Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w80 10/1 kur. 4-6
  • Waja—Ulimwengu Usio na Maumivu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Waja—Ulimwengu Usio na Maumivu
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • JAMBO JIPYA LIKO MBELE YETU
  • MATUKIO CHINI YA UTAWALA WA UFALME
  • MAUMIVU AMBAYO YATATOWEKA
  • VYANZO VYA MAUMIVU VYAONDOLEWA
  • WAWEZA KUWA WAKO​—UKIUTAKA
  • Ni Nani Anayehitaji Maumivu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
  • Dunia Isiyo na Maumivu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
  • Karibuni—Ulimwengu Usio na Maumivu!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Maumivu Ambayo Hayatakuwapo Tena
    Amkeni!—1994
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
w80 10/1 kur. 4-6

Waja​—Ulimwengu Usio na Maumivu

“Nikaona mbingu mpya na nchi mpya; kwa maana mbingu za kwanza na nchi ya kwanza zimekwisha kupita, wala hapana bahari tena. Nami nikauona mji ule mtakatifu, Yerusalemu mpya, ukishuka kutoka mbinguni kwa Mungu, umewekwa tayari, kama bibi-arusi aliyekwisha kupambwa kwa mumewe. Nikasikia sauti kubwa kutoka katika kile kiti cha enzi ikisema, Tazama, maskani ya Mungu ni pamoja na wanadamu, naye atafanya maskani yake pamoja nao, nao watakuwa watu wake. Naye Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao. Naye atafuta kila chozi katika macho yao, wala mauti haitakuwapo tena; wala maombolezo, wala kilio, wala maumivu hayatakuwapo tena; kwa kuwa mambo ya kwanza yamekwisha kupita.”​—Ufu. 21:1-4.

KUONA maumivu ya mwilini kwaweza kumfahamisha mtu juu ya umizo ambalo kama hangeona maumivu hayo lingeendelea kwa muda fulani bila kujulikana. Kwa hakika, kuna nyakati ambazo kuweza kuona maumivu kama hayo kwaweza kuokoa maisha ya mtu. Hata hivyo Neno la Mungu laahidi ulimwengu ambao hautakuwa na maumivu. Mtume Mkristo Yohana aliongozwa na Mungu aandike hivi:

“Kisha nikaona mbingu mpya na nchi mpya; kwa maana mbingu za kwanza na nchi ya kwanza zimekwisha kupita, wala hapana bahari tena. Nami nikauona mji ule mtakatifu, Yerusalemu mpya, ukishuka kutoka mbinguni kwa Mungu, umewekwa tayari, kama bibi-arusi aliyekwisha kupambwa kwa mumewe. Nikasikia sauti kubwa kutoka katika kile kiti cha enzi ikisema, Tazama, maskani ya Mungu ni pamoja na wanadamu naye atafanya maskani yake pamoja nao, nao watakuwa watu wake. Naye Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao. Naye atafuta kila chozi katika macho yao, wala mauti haitakuwapo tena; wala maombolezo, wala kilio, wala maumivu hayatakuwapo tena; kwa kuwa mambo ya kwanza yamekwisha kupita.”​—Ufu. 21:1-4.

Ndiyo hiyo​—ahadi kutoka kwa Mungu kwamba “maumivu hayatakuwapo tena.” Hiyo ingeweza kuwa na maana gani? Itakuwa na matokeo gani kwa wanadamu?

JAMBO JIPYA LIKO MBELE YETU

Maulizo kama hayo yanahitaji kujibiwa. Walakini maneno hayo yaliyoandikwa karne 19 zilizopita yanamaanisha mengi zaidi. Yanadokeza kwamba kuna jambo jipya mbele yetu. Ebu fikiria kwa ufupi yanayomaanishwa na unabii huu.

“Mbingu mpya” ambazo zimetabiriwa ndio ule ufalme wa kimbinguni wa Yesu Kristo. ‘Warithi washirika’ wake ambao ‘’watashirikiana naye katika utawala wanaitwa hapa “Yerusalemu mpya.” (Rum. 8:14-17) “Dunia mpya” ambayo imeahidiwa si sayari iliyo tofauti. Mahali pake, ni jamii mpya ya kibinadamu iliyo na umoja na yenye haki chini ya ufalme wa Kristo.​—Linganisha Zaburi 96:1; Mhubiri 1:4.

Mahali pa ‘mbingu za kwanza na dunia ya kwanza,’ ile taratibu ya kwanza iliyojaa machozi, kifo, maombolezo na maumivu yenye kutaabisha patachukuliwa na mbingu mpya na dunia mpya. Na ijapokuwa bahari halisi yenye kujaa maji itaendelea kuwapo, “bahari” ya mfano ya watu wasiotulia na wasiomwogopa Mungu haitakuwapo tena.

MATUKIO CHINI YA UTAWALA WA UFALME

Ni matukio mazuri kama nini yaliyo mbele yetu! Chini ya utawala wa Ufalme, Mungu “atafuta kila chozi” katika macho ya wanadamu. Bila shaka hiyo haina maana kwamba vifereji vya machozi havitatoa tena umajimaji wake wa asili​—jambo ambalo linaufaidi mwili. Wala machozi yanayotokana na furaha hayataondolewa, kwa kuwa dunia itajaa furaha.

Kilio na maombolezo yanayoletwa na sababu mbalimbali zenye kutaabisha yataondolewa polepole wakati wa utawala wa miaka 1,000 wa Yesu Kristo. (Ufu. 20:6) Kama matokeo, machozi yanayosababishwa na huzuni yataacha kutiririka katika macho ya kibinadamu. Lakini namna gani kuondolewa kwa maumivu​—jambo ambalo vilevile limeahidiwa?

MAUMIVU AMBAYO YATATOWEKA

Uwezo wa kuona maumivu ya mwilini unaweza kufaidi. Kwa kweli, ni jambo la lazima katika maisha ya kibinadamu. Kwa hiyo, ahadi ya Mungu kwamba maumivu hayatakuwapo tena haingemaanisha kwamba raia za kidunia za utawala wa Ufalme hawataweza tena kuona maumivu yote.

Mahali pake, ahadi hii ya kwamba “maumivu hayatakuwapo tena” yaonyesha kwamba maumivu makali ya mwili, ya moyoni na ya akilini yatatoweka. Maumivu ya namna hiyo yametokezwa na dhambi na kutokamilika. (Rum. 5:12; 8:21, 22) Ni kwa namna gani “hayatakuwapo tena”? Katika maana ya kwamba matokeo yake yataondolewa.

VYANZO VYA MAUMIVU VYAONDOLEWA

Ebu fikiria baadhi tu ya baraka zitakazofurahiwa na wanadamu chini ya utawala wa Ufalme. Pengine wewe waweza kujiwazia ukiwa kati ya umati utakaofurahia bila shaka ulimwengu huo usio na maumivu ulioko mbele yetu. Ingekuwaje kuishi duniani baada ya vyanzo vifuatavyo vya maumivu kuondolewa?

Misiba haitakuwapo tena, na pamoja nayo maumivu ya moyoni yanayotokezwa nayo. Umaskini​—ambao bila shaka unaonyesha kuwapo kwa msiba katika visa vingi—​hautakuwapo tena. Twawezaje kuwa na uhakika? Basi, Mungu Mwenye Nguvu Zote, ambaye ndiye mwenyeji wa dhahabu na fedha zote za dunia, anaweza kushindwa kuuondoa umaskini? (Hag. 2:8) Pasipo shaka, Yehova Bwana Mwenye Enzi Kuu anaweza kuondoa naye ataondoa chanzo hicho cha maumivu.

Chini ya utawala wa Ufalme njaa pamoja na ukosefu wa chakula kinachofaa, mambo ambayo huleta maumivu yataondolewa. “Kama ningekuwa na njaa,” asema Yehova, “singekuambia, maana ulimwengu ni wangu, navyo viujazavyo.” (Zab. 50:12) Tena, Neno la Mungu latuhakikishia hivi: “[Kutakuwapo] wingi wa nafaka katika ardhi juu ya milima.” (Zab. 72:16) Naye bila shaka Mfanyiza wanadamu aweza kuhakikisha naye atahakikisha kwamba watu wamegawiwa chakula kingi cha dunia bila choyo, jambo hilo likimaliza kabisa maumivu yanayoletwa na njaa.

Uonevu, chanzo kingine cha maumivu ya akilini na ya moyoni, vilevile kitaondolewa. Twahakikishiwa hilo katika maneno ambayo yatatimizwa kabisa chini ya utawala wa Yesu Kristo: “Kwa maana atamwokoa mhitaji aliapo, na mtu aliyeonewa iwapo hana msaidizi. Atamhurumia aliye dhaifu na maskini, nafsi za wahitaji ataziokoa. Atawakomboa nafsi zao na kuonewa na udhalimu, na damu yao ina thamani machoni pake.” (Zab. 72:12-14) Je! kwaweza kuwa na shaka yo yote kwamba wakati huo maumivu yaletwayo na uonevu yatakuwa jambo la zamani?

Ugonjwa, ambao vilevile ni chanzo kingine cha maumivu ya akilini na ya moyoni hautaharibu hata kidogo utulivu na furaha ya jamaa zenye kumwogopa chini ya utawala wa Ufalme. Yehova Mungu ana uwezo wa kuondoa magonjwa. (Kut. 15:26; 23:25; Kum. 7:15) Nabii wake Isaya aliandika juu ya wakati ambapo “hapana mwenyeji atakayesema, Mimi mgonjwa.” (Isa. 33:24) Kuondolewa kwa maumivu yote ya mwilini, ya akilini na ya moyoni hakutakuwa tatizo lisiloweza kushindwa na Tabibu wa Kimungu.

Kifo​—adui mkubwa anayeletea wanadamu maumivu—​‘hakitakuwapo tena’ wakati mapenzi ya Mungu yatakapofanywa kabisa mbinguni na duniani. (1 Kor. 15:26; Ufu. 21:4; Mt. 6:9, 10) Bila shaka, maombolezo na kilio yatakuwa mambo yasiyofaa kuwapo wakati ufufuo wenye furaha utakapochukua mahali pa mazishi yenye huzuni na wakati ‘mauti na Hadeze zitakapotoa wafu waliomo ndani yazo.’​—Yohana 5:28, 29; Ufu. 20:13, ZSB.

WAWEZA KUWA WAKO​—UKIUTAKA

Ndiyo, ulimwengu usio na maumivu unakuja. Waweza kuwa wako kwa kuwa waweza kuwa na tumaini kama hilo. Kutokuwapo kwa maumivu yanayoletwa na misiba, uonevu, magonjwa na kifo itakuwa baraka moja kati ya baraka nyingi zitakazofurahiwa na wanadamu watiifu na wenye kumwogopa Mungu.

Je! watu wanaoishi sasa waweza kuwa na tumaini hilo wakiwa na uhakika kabisa? Ndiyo, kwa kuwa ulimwengu usio na maumivu umeahidiwa na Yeye ambaye peke yake aweza kuuleta​—Yehova, ‘Aliye juu, juu ya nchi yote.’​—Zab. 83:18.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki