Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w78 4/1 kur. 8-12
  • ‘Makaripio Ndiyo Njia ya Uzima’

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • ‘Makaripio Ndiyo Njia ya Uzima’
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • TUNAPOSUMBULIWA NA MOYO
  • KUSHUGHULIKA NA MAELEKEO YASIYOFAA
  • VI5A VYA MAKOSA MAKUBWA YANAYOHITAJI KARIPIO
  • KUENDELEZA HALI KAMA YA JAMAA
  • Kukaripia “Mbele ya Watazamaji Wote”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
  • Kukaripia Watu Wanaozoea Dhambi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
  • Toba Inayorudisha Mtu Kwa Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
  • Kwa Nini Lililo Baya Liripotiwe?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
w78 4/1 kur. 8-12

‘Makaripio Ndiyo Njia ya Uzima’

Mnara wa Mlinzi wa Mei 1, 1977 ulikuwa na mfululizo wa makala kuhusu karipio. Wasomaji wengi walizithamini habari hizo na kusema wangependa habari zaidi zichapwe ili kupanua mambo yaliyoelezwa humo. Makala za mafunzo zilizomo katika toleo hili zimetayarishwa kwa kusudi hilo.

“Amri hiyo ni taa, nayo sheria ni nuru, nayo makaripio ya adabu ndiyo njia ya uzima.”​—⁠Mit. 6:23, NW.

1. Ni hali gani ya wanadamu Inayotokeza ulizo juu ya jinsi tunavyoweza kupata na kudumisha msimamo usio na mawaa mbele za Yehova? (Rum. 3:23)

MARA nyingi sisi wanadamu tusio wakamilifu tunakosa kwa usemi, nia na matendo. Akiandikia Wakristo wenzake, mtume Yohana alisema hivi: “Tukisema kwamba hatuna dhambi, twajidanganya wenyewe, wala kweli haimo mwetu.” (1 Yohana 1:8) Yakobo mwanafunzi Mkristo alikubali hivi: “Twajikwaa sisi sote pia katika mambo mengi. Mtu asiyejikwaa katika kunena, huyo ni mtu mkamilifu, awezaye kuuzuia na mwili wake wote kama kwa lijamu.” (Yak. 3:2) Basi, tunawezaje kupata na kudumisha msimamo mzuri mbele za Mungu?

2. (a) Lazima mtu afanye nini ili aonekane na Yehova kuwa safi? (1 Fal. 8:46-50; Isa. 1:16-18; 55:6, 7; Kol. 1:13, 14; Ufu. 7:14) (b) Karipio linalotegemea Biblia linatusaidiaje kuendeleza msimamo usio na mawaa mbele za Mwenye Nguvu Zote? (Mit. 3:12; Ufu. 3:19)

2 Tunahitaji kusamehewa dhambi zetu. Hapo tunatakiwa tumwungamie Aliye Juu Zaidi makosa yetu, tuonyeshe toba au majuto ya kweli, na kuomba msamaha kwa kutegemea dhabihu ya Yesu inayolipia dhambi Biblia inasema, “Tukiziungama dhambi zetu, Yeye ni mwaminifu na wa haki hata atuondolee dhambi zetu, na kutusafisha na udhalimu wote.” (1 Yohana 1:9) Karipio linalotegemea Neno la Mungu na kanuni zake zenye haki linaweza kutuonyesha waziwazi jinsi hasa tunavyotenda dhambi, na kutusaidia tuchukue hatua zinazohitajiwa ili kupata msamaha wa Mungu tuendelee kuwa na msimamo usio na mawaa mbele zake. Karipio hilo linaweza kutusaidia tuepuke pia kufanya makosa makubwa zaidi.

3. Ni nini kinachoweza kutufanya tujikaripie wenyewe, na tunafanyaje hivyo? (Mit. 1:20-25)

3 Tunapoisoma Biblia au mashauri yanayotokana na Biblia, au tunaposikia Neno la Mungu likizungumzwa katika mkutano wa kundi, huenda tukajua kwamba tumetenda dhambi kwa njia fulani. Huenda tukajutia makosa yetu kwa moyo mweupe, tuombe tusamehewe na kusaidiwa na roho ya Mungu tufanye maendeleo zaidi ya kupatanisha maisha yetu na mapenzi yake. Tunapothamini mashauri ya Biblia kwa moyo hivyo na kuyatumia, tunajikaripia wenyewe.

TUNAPOSUMBULIWA NA MOYO

4. Kwa sababu gani huenda mtu akapata kujisikia hastahili kumwendea Yehova katika sala? (b) Mtu aliye katika dhiki ya kiroho anapaswa kufanya nini, na jambo hilo linaweza kumsaidiaje?

4“Halafu, tena, huenda mtu akajisikia hastahili kumfikia Mungu katika sala kwa sababu amefanya kosa au ana kawaida ya kutenda dhambi. Huenda dhiki yake ya kiroho ikaharibu afya yake ya kimwili. Huenda ikawa hivyo ingawa mtu huyo analichukia kosa hilo kikweli na anataka kufanya yaliyo haki kwa moyo mweupe. Akijiona katika hali hiyo, anaweza kufanya nini? Mwanafunzi Yakobo anajibu hivi: “Na awaite wazee wa kanisa; nao wamwombee.” (Yak. 5:14) Huenda mtu huyo akapata nguvu za kumkaribia Yehova katika sala asikiapo sala ambayo mzee anamtolea kwa moyo na juhudi. Tena, huenda akasaidika awaze kwa njia hii inayofaa: ‘Ikiwa wengine wana hakika kwamba Yehova atawajibu sala wanazotoa kwa ajili yangu, mbona mimi nami nisiweze kuwa na hakika kwamba atanijibu sala zangu?’

5. (a) Kwa sababu gani hakuna haja ya kukaripia mtu anayesikitikia sana dhambi ambazo amefanya? (b) Wazee wanaweza kumsaidiaje mtu huyo?

5 Mtu huyo mwenye kutubu hana haja ya kukaripiwa na mtu mwingine ili kumjulisha uzito wa dhambi yake. Moyo wake mwenyewe umekwisha mkaripia, naam, ukamlaumu. (1 Yohana 3:19-22; linganisha 2 Samweli 24:10; Zaburi 32:3-5.) Kwa hiyo, huenda kukawa na uhitaji wazee wamkumbushe mtu aliye dhaifu kiroho kwamba Yehova ni mwenye rehema na ana nia ya kusikia sala zetu. (Neh. 9:17; Mt. 7:7-11) Huenda ikawa lazima mipango ifanywe kumjenga kiroho muda kwa muda, kwa kipindi cha juma nyingi au hata miezi mingi. Mtu mwenye uhitaji huo asidharau msaada ambao wazee wanataka kumpa.

KUSHUGHULIKA NA MAELEKEO YASIYOFAA

6. Ni maelekeo gani yasiyofaa yanayoweza kusitawi kundini, na inawapasa wazee wafikirie nini?

6 Bila shaka, kuna nyakati ambazo wazee wanahitaji kukaripia watu mmoja mmoja au kundi lote kwa ujumla kuhusu maoni au matendo fulani. Huenda watu wakawa wanasitawisha maelekeo yasiyofaa. Huenda wengine wakawa ‘wameacha upendo wao wa kwanza’ na sasa hawajali sana madaraka yao ya kiroho. (Ufu. 2:4; 3:15-18) Labda uulimWengu unaingizwa kidogo kidogo katika vikusanyiko vya kujifurahisha (karamu). (1 Pet. 4:3) Huenda watu fulani wakawa wanaeneza porojo zinazoweza kuumiza wengine au huenda wakawa hawazuii ndimi zao kwa njia nyinginezo. (Efe. 4:29, 31; 5:3, 4) Huenda wazazi wakawa ni wazembe sana katika kuzoeza watoto wao. (Efe. 6:4) Huenda wengine wakawa wanakunywa vileo kupita kadiri, au labda ndugu wengine wana tabia mbaya wanapokuwa na wanawake, au akina dada wanakuwa vivyo hivyo wanapokuwa na wanaume. (Efe. 5:18-20; linganisha 1 Timotheo 5:1, 2.) Kundi likiwa na hali za jinsi hiyo, ingekuwa vizuri wazee wazungumze pamoja mambo wanayoweza kufanya wasaidie watu mmoja mmoja na ndugu wote kwa ujumla.

7. Ni njia gani moja ambayo wazee wanaweza kutumia watoe karipio la Maandiko katika nyumba za ndugu zao?

7 Labda wanaweza kuchagua sura za Biblia zinazofaa, au makala zinazohusu Biblia, wazisome na kuzizungumza faraghani pamoja na mtu aliye na matatizo makubwa ya kiroho. Kwa kuhakikisha kwamba mtu anayehitaji msaada anafahamu maana ya maandiko yanayozungumzwa na jinsi yanavyoihusu hali yake, hapo wazee watakuwa wakimsahihisha au kumkaripia. Kwa kawaida mzee mmoja au wawili wanatosha kufanya hivyo nyumbani kwa mtu huyo katika hali za kikawaida, wala si lazima mkutano rasmi upangwe.​—⁠Linganisha Matendo 20:18-20, 31.

8. Hotuba zenye kutegemea Biblia zinazohusu mambo yasiyopendeza kundini zinawezaje kuwakaripia wasikilizaji?

8 Kwa upande mwingine huenda wazee wakaona inafaa kutoa hotuba za Maandiko zinazopatana na mambo yasiyopendeza ambayo yameanza kutokea kundini, na kuyazungumza kwa kutoa sababu. (2 Tim. 4:2; Tito 1:10-14) Hotuba hizo za Biblia zilizo wazi na zenye mkazo zinapasa ziongoze wasikiaji wajichunguze na kufanya mabadiliko wanayohitaji sana maishani mwao. (Linganisha Yakobo 1:22-25.) Waonapo kwamba maandiko yanayozungumzwa yanawahusu wao bi nafsi, hapo watakuwa wamekaripiwa.​—⁠Linganisha 1 Wakorintho 14:24, 25, NW, panaposema kwamba asiyeamini anakaripiwa na mambo anayosikia katika mkutano wa kundi.

VI5A VYA MAKOSA MAKUBWA YANAYOHITAJI KARIPIO

9. (a) Ni dhambi za jinsi gani zinazoweza kuletea kundi suto kubwa. (b) Kwa sababu gani mtu ambaye amefanya dhambi nzito mara moja tu anaweza huwa mchafu bado mbele za Yehova?

9 Kama ilivyokuwa katika karne ya kwanza, leo Wakristo fulani waliobatizwa wanafanya dhambi kubwa zinazoletea kundi suto. (Angalia mifano ya makosa hayo katika 1 Wakorintho 5:11; Wagalatia 5:19-21 na 1 Timotheo 1:9, 10.) Huenda wakafanya kosa zito mara moja tu au huenda wakaendelea kutenda dhambi kwa muda fulani. Mtu anayefanya kosa kubwa, hata ikiwa ni mara moja tu, anaendelea kuwa mchafu machoni pa Yehova mpaka wakati atakapomtubia na kumwomba amsamehe.

10. Wazee wana wajibu wa kufanya nini juu ya watu wenye hatia ya dhambi nzito?

10 Wazee wanapaswa kufanya nini kwa habari ya watu wanaofanya makosa makubwa? Inawapasa wajitahidi sana kuwasaidia kiroho, kuwasaidia watubu, ikiwa watu hao hawajafanya hivyo. Wazee wanahitaji kusali na kutumia uangalifu wanapofikiria njia bora ya kufanya hivyo.

11. Kwa sababu gani mtu ambaye ametubia kosa lake anaweza kuhitaji kukaripiwa zaidi?

11 Nyakati nyingine mtu aliyetumbukia katika kosa kubwa anakuwa na huzuni ya kimungu na kuonyesha amekaza nia afanye yaliyo haki. Maneno yake yanaonyesha kwamba anafahamu dhambi yake ilikuwa mbaya sana. Kwa hiyo, hana haja ya kusadikishwa ametenda kosa zito ili atubu. Lakini huenda akakosa kufahamu sana kwamba kuna dhambi nyingine zilizomwongoza kufanya kosa lake zito. Huenda akawa alianza kuwa na mawazo machafu. Huenda akawa alikuwa akisoma vitabu vibaya na kufanya tafrija zisizofaa. Labda alipumbaa katika fahamu zake hata asiweze kupambanua mema na mabaya kwa sababu ya kujiacha aongozwe sana na mambo ya kilimwengu. (Ebr. 5:11, 14) Basi, ni wazi kwamba anahitaji kukaripiwa, na huenda wazee wakatakiwa kutumia wakati mwingi wamsaidie afahamu maana halisi ya kuwa Mkristo. Huenda ikawapasa kumwonyesha jinsi alivyoyapuza mara nyingi maonyo ya upole ya Maandiko. Zaidi ya kutubia dhambi kubwa aliyofanya, huenda pia ikawapasa kumjulisha ubora wa kutubia dhambi zile nyingine ndogo zilizomwongoza kufanya hiyo kubwa.

12. Ni mambo gani yanayoweza kufanya wazee wakaripie mshiriki wa kundi hadharani?

12 Ili kundi liwe na woga mzuri wa kutofuata mwendo wenye dhambi, wazee wanaweza kuamua kulizungumzia mambo yanayohusu tatizo la mtenda kosa, kwa kutumia Maandiko. Ingawa huenda wasitaje jina lake, yeye mwenyewe atajua kwamba anakaripiwa mbele ya wote, na pia wale wanaoijua hali yake watafahamu hivyo. (1 Tim. 5:20, NW) Wakati wazee wanapoamua kama karipio linapasa litolewe juu ya mwenendo mbaya wa mtu, inawapasa wafikirie kama karipio hilo litalifaa sana kundi, pamoja na mtenda kosa. Inawapasa pia wafikirie vizuizi anavyopaswa kuwekewa mtu huyo anayekaripiwa.

KUENDELEZA HALI KAMA YA JAMAA

13. Uhakika wa kwamba kundi ni kama jamaa unaamuaje jinsi wenye kutenda makosa wanavyopaswa kutendewa?

13 Wakati wazee wanapokaripia watenda makosa, wanahitaji kukumbuka kwamba kundi ni kama jamaa, ni ‘ushirika wa ndugu.’ (1 Pet. 5:9, NW) Walio katika kundi wanapasa watendewe mambo kwa fadhili na heshima kama vile mtu anavyoweza kutendea washiriki wa jamaa yake mwenyewe. (1 Tim. 5:1, 2) Wazazi wazuri hawasikilizi jinsi kosa la watoto wao lilivyokuwa kisha wanatangaza uamuzi kama hakimu anavyofanya mahakmani. Wanajaribu kusaidia watoto waliopotoka warudiwe na fahamu na kuenenda wakati ujao kwa njia itakayoletea jamaa sifa njema, si aibu.

14. Wazazi wazuri wanaweza kushughulikiaje makosa ya watoto wao?

14 Kwa kawaida wazazi wanaongea na mwana au binti yao anayefanya kosa wakiwa faraghani, wala hawalitangazi kosa lake mbele ya jamaa yote ili kumwaibisha. Lakini wanapoona wanahitaji sana kueleza watoto wale wengine jambo lililotukia, wanafanya hivyo ili kuonya jamaa isitende kama mshiriki huyo asiyetii. Kwa muda fulani wazazi wanaweza kuvumilia hata makosa ya mwana au binti ambaye ni mtu mzima, anayeishi nyumbani bado. Halafu, wakiendelea kumsahihisha mara nyingi lakini awashinde, wanaweza kumwagiza aondoke nyumbani aende zake. (Linganisha jambo hilo na lile lililofanywa na wazazi Waisraeli kupatana na amri iliyo katika Kumbukumbu la Torati 21:18-21.) Wanapochukua hatua hiyo, huenda pia kusudi lao likawa ni kukinga watoto wao wadogo wasifuate maongozi yake mapotovu.

15. Lengo la kwanza la wazee linapasa kuwa nini kwa habari ya watenda makosa, na ni wakati gani peke yake watakapotenga mtu na ushirika?

15 Ingawa wazee si kama wazazi kundini, bali ni kama ndugu wakubwa katika jamaa, inawapasa wao pia wajitahidi sana kuwasaidia watenda makosa watubu kwanza. Ili waweze kuwapa karipio la Maandiko linalofaa, huenda wakahitaji kutumia wakati mwingi. Hata Yesu Kristo alisema yafuatayo juu ya mwanamke Yezebeli wa kundi la Thiatira: “Nimempa muda ili atubu, wala hataki kuutubia uzinzi wake.” (Ufu. 2:21) Ikiwa mtu anafuata mfano wa kutotubu wa mwanamke Yezebeli, hapo inawapasa wazee wamtenge na ushirika, waiondoe “chachu” yenye kulichafua kundi.​—⁠1 Kor. 5:6, 7.

16. Ni baadhi ya mambo gani ambayo wazee watahitaji kufanya ili kusaidia sana watenda makosa?

16 Ili wazee waweze kusaidia sana watenda makosa, lazima wafikirie mambo kupatana na Neno lote la Mungu, wala wasitegemee vifungu vichache tu vinavyotaja makosa fulani yaliyo wazi. Kwa kutazama kosa kijuujuu, huenda likaonekana kama linafanana kabisa na jingine lililoshughulikiwa hapo kwanza. Lakini, hali, nia na makusudi ya watu wanaohusika huenda yakawa yanatofautiana sana. Mambo yote yanapasa yafikiriwe kwa uangalifu kupatana na Maandiko, ili kuwa na hakika ya kufanya jambo litakalolifaa sana kundi pamoja na mtenda kosa. Karipio lo lote la Maandiko litolewe kupatana na mahitaji ya mtu. Baada ya kupata habari zote juu ya kosa lililofanywa na mambo yaliyoongoza mtu kulifanya, wazee wanaoshughulikia tatizo hilo watapaswa kutumia wakati ili kila mmoja wao atafakari na kusali akiyafikiria Maandiko kabla ya kukutana pamoja wazungumze jambo la kufanya. Hapo watakuwa katika hali nzuri zaidi ya kutoa karipio linalofaa na msaada wa kiroho unaohitajiwa.

17. Sisi washiriki wa kundi tunapaswa kujikaza tufanye nini, nasi tutapata thawabu gani?

17 Hakika karipio la Maandiko linasaidia sana washiriki wote wa kundi wafuate mwendo unaowaongoza kwenye uzima wa milele. Basi, acheni .sisi mmoja mmoja tuendelee kuyasikiliza makaripio yaliyo katika Biblia, tupinge vishawishi tusiingie katika mwenendo unaoweza kuleta suto juu ya Mungu Aliye Juu Zaidi na kundi la watu wake wenye kujitoa kwa moyo. Tukifanya hivyo, tunaweza kuwa na hakika ya kupata baraka za Yehova sasa na thawabu ya uzima wa milele katika taratibu yake inayokuja, iliyo mpya na yenye haki. ​—⁠Yohana 17:3.

[Picha katika ukurasa wa 10]

Huenda tukakaripiwa kwa njia mbalimbali, kwa mfano kwa kusoma Maandiko au kitabu kinachotusaidia tuifahamu Biblia, kwa kushauriwa binafsi na mtu fulani na kwa kusikia hotuba yenye Maandiko katika mkutano wa kundi

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki