‘Mwenye Hekima na Awe Mpumbavu’
■ Ungemwonaje mtu ye yote anayetia moyo mtu mwenye hekima awe mpumbavu? Yaelekea ungefikiria shauri la namna hiyo kuwa lisilofaa. Walakini, kunazo nyakati ambazo shauri hilo ndilo lililo bora zaidi. Mtume Paulo aliwaandikia Wakristo katika Korintho hivi: “Kama mtu akijiona kuwa mwenye hekima miongoni mwenu katika dunia hii, na awe mpumbavu, ili apate kuwa mwenye hekima.” (1 Kor. 3:18) Mtu fulani anaweza kuonekana na wengine mwenye hekima, akiwa na ujuzi fulani, busara au masomo ya kifilosofia. Lakini ili awe mtumishi anayekubaliwa wa Yehova Mungu, anapaswa maisha yake yawe katika ibada ya kweli. Imani yake, inayoungwa mkono na matendo ya Kikristo, inamfanya kuonekana mjinga machoni pa ulimwengu. Walakini, kuwa kwake mpumbavu katika wazo hilo kunamfanya mwenye hekima, kwa maana kunaleta baraka nyingi sasa na kunatoa ahadi ya uzima wa milele katika taratibu mpya ya Mungu.