Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w78 5/1 uku. 23
  • Maswali Kutoka Kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka Kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
  • Habari Zinazolingana
  • Mkaribie Mungu Katika Sala
    Biblia Inafundisha Nini Hasa?
  • Kusali Mbele ya Wengine Kwa Moyo Mnyenyekevu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Yehova Anathamini Unaposema “Amina”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2019
  • Sala Ambazo Zinajibiwa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
w78 5/1 uku. 23

Maswali Kutoka Kwa Wasomaji

● Je! ni vibaya kurekodi katika utepe sala zinazotolewa hadharani?

Wakristo fulani wanaona ni afadhali wasifanye hivyo. Lakini Biblia haikatazi watu kuweka kumbukumbu la maneno yaliyosemwa katika sala, kwa kuyaandika au kwa kutumia njia nyingineyo.​—2 Nya. 33:18.

Huenda mtu akarekodi mkutano wa Kikristo katika tepu ili akajikumbushe baadaye au ukasikilizwe na wale ambao hawakuweza kuhudhuria. Wakati wa kurekodi mambo kama hayo, Wakristo wengine wanaanza kurekodi baada ya sala ya kufungua na kuacha kurekodi kabla ya sala ya kumalizia.

Huenda wakawa wanawaza kwamba sala si njia rasmi ya kufundisha watu. Bali, sala inafikiriwa kuwa maneno ambayo mtu mwenyewe anamwambia Mungu, ingawa huenda wengine waliopo wakasikiliza na kukubaliana naye kwa kusema “Amin.” Tena, mtu anayerekodi mkutano huo anajua kwamba baadaye hatasema “Amin” anaposikiliza sala aliyorekodi, kama kwamba sala hiyo inakwenda kwa Mungu kila mara anapoufungua utepe wake.

Hata hivyo, inafaa kuangalia kwamba sala nyingi zimeandikwa katika Biblia. (Mwa. 24:10-14; Mt. 26:36-39; Yohana 11:41, 42; 17:1-26; Matendo 4:23-30) Hatuzichukui sala hizo kama kwamba tunatakiwa tuseme “Amin” wakati tunapozisoma.​—Rum. 8:26, 27.

Bila shaka, sala hizo ni sehemu ya Biblia; zimeandikwa humo kwa sababu Mungu alitaka ziandikwe. (2 Tim. 3:16) Tena huenda watu wengine wakaiona sala iliyorekodiwa katika utepe kwa njia iliyo tofauti na vile wanavyoiona sala iliyo katika Biblia. Kwa hiyo, ikiwa watu hawakuambiwa wasirekodi sala, Mkristo anaweza kujiamulia kama atazirekodi sala pia anaporekodi mkutano wa Kikristo katika utepe. Kulingana na Maandiko, hakuna ubaya wa kufanya hivyo.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki