Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w77 11/15 uku. 509
  • Mwenye Hekima Alikuwa na Maana Gani?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mwenye Hekima Alikuwa na Maana Gani?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Ubora wa Jina Zuri
  • Jifanyie Jina Zuri Pamoja na Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
  • Mwenye Hekima Alikuwa na Maana Gani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
  • Mwenye Hekima Alikuwa na Maana Gani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
  • Mwenye Hekima Alikuwa na Maana Gani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
w77 11/15 uku. 509

Mwenye Hekima Alikuwa na Maana Gani?

Ubora wa Jina Zuri

Jina zuri au sifa nzuri ina ubora mwingi sana, na inastahili kulindwa. Mfalme Sulemani mwenye hekima alisema: “Heri sifa njema kuliko marhamu nzuri; na siku ya kufa kuliko siku ya kuzaliwa.” (Mhu. 7:1) Nyakati za kale mafuta mazuri yalithaminiwa sana. Yalikuwa na manukato. Sifa njema ni nzuri kuliko manukato ya mafuta mazuri. Sifa ya mtu inajulikana akiishi muda wa kutosha, halafu anajulikana hasa jinsi alivyo. Anapokufa jina lake au sifa yake inatiwa muhuri, hali zake zinajulikana kabisa. Kwa kuwa mtu hawi na sifa anapozaliwa, ‘siku ya kufa ni bora kuliko siku ya kuzaliwa.’

Ili mtu ajipatie jina zuri haimpasi kuchezea maisha. Sulemani alipendekeza hivi: “Heri kuiendea nyumba ya matanga, kuliko kuiendea nyumba ya karamu. Kwa maana huo ndio mwisho wa wanadamu wote, naye aliye hai atautia moyoni mwake.”​—Mhu. 7:2.

Wakati jamaa fulani inapofiwa, huo sio wakati wa kuwasahau na kuendelea kufanya karamu na shangwe bila kujali. Bali, hiyo inakuwa nafasi ya kufariji wenye kuomboleza. Mtu anaweza kujifaidi mwenyewe pia kwa kuiendea “nyumba ya matanga.” Anapokwenda anakumbuka sana kwamba maisha ni mafupi na kwamba mipango na kazi za mtu zinaweza kukomeshwa upesi sana. Jambo hilo linaweza kumpa mtu nafasi ya kufikiria sana jinsi yeye mwenyewe anavyotumia maisha yake. Hali inayokuwa katika nyumba ya karamu haiwezi kumsaidia afikiri kwa uzito hivyo.

Sulemani anaendelea kusema hivi: “Huzuni ni afadhali kuliko kicheko, maana simanzi ya uso ni faida ya moyo. Moyo wake mwenye hekima umo nyumbani mwa furaha.”​—Mhu. 7:3, 4.

Mtu aliye katika “nyumba ya matanga” anafahamishwa kwamba maisha ni mafupi kisha anaudhika kwa sababu ya matukio yasiyotazamiwa ya maisha hayo. Uso wake unakuwa wenye huzuni nyingi badala ya kuwa na vicheko anavyoweza kuwa navyo katika “nyumba ya karamu.” Hali ya uzito inayoonekana usoni inaweza kufaidi moyo, kumbadilisha mtu awe bora. “Moyo wake mwenye hekima umo nyumbani mwa matanga” katika maana ya kwamba moyo wake unafikiria jinsi anavyopaswa kutumia maisha yake, na sababu ya kufanya hivyo. Moyo wake hauwi katika hali ya kutojali inayokuwa mahali pa shangwe.

Sulemani anaendelea kutoa sababu na kusema: “Heri kusikia laumu ya wenye hekima, kuliko mtu kusikia wimbo wa wapumbavu; maana kama mlio wa miiba chini ya sufuria, ndivyo kicheko cha mpumbavu. Hayo nayo ni ubatili.”​—Mhu. 7:5, 6.

Mtu akiiacha njia inayofaa atafaidika akikemewa na mwenye hekima. Lakini angepata faida gani akisikia wimbo wa mpumbavu au akisifiwa-sifiwa naye kwa uongo? Kusifiwa hivyo kungeficha makosa yake na kumfanya aendelee kutembea katika njia mbaya na kuharibu sifa yake. Wakati mpumbavu anapocheka ovyo wakati usiofaa, kicheko chake kinaweza kuchukiza masikio ya mtu kama mlio wa miiba inayochomwa chini ya sufuria, kisimfaidi kwa njia yo yote.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki