Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w80 9/15 kur. 22-23
  • Mahubiri ya Mlimani—“Ingieni kwa Kupitia Mlango Ulio Mwembamba”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mahubiri ya Mlimani—“Ingieni kwa Kupitia Mlango Ulio Mwembamba”
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
  • Habari Zinazolingana
  • Je, Dini Zote Ni Nzuri?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Iweni Watendaji wa Neno, Si Wasikiaji Tu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • “Njia Iliyo Pana na Rahisi”
    Amkeni!—1990
  • Barabara Nyembamba Iendayo Kwenye Uhuru
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
w80 9/15 kur. 22-23

Mahubiri ya Mlimani​—“Ingieni kwa Kupitia Mlango Ulio Mwembamba”

BAADA ya kuwatia moyo wasikilizaji wake waombe kwa bidii wapate msaada katika kufanya mapenzi ya Mungu, Yesu alisema hivi: “Ingieni kwa kupitia mlango ulio mwembamba; maana mlango ni mpana, na njia ni pana iendayo upotevuni, nao ni wengi waingiao kwa mlango huo. Bali mlango ni mwembamba, na njia imesonga iendayo uzimani, nao waionao ni wachache.”​—Mt. 7:13, 14.

Katika nyakati za kale, njia za kuingia mijini zilipitia kwenye mlango, au malango. Mara nyingi Maandiko yanafananisha mwendo wa maisha wanaofuata watu na njia au barabara. (Mit. 4:18, 19) Kulingana na alivyosema Mwana wa Mungu, njia iongozayo “upotevuni,” au mauti kwa kukosa kibali ya kimungu, ni “pana.” Inawaruhusu watu waishi kama wanavyopenda, pasipo kufanya mabadiliko ili wapatane na kanuni za mwenendo za Kibiblia. “Wengi” wamechagua njia hiyo ya kuishi ‘maisha rahisi.’

Kwa upande mwingine, Biblia inaulinganisha ufalme wa Mungu wa Kimasihi na mji, ambao waingiwa kwa kupitia kwenye mlango “mwembamba” na njia ambayo “imesonga.” (Angalia Waebrania 11:10; 13:14.) Watu walio katika hii “njia iendayo uzimani [wa milele]” lazima wazoeze mioyo yao isitawishe makusudi yanayofaa. Lazima wajiweze katika sehemu zote zinazohusu mwenendo wa kibinadamu; na katika nyakati nyingine, “Njia” ya ibada ya kweli inawahitaji wavumilie mateso yenye jeuri. (Matendo 9:2; 19:9, 23; 22:4) Kwa kuwa watu walio wengi wanapendelea kuishi pasipo kujitahidi kujizuia katika kujinyima, wao hawatafuti njia ya maisha inayompendeza Mungu. Kwa hiyo, ‘wachache ndio wauonao’ huo mlango mwembamba na njia ambayo imesonga iongozayo kwenye uzima.​—Linganisha Mathayo 7:8; Luka 13:24.

Kufuata hayo, Yesu aliwapa onyo wale watu ambao wangetaka kuendelea kukaa katika hiyo njia iongozayo uzimani: “Jihadharini na manabii wa uongo, watu wanaowajia wamevaa mavazi ya kondoo, walakini kwa ndani ni mbwa-mwitu wakali.”​—Mt. 7:15.

Kwa “manabii wa uongo,” Yesu alikuwa akimaanisha waalimu wa uongo wa kidini waliodai kwa uongo kumwakilisha Mungu. Wadanganyaji hao wangejitokeza wakiwa “wamevaa mavazi ya kondoo.” Kwa kujionyesha kwa unafiki kuwa waungwana, wapole na sifa nyinginezo za watu wa namna ya kondoo, wangejaribu kujionyesha kuwa sehemu ya “kundi” la waabudu wa Mungu. (Angalia Zaburi 78:52; 80:1; 100:3.) Walakini kwa ndani, manabii hao wa uongo wangekuwa “mbwa-mwitu wakali,” yaani, wenye kutamani sana, wenye kunyakua na wenye juhudi sana katika kuwatumia wengine watosheleze tamaa zao wenyewe.

Mwana wa Mungu alisema kwamba hawa manabii wa uongo ‘wangewajia,’ yaani, kutoka nje ya kundi ambalo yeye, akiwa “mchungaji mwema,” angekusanya pamoja. (Yohana 10:11) Badala ya wao kuwa hatari ya wakati ujao uliokuwa mbali, wadanganyaji hao hata wakati huo walikuwapo hapo. Kwa wazi sana sana Yesu alikuwa akiwafikiria Mafarisayo, ambao kwa uongo walidai kuwa wanenaji wa Mungu. Walikuwa “wameketi katika kiti cha Musa,” wakidai kuwa wafasiri halali wa sheria ya kimungu. (Mt. 23:2) Walakini Mafarisayo walikuwa wanafiki ambao kwa hakika walikuwa wakiwazuia watu wasiuone ule mlango mwembamba na ile njia ambayo imesonga iongozayo uzimani. (Mt. 23:13-15; Luka 6:39) Na kwa habari ya “mavazi ya kondoo” yenye kudanganya, maneno ya Yesu aliyoyasema katika pindi fulani baadaye ni yenye kufahamisha:

“Ole wenu, waandishi na Mafarisayo, wanafiki! kwa kuwa mmefanana na makaburi yaliyopakwa chokaa, nayo kwa nje yaonekana kuwa mazuri, bali ndani yamejaa mifupa ya wafu, na uchafu wote. Vivyo hivyo ninyi nanyi, kwa nje mwaonekana na watu kuwa wenye haki, bali ndani mmejaa unafiki na maasi.”a—Mt. 23:27, 28.

Mtu awezaje kuwatambua hao ‘mbwa-mwitu wenye kuvalia mavazi ya kondoo’? Yesu alitoa uongozi wa msingi pamoja na mfano: “Mtawatambua kwa matunda yao. Je! watu huchuma zabibu katika miiba, au tini katika mibaruti? Vivyo kila mti mwema huzaa matunda mazuri; na mti mwovu huzaa matunda mabaya. Mti mwema hauwezi kuzaa matunda mabaya, wala mti mwovu kuzaa matunda mazuri. Kila mti usiozaa tunda zuri hukatwa ukatupwa motoni.”​—Mt. 7:16-19.

Kila mti wenye kuzaa matunda au mmea huzaa matunda ya namna yake. Si miti yote inayozaa matunda yanayoweza kuliwa na wanadamu. Ingekuwa kazi bure kutafuta matunda yanayoweza kuliwa kama vile zabibu au tini katika miiba na mibaruti. Matunda yanayofaa kuliwa na wanadamu lazima yatoke kwenye mti wenye afya na tena wa namna, inayofaa. Mti ukiendelea kuzaa “matunda mabaya,” ungekuwa wonyesho hakika kwamba mti huo wenyewe umekuwa “mwovu.” Mti mwovu kama huo ‘ungekatwa’ na kutumiwa pamoja na miiba na magugu kuwashia moto.​—Linganisha Zaburi 58:9; Mhubiri 7:6; Isaya 44:14-16; Mathayo 6:30; 13:30.

Wakati wasikilizaji wake walipokuwa bado wakikumbuka mfano huu uliohusu ukulima, Yesu aliirudia kanuni ya msingi: “Ndiposa kwa matunda yao mtawatambua.” (Mt. 7:20) Katika maana ya mfano “matunda” hayo yangetia ndani maneno ambayo manabii hao wa uongo wangenena katika kufundisha. Juu ya hilo, Yesu aliongeza kusema hivi: “Mtu mwema katika hazina njema ya moyo wake hutoa yaliyo mema, na mtu mwovu katika hazina mbovu ya moyo wake hutoa yaliyo maovu; kwa kuwa mtu, kinywa chake hunena yale yaujazayo moyo wake.”​—Luka 6:45.

Matunda yanayofunua hali ya kweli ya manabii wa uongo yangehusu vilevile mwendo wa kawaida wa mwenendo wao. (Linganisha Mathayo 7:21-23.) Mtu hawezi kuficha hali ya kweli ya moyo wake kwa wakati usiojulikana. Mwishowe maneno na matendo yake yatafunua namna yeye alivyo hasa.

[Maelezo ya Chini]

a Kwa habari ya Mafarisayo kama manabii wa uongo, David Hill aandika hivi katika gazeti Biblica (1976, Vol. 57); “Josephus awajua Mafarisayo waliokuwa na [uwezo wa kutabiri] matukio ya wakati ujao nao walitumia kipawa chao kuendeleza siasa (Ant. XVII 41-45), na mahali pengine anazungumza juu ya mtu fulani aitwaye Pollion na mwanafunzi wake Samaias waliotabiri (Ant. XIV 172-176; XV 3, 370). Walakini ulio wa maana hata zaidi ya habari ya Josephus iliyo chache na pengine iliyovurugika ni uhakika wa kwamba Mafarisayo kama kikundi walijiona wenyewe kuwa warithi wa mapokeo makubwa ya kiunabii: walirithi mapokeo hayo kutoka kwa wanaume wa ule Mkusanyiko Mkubwa ambao uliyarithi kutoka kwa nabii wa mwisho wa nasaba ya manabii. Wakiwa wafasiri wenye ujuzi wa Maandiko Mafarisayo walitumia njia iliyokaribia sana katika wakati wao ufunuo uliopelekwa kupitia kwa manabii wa wakati wa mapema. . . . Kwa habari yao, na warithi wao, ingeweza kusemwa kwamba ‘Ikiwa wao si manabii, hata hivyo wao ni wana wa manabii’ (ilisemwa juu ya Hillel [rabi aliyeishi karibu na wakati ule ule mmoja na Yesu]). Linalopatana kabisa na hili ni lile neno la Yesu juu ya Mafarisayo wakijenga makaburi ya manabii na kuyapamba maziara ya wenye haki (Mt. 23:29). Kwa hiyo si Jambo lisilowezekana kwamba Mafarisayo katika siku za Yesu walidai kuwa na cheo na mamlaka (ikiwa hawakudai jina) la nabii.”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki