Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w79 3/15 kur. 17-19
  • Elimu Inayoridhisha

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Elimu Inayoridhisha
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Je! ni Ndoto Tu?
  • Elimu Iliyo Kuu Zaidi
  • Faida za Sasa
  • Mashahidi wa Yehova Wana Maoni Gani Kuhusu Elimu?
    Maswali Yanayoulizwa Mara Nyingi Kuhusu Mashahidi wa Yehova
  • Elimu—Gharama Yake? Faida Yake
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
  • Elimu—Itumie Kumsifu Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
  • Je, Biblia Inapinga Elimu?
    Amkeni!—1998
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
w79 3/15 kur. 17-19

Elimu Inayoridhisha

UKITOLEWA nafasi ya kujifurahisha furaha ya kweli, afya njema pamoja na usalama wa kweli, je! ungeichukua nafasi hiyo? Bila shaka ungefanya hivyo. Walakini, huenda ukasema: ‘Hivyo ni vizuri sana. Lakini je! kweli kuna nafasi kama hiyo?’ Ndiyo, iko. Faida hizi zaweza kupatikana kutokana na elimu inayo-tolewa kwa watu wote bure duniani pote.

Leo inakubaliwa mahali pote kwamba elimu ina thamani nyingi. Watu wengi wanalinganisha elimu na ufanisi, fahari na fedha nyingi. Kwa hiyo wanakuwa na nia ya kutumia fedha nyingi na wakati mwingi ili wapate elimu bora. Kwa mfano, katika nchi za Asia wazazi wengi wanafanya kazi kwa bidii sana ili waweze kuwatuma watoto wao katika shule za pekee na katika vyuo vikuu. Watoto wenyewe wanajifunza usiku na mchana ili wafaulu mitihani yao, wakiwa na mradi wa kupata elimu bora. Hiyo, nayo, huenda ikawawezesha kupata kazi yenye mshahara mzuri na kusonga mbele katika ulimwengu. Kwa upande mwingine, wengine wa-natafuta elimu ya juu ili wajitayarishe kuwatumikia zaidi wanadamu wenzao.

Ni kweli, wale wanaopata elimu nzuri ya kilimwengu huenda wakapata kadiri fulani ya uradhi wanapofikia miradi yao maishani. Walakini, uradhi wa namna hiyo huwa wa muda mfupi tu. Wanadamu wote, wawe na elimu bora au hapana, wanapatwa na mambo yale yale, kuzeeka na kufa. Licha ya hayo, ni mara ngapi tumeona wanaume na wanawake ambao, maisha yao hukatizwa na ugonjwa au misiba ya barabarani, mara tu baada ya kupata elimu bora!

Hakika, bila uzima kila kitu kinakuwa bure, kwa vile mtu hawezi kujifurahisha cho chote anapokufa. Yesu Kristo, mwalimu mkuu zaidi aliyepata kutembea hapa duniani, alivuta fikira zetu kwenye uhakika huu usioweza kukanushwa, akiuliza: “Kwani atafaidiwa nini mtu akiupata ulimwengu wote, na kupata hasara ya nafsi yake?”​—⁠Mt. 16:26.

Huenda wengine wakasema: ‘Kwa kuwa hakuna anayeweza kuepuka kifo, basi afadhali mtu akubali uhakika huu wa kifo aridhike na kujifurahisha maisha wakati angali hai.’ Walakini, si lazima uridhike na kujifurahisha maisha kwa miaka michache tu. Kwa kweli, nafasi iko wazi kwako ujifurahishe uzima milele chini ya hali nzuri na zenye kuridhisha zaidi.

Je! ni Ndoto Tu?

Je! hii ni ndoto tu, au ahadi ya bure tu isiyoweza kutimizwa? Hapana, kwa sababu Yesu Kristo, mnenaji mkuu zaidi wa Muumba, alituhakikishia kwamba kuna uwezekano wa kupata uzima wa milele, ikiwa mtu atapata elimu inayofaa. Elimu ya namna gani? Maneno ya sala ya Yesu kwa Baba yake Yehova Mungu yalifunua hili: “Na uzima wa milele ndio huu, Wakujue wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na Yesu Kristo uliyemtuma.”​—⁠Yohana 17:3.

Kama vile tunavyoweza kujifunza kutokana na maneno ya Yesu, ni mapenzi ya Mungu kwamba wanadamu wapate kujifurahisha zawadi ya uzima wa milele. Kwa kweli, Mungu alipoumba mwanadamu mwanzoni, Yeye alimwekea mbele yake taraja la kuishi milele duniani, ikiwa angetimiza takwa jepesi la kumpenda na kumtii Muumba wake. (Mwa. 2:​16, 17) Vilevile Biblia inafunua kwamba mwanadamu aliumbwa kwa mfano wa Mungu, akapewa sifa njema mbalimbali za Yehova Mungu. Hii ilimweka mwanadamu katika cheo cha pekee sana kati ya viumbe vya dunia, kwa kuwa hakuna mnyama ye yote aliyeumbwa kwa mfano wa Mungu.​—⁠Mwa. 1:27.

Kwa kuwa Yehova Mungu ndiye Muumba wa wanadamu, yeye anajua vizuri zaidi namna ya kutosheleza mahitaji ya wanadamu, ya kiroho na ya kimwili (Zab. 145:16) Lo! namna ametoa kwa wingi sana mahitaji ya kimwili kwa wanadamu! Je! wewe unaweza kuweka orodha ya namna zote mbalimbali za vyakula na vinywaji vipatikanavyo duniani? idadi hiyo ni kubwa ajabu! Kwa hiyo, je! si jambo la akili kutazamia kwamba Muumba mkarimu na mwenye upendo angetoa vilevile mipango ya kutosha ya kutosheleza mahitaji ya kiroho ya wanadamu?​—⁠Mt. 4:4.

Elimu Iliyo Kuu Zaidi

Ili mtu apate furaha ya kweli na uradhi, anahitaji kumjua Muumba wake, aongozwe na Mungu na kuwa na uhusiano (urafiki) wa karibu pamoja naye. Kwa hiyo, kupata maarifa ya makusudi ya kimungu ndiyo elimu iliyo kuu zaidi ambayo mtu angeweza kupata. Imeonekana kwamba watoto wa nyumba zilizofarakana, ambao wamekosa upendo wa wazazi wao pamoja na uongozi, mara nyingi wanakuwa hawana furaha na wanakuwa na maelekeo mabaya. Mwanadamu ye yote asiyemjua Mungu na ambaye haongozwi naye yuko katika hali inaolingana na hiyo. Maisha ya watu kama hao yanakosa kusudi la kweli na huwa hayana maana. Mara nyingi watu hawa wanaona maisha kuwa ya bure, ambayo mara nyingi yanakatizwa na mauti. Wakikosa uongozi wa kweli, mara nyingi huwa hawajui namna ya kushindana na magumu mengi yanayotokea maishani.

Kwa kufaa Biblia inayaeleza matokeo mabaya ya mwanadamu kutenganishwa na Mungu, ikisema: “Akili zao zimetiwa giza, nao wamefarikishwa na uzima wa Mungu, kwa sababu ya ujinga uliomo ndani yao, kwa sababu ya ugumu wa mioyo yao; ambao wakiisha kufa ganzi wanajitia katika mambo ya ufisadi wapate kufanyiza kila namna ya uchafu kwa kutamani.”​—⁠Efe. 4:​18, 19.

Tunaweza kuamua kwa kufaa kwamba adili baya na uvunjaji wa sheria unaoenea pote ulimwenguni leo ni kwa sababu ya mwanadamu kutomjua Mungu na kwa kutoelimishwa katika njia Zake. Ni kweli, watu milioni nyingi hudai kwamba wanamwabudu Mungu wa Biblia. Lakini je! wao wanamjua Mungu katika maana ya kujua na kufuata kanuni zake za haki? Tukiamua kwa njia ambayo katika hiyo watu wanajiongoza wenyewe, hali yao inalingana na ile ya Waisraeli wa kale, ambao pia walidai kwamba walikuwa wakimwabudu Mungu. Walakini, kupitia kwa nabii Hosea, Mungu aliwaambia hivi: “Lisikieni neno la [Yehova], enyi wana wa Israeli; kwa maana [Yehova] ana mateto nao wakaao katika nchi, kwa sababu hapana kweli, wala fadhili, wala kumjua Mungu katika nchi. Hapana neno ila kuapa kwa uongo, na kuvunja ahadi, na kuua, na kuiba, na kuzini; huruka mpaka, na damu hugusana na damu.” (Hos. 4:​1, 2) Hivyo inaonekana kwamba kumjua Mungu kunamaanisha zaidi kuliko kudai tu kumwamini. Kunamaanisha pia kumtii na kufuata njia zake za haki.

Faida za Sasa

Ili mtu afuate njia za Mungu, lazima kwanza aelimishwe katika hizo. Kama vile tumekwisha ona, maarifa yaliyo sahihi ya Mungu yanaweza kuleta uzima wa milele. Walakini, hii haina maana kwamba faida za mwendo kama huo zitafurahiwa tu katika wakati ujao. Hapana! Mwendo wa utawa unaleta faida za sasa, kwa kuwa “utauwa hufaa kwa mambo yote; yaani, unayo ahadi ya uzima wa sasa, na ya ule utakaokuwako.”​—⁠1 Tim. 4:8.

Ijapokuwa milioni zinazozidi kuongezeka za watu ulimwenguni leo wanataabishwa na ndoa zenye kuharibika, uasi wa watoto na upweke, matokeo ya kuishi kulingana na kanuni za Biblia yamekuwa nini? Jamaa nyingi zilizoungana, zenye furaha zisizo na magumu ya ndoa zenye kuharibika, mtengano wa wazazi na watoto pamoja na uvunjaji wa sheria wa watoto! Shauri la Biblia linatuhakikishia kwamba kutumia kanuni za Maandiko kunaweza kuleta maendeleo makubwa sana katika maisha ya nyumbani.

“Inawapasa waume nao kuwapenda wake zao kama miili yao wenyewe,” akasema mtume Paulo. “Ampendaye mkewe hujipenda mwenyewe. Maana hakuna mtu anayeuchukia mwili wake po pote; bali huulisha na kuutunza kama Kristo naye anavyolitendea Kanisa.” Wake, nao, wanashauriwa kwa upendo hivi: “Mke asikose kumstahi mumewe.” Lakini, namna gani watoto? Wanaagizwa ‘kuwatii wazazi wao katika Bwana.’ Sababu gani? Sababu “hii ndiyo haki,” na kwa hiyo inampendeza Yehova. Zaidi ya hayo, kuwaheshimu wazazi kunaambatana na ahadi: “Upate heri, ukae siku nyingi katika dunia.” Sana sana baba ndiye mwenye daraka la kuwapa watoto wake mafundisho ya kiroho, kwa kuwa ameambiwa ‘awalee katika adabu na maonyo ya Bwana.’​—⁠Efe. 5:​28–6:4.

Vilevile kuelimishwa katika njia za Mungu kunawezesha mtu kupata rafiki wengi wenye upendo wanaomhangaikia kikweli. Elimu kama hiyo ambayo msingi wake ni Biblia itamleta katika ushirika na Wakristo wa kweli, wanaojitahidi kwa unyofu kufuata shauri hili: “Lakini mtu akiwa na riziki ya dunia, kisha akamwona ndugu yake ni mhitaji, akamzuia huruma zake, je! upendo wa Mungu wakaaje ndani yake huyo? Watoto wadogo, tusipende kwa neno, wala kwa ulimi, bali kwa tendo na kweli. Na amri hii tumepewa na yeye, ya kwamba yeye ampendaye Mungu, ampende na ndugu yake” pia. (1 Yohana 3:​17, 18; 4:21) Je! wewe hukubali kwamba kushirikiana na rafiki kama hao kutaleta furaha nyingi pamoja na uradhi maishani mwako?

Na zaidi ya yote, wale wanaopata elimu hii yenye kutoa uzima wanaweza kupata amani ya akili ambayo inapatikana tu kwa kuwa na uhusiano (urafiki) wa pekee pamoja na Mungu. Ijapokuwa watu kwa ujumla wanazidi kutaabika na kuwa na wasiwasi juu ya magumu yanayozidi kuongezeka pamoja na wakati ujao usio na matumaini unaouelekea ulimwengu leo, watu wengi kila mahali wanapata faraja kutokana na hakikisho hili la Biblia: “Msijisumbue kwa neno lo lote; bali katika kila neno kwa kusali na kuomba, pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane na Mungu. Na amani ya Mungu, ipitayo akili zote, itawahifadhi mioyo yenu na nia zenu katika Kristo Yesu.”​—⁠Flp. 4:​6, 7.

Kwa kuwa Muumba mwenye upendo anawahangaikia wanadamu naye anataka kuona wakifurahi na kuridhika, yeye anatoa leo elimu ya bure duniani pote kupitia kwa mpango wa funzo la Biblia unaoongozwa na mashahidi wake Wakristo katika nchi zaidi ya 200. Ndiyo, Mungu anawakaribisha kwa fadhili watu wote wa ulimwengu. (Isa. 55:​1, 2) Milioni nyingi kuzunguka dunia wamekubali ukaribishaji wake nao wameona kwamba wanaweza kumwunga mkono kwa moyo wote mwandikaji wa zaburi, aliyesihi hivi: “Onjeni mwone ya kuwa [Yehova] yu mwema; heri mtu yule anayemtumaini.” (Zab. 34:8) Je! wewe utatafuta elimu hiyo iletayo faida hizo zinazofaa?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki