Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • pr seh. ya 4 kur. 16-19
  • Jumuiya ya Wakristo Imesaliti Mungu na Biblia

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Jumuiya ya Wakristo Imesaliti Mungu na Biblia
  • Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai?
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Mafundisho Yasiyo ya Kibiblia
  • Matendo Yasiyo ya Kimungu
  • Si ya Kikristo
  • Ushindi wa Kimungu—Maana Yake kwa Wanadamu Wanaotaabika
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • Hukumu ya Mungu Dhidi ya “Mtu wa Kuasi [Sheria]”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Jumuiya ya Wakristo Yafichuliwa Kuwa Ndiyo Mwendelezaji wa Ibada Bandia
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Rafiki Bandia ya Biblia
    Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu?
Pata Habari Zaidi
Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai?
pr seh. ya 4 kur. 16-19

Sehemu ya 4

Jumuiya ya Wakristo Imesaliti Mungu na Biblia

1 Watu katika mabara mengi wameiepuka Biblia na wamekosa kuistahi kwa sababu ya mwenendo mbaya wa wale wanaodai kuifuata. Katika mabara fulani imesemekana kwamba Biblia ni kitabu kinachoongoza kwenye vita, kwamba ni kitabu cha wazungu, na kwamba ni kitabu kinachounga mkoni ukoloni. Lakini hayo ni maoni yasiyo sahihi.

2 Biblia, iliyoandikwa katika Mashariki ya Kati, haiungi mkono vita vya kikoloni na unyonyaji wa kipupa ambao umeendelezwa katika jina la Ukristo kwa muda mrefu sana. Kinyume cha hilo, kwa kusoma Biblia na kujifunza mafundisho ya Ukristo wa kweli yaliyofundishwa na Yesu, utaona kwamba Biblia hushutumu vikali kupigana vita, ukosefu wa adili, na kuwanyonya wengine. Watu wenye pupa ndio wenye kosa, si Biblia. (1 Wakorintho 13:1-6; Yakobo 4:1-3; 5:1-6; 1 Yohana 4:7, 8) Kwa hiyo usiruhusu mwenendo mpotovu wa watu wenye ubinafsi wanaoishi kinyume cha mashauri bora ya Biblia ukuzuie usinufaike na hazina zayo.

3 Wanaotiwa ndani ya wale wasiofuata mashauri ya Biblia ni vikundi vya watu na mataifa ya Jumuiya ya Wakristo. “Jumuiya ya Wakristo” hufasiliwa kuwa ile sehemu ya ulimwengu ambamo Ukristo umo sana. Hasa hiyo ni ulimwengu wa Magharibi pamoja na mifumo yao ya makanisa, ambao kuanzia karibu karne ya nne W.K. ilikuja kuwa yenye kutokeza sana. Jumuiya ya Wakristo imekuwa na Biblia kwa karne nyingi, na makasisi wayo hudai kuifundisha na kuwa wawakilishi wa Mungu. Lakini je, makasisi na wamishonari wa Jumuiya ya Wakristo hufundisha kweli? Je! matendo yao huwakilisha Mungu na Biblia kwelikweli? Je! kweli Ukristo unashinda katika Jumuiya ya Wakristo? La. Tangu dini yayo ijitokeze mbele katika karne ya nne, Jumuiya ya Wakristo imethibitika kuwa adui ya Mungu na ya Biblia. Naam, mambo hakika ya historia huonyesha kwamba Jumuiya ya Wakristo imesaliti Mungu na Biblia.

Mafundisho Yasiyo ya Kibiblia

4 Mafundisho ya msingi ya Jumuiya ya Wakristo hayategemei Biblia, bali yanategemea ngano za kale—zile za Ugiriki, Misri, Babuloni, na nyinginezo. Mafundisho kama vile kutokufa kulikorithiwa kwa nafsi ya kibinadamu, kuteswa milele katika moto wa helo, purgatori, na Utatu (watu watatu katika Mungu mmoja) hayapatikani katika Biblia.

5 Kwa kielelezo, fikiria lile fundisho la kwamba watu wabaya watateswa milele katika moto wa helo. Wewe wahisije juu ya wazo hili? Wengi huliona kuwa chukizo sana. Wao huliona kuwa jambo lisilo la akili kwamba Mungu angewatesa wanadamu milele, akiendelea kuwaweka katika uchungu mwingi. Wazo la kikatili kama hilo ni tofauti na Mungu wa Biblia, kwa kuwa “Mungu ni upendo.” (1 Yohana 4:8) Biblia husema wazi kwamba fundisho kama hilo “halikuingia moyoni” mwa Mungu Mweza Yote.—Yeremia 7:31; 19:5; 32:35.

6 Leo dini nyingi, kutia na makanisa ya Jumuiya ya Wakristo, hufundisha kwamba wanadamu wana nafsi isiyoweza kufa, ambayo huenda mbinguni au helo baada ya kufa. Hili si fundisho la Biblia. Badala ya hivyo, Biblia husema hivi waziwazi: “Walio hai wanajua ya kwamba watakufa; lakini wafu hawajui neno lo lote, . . . kwa kuwa hakuna kazi, wala shauri, wala maarifa, wala hekima, huko kuzimu [kaburi] uendako wewe.” (Mhubiri 9:5, 10) Na mtunga zaburi asema kwamba baada ya kufa mtu “huurudia udongo wake, siku hiyo mawazo yake yapotea.”—Zaburi 146:4.

7 Kumbuka pia, kwamba, wakati Adamu na Hawa walipovunja sheria ya Mungu, adhabu haikuwa kutokufa. Hiyo ingalikuwa thawabu, si adhabu! Badala ya hivyo, wao waliambiwa kwamba ‘wangeirudia ardhi, ambayo katika hiyo wao walitwaliwa.’ Mungu akamkazia Adamu hivi: “Kwa maana u mavumbi wewe, nawe mavumbini utarudi.” (Mwanzo 3:19) Hivyo, fundisho la kutokufa kulikorithiwa kwa nafsi halimo katika Biblia bali lilitwaliwa na Jumuiya ya Wakristo kutoka kwa watu wasio Wakristo walioishi kabla yao.

8 Pia, fundisho juu ya Utatu la Jumuiya ya Wakristo hufanya Mungu aonekane kuwa Mungu wa kifumbo wa watatu katika mmoja. Lakini fundisho hilo pia halipatikani katika Biblia. Mathalani, kwenye Isaya 40:25, Mungu husema hivi waziwazi: “Mtanifananisha na nani, basi, nipate kuwa sawa naye?” Jibu liko wazi: Hakuna mtu awezaye kuwa sawa naye. Pia, Zaburi 83:18 husema hivi kwa usahili: “Wajue ya kuwa Wewe, uitwaye jina lako YEHOVA, Ndiwe peke yako Uliye juu, juu ya nchi yote.”—Ona pia Isaya 45:5; 46:9; Yohana 5:19; 6:38; 7:16.

9 Mafundisho ya Biblia kuhusu Mungu na makusudi yake yako wazi, rahisi kueleweka, na ya akili. Lakini mafundisho ya makanisa ya Jumuiya ya Wakristo hayako hivyo. Kwa ubaya hata zaidi, hayo hupingana na Biblia.

Matendo Yasiyo ya Kimungu

10 Zaidi ya kufundisha mafundisho bandia, Jumuiya ya Wakristo imesaliti Mungu na Biblia kwa matendo yayo. Yale ambayo makasisi na makanisa yamefanya katika karne zilizopita, na yameendelea kufanya katika wakati wetu, ni kinyume cha yale ambayo Mungu wa Biblia hutaka na kinyume cha yale ambayo Mwanzilishi wa Ukristo, Yesu Kristo, alifundisha na kufanya.

11 Mathalani, Yesu alifundisha wafuasi wake wasijiingize katika siasa za ulimwengu huu wala wasihusike na vita vyao. Pia yeye aliwafunza wawe wapenda amani, wafuataji sheria, na wawapende wanadamu wenzao bila ubaguzi wowote, hata wawe wenye nia ya kudhabihu uhai wao badala ya kuua wengine.—Yohana 15:13; Matendo 10:34, 35; 1 Yohana 4:20, 21.

12 Kwelikweli, Yesu alifundisha kwamba kuwapenda wanadamu wenzao kungekuwa alama ambayo ingetambulisha Wakristo wa kweli na Wakristo bandia, wenye kujifanya. Yeye alisema hivi kwa wale ambao wangemfuata: “Amri mpya nawapa, Mpendane. Kama vile nilivyowapenda ninyi, nanyi mpendane vivyo hivyo. Hivyo watu wote watatambua ya kuwa ninyi mmekuwa wanafunzi wangu, mkiwa na upendo ninyi kwa ninyi.”—Yohana 13:34, 35; 15:12.

13 Hata hivyo, karne baada ya karne, makasisi wa Jumuiya ya Wakristo wamejiingiza katika siasa na wameunga mkono vita vya mataifa yao. Wao hata wameunga mkono pande zinazopingana katika vita miongoni mwa Jumuiya ya Wakristo, kama vile vita vya ulimwengu viwili vya karne hii. Katika mapambano hayo makasisi wa kila pande walisali wapate ushindi, na washiriki wa dini moja kutoka nchi moja walikuwa wakiua washiriki wa dini iyo hiyo wa kutoka nchi nyingine. Lakini Biblia husema kwamba hivyo ndivyo watoto wa Shetani hutenda, si wale wa Mungu. (1 Yohana 3:10-12, 15) Hivyo, ingawa makasisi na wafuasi wao wamedai kuwa Wakristo, wao wamepinga mafundisho ya Yesu Kristo, aliyewaambia wafuasi wake ‘wauweke upanga mbali.’—Mathayo 26:51, 52.

14 Kwa karne nyingi makanisa yalishirikiana na mataifa ya Jumuiya ya Wakristo wakati mataifa hayo yaliposhinda, yakatia watu katika utumwa, na kuwatweza watu wengine wakati wa enzi ya ukoloni. Mambo yalikuwa hivyo kwa karne nyingi katika Afrika. Uchina pia ilipatwa na mambo hayo, wakati mataifa ya Magharibi yalipojitwalia ardhi yao kwa nguvu, kama vile katika Vita vya Afyuni na Mapinduzi ya Wanandondi.

15 Dini za Jumuiya ya Wakristo pia zimekuwa katika mstari wa mbele wa kuwanyanyasa, kuwatesa, na hata kuwaua wale wasiokubaliana nao wakati wa karne hizo za historia zinazoitwa Enzi za Giza. Wakati wa kipindi cha Baraza la Kuwahukumu Wazushi wa Kidini, ambalo liliendelea kwa mamia ya miaka, mazoea ya kikatili, kama vile kutesa na kuua kimakusudi, yaliidhinishwa na kutekelezwa dhidi ya watu wema, wasio na hatia. Wachochezi walikuwa makasisi na wafuasi wao, wote wakidai kuwa Wakristo. Wao hata walijaribu kuondolea mbali Biblia ili watu wa kawaida wasiweze kuisoma.

Si ya Kikristo

16 La, mataifa na makanisa ya Jumuiya ya Wakristo hayakuwa ya Kikristo, na si ya Kikristo. Hayo si watumishi wa Mungu. Neno lake lililopuliziwa husema hivi juu yao: “Wanakiri ya kwamba wanamjua Mungu, bali kwa matendo yao wanamkana; ni wenye machukizo, waasi, wala kwa kila tendo jema hawafai.”—Tito 1:16.

17 Yesu alisema kwamba dini bandia ingeweza kutambuliwa kwa yale ambayo ingetokeza, matunda yayo. Yeye alisema hivi: “Jihadharini na manabii wa uongo, watu wanaowajia wamevaa mavazi ya kondoo, walakini kwa ndani ni mbwa-mwitu wakali. Mtawatambua kwa matunda yao. . . . Kila mti mwema huzaa matunda mazuri; na mti mwovu huzaa matunda mabaya. Mti mwema hauwezi kuzaa matunda mabaya, wala mti mwovu kuzaa matunda mazuri. Kila mti usiozaa tunda zuri hukatwa ukatupwa motoni. Ndiposa kwa matunda yao mtawatambua [manabii hao bandia].”—Mathayo 7:15-20.

18 Hivyo, kwa yale ambayo zimefundisha na kwa yale ambayo zimefanya, dini za Jumuiya ya Wakristo zimedhihirisha kwamba dai lazo la kuamini katika Biblia na la kuwa watu wenye kumhofu Mungu na la kuwa Wakristo ni la uwongo. Wao wamesaliti Mungu na Biblia. Katika kufanya hivyo, wamechukiza sana mamilioni ya watu na kuwafanya wageukie mbali wasiamini katika Mtu Mkuu Zaidi Sana.

19 Hata hivyo, kushindwa kwa makasisi na makanisa ya Jumuiya ya Wakristo, pamoja na kushindwa kwa dini nyinginezo nje ya Jumuiya ya Wakristo, hakumaanishi kushindwa kwa Biblia. Wala hakumaanishi kwamba Mungu ameshindwa. Badala ya hivyo, Biblia hutuambia kuhusu Mtu Mkuu Zaidi Sana ambaye yuko na ambaye hutujali sisi na wakati wetu ujao. Hiyo huonyesha jinsi atakavyothawabisha watu wenye mioyo ya haki wanaotaka kufanya yanayofaa, wanaotaka kuona haki na amani vikidumu kotekote duniani. Hiyo pia huonyesha kwa nini Mungu ameruhusu uovu na kuteseka kuwepo na jinsi atakavyoondoa duniani wale wanaoumiza wenzao, kutia na wale wanaodai kumtumikia lakini hawamtumikii.

[Maswali ya Funzo]

1, 2. Kwa nini watu wengine hukosa kuistahi Biblia, lakini Biblia husema nini?

3. Mambo hakika ya historia huonyesha nini juu ya Jumuiya ya Wakristo?

4, 5. Ni mafundisho gani yasiyo ya kibiblia hufundishwa na makanisa?

6. Biblia hukanushaje fundisho la kutokufa kwa nafsi?

7. Adhabu waliyopewa Adamu na Hawa ilikuwa nini kwa kuvunja sheria ya Mungu?

8. Biblia hukanushaje fundisho juu ya Utatu la Jumuiya ya Wakristo?

9. Tunaweza kusema nini kuhusu mafundisho ya Biblia na kuhusu mafundisho ya makanisa ya Jumuiya ya Wakristo?

10, 11. Ni katika njia zipi mafundisho ya Biblia hutaka mambo yaliyo kinyume cha yale ambayo makanisa ya Jumuiya ya Wakristo yamekuwa yakifanya?

12. Yesu alisema ni nini kingewatambulisha Wakristo wa kweli?

13, 14. Ni nini kinachoonyesha kwamba makanisa ya Jumuiya ya Wakristo hayamwakilishi Mungu?

15. Ni maovu gani yamechochewa na Jumuiya ya Wakristo?

16, 17. Kwa nini tunaweza kusema kwamba makanisa si ya Kikristo?

18. Ni nini kimetokea kwa sababu ya mafundisho na matendo ya Jumuiya ya Wakristo?

19. Je! kushindwa kwa Jumuiya ya Wakristo kunamaanisha kwamba Mungu ameshindwa pamoja na Biblia?

[Picha katika ukurasa wa 17]

“Moto” wa Dante

[Hisani]

Kielezi cha Doré cha Barrators—Giampolo ya Divine Comedy ya Dante

[Picha katika ukurasa wa 17]

Utatu wa Jumuiya ya Wakristo

[Picha katika ukurasa wa 17]

Utatu wa Kihindu

[Hisani]

Hisani ya The British Museum

[Picha katika ukurasa wa 17]

Utatu wa Kimisri

[Hisani]

Museo Egizio, Turin

[Picha katika ukurasa wa 18]

Kinyume cha mafundisho ya Yesu, makasisi wa pande zote mbili wameunga mkono vita

[Hisani]

Picha ya U.S. Army

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki