Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w75 7/15 kur. 324-330
  • Kufuatia Njia ya Maisha Yenye Kuridhisha

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kufuatia Njia ya Maisha Yenye Kuridhisha
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • UHURU WA KUTOKUKATA TAMAA
  • JITIHADA INAHITAJIWA
  • Je, Biblia Inazungumza Kuhusu Toharani?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Imani Yako Katika Ufufuo Ni Yenye Nguvu Kadiri Gani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
  • Je, Unaweza Kuwasaidia Wafu?
    Amkeni!—2006
  • Jumuiya ya Wakristo Imesaliti Mungu na Biblia
    Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai?
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
w75 7/15 kur. 324-330

Kufuatia Njia ya Maisha Yenye Kuridhisha

1. Kwa sababu gani mamilioni ya watu leo hawaridhishwi na maisha?

IDADI kubwa za wakaaji wa dunia hawapati uradhi wa kweli katika maisha. Wengi wanatumikishwa kwa sababu ya mafundisho ya dini za uongo juu ya kifo na wafu. Wengine wanashindwa na mawazo ya ndani ya kujiona hawana tumaini na kukata tamaa. Mamilioni na mamilioni ya watu wanahitaji sana ukombozi wapate kuanza kufuatia njia ya maisha yenye kuridhisha kweli kweli. Fikiria:

2-4. Imani juu ya wafu zimehusuje washiriki wa dini zisizo za Kikristo?

2 Mamilioni ya watu katika karibu Asia yote na sehemu za Afrika wanaamini kwamba maisha yao yote lazima wawape babu zao waliokufa heshima. Mbele ya nguzo za jamaa zao waliokufa, wanafukiza ubani, wanasali, kuweka maua na hata kutoa chakula kama sadaka. Kwa sababu gani wanafanya mambo haya? Wamefundishwa kwamba heshima hiyo itawasaidia wafu wafurahie kuwako kwenye kupendeza katika maisha yafuatayo na kuwazuia wasiwe roho wakatili.

3 Hasa katika habari ya maombolezo na mazishi waokokaji wanajitahidi sana wakifanya mambo mengi ya gharama nyingi kuwasaidia waliokufa. Ziko sehemu za Mashariki ambako nyumba za karatasi na vyombo vingine vya karatasi vyenye thamani ya mamia ya shilingi, nyakati nyingine hata maelfu ya shilingi, zinachomwa kuzisaidia roho za wafu.

4 Imani katika purgatori (tohara) ndio msingi mkuu wa mazoea haya. Baada ya kufa kwa mtu, roho inaaminiwa kutanga-tanga purgatori miaka miwili, ikihitaji msaada kuingia mbinguni. Sadaka zinazotolewa za vifaa vya karatasi zimekusudiwa kuonyesha kwamba mtu aliyekufa aliishi maisha mema na anacho kila kitu kinachohitajiwa ili aendelee kufanya kazi katika ulimwengu ufuatao. Watu wengi wa nchi za Mashariki wanaamini kwamba ataondolewa purgatori karibuni zaidi kwa kutumia njia hizo.

5. Wengi katika Jumuiya ya Wakristo wamefanya nini wakitumaini kupunguza wakati wao wenyewe au wa wapendwa wao katika purgatori?

5 Je! mambo yako tofauti katika Jumuiya ya Wakristo? Hasha. Kwa karne nyingi matajiri na maskini pia wamekuwa wakilipa fedha nyingi kwa matengenezo ya kidini wakitumainia kupunguza wakati wao na wa wapendwa wao wenyewe katika purgatori. Katika habari ya mazoea haya, mtungaji Corliss Lamont katika kitabu chake The Illusion of Immortality anasema hivi:

“Tangu [mwaka wa 500 mpaka wa 1500 wa Wakati wetu wa Kawaida] Kanisa la Katoliki limepata pesa nyingi sana kutoka kwa matajiri na maskini pia, kwa kutolewa kwa mapendeleo tu. Mapendeleo haya, yaliyotolewa baada ya malipo ya fedha, kutoa sadaka za kusaidia maskini au sadaka za namna nyingine, yanaamuru kwamba nafsi ya mtu mwenyewe au nafsi ya jamaa aliyekufa au rafiki iondolewe adhabu yote au sehemu fulani yake iliyopangiwa katika purgatori. . . . Katika Urusi Kanisa la Orthodoksi lilikusanya utajiri mwingi sana kwa kutoa maombi kama hayo kwa ajili ya wafu. Zaidi ya mapato ya kawaida kutoka kwa wafanya kazi na wakulima wenye hamu nyingi ya kupunguza kisasi cha kimungu, washiriki wengi makabaila na matajiri walikabidhi nyumba za watawa na makanisa mali zao kwa sharti la kwamba sala za kila siku zitatolewa kwa ajili ya nafsi zao marehemu.”​—Kur. 17, 18.

6. Watu wengi wana maoni gani juu ya wanayoweza kufanya wafu kwa walio hai?

6 Imani ya kwamba walio hai wanahitaji kulindwa na wafu imeenea sana pia. Katika sehemu nyingi za Afrika, wakati ugonjwa unapoingia katika jamaa, wakati mtoto anapokufa, wakati biashara inapoharibika au misiba mingine yo yote inapotokea, mwanamume anamwendea mchawi kwa haraka. Kwa kawaida mchawi anamwambia kwamba mshiriki wa jamaa aliyekufa amekosewa. Mwaguzi anafikiwa na dhabihu kuagizwa. Kwa kweli, mchawi anatoza pesa nyingi kwa jambo hili. Pia anapewa nyama ya mnyama anayetolewa kama dhabihu.

7, 8. Biblia inafunua nini juu ya hali ya wafu?

7 Kweli ya Neno la Mungu inakomboa na uongo huo wenye kutumikisha. Biblia inaonyesha waziwazi kwamba nafsi inakufa na kwamba hakuna cho chote kinachoendelea kuwa hai baada ya kufa kwa mwili. (Eze. 18:4, 20, NW) Hakuna sababu ya kuwaogopa wafu. Mhubiri 9:6 anasema hivi juu yao: “Mapenzi yao na machukio yao, na husuda yao, imepotea yote pamoja; wala hawana sehemu tena katika jambo lo lote lililofanyika chini ya jua.”

8 Kwa sababu kama hizo, wafu hawawezi kusaidiwa na walio hai. Wameyarudia mavumbi yasiyo na uhai. (Mwa. 3:19; Zab. 104:29) Wakiwa wasio na uhai, wasio na fahamu, wasingeweza hata kidogo kuwa mahali po pote pa mateso ya milele au ya muda. Neno la Mungu, katika Warumi 6:7, linasema waziwazi hivi: “Yeye aliyekufa amehesabiwa haki mbali na dhambi.” Hiyo isingekuwa kweli kama angeendelea kuadhibiwa kwa sababu ya dhambi zake baada ya kufa. Badala ya kuhesabiwa haki, angekuwa bado akitaabika kwa sababu ya dhambi zake.

9, 10. Wanadini wa Jumuiya ya Wakristo wanakubali mambo gani juu ya nafsi ya kibinadamu, ‘‘hell” na purgatori?

9 Wanafunzi wa Jumuiya ya Wakristo wanajua yale Biblia inayofundisha juu ya hali ya wafu. Katika vitabu vyao vya dini wanakubali kwamba Maandiko hayafundishi kutokufa kwa nafsi ya kibinadamu na kwamba fundisho hili na mafundisho mengine yametokana na filosofia ya kipagani ya Wagiriki. Mtaalamu Douglas T. Holden anaandika hivi, “Uanadini wa Kikristo umechangamana sana na filosofia ya Kigiriki hata imefanyiza watu wenye sehemu tisa za wazo la Kigiriki na sehemu moja ya wazo la Kikristo.”(Death Shall Have No Dominion, uk. 14) Naye mwanadini Mfaransa Oscar Cullman aliitaja imani juu ya nafsi isiyokufa kama “mojawapo la makosa makubwa zaidi ya Ukristo.”​—Immortality of the Soul or Resurrection of the Dead?, uk. 15.

10 Kwa habari ya wazo la mateso ya milele katika hell yenye moto, gazeti la Katoliki la Commonweal (Januari 15,1971, uk. 370) lasema hivi: “Kwa watu wengi, kutia na wanafilosofia fulani, heli inatosheleza haja ya kuwaza kwa kibinadamu​—ni namna ya kinyume cha roho ya Krismas, . . . Ni nani kati ya wenye haki asiyependa kuona wadhalimu wakiadhibiwa kwa haki fulani? Na iwapo si katika maisha haya, mbona isiwe hivyo katika yatakayofuata? Walakini, maoni hayo hayapatani na Agano Jipya, linalomtia moyo mwanadamu aishi na kupenda.” Kwa habari ya fundisho la purgatori, New Catholic Encyciopedia kinakubali waziwazi hivi: “Fundisho la Katoliki juu ya purgatori ni lenye msingi wa mapokeo, si Maandiko Matakatifu.”​—Vol. 11, uk. 1034.

11, 12. (a) Kwa sababu gani inaweza kusemwa kwa kufaa kwamba viongozi wa kidini wa Jumuiya ya Wakristo wamekuwa wakieneza “mafundisho ya mashetani”? (b) Ni udanganyifu gani umeendeshwa na viongozi wa kidini wa Jumuiya ya Wakristo kwa faida yao wenyewe?

11 Lakini kwa kweli mambo haya yanafundishwa makanisani? Je! viongozi wa kidini wanaambia makundi yao kwamba nafsi inakufa, kwamba fundisho la mateso ya milele katika “hell “yenye moto ni kinyume cha roho ya Ukristo na kwamba imani katika purgatori haina msingi wa Biblia? Au, mapadre kwa ujumla wanazidi kueneza “mafundisho ya mashetani”? (1 Tim. 4:1) Je! jibu la Ndiyo kwa ulizo la mwisho ni hukumu kali mno? Basi, je! wanafunzi wa Jumuiya ya Wakristo wenyewe hawakubali mafundisho hayo kuwa ya uongo? Na ikiwa mapadre wanazidi kufundisha mafundisho yanayojulikana kuwa ya uongo, je! wao hawafuati mfano wa yeye ambaye Yesu alimsema kuwa ‘baba wa uongo’? (Yohana 8:44) Zaidi ya hayo, je! fundisho la mateso ya milele halionyeshi nia ya kutisha, mbaya sana na ya ukatili ya mashetani?

12 Biblia inasema: “Mungu ni upendo.” (1 Yohana 4:8) Lakini mafundisho ya moto wa “hell” na purgatori yanamsingizia vibaya sana. Kwa hiyo wanaofundisha mafundisho hayo wanasema makufuru juu ya Mungu. Kwa kuwa ndivyo ilivyo, matengenezo ya kidini yamekuwa pia yakipata pesa nyingi sana kwa kujisingizia. Badala ya kufariji yatima na wajane katika wakati wao wa huzuni nyingi sana, viongozi wengi wa kidini kwa ushupavu wa moyo wamewatumia kwa faida yao wenyewe kwa kukubali pesa za sherehe zisizofaa kitu. Hii imeletea maskini hasa magumu, ambao wangaliweza kutumia pesa hizo kwa riziki.

13. Kwa sababu gani mapadre wa Jumuiya ya Wakristo hawawezi kutolea sababu kufundisha kwao mafundisho ya uongo?

13 Ingawa huenda viongozi wengine wa kidini wakawa hawafahamiani na ushuhuda wa Biblia, imewapasa wafahamiane nao. Wanajitokeza kama wenye kusema ujumbe wa Mungu na kwa hiyo wako chini ya wajibu wa kujua Biblia isemavyo. Bila shaka wanajua sana kwamba wanayoyafanya na kusema yaweza kubadili sana maisha za wale wanaowategemea kwa maagizo. Hiyo imepaswa iwafanye waangalifu katika kuhakikisha mafundisho yao. Kusingizia ko kote kubaya juu ya Mungu kwaweza kuondoa watu katika ibada ya kweli, kuwaelekeza kwenye madhara.

14. Kwa sababu ya masingizio ya dini ya uongo juu ya Mungu na kutumia watu wake kwa kujifaidi yenyewe, ni maulizo gani tunayoweza kujiuliza?

14 Je! wewe waonaje juu ya kutumia watu vibaya kwa dini ya uongo na kusingizia kwake kubaya juu ya Muumba wetu? Je! wataka kuona jina la Mungu likiondolewa lawama iliyoletwa juu yake kupitia kwa mafundisho ya uongo? Je! watamani kuona kila jitihada ikitiwa ili kuwaweka huru watu wenye mioyo minyofu na uongo wa kidini? Je! una nia ya kushiriki katika kufunua wazi makosa ya kidini? Hiyo bila shaka ndiyo tamaa ya kila mtumishi mwaminifu wa Yehova Mungu.

UHURU WA KUTOKUKATA TAMAA

15. Kwa sababu gani wengi wanaotambua dini ya uongo inatumia watu kwa faida yao wenyewe hawaridhishwi bado na maisha?

15 Bila shaka, watu wengi leo wamegundua kwamba dini ya uongo inatumia watu kwa kujifaidi yenyewe. Lakini hilo halikutosha kuwapa uhuru wa kweli na kuwaweka katika njia ya maisha yenye kuridhisha kweli kweli. Sababu gani sivyo? Kwa sababu wanakosa imani ya kweli na tumaini. Kwa hiyo hawalindwi na pigo lenye madhara ambalo wanaweza kulipata kutoka kwa matukio ya ulimwengu kwa akili na katika mawazo ya moyoni.

16. Kumekuwa kukitukia nini hasa ulimwenguni, na hii imeleta nia gani kati ya watu wengi?

16 Fikiria kidogo ambayo yametukia. Mamilioni yametoweka kama mateka ya vita, uvunjaji wa sheria, ghasia na njaa kuu. Hewa na maji yenye kutegemeza uhai yanachafuliwa kwa kadiri ya kuogofya. Yaelekea kutoka kila upande maisha ya mwanadamu yanatishwa. Na hakuna lo lote la kutoa uhakikisho wa kweli kwamba wanadamu wataweza kutatua magumu yao wakati ujao ulio karibu. Hii imefanya hata wengi wa wale ambao wameipa dini ya uongo kisogo wajitenge kando kwa kukata tamaa kabisa. Kwa kadiri wawezavyo kuona, uzima ndio uu huu tu. Kwa kufaa Biblia inaisimulia nia yao. Wao wanasema: “Na tule, na tunywe, maana kesho tutakufa.”​—1 Kor. 15:32.

17. Watu wengi wanafanya nini leo katika jaribio la kuepuka magumu ya maisha?

17 Katika jitihada ya kuepuka magumu ya maisha, wengi wanaanza kutumia vileo vikali sana au dawa za kulevya. Wengine wanajaribu kutafuta njia ya kutoka katika migogoro yao na wasiwasi kwa kujitia katika ufisadi. Wanazoea uasherati, uzinzi, kulalana na wanaume wenzao au wanawake wenzao. Kwa habari ya matokeo ya wasiwasi wa maisha yanayowapata watu, Ignace Lepp, katika kitabu chake Death and Its Mysteries (kilichotafsiriwa kutoka kwa Wafaransa na Bernard Murchland,) anasema hivi: “Yaelekea kuwa watu wengi zaidi walio timamu leo wanapatwa na woga huu wa kufa kabisa, angaa kwa kutokujua. Walau haya ni maelezo machache juu ya sababu ya kuwapo mchafuko wa nyakati zetu, uharabu wa ovyo ovyo wa vitu, nyege na mwendo unaoongezeka wa maisha. Hata muziki wa kisasa na dansi zaelekea kuonyesha kukata tamaa kwa wanadamu wasiouamini wakati wao ujao tena.” (Uk. 49) Matokeo ya kushindwa na mawazo ya kukata tamaa kisha kujaribu kuyaepuka yamekuwa nini?

18-20. Matunda gani mabaya yametokana na kunywa kupindukia, mazoea ya kutumia dawa za kulevya na ufisadi?

18 Huenda wale wanaolewa kupindukia wakasahau shida zao kwa muda. Lakini wanajipotezea heshima yao na, wanapokuwa wamelewa, nyakati nyingine wanajidhuru wenyewe au wengine. Na kesho yake, wanakuta kwamba wameongeza maumivu mengi ya kichwa kwa taabu walizokuwa wamekwisha zipata. Magonjwa mabaya sana pia yanaletwa na kunywa kupindukia.

19 Wenye kuzoea dawa za kulevya, pia, wanagharimiwa sana na jitihada zao za kuepuka magumu ya maisha. Mara nyingi wanapatwa na madhara yenye kuendelea ya kimwili na ya akili. Na ili kutegemeza tabia yao yenye gharama, wengi wanajishusha kwa kujitia katika wizi au umalaya.

20 Namna gani juu ya ngono za ovyo ovyo? Je! zinasaidia kuendeleza maisha ya mtu? Sivyo, bali matunda yake mara nyingi ni magonjwa ya kuchukiza sana kama kisonono na kaswende, mimba zisizotakiwa, watoto wa haramu, kutoa mimba, nyumba zilizogawanyika, wivu mkali sana, kupigana na hata uuaji.

21, 22. Ni matokeo gani mema yanayotokana na kutumia kanuni za Biblia?

21 Watu wengi kweli kweli ni wenye huzuni. Wanahitaji tumaini na imani ya kweli wapate kuwekwa huru na kukata kwao tamaa na magumu yanayotokea kwa sababu hiyo. Neno la Mungu linaweza kuwasaidia, ikiwa tu watajifunza na kulitumia. Haya ndiyo yamekuwa maono ya mashahidi wa Yehova wa Kikristo. Wao wameona kwamba kutumia kanuni za Biblia kunafanya uhusiano nyumbani uwe bora, kazini na katika shughuli za kila siku na wengine. (Rum. 12:17-21; 13:8-10; Efe. 5:22-6:4; 1 Pet. 3:1-7) Hii imesaidia sana kufanya maisha yao yawe yenye furaha zaidi na yenye kuridhisha zaidi hata sasa.

22 Je! hii maana yake ni kwamba mtu anayetumia kanuni za Biblia katika maisha yake ya kila siku hawezi kupatwa na magumu na mikazo ya ulimwengu? Sivyo, yeye angali yumo kati ya watu ambao hawapendi haki. Lakini anaweza kushindana na magumu ya maisha kwa kufaa zaidi kuliko wale wanaotegemea kuwaza kwa kibinadamu tu. Yeye haoni uchungu kwa sababu ya udhalimu ambao huenda ukampata. Anajua sababu yake na anasadiki kabisa kwamba ufalme wa Mungu kupitia kwa Kristo karibuni utakomesha mambo yote yanayozuia furaha kamili ya maisha. (2 Pet. 3:11-13) Yeye analindwa asije akakata tamaa na kujidhuru mwenyewe katika majaribio ya bure ya kuepuka kukata tamaa.

23, 24. Faida ambazo tumepata kwa kuzoea ibada ya kweli zimepaswa zihusuje tunayofanyia wanadamu wenzetu?

23 Wakifahamu hili, Wakristo walio wakf imewapasa bila shaka wachochewe mioyoni mwao kusaidia wanadamu wenzao waanze kufuata njia ya maisha yenye kuridhisha. Hiyo maana yake ni kujihakikisha kuwa namna ya mtu ambaye Yesu Kristo alizungumza juu yake katika Mathayo 13:23: “Huyu ndiye alisikiaye lile neno [la ufalme], na kuelewa nalo; yeye ndiye azaaye matunda, huyu mia, na huyu sitini, na huyu thelathini.”

24 Je! wewe ni wa namna hiyo? Je! moyo wako unaendelea kuitikia kwa kulithamini ‘neno la ufalme’? Je! hili linakuvuta utafute nafasi ya kushiriki na wengine ujumbe wa Ufalme ili wao wapate kuanza kuifurahia njia bora kupita zote ya maisha sasa? Ikiwa ndivyo, unaweza kubaki ukiwa na uhakika wa kibali na baraka ya Yehova.

JITIHADA INAHITAJIWA

25. Kwa sababu gani jitihada inatakiwa kufuatia njia ya maisha yenye kuridhisha?

25 Kufuatia njia ya maisha yenye kuridhisha kunataka tutie jitihada nyingi. Sisi wanadamu ni watenda dhambi na kwa hiyo tunapaswa kujitahidi tuzuie maelekeo ya kutenda dhambi. Hatuwezi kuruhusu maelekeo hayo yatushinde, kwa njia hiyo yatutie utumwani mwa mtawala wa ulimwengu huu, Shetani. (Yohana 14:30; 2 Kor. 4:4) Kwa habari yake mwenyewe, mtume mwaminifu Paulo aliwaandikia Wakorintho hivi: “Nautesa mwili wangu na kuutumikisha; isiwe, nikiisha kuwahubiri wengine, mwenyewe niwe mtu wa kukataliwa.” (1 Kor. 9:27) Yeye alitumia kila njia aliyoweza kupata atiishe maelekeo yenye dhambi, akapata ushindi juu yake.

26. Ni nini kinachoonyesha kwamba mapadre wa Jumuiya ya Wakristo wanakosea kudai kwamba imani katika moto wa “hell” inasaidia kama kichocheo cha kufuata mwenendo ufaao?

26 Ni nini kilichomvuta Paulo na wanafunzi wengine waaminifu wa Yesu wafanye hivi? Viongozi wengi wa kidini wa Jumuiya ya Wakristo wamedai kwamba woga wa mateso ya moto unakuwa kama kichocheo cha kuwa na mwenendo ufaao. Lakini mambo ya hakika ya historia yaonyesha vingine. Mauaji ya kutisha ya wazushi wa dini na mapigano ya umwagaji wa damu ya imani za Jumuiya ya Wakristo ni uhakikisho wa kwamba mengine ya matendo ya ukatili yaliyo makuu kupita yote yamefanywa na waamini katika fundisho lisilolingana na Maandiko la moto wa mateso.

27. Nia inayofaa ya kumtumikia Yehova Mungu ni nini?

27 Kuogopa adhabu sicho kichocheo kifaacho cha kumtumikia Mungu. Yehova Mungu anataka ibada yetu ichochewe na upendo. Hiyo imekuwa tamaa yake sikuzote juu ya viumbe vyake vyenye akili. Liangalie ombi ambalo Musa aliwafanyia Waisraeli: “Nimekuwekea mbele yako uzima na mauti, baraka na laana; basi chagua uzima, ili uwe hai, wewe na uzao wako; kumpenda [Yehova], Mungu wako, kuitii sauti yake, na kushikamana naye; kwani hiyo ndiyo uzima wako, na wingi wa siku zako.”​—Kum. 30:19, 20.

28, 29. (a) Kwa sababu gani tuna sababu nzuri kumpenda Yehova? (b) Mtume Petro anatiliaje jambo hili mkazo katika barua yake ya kwanza?

28 Bila shaka tuna sababu nzuri ya kumpenda Yehova sana sana na kuonyesha upendo wetu kwa kutii amri zake. Yehova ndiye aliyechukua hatua ya kwanza katika kutuonyesha upendo mwingi sana. Kama wanadamu wasiokamilika tusingeweza kuwa na hali yenye kukubalika mbele zake kwa ustahili wetu wenyewe. Mshahara wa pekee ambao sisi wenye dhambi twaustahili ni mauti. (Rum. 6:23) Lakini katika upendo wake usio na mipaka Yehova Mungu alimtoa Mwanawe kwa ajili yetu ili dhambi zetu zilipiwe na kuweza kuwa na hali yenye haki. Hilo halikuwa jambo dogo kwa upande wa Yehova. Yeye alimpenda Mwanawe sana lakini akamwacha apatwe na aibu nyingi sana, ndiyo, hata kifo cha aibu juu ya mti wa kufishia. Kwa habari ya Yesu Kristo, yeye alikuwa na nia ya kupatwa na haya kwa kuonyesha upendo wake kwa wanadamu.​—Yohana 10:17, 18.

29 Kwa kweli, yale ambayo Yehova Mungu na Kristo Yesu wamefanya kwa ajili yetu yamepaswa yachochee ndani ya mioyo yetu shauku ya kujiongoza kupatana na mapenzi ya kimungu. Hii ndiyo maana ambayo mtume Petro alionyesha alipokuwa akiwatia moyo waamini wenzake: “Enendeni kwa hofu [yaani, kwa hofu ifaayo ya kutotaka kumchukiza Yehova Mungu] katika wakati wenu wa kukaa hapa kama wageni. Nanyi mfahamu kwamba mlikombolewa si kwa vitu viharibikavyo, kwa fedha au dhahabu; mpate kutoka katika mwenendo wenu usiofaa mlioupokea kwa baba zenu; bali kwa damu ya thamani, kama ya mwanakondoo asiye na ila, asiye na waa, yaani, ya Kristo. Naye amejulikana kweli tangu zamani, kabla haijawekwa misingi ya dunia; lakini alifunuliwa mwisho wa zamani kwa ajili yenu; ambao kwa yeye mmekuwa wenye kumwamini Mungu, aliyemfufua katika wafu akampa utukufu; hata imani yenu na tumaini lenu liwe kwa Mungu.”​—1 Pet. 1:17-21.

30, 31. Tofautisha mwenendo wa Wakristo wa kweli na namna walivyoishi kabla ya kujifunza kweli.

30 Je! wewe unaithamini kweli dhabihu yenye thamani nyingi ya Yesu Kristo? Je! unaonyesha hivi kwa namna unavyojiongoza mwenyewe? Je! unafanya yafaayo yanayostahili kufanywa na mtu ambaye ameonyeshwa upendo na ambaye kwa ajili yake dhabihu hiyo isiyolinganika thamani yake ilitolewa? Imetupasa sote tufanye hivyo. Kwa sababu hiyo, twaombwa hivi katika 1 Petro 1:14, 15: “Kama watoto wa kutii msijifananishe na tamaa zenu za kwanza, za ujinga wenu; bali kama yeye aliyewaita alivyo mtakatifu, ninyi nanyi iweni watakatifu katika mwenendo wenu wote.”

31 Ikiwa tu Wakristo walio wakf bila shaka tumefaidika kutokana na dhabihu ya Yesu yenye kulipia dhambi. Kwa hiyo imetupasa tuchukie namna ambavyo tuliishi kabla hatujawa na imani ya kweli na tumaini, wakati tulipokuwa hatuthamini yale ambayo Yehova Mungu na Yesu Kristo walitufanyia. Katika ujinga wetu, tuliishi kwa kujitafutia faida zetu wenyewe tu. Tulishindwa na tamaa zetu, isipokuwa tu tulipozuiwa na kuogopa mamlaka au kuogopa kudhuru afya zetu, mali zetu au sifa zetu. Lakini ni wangapi kati yetu waliojiona hasa kuwa wenye wajibu kwa Muumba na Mpaji wa Uzima?

32. Ni nini linalomaanishwa na kuwa kwa Yehova “mtakatifu”?

32 Walakini, sasa tuna kichocheo chenye nguvu cha kujipatanisha na kanuni ya utakatifu tuliyowekewa kama mfano na Baba yetu wa kimbinguni mwenye upendo. Yehova Mungu ni “mtakatifu,” asiye na waa na safi kabisa. Yeye ni mwema kabisa tena kabisa, asiye na waa lo lote lile la ubaya au upotovu. Yeye ndiye Chanzo cha kanuni na sheria zote za haki.​—Zab. 19:7-10; 119:137, 138, 160.

33, 34. Kufuata shauri la 1 Petro 2:1 kunataka nini kwetu?

33 Tukivutwa na kumpenda yeye, imetupasa tutake kuwa kama yeye. Kwa hiyo imetupasa tutake kutupilia mbali maelekeo yo yote yanayoupinga utakatifu wake. Hilo ndilo onyo linalotolewa katika 1 Petro 2:1, ambapo tunasoma hivi: “Wekeni mbali uovu wote na hila yote, na unafiki na husuda na masingizio yote.” Hii inataka nini kwetu?

34 Nia kuu ya mioyo yetu imepaswa isiwe na ubaya wa namna yo yote. Imetupasa tuzuie hata wazo la kudanganya wengine kwa faida ya kichoyo, hata liwe kubwa au dogo namna gani. Maelekeo ya kuona kijicho yamepaswa yaangaliwe tusije tukapunja au kufanya mazoea mengine ya udanganyifu ili kupata vitu walivyo navyo wengine. Wala hatutaki kutumbukia katika mtego wa kusengenya-sengenya, kujaribu kushusha heshima ya Wakristo wenzetu kwa kulaumu-laumu isivyofaa au kwa kutilia mashaka uwezo wao mbalimbali na makusudi yao ya kufanya mambo. Tunayosema yamepaswa yawe ya kupendeza, ya kujenga wengine wala si kuwabomoa. Hatutaki tuwe kama wanafiki, tukijafanya tuko ambavyo hatuko na kuficha hila za uovu kwa kusingizia tuna namna ya utawa.

35. Pande zote za maisha ya Mkristo zimepaswa zionyeshe nini wazi, na hii inaweza kuwa na matokeo gani yenye kufaa juu ya wengine?

35 Ndiyo, mambo tunayofanya kila siku​—nyumbani, kazini, shuleni, katika shughuli zetu za kila siku na wengine​—yamepaswa yatoe ushuhuda wa kwamba maisha yetu ni yenye kuridhisha zaidi kuliko yalivyokuwa kabla hatujaanza kutii Neno la Mungu la kweli. Hiyo hasa imepaswa iwe tamaa yetu kwa sababu ya matokeo mema ambayo mwenendo mwema unaweza kuwa nayo juu ya watazamaji wanyofu. Mtume Petro alisema hivi: “Mwe na mwenendo mzuri kati ya Mataifa, ili, iwapo huwasingizia kuwa watenda mabaya, wayatazamapo matendo yenu mazuri, wamtukuze Mungu siku ya kujiliwa.”​—1 Pet. 2:12.

36, 37. Ni faida gani nyingine ambazo watumishi wa Yehova wanafurahia, na hii imepaswa iwafanyishe nini?

36 Ikiwa tu Wakristo waaminifu, tunapata kweli baraka na furaha nyingi. Kwa kuuzuia mkazo wa kushindwa na choyo, twapata uradhi kwa kuweza kuhakikisha kwamba utumishi wetu kwa Mungu unavutwa na upendo. Twapata uongozi wa Yehova, uangalizi na msaada tunapopambana na magumu ya maisha. Tunafurahia afya ya kiroho na uradhi. Tunahifadhi amani ya akili na moyo ambayo ni dhamiri safi tu iwezayo kutupa. Maisha yetu yana uongozi wenye kusudi kwa sababu yanategemea uhusiano wenye kuendelea na Yehova Mungu.

37 Kwa kweli, Wakristo walio wakf wana sababu ya kuendelea kujitahidi waendeleze uhuru ambao wameupata kwa kujipatanisha na kweli ya Mungu? Je! hilo ndilo wewe unafanya? Je! nia yako, maneno na matendo yako yanakaribia zaidi kanuni ya Mungu ya utakatifu? Je! imani na tumaini lako zinakulinda na cho chote ambacho kingeweza kuharibu uhusiano mwema na Yehova Mungu na kufanya upoteze “uzima . . . ule utakaokuwapo baadaye”? (1 Tim. 4:8) Ikiwa ndivyo, endeleza jitihada zako nzuri. Utii onyo la upole lililoongozwa na Mungu: “Uwe na furaha nyingi sana katika Yehova, naye atakupa maombi ya moyo wako.” (Zab. 37:4, NW) Furaha yako ya kweli na iendelee kuwa katika kudumisha upendo na kibali ya Yehova Mungu, ukisadiki kwamba hii inaongoza kwenye uradhi sasa na kuweka ahadi ya uzima wa milele katika taratibu mpya ya Mungu yenye haki, ambayo inakaribia sana.​—Ufu. 21:3, 4.

​—Kutoka The Watchtower, Jan. 15, 1975.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki