Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w77 10/1 uku. 466
  • Msimamizi Mpya wa Watch Tower Achaguliwa

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Msimamizi Mpya wa Watch Tower Achaguliwa
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
  • Habari Zinazolingana
  • Kujulisha Habari Njema Bila Kuacha (1942-1975)
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
  • Jinsi Baraza Linaloongoza Linavyotofautiana na Shirika la Kisheria
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
  • Neno la Yehova Laendelea Kusonga Mbele Kasi (1976-1992)
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
  • Kuzitangaza Habari Njema Duniani Pote
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
w77 10/1 uku. 466

Msimamizi Mpya wa Watch Tower Achaguliwa

KAZI ya Yehova duniani inaendelea kusonga mbele sana ikiwa chini ya uongozi wa Mfalme aliyetawazwa, Yesu Kristo. Ndugu yetu mpendwa Nathan H. Knorr alipokufa Juni 8, 1977, ilikuwa lazima kuchagua msimamizi mpya wa Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania, ambalo ndilo shirika linaloendesha kazi za Mashahidi wa Yehova ulimwenguni pote, na vilevile ilikuwa lazima kuchagua msimamizi wa Watchtower Bible and Tract Society of New York, Inc., ambalo ndilo shirika la kisheria la kusimamia mambo ya Mashahidi wa Yehova katika United States. Viongozi wa mashirika hayo mawili walifuata pendekezo la washiriki wote kumi na watano wa Baraza Inayoongoza ya Mashahidi wa Yehova, wakakutana pamoja Juni 22, 1977, naye Frederick W. Franz akachaguliwa awe msimamizi wa mashirika yote mawili. Inapendeza kuona kwamba Ndugu Franz ndiye aliyetoa hotuba wakati wa kuzamishwa kwa Ndugu Knorr Julai 4, 1923, halafu mwaka uliofuata akatumikia akiwa karibu sana na Ndugu Knorr katika makao makuu ya ulimwengu ya Mashahidi wa Yehova, katika Brooklyn, New York. Ndugu Franz ametumikia kama msaidizi wa msimamizi wa shirika la Pennsylvania tangu mwaka 1945. Septemba 12, 1977, atakuwa na umri wa miaka 84. Yeye angali mwenye bidii nyingi katika utumishi wa Yehova, na hivi karibuni amerudi baada ya ziara ya juma saba ya kutoa hotuba katika nchi kumi na moja, kutoka Ireland mpaka Israeli. Yeye ni mwenye sifa nyingi sana ya kujifunza sana Biblia na kufanya kazi bila kuchoka kwa ajili ya faida za Ufalme, na kwa sababu hiyo ametumainiwa na kuungwa mkono na Mashahidi wa Yehova kila mahali. Anapenda sana watu wa Yehova waendelee kufanya kazi, watumikie na kusali pamoja mpaka mwisho wa taratibu hii ya mambo.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki