Je! Unakumbuka?
● Je! ahadi ya Mungu inayosema ataondoa “maumivu” ina maana ya kwamba hali zote za kuona maumivu mwilini zitakwisha?—Ufu. 21:4.
Hapana, kuona maumivu kunasaidia mtu kwa kumwonyesha hatari na kumwezesha achukue hatua ya haraka kukiepuka kitu kinachomletea maumivu. Maumivu ‘hayatakuwapo tena’ katika maana ya kwamba mambo yote yenye kuletea wanadamu taabu, yaani, kuonewa, uvunjaji wa sheria, magonjwa, kifo na mengineyo, yataondolewa duniani.—M9/15/77 415.