Kutumia Ulimi Katika Panama
MSICHANA Mpanama wa miaka 12 aliyepooza tangu kuzaliwa kwake, hangeweza kutumia mikono na miguu yake ambayo imelemaa. Lakini ana akili nzuri sana akaruhusiwa na mama yake ajifunze Biblia na Mashahidi wa Yehova. “Nilishangaa angewezaje kufungua kurasa za Biblia apate andiko la Biblia,” akasema Shahidi aliyekuwa akijifunza na msichana huyo, “lakini haoni shida yo yote. Yeye analala kwa tumbo kitandani, vitabu vyake vikiwa mbele yake naye anafungua kurasa kwa kutumia ulimi wake kwa njia ya ufundi sana, mara nyingine akipata maandiko hata kabla sijayapata mimi.”