Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w78 8/15 kur. 23-24
  • Maswali Kutoka Kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka Kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
  • Habari Zinazolingana
  • Mzeituni Wenye Kuzaa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
  • ‘Lo! Jinsi Kilivyo Kina cha Hekima ya Mungu!’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Wazaaji wa Matunda Wenye Umoja
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
  • “Ni Nani Amepata Kujua Akili ya Yehova?”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
w78 8/15 kur. 23-24

Maswali Kutoka Kwa Wasomaji

● Je! maneno ya Yesu katika Yohana 15:1-6 kwamba yeye ni mzabibu nao wanafunzi wake ni matawi, yanalingana na mzeituni na matawi yake unaosimuliwa katika Warumi 11:17-27?

Katika wakati uliopita Yohana 15:l-6 lilitumiwa kama mfano wakati wa kuzungumza Warumi 11:17-24? Lakini uchunguzi wa uangalifu unaonyesha kwamba habari hizi mbili zinahusu mambo mawili yaliyo tofauti. Moja linahusu Kristo, na jingine lahusu Ibrahimu. Na tuangalie kila mojawapo.

Katika usiku wake wa mwisho kuwa na mitume wake Yesu alisema hivi: “Mimi ndimi mzabibu wa kweli, na Baba yangu ndiye mkulima. Kila tawi ndani yangu lisilozaa huliondoa; na kila tawi lizaalo hulisafisha, ili lizidi kuzaa. Mimi ndimi mzabibu; ninyi ni matawi; akaaye ndani yangu nami ndani yake, huyo huzaa sana.”​—⁠Yohana 15:1, 2, 5.

Yesu alijilinganisha mwenyewe na mzabibu. Wanafunzi wake, ambao katika Pentekoste ya mwaka 33 W.K. walizaliwa kwa roho takatifu, wakawa matawi ya mzabibu. Kristo aliwahimiza kwamba wakiisha kuwa matawi wanapaswa waendelee kukaa ndani yake na kuzaa matunda ili wasitupiliwe mbali na kupoteza uzima wa milele. (Yohana 15:6) Kuzaa matunda kungehusu kuonyesha kwao sifa ambazo, yeye, Yesu, alionyesha. Kwa kukaa ndani yake wangesitawisha tunda la roho. (Gal. 5-22, 23) Na wangekuwa na kazi ya kuongea juu ya Ufalme.​—⁠Luka 8:8

Ijapokuwa maneno katika Yohana 15:1-6 yalimpasa Yesu, mfano wa Paulo wa mti wa mzeituni katika Warumi 11:17-24 inampasa Ibrahimu. Unaonyesha uhitaji ya kuwa na imani kama ya Ibrahimu ili mmoja awe sehemu ya uzao wake ulioahidiwa. Mfano huu ni wa mzeituni mwema, au wa shamba ambao kutoka huu wa matawi ya asili yalikatwa. Halafu matawi ya mzeituni mwitu yakupandikizwa mahali pake. Matawi ya asili yalifananisha Wayahudi wa asili. Matawi ya mzeituni mwitu yanafananisha waamini wa Mataifa ambao, kwa sababu imani yao, waliwekwa mahali pa Wayahudi wa asili wasioamini kwamba sehemu ya uzao wa Ibrahimu ulioahidiwa. Hii inaweza kuonekana vizuri zaidi kwa kuchunguza namna Mungu alivyomtendea Ibrahimu na nia ya Wayahudi alipotokea Masihi.

Kwa sababu Ibrahimu alionyesha imani, Yehova Mungu alifanya agano naye juu ya “uzao” ambao katika huo mataifa yote “watajibarikia.” (Mwa. 22.17, 18; Gal. 3:8) Jambo hili lilihusu namna Mungu angewatendea wazao wa asili wa Ibrahimu, Waisraeli. (Kum. 7:7, 8; 2 Kor. 11:22) Wayahudi katika karne ya kwanza walijisifu kwa kuwa waliweza kusema: “Baba yetu ndiye Ibrahimu!” (Yohana 8:39; Mt. 3:9) Walidhani kwamba kwa sababu wao ni uzao wa asili wa Ibrahimu walikuwa na hakika ya kuwa na upendeleo wa Yehova. Walakini, katika kitabu cha Warumi, Paulo alionyesha kwamba, ingawa kuwa wazao wa asili wa Ibrahimu kuliwafaidi bila shaka, hakukutosha. Namna gani hivyo?

Sababu ya hili ilikuwa kwamba Yehova Mungu alikusudia kutokeza uzao wa kiroho kupitia kwa agano la Ibrahimu. Masihi, Yesu, ndiye aliyekuwa mkuu katika uzao huo wa kiroho wa Ibrahimu, kama vile Paulo alivyokuwa ameeleza mapema katika barua aliyowaandikia Wagalatia. (Gal. 3:16) Lakini vilevile alikuwa ameonyesha kwamba uzao huo wa kiroho ungekuwa na washiriki wengi; washiriki hao walikuwa Kristo pamoja na warithi wa shirika pamoja naye, ambao baadaye ilifunuliwa kuwa wangekuwa 144,001 hesabu yao. Paulo aliandika hivi: “Kama ninyi ni wa Kristo, basi, mmekuwa uzao wa Ibrahimu, warithi sawasawa na ahadi.” (Gal. 3:29; Ufu. 7:4-8; 14:1) Lakini je! sehemu ya pili ya uzao wa Ibrahimu, wale 144,000, wangekuwa Wayahudi peke yao tu, washiriki wa uzao wa asili wa Ibrahimu?

Ingekuwa hivyo. Kuanzia mwaka 29 W.K. mpaka mwaka 36 W.K. nafasi ya kutokeza uzao huo wa kiroho ilitolewa kwa wale ambao kwa asili walikuwa “wana wa ukoo wa Ibrahimu.”a (Matendo 13:26; Mt. 15:24) Katika kitabu cha Warumi, Paulo alitaja kifungo hiki cha asili mara nyingi. Alisema juu ya imani “ya Ibrahimu, baba yetu kwa jinsi ya mwili.” (Rum. 4:1) Tena, katika Warumi 11:1, alisema hivi: “Je! Mungu aliwasukumia mbali watu wake? Hasha! Kwa kuwa mimi nami ni Mwisraeli, mmoja wa wazao wa Ibrahimu.” Na katika mfano unaofuata wa mti wa mzeituni, yeye aliendelea kumtaja Ibrahimu.

Wazao wa asili wa Ibrahimu walikuwa kama matawi ya mzeituni shamba. Lakini agano la Ibrahimu lilipaswa litokeze uzao wa kiroho. Kwa hiyo, ili wayahudi wawe sehemu yake iliwapasa wamkubali Masihi, wazaliwe kwa roho takatifu wawe wana wa kiroho wa Ibrahimu Mkuu, Yehova Mungu. (Rum. 4:16, 17) Ni mabaki tu ya Wayahudi wa asili waliofanya hivyo, kwa njia hiyo wakawa matawi ya kuendelea ya mzeituni. Wengi wa uzao wa asili wa Ibrahimu hawakuonyesha imani katika Masihi. Hivyo, kulingana na mfano huo, walikatwa kutoka kwa mzeituni na hawakuwa sehemu ya uzao wa kiroho wa Ibrahimu.​—⁠Mt. 21:43.

Kwa matokeo hayo, Mungu aliwageukia Mataifa. Kuanzia mwaka 36 W.K. na kuendelea, wenye kuamini wasio wayahudi wangeonyesha imani wawe Wakristo waliotiwa mafuta, sehemu ya uzao wa kiroho wa Ibrahimu. (Matendo 10:34-47; 15:14) Paulo aliwalinganisha Wakristo hawa wa Mataifa na matawi ya mzeituni mwitu yaliyopandikizwa katika mzeituni shamba. Kwa hiyo, hata ingawa hawakuwa na uhusiano (ukamatano) wa kimwili na Ibrahimu, walionyesha imani kama ya Ibrahimu wakawa sehemu ya uzao wake wa kiroho. Kwa kweli, ikiwa baadaye, hata baada ya kipindi cha pekee kwisha, Myahudi ye yote angeonyesha imani katika Yesu, angepandikizwa tena katika mti wa mzeituni, awe sehemu ya uzao wa kiroho wa Ibrahimu. (Tofautisha hili na namna ingetokea kwa tawi lililokatwa kutoka kwa mzabibu wa Yesu. [Yohana 15:6])​—⁠Rum. 11:17-24.

Kwa hiyo mfano wa Paulo unatoa mkazo juu ya Ibrahimu, “shina” lenye haki ambaye Yehova aliweka agano naye na ambaye “matawi” yalihitaji kuungamanishwa naye kwa imani.​—⁠Rum. 4:9-16; 11:16.

Kama inavyoweza kuonekana sasa, maneno ya Yesu katika Yohana 15:1-6 yanaonyesha mambo yaliyo tofauti kabisa yakilinganishwa na yale ya Paulo katika Warumi 11:17-24. Moja linampasa Yesu; jingine linampasa Ibrahimu. Hata hivyo, yote pamoja, yanaonyesha kwa nguvu sana kwamba Ukristo si jambo linaloweza kuchukuliwa vivi hivi tu. Imani inahitajiwa, kama “imani ya Ibrahimu.” (Rum. 4:16) Vilevile, ni jambo la maana sana kuendelea katika umoja na Yesu na kuzaa matunda mema, kwa kufuata mfano wa Yesu.

[Maelezo ya Chini]

a Tazama Mnara wa Mlinzi wa Mei 15, 1975, kurasa 222-236.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki