Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w78 2/15 kur. 13-18
  • Je! Furaha Inaweza Kupatikana Katika Jamaa Zilizogawanyika?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Furaha Inaweza Kupatikana Katika Jamaa Zilizogawanyika?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • NYUMBA ZIUZOGAWANYIKA KIDINI
  • JAMAA NA NDOA ZILIZOVUNJIKA
  • UNAPOPATIKANA MSAADA
  • TATIZO JINGINE LA JAMAA ZILIZOGAWANYIKA
  • SHIRIKIANENI KWA FURAHA
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2002
  • Kujenga Maisha ya Furaha ya Jamaa
    Kweli Iongozayo Kwenye Uzima wa Milele
  • Faida Zenye Kudumu Kutokana na Kuifuata Biblia Kama Jamaa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Kushirikiana ili Kuleta Umoja Katika Jamaa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
w78 2/15 kur. 13-18

Je! Furaha Inaweza Kupatikana Katika Jamaa Zilizogawanyika?

1, 2. (a) Maneno ya Yesu yaliyo katika Mathayo 10:34-36 yanatumikaje? (b) Ni jambo gani linalotamanika sana, na kwa kawaida linaweza kupatikanaje?

UJUMBE wa kweli, neno la Mungu, ni kama “upanga” na nyakati nyingine unaleta migawanyiko mikubwa kati ya washiriki wa jamaa. Yesu Kristo mwenyewe alisema yafuatayo juu ya hali hizo: “Nalikuja kumfitini mtu na babaye . . . Na adui za mtu ni wale wa nyumbani mwake.” (Mt. 10:34-36) Bila shaka, umoja unatamanika sana katika jamaa, na inawapasa wale wanaoutii ujumbe wa Ufalme wafanye yote wawezayo waviondoe vipingamizi vinavyoletwa na Shetani, ili “nuru ya injili ya utukufu wake Kristo” iwazukie washiriki wengine wa jamaa.​—2 Kor. 4:4.

2 Baadaye huenda mwamini akasaidia asiyeamini wahojiane Biblia akimwonyesha fadhili, upole na ustahimilivu unaoambatana na utu mpya wa Kikristo, huku akitenda sana mambo mema yanayohusu maisha ya Kikristo na kujiangalia asimhubiri-hubiri mwenzake nyakati zote. (Kol. 3:10, 12) Nao wazee au watu wengine katika kundi wanaweza kumwondolea asiyeamini maoni yake mabaya yasiyo na msingi kwa kukubali kumtembelea wanapokaribishwa wakale chakula, au kumtendea mambo mengine. Kuvumilia bila kuchoka kumekuwa na matokeo mazuri hata baada ya miaka mingi kupita, kwa sababu wasioamini wamegeuka wakawa mawakili wenye juhudi wa “habari njema ya ufalme.”​—Mt. 24:14.

NYUMBA ZIUZOGAWANYIKA KIDINI

3. (a) Sababu kubwa inayoleta mgawanyiko wa kidini katika jamaa ni nini? (b) Humu ni wenzi wasioamini wa namna gani mbili ambao habari zao zimezungumzwa?

3 Hata hivyo, wenzi wengi wanaoamini, hasa wanawake Wakristo, wanalazimika kulikabili tatizo la kuwa na jamaa iliyogawanyika. Wanawake hao waaminifu wanajua jinsi Neno la Mungu linavyoshauri, yaani, waolewe “katika Bwana tu.” (1 Kor. 7:39) Lakini, wengi wa watumishi wa Yehova walio katika jamaa zilizogawanyika wamejifunza kweli baada ya kuoa au kuolewa, na hapo ndipo wakaona kwamba wenzi wao hawataki kuifuata njia ya kweli wala kushirikiana nao katika utumishi wa Ufalme. Wameoana na mtu asiye na maoni mamoja nao juu ya kweli ya Neno la Mungu inayokubaliwa kwa bidii nyingi na Mashahidi wa Yehova. Mwanamke aliye katika hali kama hizo anawezaje kumwonyesha mumewe kwamba yeye ni mke hodari na kuonyesha watoto wake kwamba ni mama hodari pia? Inategemea sana nia ambayo asiyeamini anayo. Ikiwa yeye ni mtu asiyevuruga mkewe kwa sababu ya imani yake, na anampa uhuru fulani wa kuhudhuria mikutano ya Kikristo na kushiriki kuutangaza Ufalme, hapo mambo si magumu sana. Ikiwa anaruhusu mkewe afundishe watoto mambo ya Biblia, ili wakue wakiwa katika ile Njia, hapo tatizo si kubwa sana. Magumu halisi yanatokea wakati mume anapopinga utendaji wa Kikristo na mkewe na wa watoto, na kuwaletea vipangamizi vingi.

4. (a) Ni shauri gani la Maandiko ambalo mwamini atakumbuka juu ya kulipa kisasi, na kutakuwa na matokeo gani mazuri? (b) Mtume Petro alishaurije wake juu ya mwenendo wao?

4 Huenda kuyavumilia matatizo hayo kukawa jaribu kubwa kwa Mkristo. Kawaida ya mtu ni kutaka kulipa kisasi. Lakini, inampasa mke Mkristo aepuke kufanya hivyo kwa kukumbuka maneno ambayo mtume Paulo aliwaambia Warumi. Paulo alisema: “Msimlipe mtu ovu kwa ovu. Angalieni yaliyo mema machoni pa watu wote. Kama yamkini, kwa upande wenu, mkae katika amani na watu wote. Wapenzi, msijilipize kisasi, bali ipisheni ghadhabu ya Mungu, maana imeandikwa, Kisasi ni juu yangu mimi; mimi nitalipa, anena Bwana. Lakini, Adui yako akiwa na njaa, mlishe; akiwa na kiu, mnyweshe, maana ufanyapo hivyo, utampalia makaa ya moto kichwani pake. Usishindwe na ubaya, bali uushinde ubaya kwa wema.” (Rum. 12:17-21) Kwanza kufanya hivyo kutamletea Yehova sifa, na pili, mke huyo Mkristo atakuwa na amani ya akili. Atakuwa amelifuata shauri zuri la mtume Petro: “Kadhalika ninyi wake, watiini waume zenu; kusudi, ikiwa wako wasioliamini Neno, wavutwe kwa mwenendo wa wake zao, pasipo lile Neno; wakiutazama mwenendo wenu safi, na wa hofu. Kujipamba kwenu, kusiwe kujipamba kwa nje, yaani, kusuka nywele; na kujitia dhahabu, na kuvalia mavazi; bali kuwe utu wa moyoni usioonekana, katika mapambo yasiyoharibika; yaani, roho ya upole na utulivu, iliyo ya thamani kuu mbele za Mungu.”​—1 Pet. 3:1-4.

5, 6. Taja hatua ambazo mke anayeamini anaweza Kuchukua afundishe watoto wake kweli.

5 Mwanamke Mkristo anaweza kufanya nini mumewe asiyeamini akijaribu kumzuia asifundishe watoto na kuwalea katika adabu za Yehova? Bila shaka, atajitahidi awezavyo amwonyeshe mumewe faida nyingi za kUwapa watoto elimu ya Kikristo. Akimweleza mambo ambayo watoto watajifunza na jinsi watakavyofaidika kutokana na mikutano na ushirika, huenda asiyeamini akapoa kidogo hata awaruhusu wahudhurie mikutano ya Kikristo.

6 Lakini, asiyeamini akiendelea kujikaza tu asiruhusu watoto wahudhurie mikutano ya Kikristo, itampasa mke atumie busara na ufahamu anapofundisha watoto njia za uzima wa milele, ingawa nyakati zote atakuwa na mwenendo safi na mnyofu, akimtegemea Yehova amwongoze kuwasaidia watoto wake kiroho. Nyakati zote anaweza kuomba wazee katika kundi wamshauri inavyofaa afanye katika hali zake.

7. Inampasa mke Mkristo awe na lengo la kutimiza nini?

7 Lakini inampasa sana mke Mkristo ajitahidi awezavyo alete furaha katika ndoa, akimpelekea Yehova sala na kuitazamia siku ambayo mwenzake labda atarudiwa na fahamu ajiunge naye katika ibada ya Kikristo. Akifanya hivyo ndoa itakuwa yenye furaha kweli kweli, huku wote wawili wakishirikiana kufaidi jamaa yao na kutazamia Uzima wa milele.

JAMAA NA NDOA ZILIZOVUNJIKA

8, 9. Mke aliyeachwa ana daraka la kufanyia nini watoto wake, naye anawezaje kufanya hivyo?

8 Nyakati nyingine, kwa sababu ya wake kutetea yaliyo haki, waume wasioamini wametengana nao. Nyakati nyingine wanawake wamepata maarifa ya kweli baada ya kutalikiana au kutengana kisheria na waume wao. Kisa cha kutengana kitokeapo, lazima watoto wafikiriwe. Ingawa kulea watoto katika nyumba yenye mwenzi asiyeamini kunaweza kutatiza, hakika inaweza kumwia mwanamke vigumu sana kulea watoto katika nyumba isiyo na mume. Bila shaka mpango wa Yehova ni kwamba wazazi, yaani, baba na mama, wazoeze watoto wao. Jamaa ikiwa na umoja mazingira yanakuwa bora kabisa kwa kuzoezea watoto. Lakini mama aliye na watoto wadogo anaweza kufanya nini ikiwa nyumbani hakuna baba wa kuzoeza watoto na kumsaidia? Ni wazi kwamba hawezi kuachilia watoto wake. Hawezi kutumia wakati wake wote akieleza watu habari njema na kuwafundisha na huku akiachilia jamaa yake. Wala hawezi kutumia wakati wake wote akijisikitikia, na kusahau watoto wake wanaohitaji uangalizi. Yeye ana daraka la kuzoeza watoto, kuwapa kila nafasi anayoweza kupata awasaidie wakue wakiwa watoto wa Yehova na Mwanawe, Kristo Yesu.

9 Basi inampasa alete watoto kwenye kundi la Kikristo wapate kushirikiana na watu wa Bwana. Huenda huo ukawa mzigo mkubwa kwake ikiwa jamaa ina watoto wengi, wanaohitaji kusaidiwa. Huenda kukawa na maelekeo ya kuchoka, kuona kwamba ni kazi nyingi mno. Lakini, akimtumaini Yehova, ajitahidi na kuonyesha anataka kuzoeza watoto wake, anaweza kutimiza mengi. Tunaweza kusema ivyo hivyo juu ya mume anayelazimika kutunza watoto bila kusaidiwa na mkewe. Kwa kawaida kundi linakuwa na watu wengine wanaoweza kusaidia. Ingawa hawawezi kujitwalia daraka la kuangalia watoto hao, wanaweza kusaidia.

UNAPOPATIKANA MSAADA

10. (a) Ni njia gani anazoweza kutumia asaidie watoto hao? (b) Kupatana na Wagalatia 6:2, wanaoishi karibu wanaweza kufanya nini?

10 Labda mtu fulani kundini anaweza kusaidia watoto wako kwa kadiri fulani. Kwa mfano, labda kuna ndugu au dada kijana ambaye ameanza, urafiki na mwanao au binti yako na anaweza kujifunza naye, kuwa na ushirika unaofaa, na kumtia moyo hivyo katika njia ya haki. Labda kuna mume na mke wasio na madaraka mengine mazito wanaoweza kusaidia watoto wako waingie katika uhusiano wa karibu zaidi pamoja na kundi na akina ndugu na dada.​—Gal. 6:2.

11. Onyesha jinsi mzazi anayeamini anavyoweza kuwa mfano mwema kwa watoto.

11 Lakini mzazi aliye katika hali hiyo anapaswa akumbuke kuwekea watoto kielelezo chema, kwa kushirikiana mwenyewe na kundi na kuishi maisha manyofu. Inampasa mwanamke aliye katika hali hiyo atunzie watoto nyumba na kuiweka katika hali safi, na kukuza sifa za Kikristo zitakazoonyesha kwamba anajitahidi kuwekea wengine mfano mwema. Na ingawa nyakati nyingine huenda akawa na sababu za kuudhika na kushindwa kujiweza, inampasa amwite Yehova amsaidie na kujizuia asiseme wala kutenda mambo yenye kuleta sifa mbaya juu ya maisha yake ya Kikristo. Ikiwa wewe una matatizo ya upande huo, ongea na wazee katika kundi. Kila hali inatofautiana na nyingine, kwa hiyo si vyepesi kushauri kwa mapana na marefu jinsi ya kufanya katika visa vyote. Nyakati nyingine watoto wanahitaji fimbo ya kuwatia adabu, lakini nyakati nyingine huenda ikatosha kuongea nao uso kwa uso na kuwasaidia wapambanue yaliyo haki na mabaya. Mmojawapo adui wakubwa zaidi wa kuzoeza watoto ni kuvurugika moyo. Inaweza kuwa hivyo hasa ikiwa mzazi mmoja tu ndiye baba na mama pia. Lakini maneno ya Mungu yaliyoandikwa katika Biblia, yenye kutuliza mtu na kumburudisha, yanaweza kusaidia watu wote.​—Mit. 16:24; Isa. 57:15.

TATIZO JINGINE LA JAMAA ZILIZOGAWANYIKA

12, 13. (a) Taja tatizo jingine linalopatikana katika jamaa zilizogawanyika. (b) Mtu anawezaje kutatua tatizo hilo?

12 Watu fulani ambao wenzi wao wamejitenga nao, au wakawapa talaka, wameiandikia Watch Tower Society kuomba mashauri juu ya jinsi ya kuondoa upweke walio nao. Hakika jambo hilo linaweza kuingiza matatizo katika maisha yao. Biblia inashauri kwamba watu waliooana wakae pamoja. (1 Kor. 7:10-13) Lakini, I huenda mwenzi asiyeamini akawa amemwacha anayeamini kwa kupenda kwake mwenyewe. Mtu anawezaje kutatua tatizo hilo maishani?

13 Bila shaka, mtu anakosa “haki” ya ndoa ikiwa ametengana na mwenzi wake. Jambo hilo linaweza kumhangaisha na kumshusha moyo. Mwenzi mwenye kutaabika akiwa katika hali hizo anaweza kufuata shauri la Paulo, “apatane” na mwenziwe na kumaliza mtengano wao. (1 Kor. 7:11) Huenda jambo hilo lisiwezekane katika hali nyingine, hasa ikiwa mwenzi wa ndoa hataki mapatano, au ikiwa anataka warudiane kwa masharti ya kwamba mwenziwe atakubali kufanya mambo yasiyompasa Mkristo, kama kuikana kweli au kuingia katika mwenendo usio wa Kikristo unaochafua malazi ya ndoa,​—Ebr. 13:4.

14, 15. Wanaoamini wanapewa mawaidha gani nyakati hizi zenye magumu?

14 Basi, ni wazi kwamba Mkristo atalazimika kujitahidi afuate mwendo unaopatana na kanuni za Kikristo, utakaomsaidia pia aondoe hali yake ya kushuka moyo na upweke alio nao. Labda anaweza kupanga mambo yake atumie wakati mwingi zaidi akieleza watu habari za ufalme wa Mungu au akijifunza Biblia na watu walioanza kupendezwa karibuni. (Linganisha Luka 2:36, 37) Njia nyingine ya kumaliza upweke ni kushughulika zaidi kusaidia wenye shida kundini.​—Zab. 105:1, 2; Rum. 12:12, 13.

15 Ikiwa wewe ni mwanamke, huenda kukawa na wanawake wazee kundini wanaohitaji ushirika, wanaohitaji mtu wa kujifunza nao, au kuwatunza kwa njia nyingine. Hiyo inaweza kuwa njia moja ya kutumia vizuri saa zako za ziada, ikiwa unaona kwamba wakati unakuzidia mno na huna la kufanya. Tazama pale na pale kundini uone unaweza kufadhili nani. Unaweza kupata furaha nyingi kutokana na utoaji wa namna hiyo. (Matendo 20:35) Au huenda kundi likawa lina wanawake wengine walio katika hali kama zako, labda walioachwa na waume zao, au walio wajane, nawe unaweza kushirikiana nao mtumie vizuri wakati wenu katika pande fulani za utumishi wa Ufalme na kujengana kiroho.

16, 17. Mtu anaweza kutafuta faraja na kitulizo wapi, na inapasa akumbuke shauri gani jema la Petro?

16 Ni hakika kwamba ni vigumu kuyakabili matatizo hayo ya upweke, ya kuona wasiwasi na kushuka moyo kwa sababu ya jamaa kuvunjika. Lakini ukitii shauri la mtunga zaburi, ‘umtwike Yehova mzigo wako,’ yeye ‘atakutegemeza’ na kukusaidia ushinde vipingamizi hivyo maishani.​—Zab. 55:22.

17 Ukumbuke sikuzote sababu inayokufanya uwe katika hali ulimo. Kwa kuwa sababu ni kwamba unataka kuwa mfuasi wa Bwana Yesu Kristo, hakika Neno la Mungu litakufariji sana kwa sababu ya mwendo unaofuata. (1 Pet. 3:17) Jaribu kutembea katika uaminifu, kufanya mapenzi ya Yehova, kisha uwe na hakika kwamba Muumba wetu Mkuu, Yehova Mungu, hatakosa kuuona mwenendo wako mwema.​—Mt. 10:36-39.

SHIRIKIANENI KWA FURAHA

18. Ni jambo gani linalowapa watumishi wa Yehova tumaini lenye furaha juu ya wakati ujao, na kulingana na Yohana 13:35 ni jambo gani linaloweza kusaidia?

18 Yehova, Mungu mwenye furaha, ameonyesha katika Neno lake la kweli mambo yanayohitajiwa ili Wakristo wa kweli wawe wenye furaha halisi. (1 Tim. 1:11; Mt. 5:3-5) Katika makundi ya watu wa Yehova duniani pote utaona watu wa namna zote, wenye hali za maisha ya namna zote. Wao wana jambo moja kwa ujumla, yaani, imani katika Yehova. Imani hiyo inawapa tumaini lenye furaha juu ya wakati ujao. Kama jamaa yenye umoja, watu wote wa Yehova wanapendezwa kuona ndugu na dada zao wa kiroho wakiwa na hali njema, na ndivyo inavyowapasa kuwa. Inawapasa wote washirikiane kuonyeshana huruma ya kweli na kupendana. Ingawaje, Yesu alisema kwamba watu wangejua sisi tu wanafunzi wake tukiwa na upendo sisi kwa sisi. (Yohana 13:35) Hiyo ndiyo alama yenye kutambulisha Ukristo wa kweli.

19. (a) Kama inavyoonyeshwa katika Yohana sura ya 10, furaha ya kweli inaweza kupatikanaje? (b) Wote wanawezaje kuwa na fungu la kuendeleza hali zenye furaha katika jamaa?

19 Udugu wa watu wa Yehova unaongezeka upesi sana ulimwenguni pote. Makumi ya maelfu ya watu wanamiminika kuingia katika zizi la Mchungaji Mwema, wakitaka kuongozwa na kuchungwa na Bwana Yesu Kristo. Yesu alieleza jambo hilo vizuri kwa kusema: “Mimi ndimi mchungaji mwema; nao walio wangu nawajua; nao walio wangu wanijua mimi.” (Yohana 10:14) Kwa kukaa ndani ya zizi la kondoo tutapata baraka na furaha ya kweli iliyo na watumishi wa Yehova. Tuwe tumeoa au tumeolewa, au tuwe hatujaoa au hatujaolewa, tuwe tunaishi katika jamaa zilizogawanyika au hata zilizovunjwa na matatizo ya ulimwengu wa zamani, sote tuna taraja la kupata uzima wa milele chini ya mpango wa Ufalme. Kwa mambo tunayotenda katika maisha ya kila siku, na kwa kujipatanisha na mwenendo unaofaa na adabu zilizoonyeshwa katika Maandiko Matakatifu, tunaweza kuonyesha kwamba watumishi wa Mungu ni watu wenye furaha kweli kweli, wenye kutumikia faida za ufalme wa milele wa Mungu na Mwanawe. Basi, kila mmoja wetu anaweza kuwa na fungu la kuendeleza hali zenye furaha katika jamaa na kulitukuza jina la Yehova kwa njia hiyo!​—

Kutoka The Watchtower, Sept. 15, 1977.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki