Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w77 5/15 uku. 238
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
  • Habari Zinazolingana
  • Faida Zenye Kudumu Kutokana na Kuifuata Biblia Kama Jamaa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Jinsi Familia Yako Inavyoweza Kuwa na Furaha
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • Daraka Lenu Kama Wazazi
    Kufanya Maisha ya Jamaa Yako Yawe Yenye Furaha
  • Kuwapa Watoto Uangalifu Wanaohitaji
    Amkeni!—2005
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
w77 5/15 uku. 238

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

● Inaonekana mara nyingi sana waume huachia wake zao daraka la kuzoeza na kufundisha watoto wao adabu. Biblia yasema nini kuhusu hilo? Je! kweli ni ‘kazi ya mke’?

Ni kweli kwamba mahali pengi wanaume wanaona mke ndiye anayepaswa kuongoza watoto na kuwasahihisha. Lakini Biblia haikubali; yaonyesha wazi kwamba wenzi wote wawili wana wajibu wa kufanya hivyo.​—Mit. 1:8.

Bila shaka, yampasa mtu awe na kiasi cha kufikiria hali zilizo katika jamaa nyingi. Mara nyingi mume hufanya kazi ya kimwili aruzuku jamaa, kwa hiyo huwa hayupo karibu mchana wote. Na nyakati nyingi mke hufanya kazi za nyumba, kutimiza fungu lake bora la kuletea jamaa yote furaha na hali njema. Ikiwa yeye huwa na mumewe na watoto kwa kawaida wakati wa siku, ni wazi kwamba yeye atawapa watoto uongozi na adabu wanazohitaji.

Lakini, linalochukiwa na wanawake wengi zaidi na zaidi ni kutotaka kwa waume kusaidia kuzoeza watoto wanapokuwa nyumbani pamoja na jamaa.

Mambo ambayo Biblia yasema juu ya kuzoea na kufundisha watoto adabu ni yenye hekima na manufaa pia. Kwa mfano, twasoma hivi: “Mlee mtoto katika njia impasayo, naye hataiacha, hata atakapokuwa mzee. Mrudi mwanao naye atakustarehesha; naam, atakufurahisha nafsi yako.” (Mit. 22:6; 29:17) Mungu amempa baba na mama pia daraka hilo. Hivyo ashauri watoto hivi: “Mwanangu, shika maagizo ya baba yako, wala usiiache sheria ya mama yako. Msikilize baba yako aliyekuzaa, wala usimdharau mama yako akiwa mzee.” (Mit. 6:20; 23:22) Kwa hiyo, hata mwanamume akiwa hayupo nyumbani wakati wa mchana, yampasa apendezwe sana na kulea watoto wake kwa njia yenye mafanikio. Kazi yake si kutafuta riziki tu.

Lakini, huenda akaja nyumbani akiwa amechoka, akitaka kutulia tu na kupumzika. Kwa hiyo, tatizo la kawaida ya kila siku linalohusu watoto likitokea, huenda akashawishika kumwambia mkewe, ‘Wewe litatue. Wewe hushinda nao mchana kutwa na kwa hiyo wewe ndiwe unayeweza kujua litakalowafaa zaidi.’ Pengine mke aweza, kama ambavyo labda amefanya wakati wa mchana. Lakini mumewe anapokuwa nyumbani, sababu gani asishirikiane na mkewe kuzoeza watoto? Hilo ndilo jambo la upendo na huruma.

Tena, yeye kama kichwa cha jamaa amekabidhiwa na Mungu daraka la kuweka mfano kwa kuongoza watoto na kuwasahihisha. Neno la Mungu lasema: “Nanyi, akina baba, msiwachokoze watoto wenu; bali waleeni katika adabu na maonyo ya Bwana.” (Efe. 6:4) Nayo Biblia yalinganisha adabu zenye manufaa zinazotoka kwa Yehova Mungu na adabu anazofundisha baba wa kibinadamu akiwa na kusudi jema, adabu zinazofanya watoto wake wawe heshima na kuleta amani.​—Ebr. 12:7-11.

Hata hivyo, hiyo haimaanishi kwamba mara afikapo nyumbani ataachiwa kazi yote hiyo. Biblia haigawi daraka hilo katika visehemu-sehemu vya saa za siku. Mume na mke wana daraka moja na yawapasa wote wahurumiane. Yawapasa wote wawili wajue kwamba wote pamoja wamepewa na Maandiko daraka la kusaidia watoto wao na kuwaongoza wakati wo wote wawezapo. (Kum. 11:18-21) Mume na mke washirikianapo kufanya hivyo, yaelekea kutakuwa na furaha na mafanikio. Bila shaka watoto watafaidiwa na uongozi wenye upendo na mafunzo ya adabu watakayopewa na wazazi wote wawili. Na pengine mume ataona kwamba mumewe hachukizwi, bali kwamba anatosheka kujua mumewe anampenda na kushirikiana naye.

Hata katika jamii ya watu au nchi ambako kuna ‘desturi’ ya kuachia wake daraka la kuzoeza watoto na kuwafundisha adabu, ni jambo lenye hekima na manufaa tufuate njia inayoonyeshwa na Muumba wetu katika Neno aliloliongoza. Kwa hiyo kuzoeza watoto na kuwafundisha adabu si ‘kazi ya mke’; ni ‘kazi ya wazazi’​—wazazi wote wawili.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki