Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w78 9/1 kur. 23-24
  • Maswali Kutoka Kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka Kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
  • Habari Zinazolingana
  • “Mti” Ambao Anguko Lake Lashtua Ulimwengu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
  • Toka Chini ya Mti Huo “Mzuri”!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
  • Shauri la Yehova Dhidi ya Mataifa
    Unabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
  • Kuhuisha Mashahidi Wawili
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
w78 9/1 kur. 23-24

Maswali Kutoka Kwa Wasomaji

● Ni nini kinachomaanishwa na “mji ule mkuu, uitwao kwa jinsi ya roho Sodoma na Misri” unaotajwa katika Ufunuo 11:8?

“Mji ule mkuu” unaotajwa katika Ufunuo 11:8 ni Yerusalemu, na kwa hiyo Ufunuo kwa msingi unataja kile kilichofananishwa na Yerusalemu wa kale.

Sura ya kumi na moja (11) ya kitabu Ufunuo inaonyesha njozi ya mtume Yohana juu ya “mashahidi wawili” wa Mungu. Wanatajwa katikati ya masimulizi juu ya Yehova Mungu akiwa amechukua ‘uwezo wake mkuu na kuanza kutawala kama mfalme.’ Mashahidi wa Yehova wanaelewa kwamba jambo hili lilitukia mwaka wa 1914 W.K! (Ufu. 11:17, 18) Lugha hii ya mfano inayotumiwa katika Ufunuo inasema kwamba mashahidi wawili walishindwa wakauawa, “maiti zao zitakuwa katika njia ya muji ule mukubwa unaoitwa kwa namna ya kiroho Sodoma na Misiri, Tena ni hapa Bwana yetu aliposulibiwa.”​—Ufu. 11:8, ZSB.

Kwa wazi hilo lilimaanisha Yerusalemu, kwa maana Yesu alihukumiwa kuuawa katika Yerusalemu akatundikwa juu ya mti nje ya kuta za mji huo. Wakaaji wa Yerusalemu wakati huo walikuwa na tabia za Sodoma ya kale na vilevile Misri. (Linganisha Isaya 1:10, 21.) Kwa mfano, Wamisri wa kale walitosheka na dini yao ya kipagani (kishenzi) na mazoea na walimkataa Mungu wa kweli siku za Musa katika sikukuu ya Kupitwa ya kwanza. Vivyo hivyo, Wayahudi katika karne ya kwanza W.K. walikataa Yesu “Mwana-Kondoo wa Mungu,” badala yake walishikilia mapokeo yao ya kidini. (Yohana 1:29; Mt. 15:3-9; 23:13-26) Kama vile Mashahidi wa Yehova wamekuwa wakionyesha kwa muda mrefu, sehemu iliyofananishwa na Yerusalemu wa kale ni Jumuiya ya Wakristo. Wengi wa washiriki wake vilevile wanadai kumwabudu Mungu kwa njia iliyo sahihi lakini, kwa ujumla, wakionyesha maoni kama hayo yaliyokuwa na Wayahudi waliomkataa Yesu.

Kulingana na hayo, kitabu “Then Is Finished the Mystery of God” kilichochapwa mwaka 1969, kilisema katika sehemu moja hivi: “Kwa sababu ya uonezi wake wa kidini na kutumikisha watu wa Yehova, Yerusalemu usioaminika ungeweza kuitwa ‘kwa namna ya mfano’ Misri. Kama vile Mwana kondoo wa kwanza wa Kupitwa alivyochinjwa huko Misri siku za nabii Musa, ndivyo na Yesu Kristo, kama Mwana-Kondoo wa Kupitwa aliyefananishwa, alivyouawa katika Yerusalemu usioaminika.” Tena kwa habari ya nyakati za kisasa, kitabu hicho kiliongeza kusema kwamba, “Usemi huu ‘mji ule mkuu’ lazima umaanishe Yerusalemu usioaminika wa mfano, yaani, Jumuiya ya Wakristo.”​—Kur. 272, 273.

Lakini ni kwa sababu gani Mnara wa Mlinzi wa Oktoba 1, 1977 ulitaja Ufunuo 11:8 kwa habari ya tengenezo la ulimwenguni pote la kisiasa ambalo liko leo?

Misri wa kale ulikuwa mamlaka ya kisiasa ya pekee wakati huo. Ezekieli sura ya 31 inatoa onyo lililoelekezwa kwa “Farao mfalme wa Misri na jamii ya watu wake.”a Katika kuzungumza habari za Ezekieli sura ya 31, Mnara wa Mlinzi wa Oktoba 1, 1977 kwa kufaa ulielekeza kwa Ufunuo 11:8. Ulifanya hivyo kusudi uonyeshe kwamba inapatana na Maandiko kuipa “Misri” maana ya kiroho. Katika utimizo wa kisasa wa mfano wa Ezekieli sura ya 31, si nchi halisi ya Misri inayomaanishwa. Badala yake, inatumiwa juu ya taratibu ya mambo ya kisiasa ya ulimwenguni pote katika siku zetu. Namna gani hivyo? Misri ya kale ilikuwa mamlaka ya kijeshi yenye kutokeza, ambayo kama mti mkubwa, ilijaribu kutandaza uwezo wake wa kuvutia ulimwenguni pote ili kwamba utie wanadamu wote chini yake. Kwa kulinganisha, leo kuna tengenezo la kisiasa ulimwenguni pote linaloweza kufananishwa na mwerezi katika mlima wa Lebanoni, ambao chini yake mataifa mengi wanakimbilia.

Kwa hiyo ingawa habari inayozunguka Ufunuo 11:8 inaonyesha kwamba utimizo wa siku zetu sana sana unafanyika katika Jumuiya ya Wakristo, mstari huu unaweza kutumiwa kwa kufaa kuonyesha kwamba inafaa kutazamia matumizi ya kiroho siku zetu juu ya “Misri” inayotajwa katika Ezekieli sura ya 31.

● Ni kiasi gani cha chakula kilichobaki baada ya Yesu kulisha maelfu kwa mwujiza?

Nyakati mbili Yesu Kristo alilisha maelfu ya watu kwa mwujiza. Wakati mmoja, kwa mikate mitano na samaki wawili, alitoa chakula kwa wanaume elfu tano, bila kuhesabu wanawake na watoto. Baada ya kila mtu kushiba, vikapu kumi na viwili (12) vilijazwa vipande vilivyosalia. (Mt. 14:19-21) Neno la Kigiriki cha asili la “vikapu” linalotumiwa katika habari hii lilitumiwa katika kipimo cha Waboeoti cha kama galoni mbili (10 litres). Kwa hiyo, vile vikapu kumi na viwili vya vipande huenda vikawa vilikuwa kipimo cha karibu pishi 40. Kwa habari ya kulisha makutano ya zaidi ya watu elfu nne kwa mikate saba na samaki wachache, kulikuwa na masazo ya vipande vya mikate makanda (vitunga) saba (vikapu vya kuwekea vyakula), yamejaa. (Mt. 15:34-37) Namna hii ya kikapu ilikuwa kubwa zaidi, mara nyingine ikiwa kubwa kiasi cha kutoshea mtu.​—Matendo 9:25.

[Maelezo ya Chini]

a Ezekieli 31:3, NW, unasema katika sehemu moja hivi: “Tazama, Mwashuru, mwerezi katika Lebanoni.” Inafaa ionwe kwamba tafsiri nyingine (UV, ZSB, n.k.) hapa zinasomwa hivi: “Tazama Mwashuru alikuwa mwerezi katika Lebanoni . . . ” Hili lilikuwa limefanya lieleweke kwamba “mti” huo mkubwa ulifananisha Ashuru wa kale. Lakini neno hili “alikuwa” halionekani katika maandishi ya Kiebrania ya kale. Na habari inayozunguka neno hilo inaonyesha kwamba onyo hilo lilitolewa kwa Farao na wingi wa watu wake, anayetajwa akifanana na “Mwashuru” na vile vile akifanana na “mwerezi katika Lebanoni.” Kwa wazi basi “Mwashuru” anatajwa tu ili kuonyesha wazo la uwezo mkubwa wa kijeshi, na hivyo ndivyo ilivyokuwa Misri ya kale.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki