‘Kuvuta Uovu kwa Kamba’
◆ Unabii wa Isaya ulitangaza “ole” juu ya wenye ‘kuvuta uovu kwa kamba za ubatili [za magari ya farasi, NW]’ (Isa. 5:18) Waisraeli walioambiwa hivyo bila shaka walizoea kufanya dhambi. Walifungamana nayo kama wanyama waliofungiliwa kwenye magari ya farasi waliyovuta kwa kamba. Watu wa namna hiyo wangepatwa na ole wakati Yehova angefikiliza hukumu yake ya haki.