Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w79 6/1 kur. 12-17
  • Wanaume Wenye Hekima, Akili na Ujuzi wa Kuongoza Watu wa Mungu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Wanaume Wenye Hekima, Akili na Ujuzi wa Kuongoza Watu wa Mungu
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • KUWAPATA WANAUME WANAOSTAHILI LEO
  • WANAUME WENYE UJUZI
  • MAENDELEO KATIKA KUONYESHA HEKIMA NA UFAHAMU
  • “Wakumbukeni Wale Wanaoongoza Kati Yenu”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
  • Uangalizi Wenye Upendo Hujenga
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
  • Wazee Wanaosimamia Vema
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
  • “Mwendelee Kuwachukua Watu wa Namna Hiyo Kuwa Wapendwa Wanaothaminika”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
w79 6/1 kur. 12-17

Wanaume Wenye Hekima, Akili na Ujuzi wa Kuongoza Watu wa Mungu

“Nami nitawapa ninyi wachungaji wanipendezao moyo wangu, watakao walisha kwa maarifa na ufahamu.”​—⁠Yer. 3:15.

1. Ni kitu gani kilichoongoza kwenye tendo la Musa linaloelezwa katika Kumbukumbu la Torati 1:12, 13?

ISRAELI walikuwa katika nyanda za Moabu wakiwa tayari kuvuka Yordani na kuingia nchi ya Kanaani. Kwa faida yao, Musa alirudia kuwasimulia yale aliyowatendea Yehova wakati wa muda wa miaka 40 walipokuwa katika jangwa la Sinai. Sehemu ya kwanza ya kipindi hicho ilikuwa yenye magumu, sana sana kwa Musa, kwa sababu ya maoni mabaya yaliyoenea kati ya taifa hilo. Sasa, Musa aliwakumbusha kwamba, kwa sababu ya kuona kwamba yeye hawezi tena kuendelea kuuchua mzigo wa watu wenye kuteta akiwa peke yake, alikuwa amefuata shauri la Yethro na alikuwa amewaambia: “Jitwalieni watu wenye akili na fahamu, watu wanaojulikana, kwa kadiri ya kabila zenu, nami nitawafanya wawe vichwa juu yenu.”​—Kum. 1:3, 12, 13; Kut. 18:17-26.

2. Ni kwa sababu gani kutumiwa kwa wanaume kama hao katika kushughulika na magumu halikuwa jambo jipya kabisa na lililo tofauti?

2 Katika kuwachagua wanaume hawa, Musa alikuwa akitumia namna inayoelekea kuwa ya zamani zaidi ya uongozi wa jamii. Baraza za wazee zinaonyeshwa kuwa zilikuwa zikitenda kati ya watu wa kale tangu nyakati zilizo za kale sana za historia ya wanadamu. Katika yale yaliyowapata, Waisraeli, wakiwa wazao wa Yakobo, walikuwa wamepata kukutana na baraza za wazee za Misri, Moabu na Midiani. (Mwa. 50:7; Hes. 22:4, 7) Majumbe wa Waarabu vilevile walikuwa wazee wa makabila, kwa kuwa neno la Kiarabu sheikh (linalotafsiriwa jumbe) linamaanisha kwa vyepesi “mzee.” (Mwa. 36:15) Kabla Musa hajawekwa awaongoze watu hao, tayari Israeli walikuwa na wazee kama hao, nao hao ndio Musa alikuwa ameambiwa awaonyeshe ushuhuda wa kuwekwa kwake kwa kimungu. (Kut. 3:16, 18) Hivyo tendo la Musa la baadaye katika Sinai, la kujitwalia usaidizi wa wazee ili wasaidie katika kushughulika na magumu, halikuwa jambo jipya kabisa.

3. (a) Musa Mkuu Zaidi alifanya mpango gani wa kuongoza kundi? (b) Sifa zinalinganaje kwa habari ya wazee waliochaguliwa na Musa na wale wanaotumikia kama wazee Wakristo?

3 Katika wakati wake Mungu uliowekwa, kundi la Kikristo liliundwa likiwa la watu wa kiroho, na ambalo lilienea duniani pote. Mwana wa Mungu, akiwa ndiye Musa Mkuu Zaidi, alifanya mpango utolewe kupitia kwa baraza za wazee za kundi. Inapendeza kuangalia sifa ambazo Musa alitaka kuona katika wazee Waisraeli aliogawia kazi yenye madaraka na kulinganisha sifa hizo na zile zinazotakiwa katika wazee Wakristo. Ulinganifu unaonekana wazi katika ordha inayofuata:

4, Baraza za wazee Waisraeli zilitimiza daraka gani katika Nchi ya Ahadi, nao wazee Wakristo wanatimiza daraka gani?

4 Baada ya Israeli kusimamishwa katika Nchi ya Ahadi, wakiishi mijini na vijijini, vikundi mbalimbali vya jamii viliongozwa na kusaidiwa na baraza za wazee. (Yos. 20:4; Amu. 8:14, 16; 1 Sam. 16:4) Walipaswa watoe shauri lenye hekima, wasaidie kunapokuwa na magumu, walinde watu na uasi wa dini na katika njia hiyo wasaidie kuleta amani, utaratibu na afya kiroho katika vikundi vyao vya jamii. Nyakati nyingine walipaswa kutumikia kama halmashauri ya hukumu katika kuamua mabishano au katika kukilinda kikundi cha jamii. (Kum. 16:18-20; 19:12; Rut. 4:1-11) Walipaswa kuwa chanzo cha faraja na nguvu katika nyakati za shida. (Isa. 32:​1, 2) Lakini hawakuwa wasimamizi wa wenyeji wenzao wala hawakuruhusiwa au kuwa na daraka la kuishi maisha ya kipekee ya wengine. Katika kuchukua madaraka mazito, wazee Wakristo wanatumikia katika njia zinazolingana na hizo. (Linganisha Matendo 20:28-35; 1 Wakorintho 3:4, 5, 21-23; 2 Wakorintho 1:24.) Kuongezea hayo yote, kundi la Kikristo limeagizwa kuhubiri habari njema za ufalme wa Mungu kwa watu wote.

KUWAPATA WANAUME WANAOSTAHILI LEO

5. Ni jambo gani linaloweza kusaidia leo katika kufanya uchaguzi wa wazee wenye hekima?

5 Kukumbuka historia ya nyakati zilizopita ya mpango wa wazee kunaweza kutusaidia tutumie uamuzi mzuri katika kuchagua wazee leo. Tunaweza kuona kundi moja moja kama kwamba lilikuwa kijiji kidogo katika Israeli. Ulizo laweza kuulizwa hivi: Kama ingekuwa hivyo, ni wanaume gani katika kundi hilo ambao wangetumikia vizuri kama wazee wa kijiji, wakiwa na uwezo wa kutoa uongozi wa hekima na wenye kufaa, wanaojionyesha kuwa wenye akili, wenye usawa na wenye kufanya uamuzi mzuri?

6. Vilevile mfano wa jamaa unawezaje kusaidia katika kufikiria sifa za wanaume wanaotumikia kama wazee?

6 Kundi la watumishi wa Mungu ulimwenguni pote linaitwa “nyumba ya Mungu” (“jamaa ya Mungu,” The Jerusalem Bible) katika 1 Timotheo 3:15. Kwa hiyo, vilevile tunaweza kuona kundi moja moja kama jamaa kubwa. Katika jamaa, ikiwa kichwa cha jamaa hayupo yeye mwenyewe, washiriki wa jamaa huwatazamia wana walio wakubwa wawakilishe na kutegemeza kanuni na maagizo ya kichwa cha jamaa. Hivyo, tunaweza kuuliza hivi: Ni akina nani katika “nyumba” ya waaminio walio kama ndugu wakubwa katika jamaa ambao washiriki wa jamaa wangewaendea wapate mashauri yanayofaa na usaidizi wa akili?​—Linganisha 1 Timotheo 5:1, 2.

7. (a) Kwa kawaida ni jambo gani litaonekana kuwa kweli kati ya wale wanaoonekana kustahili kuwa wazee? (b) Je! kuwekwa kuwa mzee ndiko kunakompa mwanamume sifa za kuwa mzee, nako kunatimiza jambo gani?

7 Kwa kweli, mara nyingi mwanamume anayependekezwa atumikie kama mzee kundini anapaswa kuwa yule ambaye washiriki wa kundi wamekwisha kumwona akiwa kama ‘ndugu mkubwa,’ katika maana ya kwamba wamekwisha mheshimu na kumtumainia kuwa mtu anayeonyesha ufahamu, usawa, na uamuzi mzuri. Kwa kweli hakuna mtu anayeweza “kufanya” mwingine kuwa mzee, lakini mwenyewe lazima awe mzee kwa kukua kiroho, kufanya maendeleo na kupata ujuzi. (Mit. 1:2-5; 4:7-9; Yak. 3:1, 13) Mwanamume kama huyo anapochaguliwa atumikie katika cheo hicho, kuwekwa kwake katika cheo hicho, huwa hasa ni kukubaliwa na kutambuliwa kwa sifa za mzee zinazotamanika ambazo tayari amekwisha onyesha. Katika Israeli wa kale, sawa na nchi nyingine, ndivyo ilivyokuwa kwamba wakati mwanamume alipoonwa na baraza ya wazee ya mahali pao kuwa anaonyesha sifa za hekima ya kimungu, uamuzi mzuri na akili alialikwa awe mshiriki wa baraza hiyo na kushiriki katika mazungumzo yao na katika kufanya maamuzi.​—1 Tim. 5:22, 25.

8. Kwa kutumikia kama mtumishi wa huduma kwa uaminifu kwa muda fulani, mtu anaweza kujipatia nini?

8 Kwa habari ya “watumishi wa huduma,” mtume anaandika kwamba “wanaume wanaohudumu katika adabu nzuri wanajipatia wenyewe sifa nzuri na uhuru mkubwa wa kusema katika imani kuhusiana na Kristo Yesu.” (1 Tim. 3:12, 13, NW) Hakuna mwanamume anayepaswa kufikiri kwamba hii yamaanisha kwamba, kwa kufanya kazi tu katika mgawo fulani, anaweza “kujipatia” haki ya kutumikia kama mzee katika kundi la Mungu. Kile anachoweza kujipatia kweli kweli ni heshima na kuthaminiwa na ndugu zake kwa ajili ya utumishi wake wenye bidii na wa uaminifu, pamoja na kuwa na tumaini kwa Mungu ambalo humwezesha kuwa na “uhuru mkubwa wa kusema.” Hiyo, yenyewe, ni thawabu nzuri sana kwa kutoa utumishi wa uaminifu.

WANAUME WENYE UJUZI

9. (a) Maandiko yanaonyesha nini kwa habari ya umri katika sifa za wazee? (b) Ni ukweli gani unaopaswa kukubajiwa kuhusu ujana juu ya jambo hili?

9 Hakuna kikomo cha umri kinachoonyeshwa waziwazi katika Biblia kwa wale wanaotumikia kama wazee. Neno “mzee” lenyewe linaonyesha uzee, ijapokuwa lazima ikumbukwe kwamba mkazo unatiliwa juu ya sifa za kiroho, wala si za mwili. Umri wenyewe silo jambo la kuamulia; hata hivyo, hata kama vile Musa alivyokubali, bila shaka ujuzi ni sifa yenye thamani kubwa kwa wanaume wanaoangalia madaraka mazito. (Kum. 1:13, NW) Mithali 20:29 yasema: “Fahari ya vijana ni nguvu zao, na uzuri wa wazee ni kichwa chenye mvi.” Ijapokuwa vijana wanaweza kuonyesha nguvu na shauku nyingi, huo si ushuhuda wa kuwa na hekima. Walakini miaka mingi ya kuishi inayoonyeshwa na nywele yenye mvi kwa kawaida hutoa sababu ya kutazamia mtu aliye nayo kuwa na hekima kadiri fulani aliyojipatia, hata kama vile alivyosema Ayubu: “Wazee ndio walio na hekima, na katika kuisha siku nyingi iko fahamu.” (Ayubu 12:12; linganisha mstari wa 20; 32:6, 7.) Kijana anaweza kuwa na nia, hata shauku ya kutumikia na kuonyesha anaweza kutumainiwa katika wakati ujao. Walakini kukosa ujuzi katika maisha kunaweza kuwa kizuizi kikubwa sana kwake anapohitajiwa kuwasaidia wale walio na umri mkubwa kuliko wake katika magumu ya maisha yaliyo mazito. Maneno yake, hata yawe ya unyofu namna gani, hayawezi kutazamiwa yawe na uzito ule ule kama ya yule ambaye ameishi miaka mingi.

10. Je! madaraka aliyopewa Timotheo yanapunguza thamani ya umri na ujuzi kati ya wazee?

10 Inaelekea Timotheo alikuwa na umri wa miaka kati ya 30 na 40 wakati mtume Paulo alipomwandikia maneno haya: “Usikubali mtu ye yote akudharau kwa sababu wewe ni kijana.” (1 Tim. 4:12, Habari Njema kwa Watu Wote) Kwa hiyo, hata akiwa na umri kama huo, watu wengi katika wakati wake bado wangekuwa na maelekeo ya kumwona kuwa “kijana.” Inapaswa kuangaliwa, vilevile, kwamba maendeleo ya Timotheo pamoja na madaraka aliyopewa hayakuwa ya kawaida, yalikuwa ya pekee. Alikuwa amefahamu Maandiko tangu utotoni naye alikuwa amekwisha onyesha maendeleo mazuri mbele ya mtume Paulo kumchagua awe msafiri mwenzake. (2 Tim. 1:5; 3:14, 15; Matendo 16:1-3) Baada ya hapo miaka mingi aliyotumia pamoja na Paulo pamoja na wengine ilimsaidia sana apate ujuzi mwingi sana pamoja na maarifa ambayo ni wachache sana wanaoweza kuwa nayo wakiwa na umri kama wake.

11. Wazee wanawezaje kusaidia wengine wachukue madaraka mazito zaidi?

11 Paulo alimtia moyo Timotheo awasaidie wazee wengine wafaidike kutokana na yale aliyokuwa amejifunza, akisema: “Na mambo yale uliyoyasikia kutoka kwangu mbele ya mashahidi wengi, hayo uwakabidhi watu waaminifu watakaofaa kuwafundisha na wengine.” (2 Tim. 2:2) Katika njia iyo hiyo, wazee wanaweza kusaidia ndugu kundini wakue kiroho, wakijaribu kupitisha kwao ujuzi na maarifa waliyo nayo. Si jambo tu la kuwasaidia wajifunze kazi fulani katika kundi, bali kuwasaidia wakue katika kufanya maamuzi, kupata ufahamu pamoja na uwezo wa kupitisha kwa wengine kanuni zinazofaa za Neno la Mungu. Na kama vile Paulo alivyomchukua Timotheo alipokuwa akitimiza agizo lake la kuwa mtume kwa mataifa na alipokuwa akitumikia kama mchungaji katika kundi la Mungu, vivyo hivyo wazee wanaweza kuwaalika wanaume wengine wanaofanya maendeleo kundini waambatane nao wanapokuwa wakitumikia katika njia kama hizo.​—Mit. 1:4, 5; 13:20.

12. (a) Ujuzi huwa na sehemu gani katika kumstahilisha mtu atumikie kama mzee? (b) Ni kwa sababu gani shauri la Paulo katika 1 Timotheo 3:6 sana sana lilifaa katika Efeso?

12 Kama vile umri, muda mrefu wa kupata ujuzi kama mwanafunzi Mkristo silo jambo peke yake la kuamulia kama mtu atakuwa mzee. Ni jambo mojawapo, umuhimu wake ukiamuliwa angawa kwa kadiri fulani na hali zilizopo. Paulo alimwandikia Timotheo kwamba, katika kuchagua wazee katika kundi la Efeso, alipaswa kuwa mwangalifu asimchague “mwanamume aliyegeuka hivi karibuni, asije labda akajitutumua kwa kiburi.” (1 Tim. 3:6, NW) Ukristo wa kweli ulikuwa umekwisha anzishwa huko Efeso kama miaka 10 hivi kufikia wakati huo na kwa hiyo lingekuwa sana sana jambo lisilofaa kumchagua mwanafunzi aliye mpya zaidi atumikie kati ya wazee wa kundi hilo.

13, 14. (a) Ni mifano gani inayoonyesha kwamba hali zinahusika katika kuamua namna ya kuona kadiri ya ujuzi wa mtu? (b) Hata hivyo ni mambo gani yanayopaswa kufikiriwa zaidi nyakati zote?

13 Akimwandikia Tito katika Krete, kwa wazi Paulo hakuona umuhimu uo huo juu ya onyo hilo la upole na kwa hiyo hakulitia ndani ya maneno yake juu ya kuchaguliwa kwa wazee. Uhakika wa kwamba ibada ya kweli ilikuwa imeanzishwa huko Krete muda mfupi tu uliopita kwa kulinganisha huenda ukawa ulihusiana na hilo. Twaona kwamba katika safari ya kwanza ya umisionari ya Paulo na Barnaba walitangaza “habari njema” katika miji kama vile Listra, Ikonio na Antiokia wa Pisidia, kisha, katika safari iyo hiyo, walirudi ‘wakawawekea wazee katika kundi.’ (Matendo 13:14, 42-52; 14:1-7, 20-23) Kwa kuwa safari yote ya umisionari inaelekea ilichukua sehemu ya miaka miwili tu, ni wazi kwamba wengine wa wanaume hawa hawakuwa na ujuzi wa miaka mingi kama wanafunzi Wakristo. Lakini kwa kuwa kulikuwako waamini Wayahudi kati yao, bila shaka wengi wa wale waliochaguliwa, ikiwa si wote, walikuwa na msingi mzuri wa maarifa ya Biblia pamoja na ujuzi katika kutumia kanuni za Maandiko ya Kiebrania hata kabla ya kuwa Wakristo.

14 Kwa hiyo, badala ya kujaribu kuweka mipaka, lazima tuongozwe na hekima pamoja na uamuzi mzuri, na kufikiria hali zinazohusu ujuzi katika ibada ya kweli za yule anayefikiriwa kuwa mzee. Katika kundi ambalo washiriki wengi wamekuwa katika kweli katika makumi mengi ya miaka, mwanamume aliyebatizwa katika muda wa miaka kama mitatu hivi anaweza kuonekana kuwa wa ‘hivi karibuni.’ Lakini katika kundi lililoundwa hivi karibuni ambalo washiriki wake waliikubali kweli hivi karibuni, ujuzi wa mwanamume kama huyo waweza kuonekana kuwa wa muda mrefu ukilinganishwa na wao. Kwa vyo vyote, ni jambo la maana kukumbuka nyakati zote kwamba ikiwa mwanamume atachukua madaraka mazito ya kulichunga kundi la Mungu anahitajiwa kuonyesha hekima, akili pamoja na uamuzi mzuri.

MAENDELEO KATIKA KUONYESHA HEKIMA NA UFAHAMU

15. Wazee wanapaswa kuonesha roho gani juu ya kufanya maendeleo katika sifa na uwezo wao?

15 Tayari Timotheo alikuwa mzee mwenye ujuzi wakati mtume Paulo alipomshauri ajishughulishe sana na mambo ya kiroho ili “kuendelea [kwake] kuwe dhahiri kwa watu wote.” (1 Tim. 4:15, 16) Mtu mwenye hekima hawi na kichwa kikubwa au kuona kwamba hawezi kufundishwa tena au kufanya maendeleo. “N’nani aliye na hekima na ufahamu kwenu?” akaandika mwanafunzi Yakobo, na kuongezea, “Na aonyeshe kazi zake kwa mwenendo wake mzuri, katika upole wa hekima.” Roho ya namna hiyo inaleta upatano kati ya baraza ya wazee, na kuondoa roho yo yote ya kutopatana, wivu au mabishano.​—Yak. 3:13-18.

16. (a) Wazee wako sawa katika maana gani? (b) Kuendelea kwao kwawezaje kuonekana kwa faida kubwa ya kiroho kwa wote waliomo katika kundi la Mungu

16 Ijapokuwa wazee wanaweza kuwa “sawa” katika madaraka na mamlaka yao katika kutumikia na kufanya kazi kwa ajili ya kundi, kwa lazima wao hawako sawa katika mambo mengine yote. Wengine wana ujuzi mwingi zaidi, katika maisha na katika kweli, nao wamefanya maendeleo kwa sababu ya kujifunza kwa uzito na kujitahidi kwa muda wa miaka mingi. Kila mmoja anakuwa na nguvu na udhaifu wake. Ikiwa sisi tutathamini na kufaidika kutokana na nguvu za wengine, sisi, vilevile, twaweza ‘kuacha kuendelea kwetu kuwe dhahiri kwa watu wote.’ (Rum. 12:3-10, 16) Kwa njia ya msaada unaotolewa kupitia kwa wachungaji kama hao wanyenyekevu, wenye juhudi wanaomwogopa Mungu walio na maarifa na ufahamu, lile neno la unabii litatimia nalo kundi la Mungu leo ‘litaongezeka na kuwa na washiriki wengi katika nchi,’ yote hayo kwa sifa ya milele ya Mungu.​—Yer. 3:15, 16.

[Chati katika ukurasa wa 14]

Kati ya Kati ya

wazee Waisraeli wazee Wakristo

(Kut. 18:21; Kum. 1:13) (1 Tim. 3:1-7, NW; Tito 1:5-9, NW)

Walio na uwezo, wenye Wenye kustahili kufundisha,

awezaye akili kutia moyo na kukaripia

wenye kumcha Mungu wenye haki, wapendao mema,

wenye kushikamana sana na neno la uaminifu katika kufundisha

watu wa kweli wasio na shtaka, washikamanifu, walioshuhudiwa vyema na walio nje

wenye kuchukia mapato si wenye pupa ya mapato ya uda

ya udhalimu nganyifu au wapenda fedha

wenye fahamu mwenye kujiweza, timamu katika

akili, wenye kusikiliza shauri

wenye ujuzi (mara nyingi) baba wa jamaa, si

waliogeuka karibuni

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki