yao, waabudu wa Yehova tayari wamepitia katika taabu nyingi. Lakini, kulingana na neno lake, Yehova sikuzote amekuwa pamoja nao, asiwakatae kamwe wasiwe mashahidi Wake. Katika taabu kuu sana ambayo ingali mbele yao, wakati ulimwengu mwovu huu unapokuja kwenye mwisho wake katika uharibifu kamili, Yehova atakuwa pamoja na waabudu wake naye atajulisha hili kwa mwujiza! Badala ya kuwaacha waharibiwe kwa njia ya aibu na adui zao wote wanaoonekana na wasioonekana, Yehova anasema hivi: “Nitamwokoa na kumtukuza,” (UV) au, “kumleta kwenye heshima.”—New English Bible.
33, 34. Baada ya kuokolewa, ni kwa njia gani waabudu wa Yehova watatukuzwa Naye?
33 Utukuzo ulioahidiwa hapa kwa lazima haumaanishi utukuzo wa washiriki wa mabaki yaliyotiwa mafuta ya Israeli wa kiroho katika mbingu pamoja na Mfalme anayetawala Yesu Kristo. Huu utatokea katika wakati wake Yehova, baada ya “maisha ndefu” zilizoahidiwa.
34 Lakini tayari Yeye ameokoa waabudu wake duniani kwa njia ya ajabu sana, na hii imewaletea utukufu wa kiroho, nayo hiyo ikaliletea jina Lake heshima. Baada ya kuokolewa huko kwa njia ya kimungu, wamependelewa kupata utukufu juu ya adui zao, ambao pia ni adui zake Yeye. Mpaka leo hii wameheshimiwa na utumishi zaidi duniani kama mashahidi wake Yeye na watangazaji wa ufalme Wake wa Kimasihi. Bila shaka, wakati wa “dhiki kubwa” ya ulimwengu inayokuja na upeo wake katika “vita ya siku ile kuu ya Mungu Mwenyezi” katika Har–Magedoni ndipo wokovu wa Yehova ulio mkuu zaidi na wa kusifika zaidi sana utakapotokea juu yao. Kwa hiyo, wataiokoka “dhiki kubwa” hiyo itakayoharibu ulimwengu waushiriki utukufu wa upande utakaoshinda wa Vita zote! Wataheshimiwa kwa kukubaliwa waingie katika taratibu mpya ya Mungu ya dunia hii.
35. Hivyo wataendelea kuishi wafurahie utukufu gani duniani, na ni nini kwa upande wa Mungu kinachowawezesha hili?
35 Hivyo wataendelea kuishi wafurahie utukufu wa kuwa wale ambao Mungu Aliye Juu Zaidi Sana ataokoa atakapofanya vita kwa ushindi kwa ajili kushuhudia enzi kuu yake ya ulimwengu wote na kutakaswa kwa jina linalostahili. (Ufu. 16:14, 16; Eze. 38:23; Zab. 83:18) Wokovu wake juu yao utawawezeshea hili. Kupitia kwa mtunga zaburi wake, Yehova anasema hivi anapomalizia zaburi hii iliyo tamu sana: “Kwa maisha ndefu nitamushibisha, na kumwonesha wokovu wangu.”—Zab. 91:16, Swahili Congo Bible.
36. Ni wakati gani tumaini la kuokoka “vita” ya Mungu katika Har–Magedoni lilipoonyeshwa kwa mabaki, nao wanaweza kuridhishwa kwa “maisha ndefu” duniani kwa kadiri gani?
36 Ni kuanzia tu mwisho wa mwaka wa 1928 tumaini lilipofahamishwa kiroho kwa mabaki yaliyotiwa mafuta ya “Israeli wa Mungu” juu ya kuiokoka “vita ya siku ile kuu ya Mungu Mwenyezi” katika Har–Magedoni na kuingia katika taratibu mpya yenye haki ya Yehova hapa duniani. (Tazama The Watch Tower chini ya tarehe ya Desemba 15, 1928, ukurasa 376, mafungu 35, 36.) Na sasa, mwaka wa 1975 unapoendelea, maelfu kadha ya mabaki yaliyotiwa mafuta, ambao wangali hai juu ya dunia hii, wanatazamia kupata tumaini hilo lenye furaha tele. “Mkutano mkubwa” unaoongezeka wa wenzi wao wenye mfano wa kondoo wanatazamia kuingia katika Taratibu Mpya bila ya kufa. Katika Taratibu Mpya Yehova Mungu ataongezea “maisha ndefu” za mabaki yaliyotiwa mafuta duniani hata awaridhishe washiriki wake. Haijulikani kama watabakizwa hapa duniani waone mwanzo wa ufufuo wa wafu wa kidunia na kukutana na mashahidi waaminifu wa kale, nyakati za kabla ya Ukristo. Wangefurahia jambo hilo, kabla ya kuondolewa duniani kupelekwa kwenye thawabu ya kimbinguni wakawe pamoja na Kristo.
37. Itawezekana washiriki wa “mkutano mkubwa” waridhishwe kwa “maisha ndefu” gani?
37 Wale wa “mkutano mkubwa,” ambao watabaki waaminifu kwa Mwenye Enzi Kuu wa Ulimwengu Wote Yehova Mungu hata kupita jaribu la kukata maneno baada ya mwisho wa utawala wa miaka elfu wa Kristo juu ya wanadamu, wataridhishwa na “maisha ndefu” hata uzima wa milele, uzima usio na kikomo katika “Paradiso ya Furaha” ya kidunia chini ya enzi kuu ya ulimwengu wote ya Yehova. Loo! ibada ya Yehova ni yenye kuthawabisha kama nini!
38. Ye yote ‘anayekaa katika pahali pa maficho’ akifa kwa uaminifu kabla ya mwisho wa vita ya Mungu katika Har–Magedoni na kutiwa kwa Shetani katika shimo refu lisilopimika, kwa sababu gani hii haitashuhudia kuwa usalama wa kiroho si wa maana kupita mwingine wo wote?
38 Je! sasa tunathamini, je! tunatamani kwa unyofu wa moyo usalama wa kiroho anaoutoa Yehova Mungu? Je! namna hii ya usalama si ya maana kupita usalama mwingine wo wote ikiwa tunataka tulindwe tukapate thawabu tukufu ambazo Yeye ameweka akibani kwa ajili ya waabudu wake waaminifu wote? Wote wale wanaobaki kwa tumaini katika mahali pa Yehova pa usalama wa kiroho, ‘wakiikala kwa pahali pa maficho yake Aliye yulu,’ ‘wataoneshwa wokovu wangu,’ na Yehova. (Zab. 91:16, Swahili Congo Bible) Hii itaendelea kuwa kweli, hata siku za mtu katika uaminifu zikifupizwa na kifo kabla ya Taratibu Mpya yenye haki kuletwa baada ya “vita” ya Yehova katika Har–Magedoni na kufungwa kwa Shetani na mashetani wake katika shimo refu lisilopimika. (Ufu. 20:1-6) Mungu Mwenye Nguvu Zote angali anaweza kutoa wokovu kutoka kifo cha uaminifu kwa njia ya ufufuo wa wafu ulioahidiwa. Wale wanaoacha mahali pa kimungu pa usalama wa kiroho hawatapita kamwe “dhiki kubwa” inayokuja wakiwa na kibali ya Mungu na kuona wokovu Wake!
39. Imempasa kila mmoja wetu atake kuwa na furaha gani, nasi tunawezaje kumwacha Yeye awe nayo?
39 Yehova atafurahia kutuonyesha wokovu Wake kupitia kwa Yesu Kristo Mwanawe. Kila mmoja wetu na amwache Yeye kwa upendo awe na furaha hii ya kimungu. Tunaweza kufanya hivyo kwa kubaki kwa ustahili katika “pahali pa maficho” pa usalama wa kiroho ambao amewapa waabudu Wake waaminifu,—Mit. 21:31; Ufu. 7:9-17.
—Kutoka The Watchtower, Dec. 15, 1974.