Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ijwbq makala 128
  • Je, Biblia Inazungumza Kuhusu Toharani?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Biblia Inazungumza Kuhusu Toharani?
  • Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Jibu la Biblia
  • Toharani
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
  • Ukweli Kuhusu Helo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Kufuatia Njia ya Maisha Yenye Kuridhisha
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Je, Waweza Kuiamini Biblia?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
Pata Habari Zaidi
Maswali ya Biblia Yajibiwa
ijwbq makala 128
Picha ya msanii ya toharani

Je, Biblia Inazungumza Kuhusu Toharani?

Jibu la Biblia

Hapana. Biblia haina neno “toharani,” wala haifundishi kwamba nafsi za watu waliokufa zinasafishwa toharani.a Fikiria kile ambacho Biblia inafundisha kuhusu dhambi na kifo na jinsi hilo linavyopingana na fundisho la toharani.

  • Imani katika damu ya Yesu ndiyo husafisha dhambi za mtu, si kuishi toharani kwa muda. Biblia inasema kwamba “damu yake Yesu, Mwana wake [Mungu], yatusafisha dhambi yote” na kwamba “Yesu Kristo . . . kwa damu yake ametufungua kutoka vifungo vya dhambi zetu.” (1 Yohana 1:7, Union Version; Ufunuo 1:5, Biblia Habari Njema) Yesu Kristo alitoa “maisha yake kuwa fidia ya watu wengi” ili kulipia dhambi zao.​—Mathayo 20:28, BHN.

  • Watu waliokufa hawajui lolote. “Walio hai hujua kwamba watakufa, lakini wafu hawajui chochote.” (Mhubiri 9:5, BHN) Mtu ambaye amekufa hawezi kuhisi chochote na hivyo hawezi kusafishwa kwa moto wowote ulio toharani.

  • Hakuna adhabu ya dhambi baada ya mtu kufa. Biblia inasema kwamba “mshahara ambao dhambi hulipa ni kifo” na kwamba mtu “ambaye amekufa ameondolewa hatia ya dhambi yake.” (Waroma 6:7, 23) Kifo ndiyo adhabu kamili ya dhambi.

Fundisho la toharani ni nini?

Toharani inafafanuliwa katika fundisho la dini ya Katoliki kuwa hali au mahali ambapo nafsi za wafu hulipia dhambi ambazo hazijasamehewa na wanasafishwa.b Kulingana na Katekisimu ya Kanisa Katoliki, kusafishwa huku kunahitajika “ili kufikia utakatifu unaohitajika ili kuingia katika shangwe ya mbinguni.” Katekisimu inasema pia kwamba “mapokeo ya Kanisa . . . Yanasema kuhusu moto wa kutakasa,” kama iliyoonyeshwa kwenye picha katika makala hii. Hata hivyo, hilo si fundisho la Kimaandiko.

Fundisho la toharani lilitoka wapi?

Wagiriki wa kale waliamini toharani na Limbo (sehemu ya ahera ziendako roho za watoto na watu wema ambao hawajabatizwa). Akiwa ameathiriwa na falsafa ya Kigiriki, Clement wa Alexandria alidai kwamba dhambi za wafu zinaweza kusafishwa kupitia moto wa kutakasa. Hata hivyo, kulingana na kitabu The History of Christian Doctrines, Papa Gregory Mkuu ndiye aliyekazia kwamba toharani ni imani isiyoweza kupingwa. Kitabu hicho kinaongezea kusema kwamba Gregory, aliyekuwa papa kuanzia 590 hadi 604 W.K., “anajulikana kama ‘mwanzilishi wa toharani.’” Kanisa Katoliki lilifafanua fundisho lake rasmi la toharani katika baraza la Lyons (1274) na la Florence (1439) na akalikazia tena katika Baraza la Trent mnamo 1547.

a Kuhusu toharani, kitabu Orpheus: A General History of Religions kinasema kwamba “hakuna jambo lolote kulihusu katika Injili.” Vivyo hivyo, kitabu New Catholic Encyclopedia kinasema: “Kwa ujumla, msingi wa fundisho la Katoliki kuhusu toharani ni mapokeo, si Maandiko Matakatifu.”​—Toleo la Pili, Buku la 11, ukurasa wa 825.

b Ona kitabu New Catholic Encyclopedia, Toleo la Pili, Buku la 11, ukurasa wa 824.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki