“Pango la Wanyang’anyi”
● Wakati Yesu Kristo alipokuwa akifukuza wavunja pesa na wauzaji wanyama wa dhabihu katika eneo la hekalu, alisema hivi: “Imeandikwa, Nyumba yangu itaitwa nyumba ya sala; bali ninyi mmeifanya pango la wanyang’anyi.” (Mt. 21:13) Basi, Yesu aliwaita wavunja fedha hao “wanyang’anyi,” pamoja na waliokuwa wakiuza wanyama wa dhabihu. Hiyo inaonyesha walikuwa wakijipatia faida nyingi kupita kiasi. Kitabu Mishnah cha mapokeo ya Kiyahudi kinaonyesha kwamba Yesu hakuwa akitia chumvi. Kinaeleza kwamba kuna wakati ambao njiwa wawili walikuwa wakiuzwa denar moja ya dhahabu au denar 25 za fedha. Bei hiyo ya juu sana ilimfanya Simeoni mwana wa Gamalieli aape kwa jina la hekalu, akisema: “Mimi sitauacha usiku huu upite kabla bei yao haijawa denar moja [ya fedha].” Basi, hiyo inaonyesha wazi kwamba njiwa walikuwa wakiuzwa kiasi kikubwa mara 25 kuliko bei iliyofaa. Kweli huo ulikuwa “unyang’anyi.”