Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w77 1/1 kur. 22-23
  • Kutosheka Ni Mradi Unaofaa

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kutosheka Ni Mradi Unaofaa
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
  • Habari Zinazolingana
  • Je! Wewe Unaridhika na Kile Ulicho Nacho?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
  • Je! Wewe Unayatumiaje Maisha Yako?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • Unaweza Kudumishaje Maoni Yaliyosawazika Kuhusu Pesa?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
  • Ni Nini Kinachofanya Maisha Yawe Yenye Kusudi?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
w77 1/1 kur. 22-23

Kutosheka Ni Mradi Unaofaa

NI FURAHA kweli kweli kutosheka na vitu ambavyo mtu anavyo. Kutosheka kunafurahisha sana mtu na kumpa amani ya akili na ya moyo.

Lakini, katika ulimwengu huu yako mambo mengi yanayoweza kufanya mtu ahangaike na kuwa asiyetosheka. Udanganyifu, udhalimu na maovu mengine yamekuwa mengi sana. Huenda watu mmoja mmoja wakajaribu kufanya yaliyo haki. Lakini ni kama vile Sulemani alivyosema juu ya jitihada za wanadamu za kuondoa makosa ulimwenguni: “Yaliyopotoka hayawezi kunyoshwa.”​—⁠Mhu. 1:15.

Ingawa hatupaswi kujipofusha tusione mabaya, yatupasa tujue kwamba yako mambo tusiyoweza kubadili. Badala ya kuacha mambo hayo yatusumbue daima, afadhali kukaza fikira zetu juu ya mambo mengine yanayofaa zaidi, yenye kujenga. Ama sivyo tutajikuta tunasumbuka sana kiasi cha kutoweza kufurahia hata mambo yanayofaa. Mithali ya Biblia yaeleza jambo hilo hivi: “Kwa mtu mwenye kuhuzunika kila siku ni mbovu, kwa moyo wenye furaha ni shangwe sikuzote.”​—⁠Mit. 15:15, Jerusalem Bible.

Naam, hata mtu anapokuwa na wingi wa vitu vya kimwili, aweza kufanya siku zake ziwe za huzuni. Akikosa kutosheka, anashindwa kuona baraka zinazomzunguka. Kwa upande mwingine, mtu mwenye vitu vichache, lakini asiyeacha atawalwe na huzuni, huona furaha ya ndani kila siku. Maoni yake yanayofaa yanamwezesha kuchangamka, kama kwamba anafurahia karamu ya daima. Ndivyo alivyokuwa mtume Paulo, aliyejitaja mwenyewe na wafanya kazi wenzake “kama wenye huzuni, bali sikuzote tu wenye furaha.”​—2 Kor. 6:10.

Lakini mtu awezaje kutosheka kwa njia itakayomfanya awe kama ana karamu sikuzote?

Jambo kubwa ni kujua kwamba furaha haitegemei ufanisi wa kimwili. Hali yenye upendo na ya amani nyumbani inaleta furaha nyingi zaidi kuliko vyakula bora au vifaa vya kimwili. Mithali mbalimbali za Biblia zinakazia hilo. Twasoma: “Chakula cha mboga penye mapendano; ni bora kuliko ng’ombe aliyenona pamoja na kuchukiana.” (Mit. 15:17) “Afadhali mali kidogo pamoja na haki, kuliko mapato mengi pamoja na udhalimu.” (Mit. 16:8) “Afadhali mego kavu pamoja na utulivu, kuliko nyumba yenye . . . magomvi.”​—⁠Mit. 17:1.

Jamaa inafaidika sana ikithamini ukweli wa mithali kama hizo za Biblia. Kwa sababu ya kufuatia vitu vya kimwili kwa kiasi, wazazi wanakuwa na wakati zaidi kuwa pamoja na watoto wao. Kufanya hivyo kunaweza kuwafanya waoneane shauku nyingi sana, kufanya nyumbani pawe mahali penye amani na mapatano.

Lakini, jambo la maana zaidi linalofanya mtu atosheke ni kufahamu kwake kwamba uhusiano mwema na Muumba ndiyo mali yake yenye thamani zaidi. Biblia yasema, “Kuwa na mali chache pamoja na kumcha [Yehova, yaani kumheshimu ifaavyo]; ni bora kuliko mali nyingi pamoja na [kuvurugika].”​—⁠Mit. 15:16.

“Kuvurugika,” yaani, kuhangaika na wasiwasi na kuwa na migogoro, huja mtu anapomsahau Muumba na kufanya mradi wake mkuu maishani uwe kufuatia mali za kimwili. Inapokuwa hivyo, anatumia nguvu zake kwa “kuvurugika” tena anatumia wakati wake ovyo, mwendo wake unaonekana hauna kusudi lo lote. Yeye hajui matokeo yatakuwa nini juu ya vitu ambavyo amekusanya wakati wa kazi yake ngumu alipokuwa hapumziki. Mtunga zaburi’ aliyeongozwa na Mungu aliandika hivi: “Kama mvuke ndivyo shughuli zake zilivyo afanyazo bila kupumzika; hujaza sana ghala zake, asijue atakayezitumia.” (Zab. 39:7, New American Bible) Vivyo hivyo, Mfalme Sulemani mwenye hekima alisema hivi: “Nami nikaichukia kazi yangu yote niliyojishughulisha nayo chini ya jua; maana sina budi kumwachia yeye atakayenifuata. Naye ni nani ajuaye kama huyo atakuwa mwenye hekima au mpumbavu? Hata hivyo atatawala juu ya kazi yangu yote niliyojishughulisha nayo.”​—⁠Mhu. 2:18, 19.

Ingawa maisha ya watu wenye kufuatia vitu vya kimwili huwa na migogoro mara nyingi na yanakuwa bila kusudi, sivyo yalivyo maisha ya wale wanaomheshimu Muumba kwa njia inayofaa. Ndiyo sababu Mfalme Sulemani alichunguza taabu ya wanadamu na jitihada zao akakata maneno hivi: “Hii ndiyo jumla ya maneno; yote yamekwisha sikiwa; Mche Mungu, nawe uzishike amri zake, maana kwa jumla ndiyo impasayo mtu.”​—⁠Mhu. 12:13.

Mtu anayemwogopa Muumba ifaavyo hakosei kwa kutegemea vitu vya kimwili maisha yake yote. Nia yake iko kama ya mtume Mkristo Paulo, aliyeandika hivi: “Kwa maana hatukuja na kitu duniani, tena hatuwezi kutoka na kitu; ila tukiwa na chakula na nguo tutaridhika na vitu hivyo.” (1 Tim. 6:7, 8) Maoni hayo yanayofaa juu ya vitu vya kimwili yanazuia mtu asikate tamaa na kuona uchungu hali zikibadilika na akipoteza mali zake.

Tena, wale wanaomwogopa Yehova Mungu hawawi na wasiwasi wanapopatwa na msiba. Wanajua kwamba Baba yao wa kimbinguni hatawaacha, kuwaacha wakiwa hoi kabisa. Wao wanawaza kama mtunga zaburi aliyeongozwa na Mungu: “Nimemtumaini Mungu, sitaogopa; mwanadamu atanitenda nini?”​—⁠Zab. 56:11.

Hata hali ziweje, mtu aliye na uhusiano wa karibu na Yehova Mungu aweza kutosheka. Anajua kwamba hata akipatwa na magumu yatakuwa ‘mepesi na ya muda tu’ yakilinganishwa na thawabu nzuri ajabu ya uzima wa milele ambayo Mungu aweza kumpa. (2 Kor. 4:17) Hiyo inamwezesha aendelee kuwa na furaha ya ndani na kuutazamia wakati ujao kwa tumaini hakika. Mtume Mkristo Paulo alifanya lilo hilo. Katika barua yake kwa Wafilipi, ilisema: “Nimejifunza kuwa radhi na hali yo yote niliyo nayo. Najua kudhiliwa, tena najua kufanikiwa; katika hali yo yote, na katika mambo yo yote, nimefundishwa kushiba na kuona njaa, kuwa na vingi na kupungukiwa. Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu.”​—⁠Flp. 4:11-13.

Kutosheka, kama mtume Paulo, ni mradi tunaopaswa kujaribu kufikia. Kunahaidia mtu aepuke maumivu, migogoro na ubatili wa maisha unaotokana na kufuatia mambo ya kimwili peke yake. Tena, kunamsaidia avumilie hali zisizopendeza, apate furaha maishani sasa, na kuleta wengine furaha.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki