Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w80 2/15 kur. 22-24
  • Mahubiri ya Mlimani—‘Zawadi Zenu za Rehema Na Zitolewe Sirini’

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mahubiri ya Mlimani—‘Zawadi Zenu za Rehema Na Zitolewe Sirini’
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
  • Habari Zinazolingana
  • Acha Maneno ya Yesu Yafinyange Mtazamo Wako
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Endelea Kuutafuta Ufalme na Uadilifu wa Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Mahubiri ya Mlimani—“Ufungapo, Jipake Mafuta Kichwani”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
  • Mahubiri ya Mlimani—“Msalipo”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
w80 2/15 kur. 22-24

Mahubiri ya Mlimani​—‘Zawadi Zenu za Rehema Na Zitolewe Sirini’

KUFUATA onyo lake la upole juu ya mtu kuwatendea wanadamu wenzake ifaavyo, Yesu alitoa shauri juu ya namna ya ibada inayokubalika kwa Mungu. Alianza sehemu hii ya Mahubiri yake ya Mlimani kwa kusema hivi: “Angalieni msifanye wema wenu machoni pa watu, kusudi mtazamwe na wao.”​—Mt. 6:1a.

Katika habari hii, “wema” maana yake ni mwenendo unaopatana na kanuni ya Mungu ya yaliyo haki. (Linganisha Mathayo 5:6, 20) Mungu ataka kuona watu wakionyesha haki katika sehemu zote za maisha. Hii inapasa kutia ndani matendo ya mtu anapokuwa peke yake pamoja na uhusiano wake na Mungu na wanadamu wenzake.

Maneno haya ya Yesu hayamaanishi kwamba matendo ya kimungu yasifanywe kamwe mbele ya wengine, kwa kuwa hiyo ingekuwa kinyume cha shauri lake la mapema, kwamba wasikilizaji wake ‘waache taa zao ziangaze mbele ya wanadamu.’ (Mt. 5:14-16) Walakini kusudi halipaswi kamwe kuwa ili ‘watazamwe nao.’ Mtu hapaswi kujaribu kujionyesha kama kwamba alikuwa jukwaani la jumba la michezo.

Yesu alitangaza hivi kwa wote ambao wangekuwa na maelekeo ya kujionyesha: “Hampati thawabu kwa Baba yenu aliye mbinguni.” (Mt. 6:1b) Hiyo ‘thawabu kutoka mbinguni,’ ambayo inatia ndani uhusiano wa kirafiki na Mungu pamoja na baraka za milele za utawala wake wa Ufalme, si ya watu mmoja mmoja ambao kusudi lao katika kumwabudu Mungu ni kuvuta fikira juu yao wenyewe.

Kwa Wayahudi katika karne ya kwanza W.K., sehemu tatu kuu za ibada zilikuwa kuwapa msaada maskini, kusali na kufunga kula. Kuhusu jambo la kwanza la haya, Yesu alisema hivi: “Basi wewe utoapo [Zawadi za rehema], usipige panda mbele yako, kama wanafiki wafanyavyo katika masinagogi na njiani, ili watukuzwe na watu:”​—Mt. 6:2a.

Usemi ‘zawadi za rehema’ wamaanisha michango ya rehema ya kuwasaidia walio maskini. Mara nyingi Maandiko ya Kiebrania hukazia umuhimu wa kuwasaidia watu mmoja mmoja wenye uhitaji. (Mit. 14:21, 28:27; Isa. 58:6, 7) Katika nyakati za baadaye, kila mtaa wa Kiyahudi ulikuwa na akiba ya fedha kwa ajili ya watu maskini ambayo ilikusanywa na kugawanywa katika masinagogi kila juma. Kila mkaaji wa mtaa huo alitazamiwa achange kulingana na uwezo wake. Watu wengi mmoja mmoja walifanya zaidi ya wajibu huu na kutoa msaada wa ziada kwa watu wenye uhitaji kwa michango ya hiari. Jambo la kupendeza ni kwamba, Yesu na mitume wake walikuwa na akiba ya fedha ya shirika kwa ajili ya maskini.​—Yohana 12:5-8; 13:29.

Hata hivyo, kwa habari ya kuwapa maskini msaada, Yesu aliwaonya wanafunzi wake kwa upole hivi: “Usipige panda mbele yako.” Maana yake, ‘Usitangazie watu wote misaada ya hiari unayowatolea watu maskini.’ Hilo lilikuwa zoea la kawaida la Mafarisayo, ambayo Yesu aliwaita “wanafiki,” yaani, watu waliokuwa wakijifanya kuwa vile wasivyokuwa. Kwa habari ya kutangaza michango ya rehema “katika masinagogi na njiani,” twasoma katika kitabu Theological Dictionary of the New Testament:

Maandishi ya [kirabi] yanatoa ushuhuda mwingi juu ya kujionyesha kwa Mafarisayo kuwa wenye haki. . . . Ijapokuwa njia ya kijamii ya kusaidia maskini ilitolewa kwa kukadiria, misaada ya ziada ya kusaidia maskini ilitegemea zawadi zilizotolewa kwa hiari. Hizi zilitangaziwa kundi katika masinagogi na wakati wa ibada za kufunga kula katika barabara zilizo wazi.” (Kitabu cha III, uku. 974) “Katika masinagogi, [sana sana] nyakati za kufunga wakati wa uhitaji mkubwa ibada ilifanyiwa mahali palipo wazi mjini . . . , mara nyingi watu mmoja mmoja waliahidi kutoa kiasi fulani kwa ajili ya sanduku la maskini. . . . Vile-vile twaambiwa kwamba waliotoa viasi vikubwa zaida waliheshimiwa kipekee kwa kuruhusiwa waketi pamoja na marabi kwenye ibada.”​—Kitabu VII, uku. 86.

Kuhusu wanafiki hao, Yesu alitangaza hivi: “Amin, nawaambieni, Wamekwisha kupata thawabu yao [kwa ukamili]” (Mt. 6:2b) Vitabu vya mafunjo kutoka katika kame ya kwanza W.K. vyafunua kwamba neno la Kigiriki linalomaanisha ‘wanapata . . . kwa ukamili’ (apékho) mara nyingi lilionekana katika karatasi za malipo na lilionyesha wenyeji kabisa wa kitu au hesabu fulani ya fedha. Katika kitabu chake Bible Students, G. Adolf Deissmann anasema kwamba, kwa sababu ya hili, maneno ya Yesu “yanakuwa na ukali na maana iliyo kinyume yakimaanisha wanaweza kutia sahihi karatasi yao ya malipo ya thawabu yao: Wanapata haki yao ya kupata thawabu, kama kwamba tayari walikuwa wametoa karatasi ya malipo kwa ajili yake.” Sifa za watu na pengine kuketi mbele katika sinagogi pamoja na marabi wenye kujulikana ndiyo thawabu peke yake ambayo wanafiki hao wangepata. Mungu asingewapa cho chote.​—Linganisha Mathayo 23:6.

“Bali wewe” Yesu akawaambia wasikilizaji wake, “utoapo [zawadi za rehema], hata mkono wako wa kushoto usijue ufanyalo mkono wako wa kuume.” (Mt. 6:3) Mkono wa kuume na mkono wa kushoto ndivyo viungo vinavyokaribiana zaidi kati ya viungo vya mwili kwa sababu ya kuwa kila upande wa kiwiliwili cha mwili na kwa kawaida inashirikiana. Mara kwa mara mkono mmoja waweza kutenda pasipo kutegemea ule mwingine. Basi, ‘kutoruhusu mkono wa kushoto ujue unalofanya mkono wa kuume,’ kungemaanisha kwamba mtu asingetangaza matendo yake ya rehema, hata kwa wale walio karibu naye kama vile mkono wa kushoto ulivyo karibu na wa kuume.

Kulingana na Yesu, tangazo la kujivuna la kutoa misaada kwa watu maskini lapaswa kuepukwa kusudi “[zawadi yako ya rehema] iwe kwa siri; na Baba yako aonaye sirini atakujazi. (Mt. 6:4) Kwa kuwa anakaa mbinguni na haonekani kwa macho ya kibinadamu, Muumba anaendelea kuwa “sirini” kwa habari ya wanadamu. (Yohana 1:18; 1 Yohana 4:20) ‘Kulipwa’ na yeye “aonaye sirini” kunatia ndani Mungu kuleta waabudu wanyenyekevu kwenye uhusiano wa kirafiki pamoja naye, kuwasamehe dhambi zao na kuwapa uzima wa milele chini ya hali kamilifu. (Mit. 3:32; Efe. 1:7; Ufu. 21;1-5) Lo! namna hilo lilivyo jambo la kupendelewa zaidi kuliko kuheshimiwa na kusifiwa tu na wanadamu wenzetu!

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki